Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Mgosi aipeleka Simba kileleni
Sunday, 06 February 2011 21:30


Oliver Albert
MSHAMBULIAJI Mussa Hassan Mgosi aliiongoza Simba kurudi kileleni mwa ligi kwa kufunga mabao mawili na kuiwezesha timu yake kushinda 2-0 dhidi ya wachezaji 10 wa Polisi Tanzania, huku kipa Juma Kaseja akiwa golini kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Mgosi alifunga bao la kwanza katika ya dakika 53, kipindi cha pili kwa mpira wa adhabu wa umbali wa mita 35, baada ya Mbwana Samata kuangushwa.Mgosi alipiga faulo hiyo na mpira ulikwenda moja kwa moja wavuni na kumwacha kipa Said Kombo asijue la kufanya.

Awali katika dakika ya 44, pia Mgosi alifunga bao kwa mpira wa adhabu aliopiga nje ya eneo la 18 baada ya kuangushwa kwa Nyagawa, lakini mwamuzi Alex Mahagi kutoka Mwanza alilikataa kwa kusema mfungaji alishindwa kufuata kanuni za upigaji wa mpira huo ambao ulitakiwa uguswe na watu wawili kwanza jambo ambalo Mgosi hakufanya na timu hizo kwenda mapumziko kwa suluhu.

Katika kipindi cha pili mshambuliaji Mussa Mgosi alifunga bao la pili katika dakika ya 84, akiunganisha vizuri kwa kichwa krosi ya Haruna Shamte kutoka upande wa kulia na kufikisha mabao sita katika msimu huu.

Kwa matokeo hayo Simba imerudi kileleni baada ya kufikisha pointi 33 ikiwa na pointi moja zaidi ya Yanga iliyo na michezo zaidi ikiwa nafasi ya pili na pointi 32.

Polisi walipata pigo katika dakika ya 63, baada ya mshambuliaji wao Semsue Juma kutolewa nje kwa kadi mbili za njano baada ya kuwachezea vibaya Amir Maftah na Kaseja katika wakati tofauti.

Katika mechi hiyo mshanbuliaji wa Simba,Mbwana Samata alipoteza nafasi za kufunga kwa kushindwa kuunganisha mpira wa kona dakika ya 60 na 71 akiwa yeye na kipa.

Baada ya kukaa benchi mechi mbili mfululizo kipa Kaseja jana alipewa nafasi ya kujirekebisha mbele ya kocha wake Mzambia Patrick Phiri.

Mchezo huo ulianza taratibu huku timu zote zikijaribu kuangalia mapungufu ya mwenzake, lakini Simba walionekana kupwaya zaidi kwenye kiungo ikiwa na Jerry Santo, Ochan Patrick na mkongwe Nico Nyagawa.

Udhaifu huo wa kiungo wa mabingwa hao ulitoa nafasi kwa wenyeji Polisi TZ kujipanga na kufanya mashambulizi katika kipindi hicho cha mwanzo mbele ya mashabiki wao.

Kasi hiyo ya mashambulizi ilimfanya kipa Kaseja kufanya kazi ya ziada katika dakika ya 17, ambapo alipangua vizuri shuti la Ally Khalid lililomfanya aumie mkono baada ya kujigonga kwenye mwamba na mpira kusimama kidogo ili apewe matibabu.

Awali mshambuliaji chipukizi Mbwana Samata alipiga shuti la mbali dakika 14 na kutoka nje kabla ya Ochan kupoteza nafasi ya wazi akiwa yeye na kipa Said Kombo kwenye dakika ya 18.

Katika mchezo huo Simba ilimpumzisha Nyagawa na kumuingiza Shija Mkina wakati Polisi wao walimtoa Deltha Thomas na kumwingiza Bantu Admin.

VIKOSI
Polisi Tanzania:
Said Kombo, Nahoja Haji, Elias Mafutaa, Noel Msakwa, Salmin Kiss, Ismail Nkulo, Sihaba Mkude, Khalid Ally, Semsue Juma, Seif Mohamed na Deltha Thomas.

Simba
Juma Kaseja, Haruna Shamte, Amir Maftah, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, Jerry Santo, Nico Nyagawa, Patrick Ochan, Mussa Mgosi, Mbwana Samata na Amri Kiemba.
 
Beki wa Yanga, Taifa Stars apata upofu Send to a friend
Sunday, 06 February 2011 21:27
0
digg

Sweetbert Lukonge
MCHEZAJI wa zamani wa timu ya soka ya Yanga, Majimaji ya Songea pamoja na Taifa Stars, Allan Shomari kwa sasa amepofuka macho na amewaomba wadau mbalimbali pamoja na wapenzi wa soka nchini kumsaidia ili aweze kukabiliana na changamoto za maisha ambazo anakumbana nazo kwa sasa.

Shomari ni miongoni wa wachezaji nyota waliowahi kutamba hapa nchini na amepoteza uwezo wake wa kuona tangu mwaka 2006, ambapo siku moja akiwa amelala aliota analishwa nyama na mtu asiyemfahamu na mara tu alipozinduka kutoka usingizini hakuweza tena kuona hadi leo hii.

Akizungumza na Mwananchi hivi karibuni nyumbani kwake katika kijiji cha Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha, Shomari alisema tangu akumbwe na tatizo hilo amekuwa na wakati mgumu kimaisha jambo linalomfanya apoteze matumaini ya kuishi kila anaposikia matatizo yanayoikumba familia yake.

"Tangu nipate matatizo haya ya kutoona kwa hakika nimepoteza kabisa matumani ya kuishi kwa sababu familia yangu kwa sasa inateseka na sijui ni nani atakayenisaidia ili iweze kuepukana na matatizo haya,"alisema Shomari.

Alisema,"Hapo awali wakati nilipokuwa mzima nilikuwa nikijishughulisha huku na kule ambapo familia yangu ilishi kwa amani huku watoto wangu wangu wakisoma bila ya wasiwasi, chakula pia kilikuwa hakiishi ndani ya nyumba,lakini kwa sasa kila kitu ni kitendawili hawajui tena nini hatima ya maisha yao ya baadaye."

"Watoto wangu wawili wameshindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya kukosa ada, mahitaji nyumbani pia yamekuwa ni mtihani jambo ambalo kwa hakika linaniumiza kichwa kila kukicha bila ya kupata majibu ukizingatia sijui nitapona lini zaidi ya kumwomba Mungu," alisema Shomari ambaye ana watoto watano huku akibubujikwa na machozi ndani ya upofu.

Alisema endapo kama angepata mtu wa kumsaidia, angependa kusaidiwa kwa kuwasomesha watoto wake watatu ambao mmoja alishindwa kuendelea na kozi yake ya uhazili, pamoja na wengine wawili ambao mmoja yupo kidato cha pili na mwingine darasa la sita.

Mbali na hilo pia anawaomba watanzania kumsaidia kulipa deni la mifuko 56 ya saruji ambalo linamkabiri ili nyumba anayoishi kwa sasa iweze kuwa ya kwake.

Nyumba anayoishi Shomari ni moja kati ya nyumba zilizojengwa na kanisa la KKKT mjini Arusha kwa lengo la kuwauzia wanawake wajane na wale ambao wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ambapo mke wa Shomari, ni mmoja kati ya wale waliofanikiwa kupata nyumba hizo zinazojengwa na kanisa la KKKT na kutakiwa kulipa mifuko 164 ya saruji ili amilikishwe nyumba hiyo kwa kipindi cha miaka mitano na mpaka sasa amebakisha mifuko 60.

Mbali na hilo pia Shomari anahitaji msaada wa kumuwezesha kupata fedha zake za NSSF kutoka kwa kampuni ya mabasi ya Mtei ambayo alikuwa akiitumikia kama dereva kabla ya kukumbwa na tatizo hilo.

Alisema amekuwa akijitahidi kadri ya uwezo wake wote kuhakikisha anapata malipo yake ya NSSF, lakini tajiri wa magari hayo amekuwa akimzungusha kumwandikia barua ambayo itamsaidia kupata fedha hizo ili aweze kukabiliana na matizo mbalimbali yanayomkabiri ikiwa ni pamoja na kupata matibabu.

Hata hivyo, uongozi wa Chama cha Wachezaji wa Soka Tanzania (Sputanza) baada ya kuulizwa kama unamsaidia mchezaji huyo ulisema kutokana na chama hicho kutokuwa na fedha za kumsaidia uliandaa utaratibu wa kuandika barua na kuzisambaza kwa wadau mbalimbali kwa lengo la kumsaidia.

Moja ya nakala za barua hizo ilikuwa ikisema kuwa, Bwana Allan Shomary ni mchezaji wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ambaye kwa sasa amepata ulemavu wa macho.

Kwa kuthamini mchango wake wa soka hapa nchini na kwa kutambua nafasi yako katika duru la michezo, Sputanza inakuomba tumchangie mwenzetu huyu kwa hali na mali ili familia yake ipate kujikwamua na hali ngumu inayomkabili kwa kuchangia kiasi chochote ulichonacho kupitia akaunti yake katika benki ya Stanbic A/c 0140609683801 au kupitia M Pesa namba 0763 617100.

Wachezaji mbalimbali wa zamani wamekuwa wakisumbuliwa na maradhi kiasi cha kuhitaji misaada ya wahisani. Mwingine aliyewahi kuibuliwa na gazeti hili ni Jellah Mtagwa.
 
Alia uhaba wa vifaa'
Sunday, 06 February 2011 21:24


Imani Makongoro
KOCHA wa timu ya taifa ya Riadha Tanzania, Endrow Baro, amesema tatizo la vifaa vya michezo linakwamisha wanariadha wa Tanzania kujifunza kwa umakini na hatimaye kufanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa.

Kocha huyo Mcuba anayelipwa na serikali yupo mkoani Arusha kwa ajili ya kuwanoa wanariadha wa Tanzania wanaojiandaa na Michezo ya Afrika itakayofanyika Septemba mwaka huu nchini Msumbiji na yale ya Olimpiki yatakayofanyika mwakani jijini London, Uingereza.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutoka Arusha, Baro alisema kuwa, "Najua tunakabiliwa na mashindano makubwa ya Afrika ambayo katika historia mara ya mwisho tulipata medali moja ya Martin Sulle.

"Nimetoka Dar es Salaam kuja Arusha kwa ajili ya kuwanoa wanariadha wengi wanaishi huku, kitu kinachokwamisha mazoezi yetu ni vifaa.

"Mchezo wa Riadha si kukimbia tu, kuna Miruko, Mitupo, Viunzi, Kutupa tufe, Kisahani, Kuruka Juu, Chini na mingine mingi, lakini tatizo linalotukabili ni kutokuwa na vifaa, tutafika kweli kama tutafanya mazoezi bila vifaa?," alihoji kocha huyo.

"Naamini suala la vifaa likipewa kipaumbele na wanariadha kujifunza michezo yote ya riadha, uhakika wa kupata medali katika michezo ya miruko na mitupo utakuwa mkubwa tofauti na sasa tunapotegemea kukimbia tu," alisema kocha.

Suala la vifaa limekuwa tatizo kwa wachezaji wa Tanzania hasa wa michezo ya Riadha, Ngumi, Kuogelea na Paralimpiki mbali na kocha huyo kulalamikia vifaa pia kocha wa ngumi Pimentel Hurtado aliwahi kulalamika kuhusu vifaa vya mazoezi kwa mabondia.

Ingawa kilio chao kimekuwa kikiishia hewani huku tukisubiri wachezaji wafanye vibaya kimataifa na kuwaita wasindikizaji tumeshindwa kuwasaidia kuanza maandalizi mapema na kuwapa vifaa bora.
 
Palestine yatua
Sunday, 06 February 2011 21:23


Sweetbert Lukonge

TIMU ya soka ya Palestine imewasili nchini jana tayari kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya Taifa Stars ambao utafanyika Jumatano jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Timu ya Palestine inaundwa na baadhi ya wachezaji wanaocheza soka la kulipwa katika nchi mbalimbali barani Asia na Ulaya na hii ni mara yeke ya kwanza kucheza soka Barani Afrika.

Akizungumza na Mwananchi jana Balozi wa Palestine nchini, Navi Abu Jeish alisema suala la Tanzania kukubali kucheza na Palestine mechi ya kirafiki ni heshima kubwa ambayo itaendeleza kudumisha uhusiano muzuri wa kihistoria uliopo baina ya nchi hizo mbili.

Alisema timu yao imekuwa ikishindwa kucheza mechi mmbalimbali za kirafiki kutokana na hali mbaya ya kisiasa iliyopo kati yao na Israel jambo ambalo limesababisha kuwa chini zaidi katika viwango vya soka vya Duniani.

"Tunaishukuru Tanzania kwa kutukubalia kucheza nao hivyo hali hii ni moja ya heshima kubwa kwetu ambayo kwa namna moja ama nyingine itasaidia kuimarisha historia nzuri iliyopo kati yetu na wananchi wa Tanzania.

"Kwa hakika tumekuwa tukipata wakati mugumu sana kupata mechi za kirafiki hii ni kutokana na hali ya kisiasa iliyopo nchini kwetu hivyo kupata mechi hii ni moja ya mafanikio makubwa na tunaishukuru Tanzania kwa hilo," alisema Jeish.

Katika hatua nyingine Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewata Watanzania kuendelea kuiunga mkono Taifa Stars na kutambua kuwa mechi hiyo ya jumatano in amuhimu zaidi kwa timu hiyo.

Alisema kutokana kutambua mchango wa wapenzi wa soka nchini viingilio vya mechi hiyo vitakuwa vya chini na ambavyo vitamwezesha kila momja kuangalia mchezo huo ambao utaandika historia mpya ya soka Duniani.
 
Yanga wavunja viti,mlango Songea

Sunday, 06 February 2011 21:22


Sosthenes Nyoni, Songea

WACHEZAJI na viongozi wa Yanga wamedaiwa kuharibu viti 12 vya plastiki na mlango mmoja wakati wa pambano kati ya Yanga dhidi ya Majimaji lililofanyika mwishoni mwa wiki mjini Songea.

Viti vinavyodaiwa kuvunjwa na wachezaji hao pamoja na viongozi wa Yanga ni vile vilivyoko katika chumba maalumu ambacho timu ngeni hususani wachezaji hutumia kubadilishia nguo.

Tukio hilo ambalo linadaiwa kufanywa na wachezaji hao baada ya mpambano huo linahusishwa na hasira zinazotokana na matokeo ya suluhu waliyoipata katika mechi hiyo.

Akizungumza na Mwananchi wakati akimwonyesha mwandishi wa habari hii uharibifu huo, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Ruvuma (FARU),Ajaba Chitete alisema kitendo kilichofanywa na wachezaji na viongozi hao ni kitendo cha aibu ukizingatia Yanga ni klabu kubwa na kongwe nchini.

"Hii ni aibu timu kubwa kama Yanga inafanya kitendo cha fedheha na hii ni mara ya pili mwandishi wanafanya hivi hata mwaka jana walileta fujo sana,"alisema Chitete.

"Hiki ni chumba chao tulichowaandalia, wao huwa kinatumika na timu ngeni,hakuna mwingine aliyefanya hivi zaidi yao, wamebomoa hadi mlango wa kule mbele kwa kushirikiana na mashabiki wao,"alisema Chitete.

Alisema wachezaji na viongozi wa Yanga walitakiwa kuwa wastaarabu hata kama walikosa ushindi katika mechi hiyo kwani hata wenyeji wao walihitaji kitu hicho, lakini hawakufanikiwa.

Chitete alisema kuwa anaamini Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) litashughulikia suala hilo kwa umakini ili kukomesha vitendo vya aina hiyo visiweze kujirudia tena.

Mwananchi lilimtafuta mwenyekiti wa Yanga Lloyd Nchunga ili aweze kujibu tuhuma dhidi ya wachezaji wake, lakini muda wote simu yake iliita pasipo mafanikio.
 
Ligi ya Dodoma inaanza leo
Sunday, 06 February 2011 21:21


Oliver Albert, Dodoma
LIGI ya soka mkoa wa Dodoma inaanza leo Jumatatu kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma kwa timu ya Vijana Mundemo kukipiga na Majengo wakati KFC wataonyeshana kazi na Kasi Mpya.

Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Dodoma (Dorefa),Nassor Kipenzi aliiambia Mwananchi kuwa ligi hiyo itashirikisha timu 14 za mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kupata timu moja itakayouwakilisha mkoa huo katika ligi ya Taifa.

''Tunaamini ligi itakuwa nzuri na timu zitaleta ushindani mkubwa ili kumpata bingwa mmoja halali wa uhakika atakayeuwakilisha mkoa wetu katika ligi ya Taifa,'' alisema Kipenzi.

Alisema ligi hiyo itachezwa katika vituo viwili kukiwa na makundi mawili ya timu na kituo cha kwanza ambacho kitakuwa na timu saba mechi zake zitachezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri na kituo kingine kitakuwa Kondoa.

''Kila kundi litatoa timu 3 ambazo zitacheza fainali zitakazofanyika Mpwapwa na mshindi mmoja tu atapatikana kwa ajili ya kuuwakilisha mkoa kwenye ligi ya Taifa,'' alisema.

Alizitaja timu hizo kuwa ni Majengo, KFC,Vijana Mundemo, Kasi Mpya, Sinza Stars, Aluta na Hazina ya Mpwapwa ambazo zitatumia uwanja wa Jamhuri wakati timu za Mnadani, City Center, Gunners, Mji Mpwapwa, Kongwa, Nyomi FC na Vijana Chamwino zitatumia uwanja wa Kondoa.

Alisema Dorefa imepanga mikakati ya kusimamia ligi hiyo vizuri na kuwataka waamuzi kuchezesha kwa haki ili mshindi apatikane kihalali kwa lengo la kuuwakilisha mkoa vizuri katika ligi ya Taifa.

'' Lengo letu kubwa ni kuhakikisha mkoa wetu unapata timu nyingine ya pili kwenye ligi kuu badaala ya Polisi Dodoma pekee, tunaanza na mkoa na tutakuja taifa na daraja la kwanza na baadae ligi kuu, tunapanga mikakati kuhakikisha malengo yetu ya kupata timu nyingine ligi kuu yanafanikiwa,'' alisema Kipenzi.

Wakati huo huo timu ya KFC imeibuka bingwa wa michuano ya kombe la Chama cha Mapinduzi (CCM ) baada ya kuifunga Kongwa FC kwa penati 6 -5 baada ya timu hizo kwenda suluhu hadi dakika za mwisho.

KFC ilikabidhiwa kombe, seti ya jezi,mpira na Sh 100,000 na raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete juzi wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya chama hicho yaliyofanyika mkoani Dodoma.
 
Messi apiga tatu, Barca yaweka rekodi mpya
Sunday, 06 February 2011 21:20

MADRID, Hispania
KLABU ya Barcelona imetegeneza rekodi mpya kwenye La Liga kwa kushinda mechi 16, na kuvunja rekodi iliyowekwa na Real Madrid miaka 50 iliyopita shukrani kwa Lionel Messi aliyefunga mabao tatu pekee waliposhinda 3-0 dhidi ya Atletico Madrid.

