Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Fergie weighs into the Charlie Adam bidding war

Published 23:00 22/01/11 By Derick Allsop




Sir Alex Ferguson has told Blackpool boss Ian Holloway that he would be "silly" to sell his inspirational captain Charlie Adam.
Manchester United play Holloway's team at Bloomfield Road on Tuesday, with Fergie hailing their Premier League performances.
Liverpool have tabled a £4million bid for Adam, but United's manager said: "I don't think Ollie will sell.
"He'd be silly to sell him in the position they're in. He may do in the summer, but I don't think he'll sell players at the moment.

"Blackpool have been a breath of fresh air. I never thought they'd play in the Premier League the way they did in the play-off final. It's as if they say if we're going to fail let's do it gloriously. Their attacking impetus is catching a lot of teams out.
"Charlie has been the star. I've known him since he was a young boy in Scotland. He always had talent.
"Buying him for £500,000 has turned out good business. He has passing ability and he scores at a good ratio for a midfield player."
But with Liverpool favourites to sign Adam at some point, Ferguson added: "If Ollie gets an offer for one of his players from one of the big clubs, he's got to let him go to give him an opportunity he'll not get at Blackpool."


 
Mourinho eyeing stunning £100m double swoop for Spurs pair - report

Published 12:40 23/01/11 By Football Spy




Real Madrid are planning a stunning double swoop on Tottenham for Luka Modric and Gareth Bale, according to reports on Sunday.
Jose Mourinho is a huge admirer of the two Spurs stars and reportedly wants to bring them to Spain, despite the fact prising the duo away from White Hart Lane could cost up to a staggering £100m.
But Mourinho is thought to be convinced they are worth the cash and Spurs boss Harry Redknapp is braced for a fight to hold on to his players.
Modric, 25, joined Spurs in April 2008 for a club record £16.5m from Dinamo Zagreb, while 21-year-old Bale arrived in 2007 from Southampton.

Both have been key to the club's resurgence under Redknapp, who has taken the club from bottom of the Premier League in 2008 to the Champions League group stages


 
Chelsea linked with surprise swoop for Arsenal star - report

Published 12:59 23/01/11 By Football Spy




Andrey Arshavin is being linked with a move to Chelsea, according to reports in Sunday's papers.
The Arsenal midfielder has been struggling with poor form this season and speculation has increased in the last few weeks that he may be set to leave the club in the summer.
But now Chelsea have emerged as a shock contender to buy the Russia star.
Arshavin is now 29 and has less than 18 months left on his current contract so would likely be available for around £10m.


 
Blackburn 2-0 West Brom - Hoilett seals win for Rovers

Published 17:59 23/01/11 By MirrorFootball




Blackburn manager Steve Kean celebrated his long-term contract with a third home victory in a row as Rovers saw off West Brom at Ewood Park to climb up to seventh place in the Barclays Premier League.
Kean this week signed a deal to keep him at the club until the summer of 2013 and, after a hotly-contested 40 minutes, he watched as Gabriel Tamas gave Rovers a huge helping hand with a powerful header into his own net.
The hosts' second came less than two minutes into the second half, Junior Hoilett sending a blistering shot into the roof of the net, and Blackburn held on reasonably comfortably, although West Brom should have had a penalty for a foul on Peter Odemwingie.
Blackburn manager Steve Kean gave starts to January signings Roque Santa Cruz and Jermaine Jones in today's Barclays Premier League clash with West Brom.

There was a blow for Kean, though, with key defender Ryan Nelsen ruled out by a knee injury while El-Hadji Diouf dropped to the bench.
West Brom welcomed back defender Jonas Olsson following suspension in their only change from last weekend's 3-2 victory over Blackpool, with the Swede replacing ankle injury victim Graham Dorrans.
Kean was looking for a third home win in a row to celebrate signing a new long-term contract this week, which ties him to Rovers until the summer of 2013.
However, the hosts were almost behind in the first minute when a mistake in midfield by Morten Gamst Pedersen allowed James Morrison to find Peter Odemwingie, and the striker's fierce volley was tipped around the post by Paul Robinson.
At the other end, Olsson, who was out for two-and-a-half months with an Achilles injury before being sent off in the FA Cup defeat by Reading two weeks ago, showed his class by halting a driving run by Nikola Kalinic.
The Rovers striker scored twice in a 3-1 win for Blackburn at the Hawthorns in the reverse fixture three weeks ago, part of a run that saw the Baggies beaten six times in a row.
Jones, signed on loan from Schalke this week, then hinted at what he has to offer with a driving run from left-back as the lively early tempo continued.
Robinson was nearly caught out in the 13th minute when Paul Scharner nipped in front of him to collect a deflected cross and laid the ball back to Jerome Thomas, whose shot beat the goalkeeper but drifted a yard wide of the far post.
Santa Cruz, making his first start at Ewood Park since leaving for Manchester City 18 months ago, was struggling to get into the game but his side were now building some momentum.
A scramble in the West Brom box following a long throw from Pedersen ended with Martin Olsson firing a shot through a crowd of players that Boaz Myhill, who retained his place at the expense of captain Scott Carson today, did brilliantly to keep out.
Then a limping Gabriel Tamas played Christopher Samba onside and his effort was also pushed away by Myhill. In the 33rd minute, the big defender was at it again but this time his 20-yard shot fizzed just wide of the post.
West Brom continued to look dangerous on the break and, after shots by Thomas and Youssouf Mulumbu had been blocked, the former saw his effort deflected just wide by Samba.
In the 41st minute, though, the Baggies found themselves behind, and it was a goal all of their own making. David Dunn swung in a decent cross from the right that Tamas, under notional pressure from Santa Cruz, headed powerfully into his own net.
Myhill then produced another terrific save as Santa Cruz rolled back the years with a run and shot that met the firm hand of the former Hull goalkeeper.
Blackburn deserved their lead, even if the goal was somewhat fortunate, but there was nothing lucky about their second, which came only 78 seconds into the second half and dealt a major blow to Albion's hopes of taking anything from the game.
A neat touch on his chest from Kalinic set Junior Hoilett on his way and the 20-year-old jinked past Tamas before unleashing a shot from 20 yards that flew over Myhill and into the net.
It was the Canadian's first Premier League goal and it may be some time before he scores a better one.
At the other end, the impressive Thomas continued to threaten the Rovers defence and he curled in a 25-yard effort that would have nestled in the far corner had Robinson not got his fingertips to it.
Blackburn right-back Michel Salgado then went after his first league goal, striking a volley that was punched away by Myhill, while Thomas and Robinson continued their battle, again the goalkeeper coming out on top.
In the 64th minute, Kean made a double change, bringing on Jason Roberts for Kalinic and Steven Nzonzi for Dunn, with the latter making his first appearance after three months out with a hamstring injury.
Having made a good impression on his debut, Jones should have blotted his copybook by conceding a penalty in the 68th minute for an inadvisable lunge on Odemwingie only for referee Mark Clattenburg to inexplicably award a free-kick instead.
The offence was clearly a yard inside the area but the Baggies' protests were in vain and Chris Brunt slammed his kick into the wall.
West Brom continued to press but they were reduced to long-range efforts as Rovers comfortably kept the visitors at bay, and indeed it was Kean's side who came closest to adding to their lead.
With the clock ticking into three minutes of injury time, Olsson drove into the box and tested Myhill with a stinging shot, with Roberts just failing to convert the rebound.
And the day almost ended in perfect fashion when Santa Cruz, looking suspiciously offside, curled a shot just over the bar with Myhill rooted to the spot.
Blackburn vs West Brom - Premier League picture special
 
Spurs planning to rush through Diarra loan deal

Published 23:00 22/01/11 By Steve Stammers




Tottenham want to sign Lassana Diarra this week.
The plan is to beat the January transfer deadline by recruiting the 25-year-old French international on loan from Real *Madrid for the rest of this season and secure the option to buy him on a *permanent basis in the summer.
Manager Harry Redknapp knows Diarra well.
He signed Diarra for £5.5million from Arsenal while he was in charge at Portsmouth three years ago and 12 months later sold him to Real for £18m.


In his 12 months at Fratton Park, Redknapp’s man management skills brought the best from the player whose style has been likened to compatriot Claude Makelele in a holding midfield role.
Diarra had first come to England six years ago from Le Havre to Chelsea for £1m. But he became *increasingly *frustrated at the failure to establish himself in the first team and moved to Arsenal for around £1m in 2007.
However, he was also at odds with Arsenal manager Arsene Wenger *because he was not an automatic choice and within six months had moved to Portsmouth.
Redknapp has made no secret of his admiration for Diarra and if he *impresses, then chairman Daniel Levy could be tempted to pay Real £10m to make him a full-time addition.
Sunderland boss Steve Bruce admits that he could go back to Spurs in his search for Darren Bent’s *successor.
The Black Cats boss paid an initial £10m to lure Bent from White Hart Lane in the summer of 2009 and a similar sum would land him Russian striker Roman Pavlyuchenko.
Bruce admitted: “Spurs might be my *begging bowl – they always have a few strikers.’’
Ideally, Bruce, armed with £18m from the shock sale of Bent to Aston Villa, would like Peter Crouch, who turned him down 18 months ago.
But Spurs boss Harry Redknapp is *adamant he wants to keep the towering Crouch and the same goes for his England striking colleague Jermain Defoe.
That would leave only Pavlyuchenko and Republic of Ireland hitman Robbie Keane to choose from as Spurs have indicated both could leave at the right price.
But Sunderland chairman Niall Quinn has already indicated that Keane isn’t the type of striker the Black Cats are looking for.
 
Newcastle to spark transfer scramble by dumping Dutch keeper

Published 23:05 22/01/11 By People Sport




A full version of this story appears in today's People. Read it online at People.co.uk
Newcastle are set to spark a transfer scramble by dumping goalkeeper Tim Krul.
The Dutchman lost the No.1 spot after Steve Harper returned from injury.
New goalkeeping coach Andy Woodman is not convinced the 22-year-old is good enough to be 35-year-old Harper's long-term replacement.


 
Newcastle to spark transfer scramble by dumping Dutch keeper

Published 23:05 22/01/11 By People Sport



A full version of this story appears in today's People. Read it online at People.co.uk
Newcastle are set to spark a transfer scramble by dumping goalkeeper Tim Krul.
The Dutchman lost the No.1 spot after Steve Harper returned from injury.
New goalkeeping coach Andy Woodman is not convinced the 22-year-old is good enough to be 35-year-old Harper’s long-term replacement.


 
QPR 2-1 Coventry: Routledge grabs winner on second Hoops debut

Published 15:44 23/01/11 By MirrorFootball




Wayne Routledge marked his second QPR debut with a goal as the npower Championship leaders came from behind to sink Coventry.
This time last year the winger left Loftus Road for Newcastle and helped guide the Magpies to promotion and the title.
He looks eager to repeat the trick having rejoined Rangers on loan and got off to the perfect start by hitting the winner against the Sky Blues.
Adel Taarabt had earlier added another dazzling solo effort to his growing collection to cancel out a shock opener from Coventry's Marlon King.


Rangers' early-season promotion charge may have slowed down to more of a canter - this was only their third win in eight outings - but they still sit a handy five points clear of the chasing pack.
Routledge set about Coventry from the off and almost set up an opening goal after 12 minutes.
The winger turned Martin Cranie inside-out before crossing to Heidar Helguson, whose downward header bounced up and over the crossbar.
Rangers were screaming for a penalty after 23 minutes when a bullet header from Helguson struck Cranie's arm but referee Mark Haywood was not interested.
Moments later City goalkeeper Keiren Westwood was called into action to tip a fierce drive from Shaun Derry over the crossbar.
Yet against the run of play the visitors opened the scoring in the 25th minute with their first attack of the game.
Gary McSheffrey's ball across the face of goal was missed by Rangers defender Matt Connolly and King was left with a simple tap-in past Paddy Kenny.
The hosts could have found themselves two down when Freddy Eastwood burst into the area and got the better of Connolly, but the former Southend frontman dragged his shot wide.
Taarabt, the player who has had more shots than any other in the Championship this season, then took aim from 25 yards but his effort flashed past the post.
But the Moroccan found his range in first-half stoppage time, jinking inside Richard Keogh before unleashing a stunning curler from the corner of the area beyond Westwood and into the net.
Rangers came agonisingly close to taking the lead six minutes after half-time when a free-kick from Alejandro Faurlin beat the dive of Westwood but came back off the inside of the post.
But they were not to be denied and with 11 minutes left Taarabt's lofted pass sent Routledge through and with a delightful first touch and finish he secured the three points.
 
Sky Sports pair Keys and Gray in sexist rant about female official and Karren Brady

Published 15:21 23/01/11 By MirrorFootball




Sky Sports duo Andy Gray and Richard Keys have found themselves at the centre of a sexism row after they were apparently recorded making derogatory remarks about a female assistant referee and West Ham vice-chairman Karren Brady.
The pair apparently thought their microphones were turned off while they were watching Liverpool's Premier League match with Wolves on Saturday, and were heard questioning whether female official Sian Massey knew the offside rule.
Keys said of Massey: "Somebody better get down there and explain offside to her."
Gray then replies: "Can you believe that? A female linesman. Women don't know the offside rule."


"Course they don't. I can guarantee you there will be a big one today. Kenny [Liverpool boss Kenny Dalglish] will go potty. This isn't the first time, is it? Didn't we have one before?" adds Keys.
Later on Keys says: "The game's gone mad. Did you hear charming Karren Brady this morning complaining about sexism? Do me a favour, love."
 
Wanachama Yanga SC dhibitini mpasuko huu


KWA takriban wiki moja sasa, ndani ya klabu ya Yanga, mmoja wa wawakilishi wetu katika michuano ya kimataifa, hali si shwari.
Hali hiyo imetokana na baadhi ya wanachama kuhoji mwenendo wa baadhi ya mambo katika klabu yao.
Hali hiyo ikazaa kikao cha viongozi wa matawi ya klabu hiyo mkoa wa Dar es Salaam kilichofanyika Januari 20, mwaka huu, kwenye makao makuu ya klabu hiyo, mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo.
Licha ya mwenyekiti wa klabu hiyo, Llyoid Nchunga, kuupinga kwamba ni batili kwa mujibu wa katiba, viongozi hao walikutana na kufanya maamuzi.
Kikao hicho kilifikia maazimio ya kutaka Nchunga abanwe na Kamati ya Utendaji na ikiwezekana asimamishwe, kabla ya suala hilo kuamuliwa na Mkutano Mkuu.
Hoja za viongozi hao wa matawi ni hatua ya Nchunga kuandika barua ya kumtaka Francis Kifukwe kufufua kampuni, bila suala hilo kupata baraka za vikao husika.
Aidha, viongozi hao walihoji uteuzi wa Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, kuwa mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya klabu hiyo.
Kwa uteuzi huo uliofanywa na mdhamini wa klabu hiyo Yusuf Manji, Mtemvu aliungana na Manji, Mama Fatma Karume na Kifukwe katika bodi hiyo.
Kwa mujibu wa viongozi hao wa matawi, mbali ya wanachama kutoshirikishwa katika suala la uteuzi, pia hawatambui kama Mtemvu ni mwana Yanga wa kuaminika.
Maazimio hayo ya viongozi hao wa matawi kutaka Nchunga abanwe na Kamati ya Utendaji, yameibua mvutano mkubwa kwa mhusika mwenyewe kusema wanachana hao hawana ubavu wa kushinikiza mwenyekiti wao achukuliwe hatua na Kamati ya Utendaji, kwani kamati hiyo haiwajibiki kwao.
Viongozi hao walikwenda mbali zaidi na kuutaka uongozi wa klabu hiyo kuweka wazi kama Manji ni mfadhili au mdhamini.
Kwa ujumla, tangu kuibuka kwa vurumai hiyo, kinachoshuhudiwa sasa ndani ya klabu hiyo ni vikumbo vya wanachama wenye mitizamo tofauti.
Wakati makundi hayo yakiibuka, kila moja kwa maslahi yake katika suala hili, imeripotiwa Katibu Mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu wa klabu amejiuzulu.
Sisi wa Tanzania Daima tukiwa kama wadau wa michezo na burudani tusioegemea upande wowote zaidi ya klabu ya Yanga kuwa taasisi inayojishughulisha na michezo, tunasikitishwa na hali hii inayozidi kuchukua sura mpya.
Kwa kinachotokea Yanga ni wazi kuwa kuna matatizo makubwa ndani ya klabu hiyo yanayotishia ustawi wake.
Sisi wa Tanzania Daima kutokana na mazingira haya, tunawasihi wanachama wa Yanga kuzidisha umoja na mshikamano hivi sasa kwa manufaa ya klabu na si kwa faida ya kundi la wachache.
Wanachama wanavyoendelea kumeguka kila kukicha, ni sawa na kugombea fito ilhali wote mnajenga nyumba moja, jambo ambalo ni hatari. Hivyo jipangeni upya kwa maslahi ya Yanga.
 
