Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Gumbo aitwa kuziba pengo la Henry
Tuesday, 28 December 2010 21:44

machupa.jpg
Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Mrisho Ngassa akichuana na Athuman Machupa wakati wa mazoezi ya timu hiyo janakwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Sosthenes Nyoni
BENCHI la ufundi la timu ya taifa ya Tanzania,Taifa Stars limemwondoa kikosini kiungo Henry Joseph na kumwita kwa mara ya kwanza nyota wa Simba, Rashid Gumbo kuziba nafasi yake.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Sunday Kayuni alisema kiungo wa Kongsvinger ya Sweden, Henry Joseph ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kutoa taarifa ya kuwa na matatizo ya kifamilia nyumbani kwao Mwanza.

"Kwa ujumla timu inaendelea vizuri na wachezaji karibu wote wameisharipoti,"alisema Kayuni.

"Isipokuwa kuna mabadiliko kidogo katika kikosi nayo ni kwamba nimepokea taarifa kutoka benchi la ufundi kuhusiana na kuondolewa kwa Henry Joseph ambaye ana matatizo ya kifamilia na nafasi yake sasa itachukuliwa na Rashid Gumbo," alisema Kayuni.

Alisema baada ya kupokea taarifa hizo benchi la ufundi lilifikia uamuzi wa kumwondoa katika kikosi hicho ili kumpa muda zaidi wa kutatua matatizo yake na kupendekeza kuitwa kwa kiungo chipukizi wa Simba, Gumbo aliyefunga mabao 5 msimu huu kwenye Ligi Kuu.

Gumbo ambaye aliisaidia Simba kumaliza mzunguko wa kwanza wakiwa vinara kwa kutoa pasi zote za mwisho kwenye ushindi wao dhidi ya Majimaji, alipoulizwa juu ya mtazamo wake baada ya kuitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars alisema,

"'Kuitwa kwenye timu ya Taifa kuna mambo mengi sana yanaangaliwa na pia kocha ni binadamu mwenye utashi wake, mtazamo, mbinu, upenzi na mitazamo yake pia.

"Hivi vyote vinapaswa kuheshimiwa katika utezi wa mchezaji, kuna watu enzi za Marcio Maximo walikuwa hawakosi Stars, lakini, leo hii hawapo tena,ninachosema tumpe muda kocha najua ipo siku ataniona na kukubali uwezo wangu basi ataniita tu."

Akizungumzia uteuzi wake jana Gumbo ambaye hadi Mwananchi inawasiliana naye alikuwa bado hajapata taarifa rasmi alisema,

"Namshukuru Mungu kwa sababu hakuna mchezaji asiyependa kuichezea nchi yake, nafikiri nahitaji kutumia michezo hii kwa ajili ya kujitangaza kimataifa Mungu akipenda na mimi nitapata timu ya kucheza nje ya nchi.

"Kila mchezaji hapa Tanzania anatamani kucheza soka ya kulipwa najua nikicheza vizuri na kuonyesha uwezo wangu wote nitafungua milango yangu.

"Mchezaji wa kulipwa ni mvumilivu na anajua nini anachotakiwa kufanya uwanjani kwani anajua maisha yake yanategemea mpira hivyo asipojituma atapoteza ulaji wake, lakini sisi wa ridhaa hatupo hivyo kabisa labda kwa sababu ya malipo kidogo na kutoheshimika."

Aidha Kiungo huyo wa zamani timu ya African Lyon alisisitiza ushirikiano miongoni mwa wachezaji wa timu hiyo ili waweze kufikia matarajio ya Watanzania.

 
Mdudu wa rushwa anukia uchaguzi ZFA
Tuesday, 28 December 2010 21:39

Vicky Kimaro
WAKATI uchaguzi mkuu wa Chama cha Soka Zanzibar, ZFA umepangwa kufanyika Ijumaa kwenye kisiwa cha Pemba, kumeibuka mizengwe kwa baadhi ya wagombea wakidaiwa kutoa shilingi 500,000 kwa wapiga kura.

Habari za uhakika ambazo Mwananchi imezipata zinasema kuwa wagombea wawili wanaowania nafasi ya rais na makamu wa rais wametoa fedha hizo juzi kwenye kikao chao maalum na viongozi wa soka wa Wilaya nne za Pemba ambazo ni Chake Chake, Kwahani, Wete na Micheweni.

