Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Blackburn 1 - 1 West Ham


Stanislas scores West Ham's equaliser to give them their 13th point of the season


By Ian Hughes


Junior Stanislas scored late in the second half to rescue a point for West Ham against Blackburn at Ewood Park.
Early on, Morten Gamst Pedersen's free-kick was the best Rovers managed, while Paul Robinson denied Luis Boa Morte.
Ryan Nelsen nudged the opener with his knee, beating Hammers debutant keeper Ruud Boffin at the second attempt.
West Ham were denied an equaliser when Matthew Upson's shot hit the post but Stanislas curled in a low effort to earn his side a reprieve.
Both teams came into the game off the back of a destabilising week. Hammers boss Avram Grant had been reportedly told he must win one of his side's next three games to avoid being sacked, while Rovers dismissed manager Sam Allardyce on Monday and put Steve Kean in temporary charge.
Please turn on JavaScript. Media requires JavaScript to play.
</p>
Click to play


Click to play




Boss Grant hails West Ham spirit

Ironically, there have been suggestions that Allardyce is waiting in the wings to replace Grant - but on the evidence of the Hammers' performance at Ewood Park, the job may not become available for a while.
The Londoners fought back gamely late on and with better delivery in the final third they might have even sneaked a win, which would have been their first on the road since August 2009.
But in a game largely short on action to help excite and warm the freezing crowd, a draw seemed a fair result.
It was understandable that the visitors would concentrate on defence and on protecting their fourth-choice keeper Boffin, who had previously played only three times for the reserves.
The Londoners also suffered a blow before kick-off when Valon Behrami injured himself in the warm-up.
606: DEBATE
We broke well but our final ball was awful


martin-hammer

However, the lack of ambition shown in the first half by a side desperate to lift themselves off the foot of the table did not bode well.
With only one other fixture surviving the weather, West Ham could have leapfrogged Wolves with a win - and possibly helped Grant save his job in the process.
They managed to fashion two chances of any note, but Frederic Piquionne fired into the side netting and Boa Morte's low shot was kept out at the near post by Robinson's legs.
Rovers fared no better, with only a curling Pedersen free-kick testing the inexperienced Boffin, who was able to enjoy a pressure-free opening 45 minutes.
But after the break the young Belgian was soon picking the ball out of the net, though he will feel a little unfortunate not to have kept a clean sheet.
His point-blank save to keep out Nelsen's shot deserved better than for the ball to find its way past him via the knee of the Rovers defender as he swung his leg in hope.
The goal seemed to stir the visitors into action and for the first time in the match they began to dictate the play.
Please turn on JavaScript. Media requires JavaScript to play.
</p>
Click to play


Click to play




Kean disappointed by dropped points

And they came agonisingly close to an equaliser when Upson's low shot, following Stanislas's cross, cannoned off the foot of the post.
Soon after they deservedly restored parity when Scott Parker embarked on a mazy run and Stanislas finished off the move with a curling shot into the bottom corner.
It was a blow for Blackburn, who had lost Jason Roberts to a hamstring injury early on and then saw Christopher Samba and his replacement Phil Jones also go off injured, but they would have restored their lead had Nelsen not been penalised for a foul in the box before David Dunn's flick in.
West Ham also pushed for a winner but let themselves down with poor crossing when they had players well placed. The result means West Ham pick up their 13th point of the season - but Grant may now have only two games left to save himself.
 
Stewart: Nimepata somo Yanga


Na Zahoro Mlanzi

KOCHA Mkuu wa Azam FC, John Stewart, amesema mchezo wa kirafiki dhidi ya Yanga, umempa mwanga wa kujua aanze vipi kupanga mikakati yake kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.Timu hizo zilikutana juzi kwenye Uwanja wa
Uhuru, Dar es Salaam, ambapo Azam iliibuka na ushindi wa mabao 3-1, katika mchezo wa kujipima nguvu kujiandaa na ligi hiyo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Stewart alisema ameridhishwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake, kwani mchezo huo atautumia kupata kikosi cha kwanza.

"Mchezo ulikuwa mzuri licha ya wapinzani wetu kuchezesha timu dhaifu kipindi cha kwanza, lakini nilipata wakati mgumu baada ya kuona akibadilisha timu nzima na ndipo sasa, mechi rasmi ilipoanza," alisema.

Alisema wachezaji walioingia kipindi cha pili ndio walikuwa kipimo tosha kwake, kwani ushindani ulikuwa mzuri na hata wachezaji wake walicheza kwa nguvu tofauti na kipindi cha kwanza.

Alisema baada ya mchezo huo, wataendelea na programu yao kesho ikiwa ni maandalizi ya mwisho, kabla ya ligi hiyo kuendelea Januari 15, mwakani.

Akizungumzia michezo mingine ya kirafiki, Stewart alisema ni vizuri kucheza zaidi na hilo atawasiliana na viongozi wake kujua kama kuna uwezekano wa kupata mechi hizo.
 
Eto'o achaguliwa mchezaji bora wa klabu bingwa za dunia Sunday, 19 December 2010 19:56

ABU DHABI, UAE

MSHAMBULIAJI wa Inter Milan, Samuel Eto'o amechaguliwa kuwa mchezaji bora katika mashindano ya klabu bingwa ya dunia baada ya timu yake kuichapa TP Mazembe mabao 3-0 katika mechi ya fainali iliyochezwa mjini Abu Dhabi.

Katika mechi hiyo ambayo Eto'o alifunga bao la pili, pia mshambuliaji wa TP Mazembe, Dioko Kaluyituka alishika nfasi ya pili na kupewa zawadi ya silver na mshindi wa tatu alikuwa ni Andres D'Alessandro wa klabu ya Inter de Porto ya Brazil.

Eto'o ni mchezaji ambaye alikuwepo katika kikosi cha Inter Milan mwaka jana ambacho kilitwaa mataji matatu ambayo ni klabu bingwa barani Ulaya, ubingwa wa ligi kuu Italia na kombe la Italia pia alikuwepo kwenye kikosi cha Barcelona cha mwaka juzi ambacho pia kilitwaa mataji matatu.

Tuzo aliyotwaa Eto'o mwaka huu, mwaka jana ilitwaliwa na nyota wa Barcelona, Lionel Messi wakati Wayne Rooney wa Manchester United alitwaa tuzo hiyo mwaka 2008.

Katika mechi ya fainali ya klabu bingwa barani Ulaya kati ya Inter Milan dhidi ya TP Mazembe, timu ya Inter Milan ilipata mabao mawili katika kipindi ha kwanza ambayo yalifungwa na Goran Pandev na Samuel Eto'o, ambapo bao lao la tatu lilifungwa kipindi cha pili na Jonathan Biabiany.

Ushindi ilioupata Inter Milan umemsaidia kocha wa timu hiyo Rafa Benitez kupata nguvu baada ya kushutumiwa sana kwa sababu hivi sasa Inter Milan haifanyi vizuri katika ligi kuu ya Italia.

Hii ni mara ya nne mfululizo kwa timu za Ulaya kutwaa ubingwa wa klabu bingwa wa dunia huku TP Mazembe ikiwa ni timu ya kwanza kutoka nje ya bara la Ulaya na Amerika ya Kusini kufika fainali ya mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya.
 
Tanzania yapanda viwango vya netiboli duniani


Na Amina Athumani, Kibaha

TANZANIA imepanda viwango vya kimataifa vya mchezo wa Nnetiboli vinavyotolewa na Shirikisho la Kimataifa la Netiboli (IFNA), kutoka nafasi ya 24 hadi nafasi ya 20.Pia, imepanda kutoka nafasi ya nne hadi nafasi ya tatu kwa ubora wa
viwango vya Afrika vinavyotolewa na Chama cha Netboli Afrika (AN).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi na Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA), Anna Bayi, alisema viwango hivyo vinavyotolewa na IFNA, vinaifanya Tanzania kutambulika zaidi kimataifa katika mchezo wa netiboli.

"Viwango hivi vimetolewa na IFNA juzi, baada ya kuona uwezo wa Tanzania waliouonesha katika mashindano ya kimataifa yaliyofanyika nchini Singapore wiki iliyopita, na Tanzania kushika nafasi ya tatu, hivyo tuna imani timu yetu itaendelea kufanya vizuri katika mchezo huu na kuitambulisha zaidi Tanzania kimataifa," alisema.

Alisema sasa ni wakati wa wadau mbalimbali wa michezo nchini, kuisaidia timu hiyo ili iweze kushiriki mashindano mengi ya kimataifa yatakayoiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kushiriki Kombe la Dunia la netiboli hapo baadae.Mwenyekiti huyo alisema ni wakati wa serikali kuipa ruzuku hata kidogo CHANETA, ili iweze kuendesha shughuli za kichama vizuri yakiwemo maandalizi ya kutosha kwa timu ya taifa.

 
*Mazishi ya Semhando Simanzi, vilio vyatawala Muheza Sunday, 19 December 2010 20:16

Enzi za uhai wake mwanamuziki mkongwe wa bendi ya muziki wa dansi, Abuu Semhando.

Steven William, Muheza
MWANAMUZIKI mkongwe wa bendi ya muziki wa dansi, Abuu Semhando amezikwa jana nyumbani kwao katika kijiji cha Kibanda wilayani Muheza mkoani Tanga.

Mazishi ya mwanamuziki huyo yalitawaliwa na simanzi kubwa na vilio kutoka kwa wanafamilia na wananchi wa wilaya ya Muheza waliofurika katika mazishi hayo.

Akizungumza na Mwandishi wetu katika mazishi hayo ndugu wa marehemu, Shaaban Omari Semhando alisema kuwa ndugu yao wamemzika katika makaburi ya familia yao.

Alisema kuwa kifo cha ndugu yao kimewashtua sana kwa kuwa alikuwa kiongozi wa familia yao na walikuwa wanamtegemea katika mchango wa mawazo ndani ya familia yao.

Ndugu huyo wa marehemu ambaye makazi yake yapo Ngorongoro mkoani Arusha alisema kuwa Abuu amefariki akiwa na umri wa miaka 68 na amefanya kazi katika bendi mbalimbali.


Mazishi ya Abuu Semhando yaliongozwa na wanamuziki wenzake wa bendi mbalimbali ambao nao walitoa nasaha zao jinsi wanavyomtambua mwenzao enzi ya uhai wake.

Viongozi wa bendi ya Twanga Pepeta walihudhuria mazishi hayo na kuhuzunishwa na kifo cha Semhando na kusema wamempoteza mtu muhimu katika fani ya muziki hapa nchni.

Marehemu Abuu Semhando alipata ajali hiyo iliyompotezea maisha baada ya kugongwa na gari ndogo aina ya Mercedes Benz wakati yeye akiwa anaendesha pikipiki.
 
Eto'o, Gyan wanukia ubora Afrika Sunday, 19 December 2010 20:07

CAIRO, Misri

MSHAMBULIAJI wa Inter Milan na Cameroon, Samuel Eto'o anapewa nafasi kubwa ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika wa mwaka huu na kufikisha mara nne kutwaa tuzo hiyo, lakini nyota wa Ghana, Asamoah Gyan anaweza kufanya maajabu leo usiku jijini Cairo.

Katika kinyang'anyiro hicho cha kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika yupo Samuel Eto'o, nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba na Asamoah Gyan ambao ni wachezaji watatu wanaowania tuzo hiyo, ambapo watakaopiga kura kumchagua mchezaji bora ni makocha na manahodha wa timu 53 za mataifa ya Afrika.

Eto'o alitua jana usiku nchini Misri akitokea Abu Dhabi baada ya timu yake kuifunga bao 3-0 TP Mazembe na kutwaa ubingwa wa klabu bingwa ya dunia.

Eto'o ,29, pia ameweka rekodi kwa kuifungia timu yake ya Taifa ya Cameroon mabao mengi katika fainali za mataifa ya Afrika.

Lakini katika tuzo za mwaka huu, Asamoah Gyan ameoneka kuwa tishio baada ya kupata mafanikio makubwa katika fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini Afrika Kusini huku akikosa penati katika mechi ya robo fainali dhidi ya Uruguay mjini Johannesburg.

Gyan,25, aliweza kufunga mabao matatu ambayo yaliisaidia Ghana kuweza kufika hatua ya nane bora, hii ni mara ya kwanza kwa Gyan kuchaguliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika.

Mshambuliaji wa Chelsea na Ivory Coast, Drogba ambaye pia ni mshambuliaji wa kiwango cha juu duniani ndiye anayeitetea tuzo hiyo ya mchezaji bora wa Afrika kwa sababu alitwaa tuzo hiyo 2009 pia aliwahi kuitwaa 2006.

Eto'o ndiyo ametwaa tuzo hiyo mara nyingi, ameitwaa 2003, 2004 na 2005.
 
Nane zatinga robo fainali
Sunday, 19 December 2010 20:06

Jesca Nangawe

TIMU za nane zimekata tiketi ya kucheza hatua ya robo fainali ya michuano ya netiboli ya taifa itakayoanza kupigwa leo katika viwanja vya Shule ya Sekondari Filbert Bayi iliyoko Kibaha, Pwani.

Timu hizo ni pamoja na Mwanza, Temeke, Pwani na Morogoro zinazotoka Kundi A wakati Dodoma, Mbeya, Ruvuma na Kinondoni zimeingia hatua hiyo zikitoka kundi B.

Katika michezo iliyopigwa jana, Mwanza iliikandamiza Lindi mabao 33-9 wakati Temeke iliirarua Arusha kwa mabao 35-18 ili hali wenyeji Pwani wakijikwamua kwa kuilaza Morogoro kwa mabao 23-20.

Kwa matokeo hayo Temeke ilifikisha pointi 10 wakati Pwani ilikusanya pointi nane, Morogoro sita na Mwanza 3.

Kutoka kundi B, Dodoma iliichapa Kinondoni mabao 31-14, Ruvuma ikaikung'uta Mtwara 43-19.

Kwa ushindi huo Dodoma ilifanikiwa kukusanya pointi 8 wakati Mbeya ilifikisha pointi 6, Ruvuma 4 na Kinondoni 2.
 
Tanga yaichakaza Kilimanjaro Umitashumta
Sunday, 19 December 2010 20:05

Sosthenes Nyoni
TIMU ya soka ya mkoa wa Tanga jana iliendeleza rekodi ya ushindi baada ya kuichapa Kilimanjaro mabao 4-0 kwenye moja ya mechi za Umoja wa Shule za Msingi na Taaluma(Umitashumta)uliofanyika kwenye Uwanja wa Shirikika la Elimu Kibaha, Pwani.

Katika mchezo huo mabao ya Tanga yaliwekwa kimiani na Omari Nurdin na nahodha wake Benedict Elias kila moja alifunga mawili.

Mpambano mwingine wa soka ni ule ulioishuhudia Iringa ikiichapa Dodoma mabao 2-1.

Katika netiboli Morogoro iliizamisha Singida kwa mabao 25-8 wakati Tanga iliikung'uta Kilimannjaro mabao 24-5.

Kwa upande wa riadha Dodoma ilionyesha umwamba pale kwakunyakua nafasi tatu muhimu katika mbio za mita 1500 (wanaume) ambapo Said Leviori aliibuka mshindi wa kwanza, Amosi Joseph alishika nafasi ya pili huku Charles Ernest akitwaa nafasi ya tatu.

Naye Stamili fundi aliibuka mshindi katika mbio za mita 1500 wanawake,wakati Chiku Shaaban alifanikiwa kutwaa nafasi ya pili na Mwanaisha Iddi aliweza kuikamata nafasi ya tatu.


 
Mashabiki wa TP Mazembe wazua vurugu


LUBUMBASHI, DRC

GHASIA zimezuka katika mji wa Lubumbashi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), baada ya timu ya TP Mazembe kushindwa katika fainali ya kuwania Kombe la Dunia kwa klabu mjini, Abu Dhabi, usiku wa kuamkia jana
.

TP Mazembe ilikuwa klabu ya kwanza kutoka barani Afrika kuwahi kufuzu fainali za mashindano hayo, ilifungwa mabao 3-0 na Inter Milan ya Italia.

Habari zinasema kuwa, mashabiki ambao walikuwa na matumaini makubwa kwamba, TP Mazembe ingeshinda mchezo huo, waliingia katika barabara za mji wa Lubumbashi na kuvamia biashara zinazomilikiwa na kampuni ya China.Inaaminika kuwa, mashabiki hao walidhani kuwa, refa aliyesimamia mchuano huo raia wa Japan, alikuwa Mchina, na walikuwa wamekasirishwa na hatua alizochukuwa mwamuzi huyo dhidi ya TP Mazembe ,wakati wa mechi hiyo.

Ilielezwa kuwa, wakati wa ghasia hizo, mali ziliporwa, lakini polisi waliweza kuwatawanya mashabiki hao kwa kufyatua risasi hewani.Kampuni nyingnei ya China zinaendesha biashara katika mji wa Lubumbashi ambao ni kitovu cha uchimbaji madini ya shaba nyekundu.
 
Matibabu ya Uhuru shaka tupu
Sunday, 19 December 2010 20:02

Clara Alphonce
RIPOTI ya madaktari kutoka hospitali ya Muhimbili ndio itatoa hatma ya mshambuliaji wa Simba, Uhuru Seleman kwenda kutibiwa India au kubaki hapa nchini.

Mchezaji huyo amekuwa akisumbuliwa na misuri ya goti kwa kipindi cha miezi minne na kukosa mechi kadhaa za ligi kuu Tanzania bara mzunguko wa kwanza.

Meneja kwa timu hiyo Innocent Njovu alisema kuwa tayari mchezaji huyo ameshafanyia uchunguzi wa awali na daktari na kwa sasa wamekuwa wakisubiri ripoti yake ambayo itaamua kwenda India au kutibiwa hapa hapa.

Katika hatua nyingine Njovu alisema kuwa wameshaanza mazoezi kwa ajili ya mashindano mbali mbali yaliopo mbele yao na baada ya sikukuu ya Krismasi timu itaenda Zanzibar kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Mapinduzi yatakayoanza kutimua vumbi Januari 2.

Alisema baadhi ya wachezaji waliokuwepo kwenye michuano ya Chalenji wameanza mazoezi na kikosi hicho kasoro wachezaji watano ambao ni Joseph Owino, Emmanuel Okwi, Patrick Ochan, Kelvin Yondani na Juma Nyosso ambao wanatakiwa kuwasili leo.

Alisema tayari wameshamaliza programu ya GYM na bahari na sasa wameanza programu ya uwanjani wakiwa chini ya kocha wao Patrick Phiri ambaye hivi karibuni ameingia mkataba upya wa miaka miwili na uongozi wa klabu hiyo.
 
Barcelona yatoa zawadi ya Krismasi
Sunday, 19 December 2010 20:00

BARCELONA, Hispania
MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Hispania Barcelona wameiachapa Espanyol bao 5-1 katika mechi ya ligi kuu na kupata ushindi wa 10 mfululizo hivyo kuiacha Real Madrid kwa pointi tano katika msimamo wa ligi.

Katika mechi hiyo Pedro Rodriguez alifunga mabao mawili na David Villa pia alifunga mabao mawili huku Xavi Hernandez akifunga bao moja, ambapo bao la Espanyol lilifungwa na Osvaldo.

Katika mechi nyingine ya ligi kuu ya Hispania, Villarreal iliichapa Mallorca bao 3-1. Mabao ya Villarreal yalifungwa na Santiago Cazorla na Giuseppe Rossi huku bao la Mallorca likifungwa na Jonathan de Guzman.

Pia timu ya Athletic Bilbao iliichapa Levante 2-1 na Deportivo La Coruna ilitoka sare ya bao 1-1 na Sporting Gijon.

Huko mjini ATHENS, Ugiriki, wachezaji wa Panathinaikos walijikuta wakikimbizwa uwanjani na mashabiki wao baada ya timu hiyo kufungwa bao 1-0 na timu ya Volos katika mechi ya ligi kuu ya nchi hiyo.

Baada ya mechi kumalizika mashabiki wengi wa Panathinaikos waliwatupia vitu mbalimbali wachezaji wao na kuharibu vibaya sehemu ya jukwaa wanalokaa watu muhimu na hivyo kusababisha hasara kubwa.

Mashabiki wa Panathinaikos walionyesha dalili za kutaka kuwafanyia vurugu wachezaji wao tokea wiki iliyopita, ambapo katika mechi dhidi ya Asteras ambayo walitoka sare ya 0-0 kabla ya mechi kuanza mashabiki hao walishika bango ambalo lilikuwa likisomeka,"sisi hatuna kazi nyinyi ni matajiri mnaoishi maisha ya anasa"...."Tunaishiwa uvumilivu". Katika mechi hiyo mashabiki wa Panathinaikos muda mwingi walikuwa wakiwazomea wachezaji wao.

Mjini Berlin, Timu ya Nuremberg iliichapa bao 3-1 Hannover katika mechi ya ligi kuu nchini Ujerumani.

Mabao ya Nuremberg yalifungwa na Andreas Wolf na lingine lililitokana na beki wa Hannover, Steven Cherundolo ambaye alijifunga katika mechi hiyo huku bao la Hannover likifungwa kwa mkwaju wa penati na Sergio Pinto.

Mechi nyingine nchini humo ilikuwa ni kati ya Mainz dhidi ya St.Pauli ambapo Mainz iliibuka na ushindi wa bao 4-2, pia Borussia Dortmund, ilijikuta ikichapwa bao 1-0 na Eintracht Frankfurt.

Huko mjini MILAN, Italia, timu ya Roma imeichapa AC Milan bao 1-0 ambapo bao la Roma lilifungwa na Marco Borriello katika mechi ya ligi kuu ya Italia.

Milan ambayo ina pointi 36 ndiyo inayoongoza ligi kuu ya italia, lakini ili kuendelea kuongoza ligi hiyo ilikuwa ikitegemea mechi za jana za timu za Juventus, Napoli na Lazio ambazo zipo nyuma yake.

Mjini LONDON, Uingereza timu ya West Ham ilitoka sare ya bao 1-1 na Blackburn hivyo kuendelea kushika mkia katika ligi kuu ya Uingereza.

Mjini PARIS, Ufaransa timu ya Rennes iliichapa Valenciennes bao 1-0
 
Klabu bingwa Afrika, Kombe la shirikisho kupangwa leo

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th December 2010 @ 23:59

MACHO na masikio yote leo yataelekezwa katika Jiji la Cairo, Misri ambako droo ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa ya Afrika na ile ya Kombe la Shirikisho kwa msimu wa mwaka 2011 itafanyika.

Mabingwa wa Ligi Kuu ya soka yaTanzania Bara, timu ya Simba itakayocheza Klabu Bingwa Afrika na watani wao wa jadi Yanga ambao watacheza Kombe la Shirikisho watajua wamepangwa na timu zipi na wataanzia wapi kampeni zao kwenye michuano hiyo.

Miamba hiyo ya soka hapa nchini itakuwa ikiomba ili iepuke kukumbana na timu ngumu hatua hiyo ya awali ya michuano hiyo inayoandaliwa na Shirikisho la soka la Afrika (CAF) itakayoanza kutimua vumbi Januari mwakani.

Kwa upande wa Zanzibar timu za Ocean View na KMKM ndizo zitapeperusha bendera katika michuano hiyo na kukamilisha idadi ya timu nne zitakazoiwakilishaTanzania kwenye michuano ya kimataifa kwa msimu wa 2011.

Zaidi ya klabu 100 kutoka vyama vya soka vya mataifa 53 ambavyo ni wanachama wa CAF zitahusika katika droo.

Simba na Yanga, wanakwenda kwenye michuano hiyo ya Afrika wakiwa na rekodi tofauti, ingawa michuano ya mwaka ujao itakuwa inawapa nafasi ya kujaribu kusawazisha makosa yao katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi za klabu.

Yanga ambayo katika msimu uliopita iliwakilisha nchi kwenye michuano ya Klabu Bingwa iliondolewa na klabu ya FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika raundi ya awali ya michuano hiyo kwa kufungwa jumla ya mabao 4-2.

Wakati wenzao Simba, ambao nao hadithi ilikuwa ileile ya kuondolewa kwenye raundi ya awali kama watani zao baada ya kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho ikiwa ni baada ya kuwanyuka Lengthens ya Zimbabwe katika raundi ya kwanza, lakini ilishindwa kufuzu hatua ya makundi baada ya kushindwa kwenye raundi ya pili na Haras El-Hodoud ya Misri kwa kufungwa mabao 6-3.

Mafanikio makubwa iliyowahi kupata Simba ni kufika hatua ya fainali ya michuano ya Kombe la CAF ambayo hivi sasa inatambulika kama Kombe la Shirikisho mwaka 1993, ambapo ilipoteza fainali hiyo kwa kufungwa mabao 2-1 na Stella Abidjan ya Ivory Coast.

Hakuna klabu nyingine ya Tanzania ambayo imewahi kufikia mafanikio kama hayo katika michuano yoyote ile hadi sasa.

Moja ya kumbukumbu ambayo haitosahaulika kwa miaka na miaka ni pale timu hiyo ilipowanyuka na kuwatupa nje ya michuano ya klabu bingwa miamba wa soka wa Misri, Zamalek ambao walikuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo mwaka 2003 na kufuzu hatua ya makundi.

Mafanikio makubwa iliyowahi kupata Yanga yalikuwa ni kufikia hatua ya makundi katika michuano ya klabu bingwa mwaka 1998.
 
Ligi ya soka la wanawake ukombozi pekee Send to a friend Sunday, 19 December 2010 20:40

Mkurugenzi wa Ufundi TFF,Sunday Kayuni

Calvin Kiwia
WIKI iliyopita Shirikisho la Soka Afrika lilitangaza ratiba ya kufuzu kushiriki michezo ya 10 ya Afrika (All Africa Games) kwa wanaume na wanawake.

Michezo ya Afrika inatarajiwa kufanyika mjini Maputo, Msumbiji kuanzia Septemba 3 mpaka 18, 2011, ambapo hatua ya kutafuta timu nane zitakazofuzu kushiriki katika michezo hiyo inaanza mwezi Januari kwa hatua za awali mpaka Julai.

Kwa upande wa wanawake, Tanzania imepangiwa kucheza raundi ya kwanza kati ya April 29-Mei 1 na mshindi wa mechi ya awali kati ya Kenya dhidi ya Sudan.
Lakini walipoulizwa TFF kuhusiana na kutoka kwa ratiba hii
Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo Sunday Kayuni amesema TFF bado hawajapata taaarifa ya ratiba hiyo huku akikisisitiza kwamba wakiipata watatoa tamko rasmi baada ya kuijadili.

Hapa ndipo iliponifanya nikumbuke wakati Twiga Stars ilipokuwa ikijiandaa kwenda kushiriki mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa upande wa wanawake yaliyofanyika nchini Afrika Kusini mwezi Oktoba mwaka huu.

Siku moja nilipata nafasi ya kutembelea mazoezi ya timu hiyo waliokuwa wakifanya kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.

Nilipata muda wa kuongea mawili matatu na wachezaji wa timu hiyo ambao ni kipa Fatuma Omary, Mwanaidi Tamba, Irine Matowo, Pulkeria Charaji, Mwanahamis Omary na nahodha wao Sophia Mwasikili.

Nilichokifuata hapo zaidi nilikuwa nataka kujua kinaga ubaga kuhusiana na ushiriki wao kwa mara ya kwanza kwenye mashindano hayo makubwa kwa bara letu la Afrika kwa upande wa soka la wanawake.

Walichonijibu hapo ni kwamba mazoezi ya Gym na kukimbia kuzunguka uwanja wanayopewa na kocha wao mkuu Charles Boniface Mkwasa na msaidizi wake Adolfu Richard.

Yenye malengo ya kujenga miili yao kinguvu, stamina na kasi ya mchezo yamewajengea kujiamini kwenda kushiriki mashindano hayo yaliyofanyika nchini Afrika Kusini na kuhakikisha wanafanya yale ambayo Watanzania wengi wanayoyatarajia.

"Mazoezi kwa ujumla ni mazuri yametufanya kuwa na nguvu na kasi ya mchezo tunafikiri tunaweza kucheza dakika 120 bila kuchoka kwa sababu waalimu wetu wanatufanyisha mazoezi zaidi ya masaa mawili" walisema wachezaji hao.

Lakini tunavyoendelea na mahojiano yetu nilijaribu kuwauliza swali juu ya uzoefu wao wa mashindano hayo ambayo yanaonyeshwa na vituo vya Luninga karibuni dunia nzima.

Walijibu huku wakionyesha sura za kushtuka huku wakisema kwa kweli hilo kwetu ni tatizo, lakini kwa vile tayari tumefuzu kucheza fainali hizo hatuna budi kupeana moyo ili tukaweze kufanye vizuri kama vile wengi wanavyotarajia.

Walisema hata kama watafanya vibaya kwenye michuano hiyo wanaliomba shirikisho la soka nchini,TFF kujizunza kupitia kwao na kuanzisha Ligi ya soka kwa upande wa wanawake kama ilivyo kwa wanaume.

Tunafikiri sisi tunastahili pongezi kwa hatua tuliyofikia ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika kwa wanawake licha ya nchi yetu kutokuwa na ligi soka ya wanawake.

Tumeona timu yetu ya wanaume ya Taifa Stars pamoja na kuwa na ligi ya mchezo wa soka imeshindwa kufuzu hata kucheza mashindano ya CHAN kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani kwa bara la Afrika.

Nadhani hatuna haja ya kurudi nyuma bali tunataka kusonga mbele nafikiri changamoto imebaki kwa shirikisho la soka nchini, TFF

Kutazama kilio hiki cha kina dada hawa kutaka kuanzishwa kwa ligi ya mchezo wa soka ili wasije kurudia makosa waliyoyafanya kule nchini Afrika Kusini endapo watapata nafasi ya kushiriki tena.

Tunafikiri kuwa chanzo cha timu hiyo kuchemsha kwenye fainali hizo zilizomalizika nchini Afrika Kusini ni kutokana na wachezaji wake kukosa uzoefu wa mashindano hayo ukilinganisha na timu ambazo zilikuwa zimepangwa kundi moja na Twiga Stars.

Kama vile timu ya taifa ya wanawake ya Nigeria, wenyeji wa michuano hiyo Afrika Kusini 'Banyana Banyana' na Mali ambapo ilipoteza michezo yote na kufungashwa virago kurejea nyumbani bila ya pointi yoyote.

Mchezo wa kwanza ilifungwa mabao 2-1 na wenyeji Banyana Banyana ikapoteza tena 3-2 dhidi ya Mali na ule wa mwisho ikachapwa na mabingwa wa fainali hizo Nigeria kwa mabao 3-0.

Wabingwa wa fainali hizo timu ya soka ya wanawake Nigeria na mshindi wa pili Equatories Guinea wataliwakilisha bara la Afrika kwenye michuano ya Kombe la Dunia kwa upande wa soka la kina mama hapo Februari mwakani litakalofanyika nchini Ujerumani.

Tunafikiri kuwa huu ndiyo muda muafaka wa shirikisho hilo kukaa chini na kuanza kutafuta mbinu za kuanzisha ligi kwa upande wa wanawake ili kuepuka na madudu haya yanayoendelea kuikumba nchi yetu kila kukicha.

Kulingana na muonekano wa ushiriki wa timu yetu kwenye mashindano yale yaliyomalizika nchini Afrika Kusini kulionyesha dhahiri kuwa tatizo kubwa lililochangia kufanya vibaya ni wachezaji kukosa uzoefu wa mashindano.

Naamini kabisa kama shirikisho la soka nchini, TFF litaanzisha Ligi ya soka kwa upande wa wanawake timu hiyo ikipata nafasi nyingine ya kushiriki itafanya vizuri zaidi na kuitangaza nchini yetu kupitia soka la wanawake.

Ni matarajio yetu kuwa TFF itaanza mikakati madhubuti kabisa ya kutafuta ufadhili wa Ligi hiyo na kutoa zawadi kubwa kwa washindi ili kuifanya iwe na ushindano mkubwa na kuwajenga wachezaji wetu kimashindano zaidi.

Hatufikirii kama TFF inaweza kukosa ufadhili wa kudhamini ligi hiyo wakiwa makini na suala hili tunalitakia kila la kheri shirikisho hili kwa kazi waliweza kuwapata Vodacom.

*Calvin Kiwia ni mwandishi wa gazeti la Mwananchi habari za michezo; 0786 350 682 / 0754 895 312
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…