Yanga msizime moto kwa majivu

Shehe Semtawa

WAKATI ikikabiliwa na mashindano ya kimataifa, timu kongwe nchini, Yanga ya jijini Dar es Salaam imekuwa ikikabiliwa na mtafaruku wa uongozi.
Mgogoro huo kama haukupatiwa ufumbuzi wa haraka, huenda ukawa chanzo cha timu hiyo kufanya vibaya katika mashindano hayo ya kimataifa na ligi ya hapa nyumbani.
Kumekuwa na kauli mbalimbali kutoka kwa baadhi ya wanachama waliokutana makao makuu ya klabu hiyo Jangwani, ambao wamemtaka Mwenyekiti Lloyd Nchunga asimamishwe kwa tuhuma za kukiuka kanuni za utawala.
Hata hivyo, Nchunga alijibu mapigo na kudai kuwa hawezi kujiuzulu na walioandaa kikao hicho watachukuliwa hatua ikiwamo kusimamishwa uanachama.
Wakati viongozi hao wa matawi wakiwashutumu mwenyekiti na mfadhili wao Yusuf Manji kuwa ndio chanzo cha migogoro klabuni hapo, kundi la wazee nalo limejichomoza kwa kumkingia kifua mfadhili huyo kuwa bado anahitajika.
Kundi hilo likiongozwa na mwenyekiti wake, Yusufu Mzimba, kwa niaba ya wazee wenzake anasema, hiki si kipindi cha malumbano, kwani timu inakabiliwa na michuano mikubwa ya kimataifa na ule wa ‘mnyama' Simba ambao uko mbele yao.
Mzimba anasema, baadhi ya wanachama wamekuwa na tabia ya kuwapendekeza viongozi kisha huwageuka mbele ya safari na kusababisha timu kuingia kwenye mivutano isiyo ya lazima.
Anasema wao wakiwa wazee wanaoifahamu klabu hiyo vizuri tangu ilikoanzia, hawakubaliani na maazimio kadhaa yaliyotolewa kwenye kikao kilichofanyika Januari 20, mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kutaka kumtoa mfadhili wao Manji ama afuate masharti ya klabu hiyo.
Si hoja yangu kuelezea mustakabali wa vikao vya makundi hayo, lengo hapo lilikuwa ni kutoa angalau picha ya kile kinachoendelea ndani ya Yanga na nini labda kifanyike kwa mtazamo wangu katika kurejea hali ya amani ya kudumu.
Kwanza kwa angalizo, napenda niweke wazi, hapa siko upande wa kundi lolote bali lengo ni kutaka hali irejee na soka lichezeke Yanga wala si amani kupotea.
Ieleweke kuwa kutokana na hali hii inayoendelea ndani ya Yanga, matokeo yake yatakuja kuwa makubwa na gharama za kuyatatua zitakuwa kubwa tofauti na wengi wanavyodhani.
Kwa mtazamo wangu naweza kusema wazee wana haki ya kusema waliyoyasema, kwani wanaonyesha kutaka kuona Yanga ikienda hasa kutokana na maelezo yao kuwa wana historia kutokana matokeo mabovu ya huko nyuma kwa kufukuzwa wafadhili na migogoro mbalimbali.
Lakini pia, viongozi wa matawi waliohoji baadhi ya mambo waliyoyaona yanakwenda sivyo wana haki na si wa kupuuzwa na hata kundi la wanachama 30 lililoibuka na maoni yake nalo halipaswi kubezwa, kwani ni haki yake kikatiba kutoa maoni.
Kwa mtazamo wangu si makundi hayo tu yaliyojipambanua hadharani wakati huu, bali wana Yanga wote walioko jijini Dar es Salaam, mikoani na hata nje ya nchi wana haki ya kusikilizwa hoja zao na kama zina maslahi kwa klabu ya Yanga zifanyiwe kazi wala si kutishana.
Kwa faida ya michezo ya nchi hii, nawaomba Wanayanga kwa pamoja kuitisha vikao halali vitakavyowakutanisha wote na kusaka ufumbuzi utakaosaidia kupatikana tiba ya kudumu na kutoruhusu udhaifu uliosababisha haya kutokea, ili yasirejee tena.
Kuendeleza kufukia moto kwa majivu Wanayanga wajue hawauzimi bali wanauhifadhi na ukija kesho upepo utauwasha tena na kazi upya itaanza.
Hivyo uandaliwe mkutano bila kuchochewa kwa hila zozote, yajadiliwe haya ambayo yameibua mtafaruku huu na tiba sahihi ipatikane bila kuonea haya wala unafiki, kinyume na hapo basi Wanayanga tambueni kuwa mtakuwa likizo fupi tu ya utulivu kabla ya kurejea kwenye mbilinge mpya ya migogoro. Naiombea amani itawale Yanga kwa manufaa ya sekta ya michezo Tanzania.
 
Yanga jiulizeni, hivi kwa nini Manji?

Tullo Chambo

NI Jumatatu nyingine tunakutana wapenzi wasomaji wa safu hii ya Uwanja wa Kuchonga, iwajiayo kila siku kama ya leo, lengo likiwa ni kupeana changamoto za kispoti ili kuleta ufanisi.
Bila shaka mu wazima wa afya na mnaendelea na majukumu mbalimbali ya ujenzi wa taifa, ila kwa wale hali zao si shwari tunawaombea nafuu na kuwatakia kila la heri.
Kwa wale ambao hatukuwa pamoja wiki iliyopita, mashabiki uwanjani tulikuwa na hoja isemayo; ‘Ngeta mbona umeanza kutuangusha mapema TFF?'.
Katika mada hiyo, tuliuangalia mwanzo wa watendaji wapya wa Shirikisho hilo chini ya Katibu Mkuu, Angetile Osiah ‘Ngeta', ambapo kimsingi hatukusita kuonyesha hofu yetu ya mapema juu utendaji makini.
Hali hiyo, ilitokana na siku chache tu, tangu Ngeta na timu yake waanze kibarua chao ndani ya shirikisho, nacho ni kutokuwa na maamuzi yaliyosimama kwa hoja zisizobadilika kama kinyonga.
Jambo lililotusukuma hadi kuhoji, inakuwaje leo unaibuka na kuutangazia umma kuwa haya kisha kesho inageuka na kutengua, tena ukipima sababu za utenguzi wa maamuzi hayo hazina msingi zaidi ya kuonyesha TFF haina msimamo ama inafanya kazi kwa kukurupuka.
Hapo tuliegemea sakata la hivi karibuni kati ya wadau wanaojitokeza kuzialika timu kutoka nje ya nchi kucheza na klabu za kwetu husasan wawakilishi wetu katika michuano ya kimataifa, Simba na Yanga, ambako wadau kwa kushirikiana na Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), iliialika Zesco ya Zambia, awali ikiwa tayari imeishaileta AFC Leopard ya Kenya.
Lakini wakati Zesco ikiwa imewasili hapa nchini, TFF iliibuka na kuutangazia umma kuwa mchezo huo hautakuwepo ikitoa sababu kadhaa, lakini kubwa ni kuwa hivi sasa kalenda ya shirikisho hilo hairuhusu kwani hivi sasa ligi kuu mzunguko wa pili umeanza.
Lakini kesho yake, TFF hiyohiyo ikalamba matapishi yake na kukubali hiyo ichezwe, kisha tukasikia kuna nyingine kutoka Brazil. Hivi hapo wadau waibebee mbeleko gani? Kimsingi inasikitisha, inavunja nguvu na inatia hasara kwa wahusika waliojitolea kufanya ‘biashara' hiyo ambayo ina manufaa kwa maendeleo ya soka la Tanzania. Hapo tuliwataka viongozi hao wa TFF, kufanyia kazi ushauri wa Rais wao Leodegar Chilla Tenga, kuwa hapo Karume ni pagumu panahitaji uadilifu na kuchunga ndimi ambazo zinaweza kuibua mtafaruku miongoni mwa wadau. Bila shaka wahusika watalifanyia kazi hilo.
Sasa turejee katika mada, hakika hivi sasa hali si shwari ndani ya klabu kongwe ya Yanga, ambako kumeibuka msigano mkubwa miongoni mwa wanachama, viongozi na mfadhili ambaye pia ni mdhamini.
Lakini tangu kuanza msigano huu, hoja kadhaa ziliibuliwa na hao waliokuwa na hoja ambao hatimaye waliongozwa na viongozi wa matawi ya Yanga chini ya Mwenyekiti Mohammed Msumi na mkutano kufanyika makao makuu ya klabu hiyo.
Katika mkutano huo wa Januari 20 ziliibuliwa hoja kadhaa ambapo ni wazi kabisa zilionyesha kuna udhaifu katika utendaji ndani ya Yanga, ikiwamo baadhi yao kujiamulia maamuzi binafsi bila kushirikisha vikao halali, ambapo katika hali hiyo hata Katibu Mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu alikiri mbele ya wanachama kuwa hayajui.
Pili ilihojiwa uhalali wa kikatiba wa mfadhili wao Yussuf Manji kumteua Mbunge wa Temeke kuwa mjumbe wa baraza la wadhamini, wakati hata naye Manji bado hajapitishwa rasmi kisheria na kutambulika na Kabidhi Wasii Mkuu.
Pili uanzishwaji wa kampuni itakayosimamia biashara za Yanga, ambako jukumu hilo alikabidhiwa mmoja wa wadhamini, Francis Kifukwe na Mwenyekiti wa Yanga, Lloyd Nchunga, jambo lilidaiwa halikupata baraka za vikao halali.
Kesho yake baada ya kikao hicho cha matawi, akaibuka Nchunga na kuelezea kuwa mkutano huo haukuwa halali, lakini hapo hapo akaanza kutoa ufafanuzi juu ya hoja zilihojiwa katika mkutano ambao anadai si halali.
Kwa akili za kawaida kabisa, kama ni mfuatiliaji wa mambo, kutokana na ufafanuzi huo wa Nchunga utagundua kuwa viongozi wa matawi walikuwa na hoja ndio maana nyingine alizijibu. Sasa tujiulize, bila viongozi wa matawi kupaza sauti kuhoji sintafahamu ile wanachama wa Yanga wangejuaye hayo yanayoendelea chini kwa chini.
Katika majibu ya Nchunga alikiri kuwa kikao chao kilichoketi siku chache nyuma kilisitisha kwanza maamuzi ya barua ya kumpa jukumu hilo Kifukwe na uteuzi wa Mtemvu. Sasa hapo unataka nini tena kama si udhaifu wa kiongozi aliyeandika barua. Pili kama kuna kikao kilitengua maamuzi nyeti kama hayo ambayo tayari yalishafikiwa, Nchunga alisubiri hadi viongozi wa matawi waitishe mkutano ya kuyaweka hadharani mapungufu hayo? Hapo tatizo kuna nini kinafichwa na viongozi wa Yanga.
Lakini ilivyo ada ya baadhi ya wana Yanga tena hasa baada ya kupatikana kwa Manji ndani ya klabu hiyo, wamekuwa wakali kila linapohojiwa jambo hata jema kwa klabu hiyo lakini kwa namna moja ama nyingine linakwaruza matakwa ya mfadhili huyo. Hoja yao kubwa huwa eti hao wanatumwa wanataka kuturudisha enzi za migogoro na Yanga ilioyokuwa yatima. Hawa ndio wanachama hatari na ndio wanaosababisha hali kama hii kutokea, kwani wamezoea kutofuata katiba yao, kisa eti mfadhili.
Ni wanachama hawahawa ambao bila haya walidiriki bila hoja za msingi kutaka kumng'oa aliyekuwa Mwenyekiti wao Imani Madega, kisa kikiwa ni mfadhili, lakini kutokana na kutotambua vema vipengele vya katiba yao waligonga mwamba.
Lakini ni wanachama hawa hawa niliowaainisha kuwa ni hatari kwa maslahi ya Yanga, ndio mwaka 2008 walipoona mafahali wawili Manji na Madega wako pamoja, ndio waliwapinga wale wenye maono ya mbali kwenye bwalo na maofisa wa polisi Oysterbay ambao walikuwa wakitaka kupewa ripoti ya fedha, wakidai wanachelewa kwenda Morogoro kuiangalia timu yao.
Hawa hawa leo eti wanaibuka kudai kuwa walihudhuria mkutano wa matawi Januari 20 ambao uliibua udhaifu huu wa utendaji wa viongozi na mfadhili, kuwa eti walidanganywa mambo mengi, sijui yapi?
Pia, wanachama hao wasiozidi 30 ambao ni watu wazima, wanadiriki kuingia kwenye moyo wa Manji na kumsemea eti, "Msimamo wetu ni kwamba hakuna baya Yusuf anaweza kufanya Yanga. Anaitakia Yanga mema na sisi hatuwezi kukubali hayo yanayopangwa dhidi yake yafanikiwe."
Ni kauli ya kinafki kujivika joho hilo, sijui kesho likitokea la kutokea wataficha wapi nyuso zao mbele ya wana Yanga ambao leo wanajitolea kutaka kuona klabu yao inaendeshwa kwa misingi ya katiba.
Hivi hawa wanachama wanaopinga wenzao wanaohoji uvunjwaji wa katiba ya Yanga kwa nia njema, wana maslahi gani?
Ni hawa hawa 2008 walibariki hesabu zisitolewe na uongozi upewe muda zaidi kisa mfadhili alikuwa karejeana na Madega ambaye walikwaruzana, leo eti wanaibuka na kudai eti Manji ndiye mtetezi wa mali za Yanga na ameandika barua kutaka hesabu hizo zitolewe leo!
Hakika wanaoitakia mema Yanga, wanapaswa kubaini hali hii na kujiuliza hivi kwa nini Manji? Haya yanatokea. Leo hii Katibu Mkuu Mwalusako kaachia ngazi, kisa misukosuko hiihii, jiulizeni mara mbili mambo haya.
 
KILI Marathon 2011: Wanariadha wa Tanzania wana deni kubwa

Mwandishi wetu

FEBRUARI 27, mwaka huu, mji wa Moshi, mkoani Kilimanjaro utazizima pale utakapovamiwa na wanariadha mbalimbali wa kimataifa na wadau wa michezo kwa ujumla kutoka nchi mbalimbali, lengo kuu likiwa ni kushuhudia na kushiriki katika tukio kubwa katika kalenda ya michezo hapa nchini. Nalo si jingine, bali ni msimu wa tisa wa mbio za kimataifa za Kilimanjaro Marathoni.
Mbio hizo ambazo hutambuliwa na Shirikisho la Riadha la Kimataifa (IAAF), hushirikisha matukio matatu ambayo ni Marathoni kamili km 42.1, Nusu Marathoni km 21.1 na zile mbio za kujifurahisha za Km 5.
Wakati msimu huu wa tisa ukinukia, unaweza kusema wanariadha wa Tanzania wana deni kubwa mwaka huu, hasa kutokana na hali halisi iliyojitokeza mwaka jana, tena mbele ya aliyekuwa mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Kayanza Peter Pinda.
Akitoa zawadi ambazo ni vitita vya fedha kwa washindi Februari 28 kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu Ushika na Stadi za Biashara Moshi (MUCCOB's), Waziri Mkuu Pinda hakusita kuelezea kinachomuuma moyoni, nacho si kingine, bali kuona zawadi hizo hasa zile kubwa zikienda nje ya nchi hasa Kenya, huku Watanzania wakishuhudia.
Hali hii ya Watanzania kushuhudia wakishindwa kung'ara katika mbio hizi ilijitokeza katika misimu kadhaa nyuma baada ya kuanza kwake 2003, ambako kuanzia 2007, uteja huo ulianza kufutwa kwa kishindo ikiwamo kuweka rekodi mpya.
2008 katika Marathoni kamili ilishuhudiwa Mtanzania Jumanne Tluway akishika nafasi ya kwanza na kuweka rekodi mpya ya saa 2:15.34 huku akifuatiwa na mwenzake Andrea Silvin 2:16.22 huku Mashaka Masumbuko akikamata nafasi ya tatu kwa kutumia saa 2:16.57. Huku kwa wanawake Banuelia Brighton saa 2:48.47 aking'ara kwa kushika nafasi ya kwanza na Flora Kagali akishika nafasi ya tatu akiwa na muda wa saa 2:53.47. Hakika ilikuwa raha kushuhudia hali hii, ambako bendera ya Tanzania ilikuwa ikipepea vema.
Tofauti na majonzi ya mwaka jana, ambako Waziri Mkuu ‘kwa shingo upande' ilibidi tu akubali matokeo na kujikuta vitita vya fedha hizo akivikabidhi kwa Stephen Chebogus aliyeibuka
Mshindi akitumia saa 2:15.28 akifuatiwa na David Kiprono 2:16.45 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Julius Tumakuil saa 2:16.55 wote kutoka Kenya.

Kwa wanawake hali ilikuwa hivyo hivyo, ambako Fredah Lodepa alishinda akitumia saa 2:40.21 na kufuatiwa na Everline Atancha 2:40.26 na Leah Kujar 2:48.22 wote kutoka Kenya.
Kwa matokeo haya ya Marathoni kamili Km 42.2 hakika Watanzania wana deni kubwa katika mbio za mwaka huu.
Wakimbiaji mahiri kama akina Jumanne Tluway, Andrea Silvin, Samson Ramadhan, Nyangero Patrick na wengineo, ambao wana rekodi za kufanya vema katika mashindano mbalimbali ikiwamo Kilimanjaro Marathon katika miaka kadhaa iliyopita, wanapaswa kutambua deni hilo kubwa la Watanzania mwaka huu kuona bendera yao inang'ara.
Hali kadhalika kwa upande wa wanawake, Banuelia, Kagali, Fabiola William na wengineo wanaoibukia kwa kasi hivi sasa, nao wanapaswa kutambua deni kwa upande wao, nalo ni kuhakikisha taji linabakia nyumbani ikiwamo hata kuandika rekodi mpya.
Kwa upande wa Nusu Marathoni ambayo angalau tunapumua kutokana na rekodi kuonyesha wanariadha wa Tanzania waking'ara na kile walichokifanya wanaume mwaka jana kinapaswa kurejewa mwaka huu, tena ikiwezekana kwa kishindo zaidi.
Katika Kili Nusu Marathoni mwaka jana, Fabian Joseph, alishinda akitumia saa 1:04.00 akifuatiwa na Dickson Marwa 1:04.19 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Damian Chopa wote kutoka Tanzania huku kwa wanawake, wao waliteleza kidogo na kumwacha Naomi Maiyo wa Kenya akishinda kwa saa 1:16.26 huku Restituta Joseph wa Tanzania akiibukia nafasi ya pili kwa saa 1:16.35 na kufuatiwa na Mkenya Lucy Karimi 1:16.49.
Hiyo ni changamoto kwa wanawake, akiwamo Restituta mwenyewe kutambua pale alipoteleza mwaka jana, chipukizi Mary Naali ambaye alishika nafasi ya nne mwaka jana na wengineo, kufanya vema mwaka huu na kurudisha heshima ya Tanzania katika riadha.
Wanariadha wa Tanzania wanapaswa kuikumbuka changamoto ya Waziri Mkuu ambaye hakufurahishwa kuona wapinzani kutoka nje ya nchi wakitawala na kunyakua zawadi zote za juu na kuwataka mwaka huu kubadilika.
Pia Chama cha Riadha Tanzania (RT), kinapaswa nacho kuchukua nafasi yake kuhakikisha kinafanikisha wanariadha wake wanafanya vema mwaka huu, hasa kutokana na dhamana yao waliyopewa na Watanzania kusimamia na kuendeleza mchezo huo hapa nchini.
Pia Kilimanjaro Marathon Club, Chama cha Riadha Mkoa wa Kilimanjaro (KAAA) sambamba na RT, waratibu wa masuala ya ufundi, wanapaswa kuangalia ushiriki mzima wa wanariadha katika mbio hizo na kuepukana na udanganyifu wowote ili mshindi apatikane kwa haki.
Kilimanjaro Marathon hudhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake ya Kilimanjaro ambao ndio wadhamini wakuu, Vodacom Tanzania, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Tanga Cement, DT Dobie, Tanzanite One, KK Security, Keys Hotel, Kilimanjaro Water, Kiwanda cha Sukari (TPC), na Precision Air huku zikiratibiwa na Wild Frontiers ya Afrika Kusini na Executive Solutions.
 
Si muda mrefu Azam itazizima Simba, Yanga

Ojuku Abraham

TANZANIA bado iko katika ugonjwa sugu wa kuzipenda timu kongwe za Simba na Yanga. Popote walipo mashabiki wa soka, lazima watagawanyika kwa misingi ya timu hizo mbili. Moja kati ya vitu vya kusikitisha ni kwamba wakongwe hao walioasisiwa miaka mingi iliyopita, bado wanaendesha timu zao kizamani mno.
Lakini katika miaka michache iliyopita, imeanzishwa timu ambayo mwanzo wake, watu waliona kama nguvu ya soda, Azam FC.
Azam ilianzishwa na kuanza kucheza madaraja ya chini, kila mmoja akiamini ingekuwa na mwisho muda siyo mrefu kama klabu nyingi zilizowahi kuanzishwa kwa mbwembwe.
Lakini hatimaye msimu ya 2008/9 ulishuhudia Azam ikifanikiwa kuingia Ligi Kuu na kudumu hadi sasa. Msimu uliopita ilifanikiwa kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu na hadi hivi sasa ligi hiyo ikiwa katika mzunguko wake wa pili, timu hiyo inashika nafasi kama hiyo.
Katika kuhakikisha timu hiyo inafanya mambo vizuri zaidi, imejenga uwanja wake wa kisasa ulioko nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, huko Mbagala.
Kwa kuangalia mikakati inayoelezwa na viongozi wa klabu hii inayomilikiwa na familia ya mfanyabiashara mkubwa, Said Salim Bakhressa, ni wazi kuwa muda siyo mrefu ujao, klabu hii itakuwa juu ya Simba na Yanga timu zilizodumu kwa miaka mingi.
Na itakuwa juu kwa maana zote, kwani licha ya kuwa na uwezo wa kifedha wa kuweza kushindana na klabu hizo katika usajili wa wachezaji nyota, hata michakato yao juu ya makocha wa kuifundisha timu hiyo inaonyesha wazi dhamira waliyonayo.
Katika kipindi cha hivi karibuni, timu hiyo imewahi kunolewa na makocha watatu wa kigeni: Wabrazil Neider dos Santos, Itamar Amorin na sasa chini ya Mwingereza, Stewart Hall.
Moja ya kitu kitakachosaidia sana kupanda kwa haraka kwa umaarufu wa klabu hii, ni kuendelea kwa mipango mibovu, migogoro na soka la magazetini la klabu zingine, hasa Simba na Yanga.
Ukiangalia kwa mfano, katika uwanja wao ambao pia watautumia katika Ligi Kuu utakapokamilika, wanayo shule ya watoto wenye vipaji ya kwao kwa ajili ya wachezaji wao vijana.
Na timu hii imekuwa ya kudumu kwa kipindi kirefu sasa ambayo hadi sasa imeweza kuwapandisha hadi kikosi cha kwanza wachezaji wake kadhaa wakiwemo Sino Augustino, Himid Mao, Mau Ali, Tumba Swed, Ali Mkuba na Samih Nuhu.
Kitu kimoja ambacho klabu hiyo inakosa kwa sasa ni kupata nafasi kubwa katika vyombo vya habari ambavyo vyote navyo bado vimeendelea na utaratibu na fikra mgando za miaka yote kuzikumbatia Simba na Yanga.
Kama ingekuwa inaandikwa mara kwa mara, klabu hiyo ndiyo yenye wachezaji wazuri na mahiri kuliko wanaokuzwa na magazeti katika Simba na Yanga.
Na bila shaka, itakuwa ndiyo klabu inayolipa mishahara mizuri zaidi kwa wachezaji wake, tena kwa uhakika kabisa, tofauti na mishahara inayolipwa kwa fedha binafsi za watu katika Simba na Yanga.
Binafsi ninafurahishwa sana na uendeshaji wa timu hii, kuanzia benchi lake la ufundi lililojitosheleza, uongozi wake na hata wachezaji.
Na mashabiki watakaoipenda timu hii, watakuwa ni hawa hawa kutoka ndani ya Simba na Yanga, lakini waliochoshwa na madudu ya uongozi wa timu hizo zisizokuwa na dira.
Badala ya kupanga mikakati ya kuziingiza katika nyakati mpya, viongozi wake hadi leo wanagombea uhalali wa kuzungumza!
Pamoja na kuwa na uzoefu wa miaka mingi katika fitina za soka, upo uhakika wa wazi kuwa miaka si mingi ijayo, kama siyo mwakani, Azam itaanza kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.
Ikifika huko, ni wazi kuwa zitakuwa ni fikra za klabu hiyo kuanza kuona ni kwa jinsi gani inaweza kuwa yenye mafanikio katika Afrika kama ilivyo TP Mazembe au zile timu kutoka Afrika Magharibi na Kaskazini.
Nichukue nafasi hii kuwapa moyo Azam FC, waendelee na mipango yao ya kuwa klabu ya mfano wa kuigwa katika Tanzania, licha ya kuwa haina mtaji wa mashabiki.
Itakapofanikiwa katika mipango hiyo mingine, kazi ndogo iliyobaki ili kuwapata mashabiki, ni kutandaza kandanda la kuvutia na watu wa kweli wa mpira watakuwa pamoja nao kama zamani ilivyokuwa kwa Pan African, Pamba ya Mwanza na Ushirika ya Moshi.
 

Sisi twende Brazil? Labda Qatar

Ojuku Abraham

NIMEMSIKILIZA kocha msaidizi wa timu ya taifa Tanzania, ‘Taifa Stars', Sylvester Marsh, alivyotoa maoni yake kuhusu utaratibu wa kuwachukua wachezaji vijana katika kikosi chake, nimesikitika sana! Marsh ambaye pia alipata kumsaidia kocha aliyetangulia, Marcio Maximo, alikaririwa na gazeti moja akisema kwamba hawawezi kuendelea na mpango ule wa zamani wa Mbrazil huyo, aliyekuwa akiteua wachezaji kutoka timu ya taifa ya vijana wanne hadi watano kwa ajili ya kupata uzoefu katika kambi ya Stars.
Kocha huyu wa zamani wa Kagera Sugar na Azam, alisema wanachokifanya wao kama makocha wa timu ya taifa ni kuwachukua wachezaji wanaong'ara katika Ligi Kuu na kuwataka wachezaji vijana kujituma zaidi ili waonwe na kuitwa kwenye timu hiyo.
Kwa maneno haya, Marsh, mmoja wa makocha ninaowaheshimu sana uwezo wao, amenisikitisha mno, kwani maneno kama hayo, yalipaswa kusikika katika jukwaa la mashabiki ‘wajinga' katika uwanja wa taifa.
Lakini kutolewa na mtaalam kama Marsh, kuna dalili moja tu ya wazi mtu unayoweza kuiona kwamba kama taifa, bado hatuna maandalizi yoyote kwa ajili ya kutengeneza timu ya ushindani ya Taifa Stars.
Hii ni kwa sababu Marsh kama kocha wa timu ya taifa, anafahamu mikakati iliyoko pale TFF juu ya kuipeleka Tanzania katika fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwaka 2014 kule Brazil.
Kwa kusema hawana mpango huo kabisa, kwa sababu kulea wachezaji vijana katika timu ya taifa hakuko akilini mwao, ni wazi kwamba kitu kama hicho hakiko katika makabrasha yao.
Nilitegemea Marsh angekuja na kauli zinazoashiria kwamba wao kama makocha, wanao mpango A, B na C katika kuhakikisha wanatengeneza kikosi kizuri kwa ajili ya ushiriki wa fainali hizo.
Na hakuna mikakati yoyote inayoweza kufanywa katika soka la sasa, bila kuwashirikisha wachezaji vijana kwa nchi yetu, kutoka Ngorongoro Heroes au Serengeti Boys.
Kuna ishara moja tu ya wazi hapa, ni ndoto ya mchana kwa Stars, chini ya makocha hawa kuweza kufurukuta hata katika michuano ya Kombe la Dunia litakalofanyika Urusi mwaka 2018, achilia mbali Brazil miaka mitatu ijayo.
Hata kama tutakaa miaka 10 ijayo kabla ya michuano hiyo, sioni ni vipi Taifa Stars inaweza kuunda kikosi cha ushindani bila mipango ya makusudi ya kuwahusisha wachezaji vijana.
Hawa wachezaji wetu wa kuokoteza, kwa kutegemea kiwango cha mtu anachokionyesha katika mechi moja au mbili, hawawezi kutusaidia kama ambavyo hawajawahi kutusaidia kwa miaka yote kutokana na kukosa mipango ya vijana.
Ni kujidanganya kufikiri kuwa vijana watajitengeneza wenyewe katika timu za Ligi Kuu bila kuwepo na mipango ya makusudi ndani ya TFF kuhakikisha timu maalum ya vijana wenye vipaji inatayarishwa.
Hawa kina Asamoh Gyan tunaowaona leo wa Ghana, hawakufikia hapo walipo kwa bahati mbaya au kwa kubahatisha, isipokuwa ni mipango maalum iliyofanywa na chama cha soka cha Ghana katika kukuza vijana wake.
Ndiyo maana kwa nchi zile za Afrika Magharibi na Kaskazini, ni washiriki wa kawaida katika michuano ya Kombe la Dunia la vijana chini ya miaka 17 na 20.
Wanazo timu zao za kudumu zinazokaa pamoja kwa muda mrefu baada ya vipaji kugunduliwa, hawachukuliwi kwa kubahatisha kama tunavyofanya sisi.
Ndiyo maana, kama tunajaribu kuwa na mawazo tunayoweza kuyafanikisha kwa vitendo, basi ni muda muafaka sasa wa kuanza kuandaa wanasoka wetu kwa ajili ya kupata timu ya ushindani kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar mwaka 2022.
Kama tutaendelea na utaratibu wetu huu wa kuokoteza wachezaji bila kuwaandaa, basi tutaishia hapa hapa na hata hiyo Chalenji, ambayo imetupumbaza licha ya kuwa tulishinda kwa mipango hatutaweza kutamba.
Wale vijana waliopatikana katika michuano ya Copa Copa Coca-Cola, ambao kwa hakika wamejaaliwa vipaji, ndiyo hasa wa kutengenezwa.
Vijana wale walikwenda na kushiriki mashindano na vijana wenzao Brazil na Afrika Kusini na walifanya vizuri, kwa nini hatuwi na mipango ya makusudi kwa ajili ya kuendeleza vipaji vyao kwa manufaa ya taifa?
TFF itajidanganya kwamba haina fedha, lakini itakuwa inafanya kosa kubwa kwa sababu kuwalea vijana hawa hakuna gharama kubwa kama tunavyozipoteza fedha nyingi kwa mipango ya zimamoto.
Sidhani kama wadhamini wa timu ya taifa, wanaweza kushindwa kusaidia kuwalea vijana hawa, hasa kama wataelezwa lengo la mpango huo maridadi.
Uwezo pia wa kupatikana kwa wafadhili wengine ni mkubwa, kwa sababu kila shabiki wa kweli angependa kuona timu yetu inapata mafanikio na hayo siku zote hayaji kwa kubahatisha.
Hatuwezi kukubali kuendelea kuwa na shirikisho ambalo kazi yake kubwa ni kusimamia Ligi Kuu tu, tena ambayo ubora na ufanisi wake unashuka kiwango kila siku.
Timu ya taifa ni ya TFF, kwa hiyo inawajibika katika kuikusanya, kuilea na kuipeleka kwenye mashindano. Kama itaandaliwa vizuri, basi hata itakapokuwa inapanga viingilio vikubwa na kutangaza hasara itakuwa na haki, badala ya kufanya hivyo kwa timu inayokusanywa kwa zimamoto kwa wiki moja na kushiriki hovyo katika mashindano.
 
Usanii wa kutuletea timu feki

Mwandishi wetu

KAMA alipewa ushauri, basi rais wa RBP Oil Industry, Rahma Al Kharous, anapaswa kuwatimua kazi washauri wake, waliomshauri ailete timu inayodaiwa kuitwa Atletico Paraneanse kutoka Brazil, huku wakipanga kuwakamua Watanzania katika kiingilio.
Rahma aliutangazia umma wa wapenda soka nchini kwamba angeileta nchini timu ya Atletico Paranaense ya Brazil ambayo imewahi kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya soka nchini humo.
Alisema kuwa lengo kuu la kuileta timu hiyo nchini ni kutaka kukuza soka na pia kuwapa burudani wapenzi wa soka ambao wana kiu ya kuona soka la kitabuni, likitandazwa dimbani.
Waliimwagia sifa timu hiyo, wakidai imestawi mno kiuchumi pamoja na kuwa na mipango mizuri ya kuendeleza kwa kuwakuza chipukizi.
Timu hiyo ilipangiwa kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya vigogo vya soka hapa nchini, Yanga na Simba; na kwamba ilipaswa kuanza na Yanga Jumanne iliyopita na mechi ya pili ikawa dhidi ya Simba, Alhamisi iliyopita.
Viingilio vilivyotangazwa kwa ajili ya kuwashuhudia Wabrazil hao, viliwatisha kama sio kuwakatisha tamaa wapenzi wengi wa soka hapa nchini, kwani kiingilio cha chini kilikuwa sh 5,000, wakati cha juu (200,000) kwa mtu mmoja.
Ukubwa huo wa viingilio, ulitosha kabisa kuthibitisha kuwa nia ya Rahma na washirika wake haikuwa kuwapa burudani Watanzania, bali kujiingizia fedha.
Viingilio hivyo vya kima cha juu na vile vya kati, havikuwa na uwiano hata kidogo na uwezo halisi wa kifedha wa mashabiki wengi wanaoingia uwanjani kushuhudia mechi mbalimbali za soka hapa nchini.
sh 200,000 na 100,000 kwa VIP, ni viwango ambavyo havina uwiano wowote na kipato cha mashabiki wengi ambao asilimia kubwa mishahara yao ni ya kima cha chini ambayo haizidi sh 250,000, hivyo ni kitu kisichoingia akilini mtu alipe nusu au robo tatu ya mshahara wake wa mwezi, kwa ajili ya kwenda kushuhudia mechi moja.
Hilo lilithibitishwa na uchache wa mashabiki waliojitokeza katika mechi dhidi ya Yanga ambapo uwanja huo ulikuwa kama mtupu, sehemu kubwa ya waliohudhuria mechi waliketi katika viti vya sh 5,000 tena wa kuhesabu kwa macho tu.
Uchache huo wa mashabiki waliojitokeza katika mechi dhidi ya Yanga, ukawasuta na kuwafanya watangaze kufuta viingilio katika mechi dhidi ya Simba.
Kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji hao wa Brazil, katika mechi dhidi ya Yanga, kilikuwa cha chini mno licha ya kuishinda Yanga kwa mabao 3-2, jambo lililotufanya tuingie kwenye mtandao na kufuatilia ukweli kuhusu timu hiyo.
Hapo ndipo ilipobainika kasheshe ya hali ya juu iliyofanywa na waratibu wa safari ya timu hiyo, kwani ratiba ya Ligi Kuu Brazil ilionyesha kuwa timu hiyo, ilikuwa ikiendelea na mechi za Ligi Kuu nchini humo.
Ratiba iliyoonyesha kuwa wakati Atletico Feki ikitua nchini Atletico ya kweli ilikuwa na mechi dhidi ya Arapongas ambao walichapwa kwa mabao 2-1 na siku tuliyotangaziwa kuwa wangecheza na Simba, timu hiyo ilikuwa ikivaana na Corinthians.
Hata baada ya kubainika kwa ‘usanii' uliofanyika na waratibu hao walishindwa kujitokeza kufafanua juu ya jambo hilo, zaidi ya fununu kuibuka eti timu iliyoletwa ni ya kikosi cha pili cha Atletico ‘original' inayoendelea ligi huko kwao.
Swali ni je, kama ni kweli walikuwa wamekileta kikosi cha pili, kwa nini walifanya siri hadi wadau wa soka walipobaini hilo kupitia mitandao ya nje? Na swali jingine ni kwa nini hawakutaka kuitisha mkutano na waandishi na kufafanua madai hayo, kama walivyokuwa wakiinadi awali kabla haijatua hapa nchini?
Timu hiyo ilipomenyana na mabingwa wa soka nchini Simba, waliambulia sare, huku wakishindwa kabisa kuonyesha samba ambalo wengi walitamani kuliona likipigwa kwenye Dimba la Taifa.
Hali hii inanifanya nijiridhishe kuwa Rahma ama alipotoshwa ama naye alipanga kuwadanganya Watanzania ili ajipatie kipato kutokana na viingilio.
Ninajiuliza, kama kweli alikuwa ana lengo la kusaka mafanikio kwa nini azilenge Simba na Yanga pekee badala ya kuandaa walau mechi moja dhidi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes'.
Ninalishauri Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuwa macho na aina hii mpya ya ‘wasanii' wanaojitokeza sasa na kutaka kuwaibia wadau kupitia viingilio, wakitumia hadaa ya majina ya timu kubwa za nje kuandaa mechi bandia.
Hili lisipokomeshwa, tutakuja kushuhudia watu wakiwachukua wauza mitumba wa soko la Karume na kutuambia ni wachezaji kutoka Nigeria, Ghana au kwingineko na siku mashabiki watakaposema basi kudanganywa hapatakalika.
Ni bahati mbaya sana kwamba mchezo wa soka umebaki asilimia kubwa kiutendaji mikononi mwa TFF, laiti kama serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ingekuwa bado ina nguvu, naamini usanii huu ungekomeshwa mara moja.
Nimalize kwa kuwakumbusha waratibu hawa kuwa kwa stahili hii ya kutuletea timu feki hatutafika popote katika ndoto zetu za kupiga hatua, zileteni timu ambazo wachezaji na wadau wa soka kwa ujumla watajifunza na haina haja ya kujaza uongo.
 
Homa Sauti za Busara yapanda


na Abdallah Menssah, Zanzibar


HOMA ya Tamasha la Sauti za Busara linalofanyika kisiwani hapa kuanzia Februari 9-13, imepamba moto vilivyo kwa wapenzi pamoja na mashabiki mbalimbali wa burudani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi, mashabiki mbalimbali walisema wanalisubiri kwa hamu tamasha hilo ili kufaidi uhondo wa burudani kutoka katika makundi kadhaa mahiri Afrika.
"Ki ukweli tuna shauku ya hali ya juu na tamasha hilo, kwa sababu miaka yote linatoa msisimko wa hali ya juu kuliko matamasha mengine yanayofanyika hapa Zanzibar," alisema shabiki aliyejitambulisha kwa jina la Ally Jumaa.
Shabiki mwingine a Saida Abdallah alisema kwa upande wake anaamini tamasha la busara la mwaka huu litakuwa ni la aina yake zaidi kutokana na kukusanya makundi mengi zaidi.
Kwa hapa Tanzania, Tamasha la Sauti za Busara mwaka huu, litashirikisha pia bendi ya muziki wa dansi ya kama The African Stars ‘Twanga Pepeta' na mabingwa wa mipasho, Jahazi Modern Taarab ‘Wana Nakshi Nakshi'.
 
Wanyambo wampigia magoti Nchimbi


na Happiness Katabazi


WASANII wa vikundi vya ngoma za asili za kabila la Wanyambo wenyeji wa wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera wamemuomba Waziri wa Habari Utamaduni, Vijana na Michezo Emmanuel Nchimbi, kuwatafutia wafadhili ili waweze kuingia studio kurekodi nyimbo zao.
Hayo yalisemwa kwa nyakati tofauti na mkuu wa kikundi cha Makondelee Rwanyango, Salvatory Byarufu, kikundi cha Kihanga Isingiro, Sabinus Leopord, na mkuu wa kikundi cha ngoma sanaa cha Rumanyika Rwantale, Seta Mathias, wakati wakizungumza na waandishi wa habari katika kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam, ambapo jana tamasha hilo lilihitimishwa ambalo lilidumu kwa siku tatu.
Mathias alisema wanaamini Nchimbi kwa niaba ya serikali ya awamu nne, wizara yake imebeba jukumu la kuulinda na kuusimamia utamaduni wa makabila ya Tanzania hivyo wanaamini kilio chao atakisikia na kukifanyia kazi kwa karibu.
Alisema Wanyambo kila kukicha wamekuwa wakilalamika kuwa wanabaguliwa na kunyanyaswa na maofisa uhamiaji kwa sababu kabila hilo limekuwa halitambuliwi na watu wengi na kuongeza kuwa makabila mengine yamekuwa yakitambuliwa kwa urahisi kutokana na makabila hayo kuuinua utamaduni wa makabila yao ikiwemo vikundi vya ngoma.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Wanyambo, Danile Rutasyamuka, aliishukuru serikali kupitia Idara ya Makumbusho ya Taifa kuwaruhusu kufanya tamasha hilo pia aliwashukuru Wanyambo wote waishio jijini Dar es Salaam na wananchi wa makabila mbalimbali na raia wa kigeni waliojitokeza kuhudhuria tamasha hilo.
Katika hatua nyingine Wanyambo wamemwagia sifa Mkuu wa Wilaya yao, Kanali mstaafu, Fabian Masawe, kwamba ni kiongozi wa kuigwa ambaye anafuatilia kwa karibu matatizo ya wananchi wake.
Walipendekeza kwamba Masawe aendelee kuwa mkuu wao wa wilaya, asihame kwa sababu amekuwa na umuhimu mkubwa kwao, tamasha hilo lilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mohamed Babu.
 
Zanzibar kuwaombea Gurumo, Mzee Yusufu


na Mwandishi wetu


MASHABIKI mbalimbali wa burudani kisiwani hapa wamewaombea nafuu mwimbaji wa Msondo Ngoma Music Band, Muhidin Maalim Gurumo, na mfalme wa mipasho wa kundi la Jahazi Modern Taarab, Mzee Yussuf.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi kisiwani hapa jana, mashabiki hao walisema wamefikia hatua hiyo ya kuwaombea nafuu, baada ya kuona kuna kundi limejitokeza ambalo linaeneza uvumi wa kuwa nguli hao wamefariki.
Walisema ni vema kwa wapenzi na mashabiki wa burudani na hata wale wasio mashabiki wa kuwaombea salama wasanii hao badala ya kuwazushia mabaya kwa kuwa ni binadamu wenzao.
"Unajua, hawa ni wanadamu wenzetu, zaidi ya hilo, ni watu ambao hutumia akili na maarifa yao mengi kutuburudisha, hivyo ni vema kuwaombea kheri kila pale wanapopata madhila," alisema shabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Yunus Amir.
Naye shabiki mwingine aliyefahamika kwa jina la Juma Idd alisema kuwa nafuu ya wasanii hao ni faraja kwa jamii kutokana na kuwa wanaelimisha rika na tabaka la watu mbalimbali kupitia tungo zao.
 
Mzee Yusuf: Jamani sijafa


na Abdallah Menssah, Zanzibar


MFALME wa mipasho na mkurugenzi wa mabingwa wa mipasho, Jahazi Modern Taarab, ameibuka na kukanusha habari kuwa amefariki kama ambayo zimekuwa zikizushwa hivi karibuni na kuwa hali yake inaendelea vema.
Uvumi huo ulioanza kuenea kwa kasi kuanzia juzi majira ya jioni, umeonekana kuwashtua na kuwaathiri mashabiki, wasanii na wadau wengi, huku mkongwe wa Taarab Asilia, Fatuma binti Baraka ‘Bi Kidude' akiwa miongoni mwao.
Akizungumza kisiwani hapa jana, Yussuf alisema kuwa hivi sasa anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa operesheni ya goti la kulia katika Hospitali ya Bulele, Kibaha Pwani, hivi karibuni na kuruhusiwa kurudi nyumbani.
"Niliporuhusiwa niliamua kuja kujituliza huku nyumbani nikiwa na wazee wangu nikingoja kupata nafuu zaidi, wanaoeneza uvumi wa kuwa nimekufa sina budi nao na waanze tu kunikusanyia michango," alisema Yussuf.
Aidha, Yussuf anawaomba mashabiki na wapenzi wake wasiwe na wasiwasi kwani maendeleo yake si mabaya, ambapo amewataka kutulia katika kipindi hiki kigumu atakachokuwa haonekani jukwaani.
Kwa sasa, Yussuf, mahiri kwa utunzi, uimbaji na upapasaji kinanda, ambaye ameshaanza kutembea mwenyewe akisaidiwa na magongo maalum, yuko mapumzikoni Michenzani, Zanzibar, Nyumba namba 2, ghorofa ya 3 na
ngazi namba 4.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…