Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
FRAT bado yaikomalia TFF
Monday, 27 December 2010 09:23

Sweetbert Lukonge
BAADHI ya viongozi wa Chama cha Waamuzi wa Soka nchini (FRAT) wamelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutoa ufafanuzi wa kina juu tuhuma za madai ya kukatwa baadhi ya majina ya waamuzi kwenye orodha ya FIFA.

Wakizungumza na Mwananchi jana kwa sharti la kutotajwa majina yao viongozi hao walisema kuwa TFF inatakiwa kutoa ufafanuzi wa kina juu ya tuhuma hizo ili kujua ni sehemu gani yenye makosa katika suala hilo.

ìLicha TFF hivi karibuni kutoa ufafanuzi juu ya tuhuma za kuyaondoa baadhi ya majina katika orodha iliyotumwa FIFA kwa lengo la kupitishwa katika orodha ya waamuzi wa kimataifa bado shirikisho hilo linatakiwa kutoa ufafanuzi wa kina juu ya jambo hilo.

ìKutokana na taarifa mbalimbali ambazo tumekuwa tukipata kutoka kwa baadhi ya viongozi wa shirikisho hilo, inasemakana TFF iliyaondoa majina ya waamuzi hao na kupitisha ya wale ambao ilikuwa ikiwahitaji.

ìHaingii akilini kuwa FIFA itoe agizo la mdomo juu ya kuwasimamisha waamuzi kwa ajili ya uchunguzi bila ya barua na baadaye FIFA iwatumie katika mashindano ya kimataifa lakini waamuzi hao wakosekane katika orodha ya wale walioteuliwa katika orodha ya waamuzi wa kimataifa, hivyo tunaomba ufafanuzi zaidi,î walisema viongozi hao.

Kwa upande wake Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema kuwa halihusiki na tuhuma hizo isipokuwa liliwasilisha majina yote FIFA ya waamuzi wote waliofikia vigezo vinavyotambuliwa kimataifa na endapo kama jina la mwamuzi yeyote halipo katika orodha iliyorudi basi hajakidhi vigezo.

Kaimu katibu mkuu wa TFF, Sunday Kayuni alisema kuwa miongoni mwa vigezo hivyo ni pamoja na Waamuzi waliopendekezwa kuwa waamuzi wa kimataifa ni lazima wawe wamefaulu jaribio la utimamu wa mwili katika eneo husika miezi minne kabla ya tarehe ya mwisho ya kuchaguliwa kwa waamuzi.

Mbali na hilo pia wawe wamefaulu vipimo vya afya zao ili kuthibitisha wanaweza kutimiza majukumu ya uamuzi katika kipindi cha miezi minne kabla ya kuchaguliwa kwa orodha ya waamuzi wa kimataifa.

Hata hivyo Chama wanachama ni lazima kipeleke FIFA matokeo yenye mpangilio wa ubora wa waamuzi wanaopendekezwa yanayotokana na alama walizopata kutokana na michezo waliochezesha katika Ligi Kuu miezi 12 kabla ya kuchaguliwa.

ìKuna vigezo vingine vingi, lakini hivi ni baadhi tu, hivyo kutokana na vigezo hivyo kama mwamuzi hana ni lazima jina lake halitopitishwa katika orodha ya waamuzi wa kimataifa kwa sabubu hajakidhi viwango na sifa zinazotakiwa.

ìKutokana na hali hiyo wale ambao majina yao hayakupitishwa inawezekana kabisa hawakukidhi viwango hivyo, hivyo TFF hatupaswi kulaumiwa kwa hilo, sisi tupo kuhakikisha kila mdau anapata haki kwa mujibu wa kanuni na sheria na zile za FIFA," alisema Kayuni.
 
40 wahitimu mafunzo ya ukocha Monday, 27 December 2010 09:22

Sweetbert Lukonge
ZAIDI ya makocha 40 mkoani Mwanza, wamehitimu mafunzo yao ya siku tatu ya mbinu za ukocha yaliyoendeshwa na kocha msadizi wa timu ya Taifa (Taifa Stars) Sylivester Marsh.

Akizungumza na Mwananchi jana Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoani Mwanza (MZFA) Jackson Songora alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kwa namna moja ama nyingine kuinua soka katika mkoa huo.

ìHatua hii ni changamoto kubwa kwa makocha wote waliofanikiwa kujifunza mengi kutoka kwa mtaalamu huyo, tunawaomba wajaribu kuhakikisha wanayafanyia kazi ili lengo letu liweze kutimia.

ìHaitapaendeza kuona kocha yeyote aliyebahatika kupata mbinu mpya za kiufundi ikiwa ni pamoja na kujifunza mifumo mbalimbali ya soka anaishia kuwa kocha wa semina tu bila ya kutumia ujuzi huo kuinua soka na kuibua vipaji mbalimbali vilivyojificha kwa faida ya soka letu,î alisema Songora.

Alisema kila kocha aliyepata mbinu hizo anatakiwa kujituma na kuwajibika ipasavyo zaidi katika soka la vijana kwa kutumia mbinu hizo ili kurudisha hadhi ya mkoa huo kuwa chimbuko la vipaji nchini.

Alisema Chama hicho kitakuwa kikiandaa timu mbalimbali za vijana ambazo makocha wote waliobahatika kupata mbinu hizo za kiufundi watakuwa wakizifundisha kwa kupokezana ili wasiishie kuwa makocha wa vyeti bila ya vitendo.
 
David wants Silva-ware for City






Updated Dec 26, 2010 4:46 AM ET
David Silva has urged Manchester City to get over Monday night's blip against Everton and make sure they stay in the Premier League title race.
City would have celebrated Christmas Day on top of the table for the first time since 1929 had they beaten Everton on Monday, but went down 2-1 at Eastlands.

Sun., Dec. 26
Fulham 1-3 West Ham | Recap
Everton PP Birmingham
Man United 2-0 Sunderland | Recap
Newcastle 1-3 Man City | Recap
Blackburn 0-2 Stoke City | Recap
Bolton 2-0 West Brom | Recap
Wolverhampton 1-2 Wigan | Recap
Blackpool PP Liverpool
Aston Villa 1-2 Tottenham | Recap
Mon., Dec. 27
Arsenal vs. Chelsea BPL Scores | Table | Fixtures

It took Silva a bit of time to adapt after his summer move from Valencia but he is starting to flourish and two City player of the month awards on the trot emphasise what a fans' favourite the Spain star has become.
"I have settled in but I owe a lot to my team-mates because they helped make the process a lot quicker," said Silva, whose side visit Newcastle tomorrow.
"The games in England are very competitive. So many sides can make life very hard for you. It is a real challenge.
"But we are going okay at the moment. Now we must continue so we are in the final shake-up."
Silva knows he could have avoided the snow and given himself Christmas off by staying in Spain - but feels life is much more interesting at Eastlands.
La Liga has shut down for a couple of weeks to give players and fans a break, and an opportunity to enjoy the festivities.
Not so over here, where Silva is about to experience the usual crush of four games in just over a week, which will do so much to shape the season as a whole.
But when the Spain star looks at the comparative league tables - Barcelona and Real Madrid streaking clear back home compared to the jostling for top spot in England - he knows where he would rather be.
"Barcelona and Real Madrid are going well and have built up quite a lead," Silva told the club's website.
"In England it is far more hard fought. You could have any number of teams getting up there near the top.
"That makes for a more entertaining and enjoyable league."
Monday's defeat to Everton, in freezing temperatures, has led to accusations that the Blues' expensively-assembled, cosmopolitan band, only show their best form in milder weather.

WHAT A YEAR!




 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom