Hajajib ila nimsaidie, swal la jamaa halikulenga kufanya mmea utoe maua, kufukuzia Moshi mmea husaudia mti wa matunda kutoa maua, hii ni kwa sababu moshi una kuwango kizur cha ethylene ambayo mmea ukichukua huyo ethlene huchochea uzalishaji wa maua.
mmea ni kitu chenye akil sana ndio maana huwez kukuta mmea unaokula maisha mazur ukazaa. Ili mmea uweze kutoa matunda unahitaji stress kama ukame kidogo, jua kali upunguf wa maji hapo mmea utaona unatoa maua kwa sababu unatambua naelekea kufa na bila kufa lazima niache watoto ndio maana unazaa maua. Mfano mzur Mahindi, yakipigwa na mvua hunawil sana na hukua vizur ila jua likawaka gafla na wenyew haujakomaa bas utatoa maua ukiwa vile vile mdogo unakuta mmea wa muhindi mdogo ila una mbele wele.
Majibu yangu ya swali:
Mti wowote wa matunda ni kawaida sana kupukutisha maua. Hiyo ni nature kwa sababu fikiria kila ua linalizalishwa na muembe bas embe litoke unadhan nn kitatokea Matawi yatakatika kwa kuzidiwa uzito, Ndio maana nasema mmea una akil pia. Kutunza maua na maembe kunahitaji kuwa na nutrient za kutosha na maji pia hali ya hewa nzur but mmea ukiona hapa siwez lea haya matunda bas automatical utapukutisha maua na kubakiza yale tu ambayo mmea utaweza kulea hii hutokea natural tu.
ila kuna sababu zingine husababishwa na baadhi ya vitu mfano, wadudu wa maua, Maginjwa hasa ukungu, Na Management tu za mkulima kuwa mbovu shamban, Jua kali kupita kiasi, Upepo mkali. So hiv vitu kuna ambavo mkulima anaweza kucontrol na vingine hawezi Mfano Hali ya hewa mkulima huwez kucontrol hili maana huwez sema utajengea Green house ya muembe no huwezi sana sana utamwagilia maji mengi lakin jua likizid sana na upepo nao ukizid lazima maua yadondoke mengi tu sometime karibia yote.
Kwa magonjwa na wadudu utahitajika kupiga dawa. Kama sio mtaalam bas piga picha peleka Kwa mtaalam yoyote akushauri dawa nzuri ya kutumia.
Nadhan kwa maelezo hayo nimeeleweka. Muwe na kazi njema.