Arsenal, Barcelona zageuka gumzo Ligi ya Mabingwa
Send to a friend Tuesday, 15 February 2011 07:47 0diggsdigg
LONDON, Uingereza
LIGI ya Mabingwa Ulaya, hatua ya mtoano (maarufu 16 bora) inaendelea kati ya leo na kesho huku macho na masikio yakielekezwa zaidi kwenye mechi baina ya Arsenal na Barcelona, kesho Jumatano ambazo zinachukuliwa na wengi kuwa klabu zinazoongoza kwa kucheza soka ya kuvutia duniani.
Pia, mechi nyingine ambayo pia inapewa nafasi kubwa ni baina ya AC Milan ambayo ina kiwango kikubwa kwa sasa itakapocheza na Tottenham Hotspur ya England.
Uwanja wa Arsenal wa Emirates jijini London unachukuliwa kama ngome ambako wapenzi wa soka watashuhudia soka ambayo inazikutanisha timu ambazo zilikutana katika robo fainali ya michuano hiyo na Barcelona kushinda kwa mabao 6-3.
Mabingwa hao wa Hispania, Barca wametwaa taji hilo mara tatu, kiasi cha kupewa nafasi kubwa msimu huu kutwaa tena ubingwa wa michuano hiyo.
Tegemeo kubwa kwa Barca itakuwa mshambuliaji Lionel Messi, ambaye mbali ya kuongoza kwa upachikaji mabao msimu huu ataiongoza safu ya ushambuliaji dhidi ya Arsenal Jumatano.
"Tunakutana na timu imara duniani, ni kitu muhimu kukutana nao tukiwa vizuri kisaikolojia ," alieleza kocha Arsene Wenger Jumamosi baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wolverhampton Wanderers, ikishika nafasi ya pili nyuma ya Manchester United.
Kwa upande wake,Tottenham ambayo imefikia hatua hiyo kwa mara ya kwanza itacheza mchezo huo bila winga wake, Gareth Bale na mchezeshaji Rafael van der Vaart katika mchezo wa leo na huenda atarejea katika mchezo wa leo kwenye Uwanja wa San Siro, mahali ambako klabu hiyo imewahi kucheza msimu huu.
Katika mchezo huo, Spurs ilishindwa kwa mabao 4-3 dhidi ya Inter Milan katika mchezo wa hatua ya makundi licha ya kustaajabisha kipindi cha pili kupitia kwa Bale, ambaye alifunga mabao matatu (hat-trick).
AC Milan, ambayo ni bingwa mara saba wa michuano hiyo inaingia katika mchezo huo ikiwa kileleni mwa Ligi Kuu ya Italia, Serie A baada ya kuiadhiri Parma kwa mabao 4-0 mwishoni mwa wiki.
"Tunahitaji ujasiri, moyo wa kujituma na kiwango cha uchezaji kama tunataka kufuzu," alieleza kiungo mzoefu Clarence Seedorf. "Matokeo dhidi ya Parma yanaonyesha kuwa tumejiandaa."
Katika mchezo mwingine,Valencia ya Hispania itakuwa mwenyeji wa Schalke 04 huku Shakhtar Donetsk, Ukraine ikiwa mgeni wa AS Roma katika mechi za leo, huku mechi nyingine nne zikisubiriwa wiki ijayo.
Arsenal inakumbuka somo ambalo ilifunzwa na Barca msimu uliopita baada ya mchezo wa awali kumalizika kwa sare ya mabao 2-2. Walijikuta wakibamizwa kwa mabao 4-1, yote yakifungwa na Messi pekee.
Mchezaji huyo bora wa dunia mara mbili, tayari amepachika mabao tisa kwenye ligi hiyo, akiwa nayo pia mabao 24 kwenye Ligi Kuu ya Hispania, La Liga.
"Unapocheza dhidi ya timu ngumu kama Barcelona, unatakiwa kuwa na wachezaji 11 walio kamilifu katika kiwango, " alisema kocha Wenger, ambaye aliiongoza Arsenal dhidi ya Barca ambao walifungwa mabao 2-1 kwenye fainali ya mwaka 2006.
"Kitu muhimu kwetu ni kucheza kwa kujiamini . Hatupewi nafasi kubwa katika mchezo huu, lakini tunaweza."
Barcelona, kwa upande wake inaingia katika mchezo huo baada ya sare ya 1-1 dhidi ya Sporting Gijon, matokeo ambayo yametibua rekodi ya ushindi wa mechi16.
Hadi sasa, Barca wamefunga mabao 60-6 dhidi ya wapinzani wao. Pia, wameshinda mechi zao zote za ugenini.
"Kwa sasa, hatuna budi kujielekeza kwenye ushindi katika hatua hii ya 16 bora," alieleza kocha Pep Guardiola. "Kwa sasa tunapaswa kucheza vema jijini London."
Guardiola atakuwa na wachezaji wake wote wa kikosi cha kwanza baada ya kuwapumzisha kiungo Sergio Busquets na beki Mfaransa Eric Abidal Jumamosi. Swali pekee kwake ni hali ya afya ya beki wake, Carles Puyol ambaye ameumia goti.
AC Milan itawakosa viungo wake, Kevin-Prince Boateng, Massimo Ambrosini na Andrea Pirlo dhidi ya Spurs, pamoja na beki Mbrazili, Thiago Silva anaweza kuhamishiwa katika kiungo.
"Kumchezesha Thiago Silva kama kiungo wa kati leo inawezekana," alieleza kocha Massimo Allegri.
Nao Spurs wanao majeruhi ambao ni pamoja na viungo Luka Modric na Tom Huddlestone. Pia, itawakosa Bale na Van der Vaart , pigo ambalo ni kubwa zaidi.
Despite the caliber of the opposition, manager Harry Kocha Redknapp ameeleza kuwa na imani kwa wachezaji wake, ambayo ilimaliza kileleni mwa kundi mbele ya Inter Milan kwenye msimu wake wa kwanza, kwa sasa inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu England.
"Milan ni timu hatari. Wanao wachezaji mahiri sana. Wanao wakali watatu, Robinho, (Alexandre) Pato, (Zlatan) Ibrahimovic. Ni wachezaji wa kiwango cha juu ," alisema Redknapp.
"Ni mtihani mgumu kwetu,lakini ninaamini kuwa tuna nafasi kubwa ya kufuzu."
Valencia ambao wamemaliza wa pili mara mbili itamkosa Juanma Mata kwa mchezo wa kwanza dhidi ya Schalke 04.
Lakini, mshambuliaji wa zamani wa Real Madrid, Raul Gonzalez anarejea Hispania katika kikosi cha Schalke kwa mara ya kwanza. Raul alifunga mabao12 dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Mestalla akiwa Real Madrid.
Mabeki Philippe Mexes na Nicolas Burdisso wanaweza kurejea kwa Roma dhidi ya mabingwa wa Ukraine , Shakhtar baada ya kuikosa mechi dhidi ya Napoli Jumamosi.