Timu hiyo ya Pep Guardiola hadi sasa imeshafunga mabao 60 na kuruhusu mabao sita tangu walipoanza kushindi wakiwa nyumbani dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Nou Camp pale Oktoba 16 mwaka jana.

Mechi hizo 16 walizoshinda ni pamoja na ile ya ushindi wa 5-0 dhidi ya mahasimu wao Real na wakawasambaratisha Almeria 8-0, kabla ya kuwachakaza 5-1 ndugu zao wa Espanyol.

Klabu hiyo ya Catalan sasa wamefikia rekodi iliyowekwa na Real wakati huo ikiwa na Alfredo Di Stefano, ambaye anatambuliki kuwa moja ya nyota bora zaidi aliyeisaidia timu hiyo kutwaa mataji matano ya kwanza ya Ulaya kuanzia mwaka 1956 na 1960.

Ni heshima ya pekee kwa timu hii kuweza kufikia rekodi hiyo na kuivunja baada ya muda mrefu kwa sababu ilikuwa ni vigumu kufikia hapo,î alisema mchezaji bora wa dunia Messi.

Kiwango cha juu alichokionyesha nyota huyo wa Argentina dhidi ya Atletico ikimefanya ampiku Cristiano Ronaldo kwa ufungaji na kufikisha mabao 24, kwa mshangao kocha Quique Sanchez Flores alimfananisha Messi na Di Stefano.

Jambo lililonishangaza mimi ni kuhusu Messi usiku huu na si magoli, lakini amekuwa akikaa nyuma na kuonyesha uwezo wake mkubwa wa kucheza na mpira,î Sanchez Flores alisema kwenye mkutano wa vyombo vya habari.

Ni wazi, kwa sasa tunazungumzia Di Stefano wa karne ya 21. Ni kama uchizi hivi.î

Guardiola alisema ni jambo la faraja kusikia Messi anafananishwa na mtu mwenye miaka 84, Di Stefano, ambaye amepewa tuzo ya heshima kubwa na Real tangu mwaka 2000.

Timu zote bora kwenye historia kunakuwa na mchezaji wenye utofauti,î alisema.

Di Stefano alikuwa wa pekee na ndivyo alivyokuwa Messi kwety,î aliongeza kiungo huyo wa zamani wa Barca na Hispania.

Tunaweza kucheza vizuri bila ya Messi, lakini isingekuwa rahisi kushinda mechi 16 mfululizo.

Kwa ujumla nawapongeza wachezaji wote kwa kucheza vizuri na kufanikiwa kupata ushindi wa aina hii si jambo rahisi.

Sifikiri kama tutaweza kuifikia rekodi ya kutwaa mataji matano mfululizo ya Ulaya, lakini tumeweza kufikia hii kwanza.

Rekodi wakati wote zinavunjwa sina shaka kwamba ipo siku itafikiwa na kuvunjwa pia,î aliongeza.
 
Simba yaidungua Polisi
*Yaitimulia vumbi Yanga FC

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba jana waliifunga Polisi Dodoma mabao 2-0 katika mchezo wa
ligi hiyo katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Jamhuri mjini hapa na kuishusha Yanga Kileleni.

Simba sasa inaongoza ligi hiyo kwa kufikisha pointi 33 na kuiacha Yanga ikiwa na pointi 32.

Katika mechi ya jana timu zote ziliunza mpira kwa kasi huku zikishambuliana kwa zamu ambapo lakini hata hivyo washambuliaji wa pande zote hawakuwa makini katika ufungaji.

Patrick Ochan alikosa bao dakika ya pili baada ya kubaki na kipa ambaye alipiga shuti lililomlenga kipa wa Polisi.

Polisi nayo walijibu shambulizi hilo baada ya kuliandama lango la Simba, lakini hata hivyo kipa Juma Kaseja alikaa imara kupangia mashuti yaliyoelekezwa mshambuliaji Juma Semsue.

Dakika ya 42 Mussa Hassan 'Mgosi', alifunga bao kwa shuti kali lakini hata hivyo, mwamuzi alilikataa kwa madai kuwa kabla ya kufunga alikuwa ameotea.

Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kuingia na uchu wa kupata mabao na dakika ya 53, Mgosi alifunga bao hilo kwa mkwaju wa adhabu iliyotolewa na mwamuzi baada ya mabeki wa Polisi kumwangusha Mbwana Samatta wakati akielekea langoni.

Katika kipindi hicho Simba ilimtoa Nico Nyagawa na kumwingiza Shija Mkina, wakati Polisi iliwatoa Detha na Sihaba Mathias, wakaingia Admin Bantu na Pascal Maige.

Polisi ilipata pengo katika kipindi hicho baada ya mshambuliaji wake tegemeo, Semsue kutolewa nje kwa kadi nyekundu na mwamuzi Alex Mahagi baada ya kumkwatua Juma Maftah, wakati awali alikuwa na kadi ya njano.

Simba iliongeza bao lake la pili dakika ya 84, lililofungwa na Mgosi kwa mpira wa kichwa baada ya kuunganisha krosi ya Haruna Shamte.
 
Kocha Minziro alia na mwamuzi
Na Zahoro Mlanzi

BAADA ya kulazimishwa suluhu na timu ya Majimaji ya Songea, Kocha Msaidizi wa Yanga, Fredy Felix 'Minziro' amemjia juu mwamuzi
Ibrahim Kidiwa, kwamba ndiye aliyeidhoofisha timu yake mpaka ipate matokeo hayo.

Timu hizo zilikutana juzi kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea katika mfululizo wa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, kwenye mchezo uliomaliza kwa mashabiki wa Yanga kumvamia mwamuzi, wakidai hakuitendea haki timu yao.

Akizungumza kwa simu mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Minziro alisema Kidiwa, amewafanyia mambo ya ajabu kwa kufanya maamuzi yasiyostahili juu yao.

"Alafu utasikia watu wanasema Simba na Yanga zinabebwa kwa uamuzi kama huu alioufanya Kidiwa, hizi timu zinabebwa vipi, dakika za mwisho mchezaji wangu amekatuliwa kwa nyuma lakini, faulo ikaamuliwa ipigwe kwetu badala ya kwa Majimaji," alilalamika Minziro.

Alisema baada ya uamuzi huo, mashabiki wa Yanga walishindwa kuzuia hasira zao na kuamua kuingia uwanjani wakiwa na nia ya kumfuata, Kidiwa kumwelezea hisia zao juu ya alichokifanya.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali kutoka mjini humo, inadaiwa mara baada ya kupyenga cha mwisho kupulizwa, mashabiki wa Yanga kwa jina maarufu Yanga Bomba, walivamia uwanja kwa nia ya kumpiga mwamuzi.

Jeshi la Polisi lililokuwepo uwanjani hapo ilibidi lifanye kazi ya ziada kuwaondoa uwanjani, waamuzi waliochezesha mchezo huo na kufanikiwa kuwatoa uwanjani.
 
Serikali kuandaa kongamano la michezo
Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imeandaa kongamano la michezo, litakalowakutanisha wadau mbalimbali wa michezo nchini.
Akizungumza Dar es Salaam juzi, Mwenyekiti wa
Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Idd Kipingu alisema kongamano hilo litangazwa hivi karibuni lengo likiwa ni kuviweka vyama vya michezo karibu.

"Kongamano hili tulipanga tulifanye tangu mwaka juzi, lakini hata mwaka jana ilishindikana ila kwa mwaka huu kama serikali tumejipanga kuhakikisha tunalifanya, ili kuwakutanisha wadau pamoja kupeana mawazo ya nini tufanye ili michezo yetu ipige hatua," alisema Kipingu.

Alisema hiyo itakuwa ni rahisi kwa kila wadau kutoa mawazo yao, ikiwa ni pamoja na kujua nini kifanyike ili wadau hao waweze kuwekeza udhamini wao kwenye michezo ambayo mingi imekuwa ikikosa udhamini.

Kipingu alisema bado mchakato wa matayarisho ya kongamano hilo yanaendelea na kwamba tarehe na wapi kongongamano hilo litafanyika, watatangaza baadaye ili wadau wote waweze kujipanga.
 
Manchester yapata kipigo cha kwanza
LONDON, Uingereza

MENDE ameangusha kabati! Hivyo ndivyo unavyoweza kuelezea kuhusu kufungwa kwa vinara wa Ligi Kuu England, Manchester United ilipocheza na timu ya
mwisho kwenye msimamo, Wolves.

Mwiko wa Manchester United, kutofungwa katika Ligi Kuu msimu huu hatimaye ulivunjwa na timu ya Wolves, baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 wakiwa ugenini katika Uwanja wa Molineux.

Wenyeji walilazimika kutoka nyuma kwa kukumboa bao waliloanza kufungwa na United katika dakika ya tatu, kupitia kwa Luis Nani.

Wolves inayonolewa na kocha, Mick McCarthy imeweza pia kuvunja rekodi ya Manchaster united ya kutofungwa mechi 30 katika Uwanja wa Molineux.

Baada ya kutagulia kufungwa, Wolves ambayo ni ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, ilikuja juu na kusawazisha kupitia kwa George Elokobi, dakika ya 10 kabla ya Kevin Doyle kufunga goli la ushindi dakika ya 40.

United ilianza kupata pigo mapema baada ya Rio Ferdinand, kuumia wakati wa maandalizi ya mechi.Jonny Evans, alichukua nafasi ya mchezaji huyo na kucheza sambamba na Nemanja Vidic.

Kuumia kwake hakukuonekana kuathiri timu ya Mashetani hao Wekundu baada ya Nani, kufunga bao la kuongoza mwanzoni mwa mchezo.

Elokobi aliiletea furaha Wolves kwa kufunga goli kwa kichwa baada ya kupata mpira kutoka kwa Matt Jarvis.

United ilionekana kuchachamaa kutaka kurejesha goli, ambapo washambuliaji Ryan Giggs na Berbatov walionekana kuwa tishio.

United ilifungwa bao la ushindi kutokana na makosa ya Evans na kufanya Doyle, akwamishe mpira wavuni.

Nenad Milijas naye nusura afunge goli baada ya kuchezewa faulo na Rafael.

Baada ya mapumziko huku United ikiwa nyuma kwa kufungwa mabao 2-1, United ilikuja juu na kipa wa Wolves Wayne Hennessey aliokoa mpira wa krosi wa Nani.

Wolves ilikuwa imara kuokoa mipira iliyokuwa ikipigwa na Rooney, Giggs na Berbatov.

Javier Hernandez alimpasia mpira mzuri
Berbatov, lakini alishindwa kufungwa.

Kipa wa United Van der Sar katika dakika ya 74 alifanya kazi ya ziada kookoa goli kwa mpira uliopigwa langoni mwake.

Dakika ya 85, United ililalamika kwa kunyimwa penalti baadaya, Evra kupiga mpira na Karl Henry aliunawa kwenye eneo la hatari.

Kwa matokeo hayo United, imeendelea kuwa kileleni ikiwa na pointi 54 baada ya kucheza mechi 25 ikifuatiwa na Arsenal, yenye pointi 50 ambayo nayo ilitoka sare ya mabao 4-4 dhidi ya Newcastle United.

Manchaster City ambayo ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi West Bromwich, yote yakiwekwa kimiani na Carlos Teves iko katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 49.
 
Carragher backing for Torres

29 comments »
Updated Feb 6, 2011 5:38 PM ET
Liverpool defender Jamie Carragher has backed Fernando Torres to be a success for Chelsea after spoiling the Spain striker's Blues debut.

Carragher has helped the Merseysiders triumph 1-0 at Stamford Bridge.


BARCLAY'S PREMIER LEAGUE
Sat., Feb. 5
Stoke City 3-2 Sunderland | Recap
Aston Villa 2-2 Fulham | Recap
Everton 5-3 Blackpool | Recap
Man City 3-0 West Brom | Recap
Newcastle 4-4 Arsenal | Recap
Tottenham 2-1 Bolton | Recap
Wigan 4-3 Blackburn | Recap
Wolves 2-1 Man United | Recap
Sun., Feb. 6
West Ham 0-1 Birmingham | Recap
Chelsea 0-1 Liverpool | Recap
BPL Scores | Table | Fixtures
Raul Meireles hooked home from close range after 68 minutes to secure three points for Kenny Dalglish's visitors - moments after Torres had been replaced by Salomon Kalou.

Carragher told Sky Sports 1: "Good players come and go.

"We've played against plenty of players (who have left)... we used to play against Robbie Fowler when he went to Leeds... it's not easy. You know the quality.

"Fernando is one of the best strikers in the world and I'm sure he'll prove that for Chelsea but he's not with us now. We've got to focus on our own team, do our own jobs and that's what we did."

The win saw the Reds move up to sixth in the Premier League standings as the club continue their recovery under caretaker boss Dalglish following the departure of Roy Hodgson.

Carragher admitted the players did not perform well enough under Hodgson, but is now keen to look to the future and would love to see Dalglish installed as permanent boss.

"I have great respect for Roy so I'd never say 'things have changed for the better' and that type of stuff," he said.

"As a club and as players we didn't do enough to help the manager out - the performances weren't good enough and obviously the managers take the brunt of it.

"Things have improved now ad Kenny coming has got everyone onside.

"That's not our decision. That's up to the club owners. For everyone, especially me and Stevie (Gerrard), he's a hero to us. The results are obviously going very well. If you're asking me, obviously I'd love him to be the manager."

Dalglish refused to drawn on whether he should be offered the manager's job full-time.




"My concern is the Wigan match next week,'' he said.

"The owners have been fantastic in their support during the transfer window.

"You've got to give credit to them. I think by their actions they are makin decisions that are in the best interests of this football club.''

Dalglish admitted Liverpool were "on a good roll at the moment''.

"That's four clean sheets on the bounce which is really important for us. And four victories. We have to take each game as it comes.''

Chelsea manager Carlo Ancelotti admitted his team were below par.

He said: "We did not play well. Our performance was not good enough to win this game.

"Liverpool defended very well and we were not able to find the space."
 
West Ham 0-1 Birmingham City

1 comments »
Updated Feb 6, 2011 10:53 AM ET
Avram Grant endured a nightmare 56th birthday as West Ham lost 1-0 at home to Birmingham to sink to the bottom of the Premier League table.

Nikola Zigic dealt the fatal blow midway through the second half of Sunday's clash when he nodded home from a Sebastian Larsson free-kick to seal the win and move Blues up to 16th.

Substitute Demba Ba rattled the woodwork on his debut but, otherwise, the Hammers rarely threatened the visitors' goal and looked poor throughout.


BARCLAY'S PREMIER LEAGUE
Sat., Feb. 5
Stoke City 3-2 Sunderland | Recap
Aston Villa 2-2 Fulham | Recap
Everton 5-3 Blackpool | Recap
Man City 3-0 West Brom | Recap
Newcastle 4-4 Arsenal | Recap
Tottenham 2-1 Bolton | Recap
Wigan 4-3 Blackburn | Recap
Wolves 2-1 Man United | Recap
Sun., Feb. 6
West Ham 0-1 Birmingham | Recap
Chelsea 0-1 Liverpool | Recap
BPL Scores | Table | Fixtures
Grant's position will now undoubtedly come under scrutiny once more as a result.

The Israeli went into the match knowing a victory would see West Ham record their first back-to-back league wins in what has been a troubled season so far.

Their attempts were hit by a calf injury to James Tomkins in the warm-up. That meant an early recall for Matthew Upson, who had missed the midweek win over Blackpool with tendonitis.

The former Birmingham centre-half was paired with Winston Reid , who came in for the injured Danny Gabbidon

Scott Parker assumed his place in midfield the day after he earned a recall to the England squad.

Cameron Jerome and Barry Ferguson both overcame ankle injuries to make a Birmingham team that was unchanged from Wednesday's 2-2 draw against Manchester City.

The match was a chance for the Londoners to avenge their Carling Cup semi-final exit to their midlands rivals last month.

Ben Foster, whose howler gifted West Ham a first-leg lead in that tie, started nervously, punching an early Gary O'Neil cross clear when it was easier to catch.

The England goalkeeper came out to snatch the ball from Frederic Piquionne's feet after he was put through by the in-form Victor Obinna.

After a quiet opening 15 minutes, West Ham started to pressure the visitors' goal.

On-loan Tottenham striker Robbie Keane played Piquionne in with a clever backheel but the former Portsmouth striker could only fire a tame curler at Foster.


FOXSOCCER.TV
The home of the best LIVE soccer and rugby awaits at FoxSoccer.tv -- don't miss a second of the action.
Obinna, who had scored five in his previous two matches before today, then struck a 25-yard effort just wide and Parker threatened with a dangerous low cross that was hooked clear.

Robert Green was called into action for the first time when he collected a low shot from Lee Bowyer on the half-hour.

Jerome beat Green to a header from a corner soon after but the former Cardiff marksman could only glance wide.

Roger Johnson beat Piquionne to a cross but flashed a free header over the bar from 10 yards.

Johnson cut out a dangerous cross from Obinna with a superb diving header as Piquionne lurked at the back post.

A late sliding challenge on David Bentley from Mark Noble earned the Hammers midfielder a yellow card.

West Ham felt they should have had a penalty late on in the first half when Lars Jacobsen's strike hit Liam Ridgewell on the arm but referee Chris Foy turned down their appeal.

Obinna had an appeal for another spot-kick turned down moments later when his shot hit Johnson on the arm in the box and Keane volleyed over under pressure in stoppage time.

Manuel da Costa came on for Upson at half-time to make his first appearance in three months.

Birmingham started the second period brightly and Bentley found the towering Zigic at the back post but he headed wide, much to Alex McLeish's frustration.

The Birmingham manager brought Larsson on for Jerome in the 57th minute and Grant replaced Piquionne with Carlton Cole soon after.

The West Ham crowd were getting frustrated with their team's scrappy play and their hopes were further dashed when Zigic gave Birmingham a 65th-minute lead.

The 30-year-old took advantage of some slack marking from Wayne Bridge to meet Larsson's free-kick at the back post and nod home from six yards for his second in two matches.

Foster was booked for time-wasting with 15 minutes remaining.

Grant looked to Demba Ba for inspiration, the Senegalese coming on to make his Hammers debut in place of Keane.

The former Hoffenheim striker almost made an immediate impact when he slammed a volley onto the woodwork after the ball ricocheted around the Birmingham box.

Da Costa almost caught Foster out with a fierce 35-yard shot but the Birmingham keeper scrambled across his line to save.

The defender was at the forefront of West Ham's late push for an equaliser as he headed just wide of Foster's goal from eight yards.

Parker slipped into the box in stoppage time but was met by a sea of Birmingham defenders.

Obinna and Da Costa were booked for late challenges in injury time and West Ham's threat petered out, the game ending with a chorus of boos from the home crowd.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom