Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #3,421
Wasanii Moro kuhamasisha Katiba mpya
na Joseph Malembeka, Morogoro
MJADALA wa haja ya kuandikwa Katiba mpya hapa nchini umeingia katika hatua nyingine baada ya taasisi isiyo ya kiserikali ya 'Tanzania Youth Culture Development Centre (TYCDC), ya mjini hapa kukusudia kuanzisha shindano la msanii bora wa maandalizi ya katiba mpya kupitia sanaa. Mwenyekiti Mtendaji wa TYCDC, Mwajabu Kibwana alisema hayo mjini hapa na kuongeza kuwa, lengo la kituo hicho kuanzisha mpango huo ni kuongeza msukumo kwa wananchi kuielewa, ili washiriki vema katika kutoa maoni sahihi jinsi wanavyotaka katiba hiyo iwe.
"Mbali na ufafanuazi wa Katiba katika mpango kazi huu tunaotaraji kuuanza mwezi ujao, tumekusudia pia kuibua nyimbo za mambo ya kitaifa yanayogusa maisha ya watu, kama kukomesha rushwa, ufisadi na masuala ya uchaguzi na zile za mapenzi ambazo zimezoeleka," alisema Mwajabu.
Mwajabu alisema, mbali na kufanya kazi ya kurekodi na kuzitangaza kazi za wasanii nchini, Taasisi hiyo ilitathimini na kubaini kuwa, ipo haja kwa wasanii hususan muziki na maigizo kushirikishwa katika mchakato huo wa mapambano.
Alisema, tayari wasanii mbalimbali maarufu nchini kutoka mkoani hapa na mikoani, wameonyesha ari ya kushirikisha vipaji vyao katika mchakato huo, akiwamo ‘Mchizi Koto'.
Hii ni taasisi ya pili kuanzisha mashindano mkoani hapa, ambako mbali na kuanzishwa kwa ajili ya kurekodi na kuzitangaza kazi za wasanii, pia inajihusisha na uboreshaji sanaa mkoani hapa.
na Joseph Malembeka, Morogoro
"Mbali na ufafanuazi wa Katiba katika mpango kazi huu tunaotaraji kuuanza mwezi ujao, tumekusudia pia kuibua nyimbo za mambo ya kitaifa yanayogusa maisha ya watu, kama kukomesha rushwa, ufisadi na masuala ya uchaguzi na zile za mapenzi ambazo zimezoeleka," alisema Mwajabu.
Mwajabu alisema, mbali na kufanya kazi ya kurekodi na kuzitangaza kazi za wasanii nchini, Taasisi hiyo ilitathimini na kubaini kuwa, ipo haja kwa wasanii hususan muziki na maigizo kushirikishwa katika mchakato huo wa mapambano.
Alisema, tayari wasanii mbalimbali maarufu nchini kutoka mkoani hapa na mikoani, wameonyesha ari ya kushirikisha vipaji vyao katika mchakato huo, akiwamo ‘Mchizi Koto'.
Hii ni taasisi ya pili kuanzisha mashindano mkoani hapa, ambako mbali na kuanzishwa kwa ajili ya kurekodi na kuzitangaza kazi za wasanii, pia inajihusisha na uboreshaji sanaa mkoani hapa.