Chanzo hicho kimesema kuwa kikao hiko kilifanyika kwenye ukumbi wa Gombani Pemba na inadaiwa kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya mpira katika wilaya hizo ikiwa ni pamoja na kujenga magoli na kununulia mipira na pia wameahidiwa iwapo watawachagua watajengewa ofisi bora ikiwa ni pamoja na kuwekewa thamani za ofisini.

"Sasa hivi kuna mvutano wa kupokea wapiga kura wanaotoka Unguja, wajumbe wanakuja Alhamisi na ZFA imeandaa basi maalum la kuwapokea na pia imewaandalia hoteli, lakini cha kushangaza wagombea hao wa Rais na Makamu wake nao wameandaa basi la kuwapokea..."

Hata hivyo wakati wagombea hao wakinadi sera zao kwa wapiga kura wa Pemba kwenye ukumbi wa Gombani, Rais anayetetea kiti chake Ally Fereji Tamim naye aliweka kikao chake na wapiga kura wa Unguja na kuwataka wapige kura kwa kuchagua kiongozi bora na mwenye uzoefu na wasikubali kurubuniwa.

Wagombea 10 wanaowania nafasi ya Rais, Makamu wa Rais wa Zanzibar na Pemba ni Ali Ferej Tamim anayetetea kiti chake, Hafidh Kassim Hafidh, Nurdin Zakaria Taib, Suleiman Mahamoud Jabir na mtangazaji wa kituo cha Channel Ten, Munir Zakaria.

Nafasi ya Makamu wa rais kwa Unguja inawaniwa na Ali Khatib Dai, Ameir Haji Ameir ‘Bosi Mpakia' na Aman Ibrahim Makungu wakati kwa upande wa Pemba inawaniwa na Ali Mohamed na Suleiman Amour Suleiman.

Kampeni za uchaguzi huo zilianza Desemba 26 na zitafikia tamati Desemba 30 wakati uchaguzi mkuu umepangwa kufanyika Desemba 31.
 
Mtibwa, Majimaji leo, Lyon yaishika Yanga
Tuesday, 28 December 2010 21:37

Doris Maliyaga na Sweetbert Lukonge
KOCHA wa Mtibwa Sugar U-20, Mecky Mexime amesema vijana wake wameiva na wataiondoa Majimaji leo, huku Yanga ikilazimishwa suluhu na African Lyon kwenye michuano ya Uhai Cup inayoendelea kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.

Mtibwa iliyoshika nafasi ya tatu kwenye michuano iliyomalizika mwaka jana na Azam FC kuibuka mabingwa, inacheza na Majimaji ikiwa ndiyo mchezo wao wa kwanza tangu kuanza kwa michuano hiyo.

Mexime ameiambia Mwananchi kuwa vijana amewwandaa vijana wake vilivyo na malengo yao safari hii ni kuibuka mabingwa.

''Timu ni nzuri tumejiandaa vya kutosha kuona tunamaliza mashindano tukiwa mabingwa na si kumaliza chini ya hapo,''alisema Mexime ambaye pia ni kocha msaidizi wa Mtibwa ya wakubwa.

''Tukiwa nyumbani tulijiandaa vema tukicheza mechi mchanganyiko za kirafiki ninazoamini zimewaimarisha vijana hawa zaidi na zaidi na upo uhakika wa kuwafunga Majimaji ,''aliongeza Mexime.

Kikosi hicho cha Mtibwa U-20 pia kinafundishwa na kocha mwingine ambaye ni mchezaji na nahodha wa zamani wa Mtibwa,Godfrey Magoli.

Timu za vijana za Yanga na African Lyon jana zilishindwa kutambiana kwenye Uwanja wa Karume kwa kutoka suluhu.

Katika mchezo huo ambao uliokuwa na ushindani mkubwa, timu zote
zilionyesha upinzani mkali katika dakika zote za mchezo huo uliomalizika kwa suluhu.

Lyon walitawala zaidi katika kipindi cha kwanza hasa sehemu ya kiungo, lakini washambuliaji wake walikosa umakini kwenye umaliziaji. Yanga ilijaribu kujibu mapigo, lakini kipa wa Lyon alikuwa makini kuokoa hatari zote.

Katika mechi nyingine za ufunguzi wa mashindano hayo zilizofanyika juzi katika uwanja wa Karume timu ya Ruvu Shooting ilifanikiwa kuyaanza vema mashindano hayo baada kuitandika Azam FC mabao 4-3 wakati Polisi Dodoma ilitoka sare ya mabao 2-2 na AFC ya Arusha.

 
Malipo mwakani Tuesday, 28 December 2010 21:38

Clara Alphonce
KAMATI ya Utendaji ya Yanga imewaahidi wachezaji wao kuwalipa fedha zao wanazodai kabla ya Januari 10 na kuwasihi wasifanye mgomo wao.

Hivi karibuni wachezaji wa klabu hiyo waliwagomea viongozi kufanya mazoezi kwa siku mbili kwa madai kuwa mpaka walipwe fedha zao milioni 70 wanazoidai klabu hiyo.

Kamati hiyo ilikutana juzi saa 11:00 asubuhi na kujadili mambo mbalimbali yakiwemo maandalizi ya michuano ya kimataifa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania bara pamoja na madai ya wachezaji wao.

Hata hivyo kamati hiyo iliwataka wachezaji wao kusitisha mgomo ambao walikuwa wamepanga kuufanya kwani kwa sasa uongozi unashughulikia masuala yao na kabla ya Januari 10 watakuwa tayari wamelipwa fedha zao wanazodai.

Mbali na suala hilo pia waliongelea suala la mchezaji wao Athuman Idd 'Chuji' ambapo walikubaliana kuwa wasubiri ripoti ya kocha wao Kostadin Papic ndipo watolee maamuzi.

Hata hivyo Papic awali alishawaambia viongozi wake kuwa angependa mchezaji huyo akapimwe akili yake kutokana na utovu wa nidhamu anaouonyesha.

Papic alifikia kusema maneno hayo baada ya wiki iliyopita mchezaji huyo kutoka mazoezini na kwenda kukaa nje bila kutoa taarifa yoyote kwa kocha huyo kitu kilichomfanya avunje mazoezi siku hiyo.
 
Viingilio poa Mapinduzi
Tuesday, 28 December 2010 21:36

Vicky Kimaro

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi imepangwa kuanza kutimua vumbi Jumapili ijayo,ambapo mechi ya ufunguzi itakuwa ni kati ya Chuoni dhidi ya Azam Fc, huku viingilio vikiwa ni shilingi 1,000 na 3,000.

Akizungumza na Mwananchi, msemaji wa kamati ya maandalizi ya mashindano hayo Maulid Ahmed Maulid alisema tayari timu ya Simba imeshawasili na kuweka kambi kwenye nyumba za Zakaria zilizopo Chukwani visiwani humo.

Simba imeenda Zanzibar kwa mafungu, fungu la kwanza liliondoka juzi likiwa na wachezaji 13 na viongozi watano wakati fungu la pili lilitarajiwa kuondoka jana likiwa na wachezaji tisa.

"Simba wamewahi kuja watajigharamia wenyewe mpaka Januari Mosi ndio sisi tutaanza kuwalipia gharama za kambi, Yanga, Azam na Jamhuri Pemba zitawasili Januari Mosi," alisema Maulid.

"Mtibwa itawasili visiwani humu Januari 2 na timu za Zanzibar ambazo ni Chuoni, KMKM na Zanzibar Ocean View zitajitegemea kambi na waandaaji wa michuano hiyo watawapa posho pekee,"alisema Maulid.

Alisema,"Mashindano yanaanza mwishoni mwa wiki hii na kufikia kilele siku ya Mapinduzi Januari 12 na mgeni rasmi atakuwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein."

Siku kabla ya fainali za michuano hiyo ambayo Mtibwa ndio bingwa mtetezi kutakuwa na mechi kati ya wachezaji soka Maveterani wa Bara na wale wa Zanzibar.

"Na katika fainali kutakuwa na mechi ya utangulizi ambapo timu ya soka ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) itacheza na timu ya Baraza la wawakilishi," alisema.
 
Ancelotti: Nakubali kubeba lawama kwa kiwango duni Tuesday, 28 December 2010 21:35

LONDON, Uingereza

KOCHA wa Chelsea, Carlo Ancelotti amekubali kubeba lawama kwa kuporomoka kiwango cha klabu yake, Chelsea.

Alisema juzi usiku baada ya kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Arsenal kwenye Uwanja wa Emirates na kukiri kuwa presha kwake imezidi kupanda.

Kutokana na kipigo hicho, mabingwa hao watetezi wamezidi kuporomoka licha ya kubakia katika nafasi ya nne wakiwa wamecheza mechi sita bila ushindi katika michuano yote.

Nafasi ya Ancelotti sasa imekuwa shakani, lakini yeye anasema kuwa hana shaka.

"Sijui ni kwa muda gani mmiliki wa klabu hiyo, Roman Abramovich ataendelea kuwa na subira nami. Sina shaka kwamba hana furaha kwa sasa ,'' alisema Ancelotti . "Nitawajibika, lakini hili ni swali ambalo kila mtu anatakiwa kujiuliza, siyo mimi.

"Sina wasiwasi kuhusiana na kazi yangu . Kila mmoja amesema kuwa nilifanya kazi nzuri msimu uliopita . Kwa sasa watu wanahoji nin kazi yangu. Tunatakiwa kufanya vizuri, sina shaka kwamba tutajitahidi. Si jambo la kawaida kwa Chelsea kukosa ushindi kwenye mechi sita.''

Arsenal imerejea katika nafasi ya pili baada ya mabao ya Alex Song, Cesc Fabregas na Theo Walcott yaliyomaliza matokeo mabaya ya mechi tano ambazo walifungwa na Chelsea, wapinzani wao wa London.

Branislav Ivanovic alifunga la kufutia machozi kwa Chelsea, lakini Chelsea walicheza mchezo mbaya na Ancelotti alikiri kuwa timu yake inatakiwa kuzinduka.

"Sina wasiwasi, hakuna shaka, kwani mechi sita hatujashinda,'' alisema . "Sifurahii kuona timu yangu ikicheza vibaya kiasi kile, hatuchezi kama tunavyotakiwa, intakuwa vigumu kucheza soka.''

"Tunajiamini, lakini si kwa jinsi ambavyo tunacheza. Sikutarajia kipigo hiki. Nilishangazwa na mchezo wetu. Niliwaeleza wachezaji wangu wajitahidi mazoezini, lakini walivyocheza.

Ancelotti aliungwa mkono na mwenzake wa Arsenal, Arsene Wenger, ambaye alisema: "Binafsi ninamheshimu Ancelotti ni mzoefu ana ujuzi katika kazi yake, hana wasiwasi na kazi yake".

Mchezo wa juu ulikuwa muhimu kwa Arsenal na ushindi huo kwake umezidisha ushindani baina yake na Manchester United, Chelsea na Man City kuwania ubingwa msimu huu.

Wenger alikiri kwamba matokeo yamezidisha matumaini kwa vijana wake, wanajiamini baada ya awali kuruhusu mabao 13 katika mechi tano dhidi ya Chelsea, kitu ambacho Wenger alisema kuwa wamejirekebisha.

"Matokeo haya yana maana mbili. Kimahesabu, tumebaki kati za zile zinazosaka ubingwa,''alisema Wenger . "Kisaikolojia, ulikuwa ushindi muhimu. Tulihojiwa kuhusu uwezo wetu wa kushinda.

"Nina furaha na aina ya timu yangu na tamaa yake ya ushindi. Tumeonyesha pia nidhamu kwa dakika 90 na tunacheza kama timu. Miaka miwili iliyopita tulikuwa na wachezaji wale wale walikuwa vijana walitishwa na Chelsea. Mwaka jana, tulianza kupanda.

"Mwaka huu, kule United na tena kwa Chelsea, tulikatishwa tamaa licha ya kucheza zaidi na tofauti inaweza kuonekana. Pengine tulicheza kwa tahadhari. Taratibu tunajifunza, tumeonyesha hilo juzi.

"Cesc Fabregas alisema pengine tunaogopa kushinda. Ni maneno mazitom, lakini yamewachochea wenzake . Haikuwa hivyo juzi usiku. Ulikuwa mchezo mgumu."
 
Eto'o aombea amani nchini Ivory Coast Tuesday, 28 December 2010 21:34

YAOUNDE, Cameroon
MCHEZAJI bora wa mwaka wa Afrika, Samuel Eto'o amepigania amani katika nchi jirani ya Ivory Coast ambayo imekumbwa na mzozo mkubwa.

Mchezaji huyo raia wa Cameroon ambaye anaichezea Inter Milan ameeleza kuwa hali ya sasa ya siasa nchini mwake yanashtua.

Kulingana na mtandao wa Sport365.fr, Eto'o amewataka wanasiasa wa nchi hiyo kutatua matatizo yao kwa njia za amani na kujiepusha na mambo ambayo yanahatarisha maisha.

"Kikubwa zaidi, ninamwomba Mwenyezi Mungu aingilie kati hali nchini Ivory Coast, alete amani na kuwalinda raia wa nchi hiyo na kuwaepusha na maovu,"alisema.

Eto'o ana mke mwenye asili ya Ivory Coast, aitwaye Georgette, ambaye amezaa naye watoto watatu.

Naye mshambuliaji raia wa nchi hiyo, Didier Drogba ameta kauli kama ile ya Eto'o wiki moja iliyopita.

Beki wa Manchester City, Kolo Toure ambaye pia anatoka nchi hiyo amesema mawazo ya Drogba ni yake binafsi hakuwahi kuwasiliana naye kabla ya taarifa ile.

Vyombo vya habari vya Ivory Coast vimekuwa vikitafsiri kauli za wachezaji hao wawili kupingana na kuzilinganisha na viongozi wa nchi hiyo kama mwanzo wa machafuko baina ya wananchi wa nchi hiyo wa kusini na kaskazini.

Drogba anatokea kusini wakati Kolo ni mzaliwa wa kaskazini, ingawa hakuna ambaye alishaeleza msimamo na fungamano lake katika siasa.
 
Gumbo amrithi Henry Joseph Stars


na Makuburi Ally


amka2.gif
KIUNGO mshambuliaji wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ya jijini Dar es Salaam, Rashid Gumbo, ameteuliwa kuziba nafasi ya mchezaji wa kimataifa, Henry Joseph, aliyepata matatizo ya kifamilia yaliyomsababishia kukosekana katika kambi ya timu ya Taifa 'Taifa Stars' inayotarajiwa kushiriki mashindano ya Nile Basin yatakayoanza kutimua vumbi Januari 5-17 mwakani, jijini Cairo Misri. Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Sunday Kayuni, alisema, hatua ya kumchukua Gumbo wamekubaliana na Kocha Msaidizi wa Stars, Marsh Sylvestre.
Kayuni alisema, wachezaji wengine wako kambini kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo, ambapo wanajifua asubuhi na jioni.
Aidha Kayuni alisema, kuhusu hatua ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Januari 15, TFF inasubiri majibu ya maombi ya kutumia viwanja vya Dar es Salaam kwa hatua za mwisho za ligi hiyo.
Kayuni pia aliongeza kuwa Stars inatarajiwa kushiriki 'All African Games' ambako itakutana na Uganda 'The Cranes' kati ya Aprili 15 na 17 mwakani, wakati mchezo wa marudiano utapigwa Aprili 29 na Mei 1 mwakani.
 
Yanga yalainika kwa Abdi Kassim 'Babi'


na Juma Kasesa


amka2.gif
BAADA ya kutangaza dau la sh milioni 100 kumuuza kiungo wake Abdi Kassim 'Babi' hatimaye Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam imelainika na iko radhi kumuachia kwa dola 40,000 za Marekani kwenda kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya DT Long ya Vietnam. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa klabu hiyo, Llyod Nchunga, Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo iliyoketi jijini Dar es Salaam juzi, imeridhia Babi kukipiga DT Long kwa lengo la kufungua milango kwa wachezaji wengine kupata nafasi ya kucheza soka ya kulipwa na kuitangaza Tanzania kimataifa.
'Tunaamini kumuuza Babi ni kufungua milango kwa wachezaji wetu kupata nafasi ya kucheza soka la kulipwa katika klabu mbalimbali duniani na ndiyo malengo ya Yanga, kuitangaza klabu na nchi,'� alisema Nchunga ambaye kitaaluma ni mwanasheria.
Iwapo DT Long wataafiki dau hilo la Yanga, Babi atakuwa Mtanzania wa pili kukipiga katika timu hiyo akiungana na mshambuliaji Danny Mrwanda ambaye anachezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo maarufu kwa jina la V-League.
Nchunga aliongeza kuwa, wanasubiri mawasiliano ya mwisho na klabu hiyo ili waweze kumwachia kiungo huyo ambaye aliisadia timu ya Taifa ya Zanzibar 'Zanzibar Heroes' katika mashindano ya kombe la Tusker Chalenji Cup yaliyomazika hivi karibuni.
Aidha, Nchunga alisema, Kamati ya Utendaji pia imeridhia Yanga kucheza Kombe la Mapinduzi kwa ajili ya kujiimarisha na Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa.
 
Hatma ya Kaseja TFF Jan. 4


na Makuburi Ally


amka2.gif
KAMATI ya Rufaa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), inatarajiwa kukutana Januari 4 kwa ajili ya kujadili rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa klabu ya Simba kupinga adhabu juu ya kipa wake Juma Kaseja. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Sunday Kayuni, alisema, Kaseja aliadhibiwa kutocheza mechi tatu na faini ya sh 500,000 na Kamati ya Mashindano ya Ligi Kuu Tanzania bara, kwa madai ya kutowapa mkono wachezaji wa Yanga katika mchezo kati ya mahasimu hao wawili uliopigwa jijini Mwanza.
Kayuni alisema, awali kamati hiyo ilikuwa iketi Jumamosi iliyopita, lakini kutokana na kutotimia kwa akidi imebidi sasa ikutane Januari mwakani.
Katika hatua nyingine, Kayuni alisema, TFF imepokea barua kutoka kituo cha michezo cha AFC Athletics Football Club ya Sweden, kumhitaji mchezaji Yusuf Soka ili akapate mafunzo katika kituo hicho.
Kayuni alisema, wataketi na mchezaji huyo na klabu yake ili kulizungumza suala hilo ambalo ni la maendeleo ya soka la Tanzania.
 
Kaseja awekwa kiporo TFF

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 28th December 2010 @ 23:55


Mmoja aachwa, mwingine aitwa Stars
Imeandikwa na Betram Lengama; Tarehe: 28th December 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 258; Jumla ya maoni: 0


12_10_qyafub.jpg

Wachezaji wa Taifa Stars Saidi Maulidi (SMG) anayecheza soka ya kulipwa Angola na Athumani Machuppa anayecheza Sweden wakifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam jana, huku makocha wasaidizi wa Stars Juma Pondamali (kushoto) na Silvestre Marsh wakiwafuatilia. Stars iko kambini kujiandaa na michuano ya Mto Nile inayotarajiwa kufanyika Januari mwakani mjini Cairo, Misri. (Picha na Yusuf Badi).




Kwa mujibu wa Kayuni kutokana na uamuzi huo benchi la ufundi la timu hiyo limeamua kumwita kiungo mahiri wa klabu ya Simba Rashid Gumbo katika kikosi hicho ili kujaza nafasi hiyo.

"Henry Joseph ameshindwa kujiunga na kambi ya Taifa Stars kutokana na kukabiliwa na matatizo ya kifamilia na hivi sasa yuko kwao Mwanza akishughulikia matatizo hayo hivyo basi kutokana na suala hilo imebidi aondolewe kwenye kikosi hicho na nafasi yake sasa itachukuliwa na Rashid Gumbo," Kayuni alisema.

Aidha Kayuni amebainisha kuwa wachezaji wote wengine walioitwa kwenye kikosi hicho wamekwisharipoti kambini na wanaendelea vyema na maandalizi ya michuano hiyo chini ya Kocha Marsh.

Kocha Mkuu wa Stars Poulsen anatarajiwa kuungana na kikosi hicho Misri Januari 3. Wakati huohuo TFF imetoa ufafanuzi juu ya ushiriki wa Tanzania kwenye michezo ya Mataifa ya Afrika (All Africa Games) ambayo fainali zake zitafanyika Msumbiji.

Kwa mujibu wa TFF, Tanzania haitocheza kwenye raundi za awali ya kusaka tiketi ya kwenda Msumbiji na imepangwa kuanza raundi ya kwanza ambapo itakumbana na Uganda mchezo wa kwanza ukifanyika kati ya Aprili 15 na 17 na ule wa marudiano utafanyika Aprili 29 au Mei 2.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom