The Boldly
JF-Expert Member
- May 21, 2017
- 2,377
- 5,147
- Thread starter
- #21
Dar es Salaam. Haruna Niyonzima anakiri kwa sasa hana furaha ndani ya Simba kwa vile hachezi, ila anafichua pia hakuondoka Jangwani kwa ugomvi hivyo kama klabu yake hiyo ya zamani itamtaka hana noma kurejea tena kikosini kupiga mzigo.
Kiungo huyo fundi alisema kilichomuondoa Yanga ni kushindwana masilahi, lakini hata leo wakitaka kumrejesha kwa kile alichokuwa akikitaka hana kinyongo kutua Jangwani kwani ni klabu anayoiheshimu na aliyoitumikia kwa mafanikio.