Shida wafanyabiashara wanawauzia NFRA. Serikali kununua haya mazao lengo ni kuwapa soko wakulima.
Na sijui kwa nini mkurugenzi wa NFRA hawasimamii mameneja wake kuzingatia hili.
Mkulima ndiye anatakiwa aiuzie NFRA, siku serikali ikiamua kusimamia hili kuna watu watafilisika.
Magufuli aliwanyoosha kwenye korosho kwa kufanya uhakiki kama kweli ni mkulima.
Hii inabidi iwe kwa mazao yote yanayonunuliwa na NFRA, ni lazima uwe mkulima ili uweze kuuza NFRA.
Haya malalamiko huwezi kuyasikia, isipokuwa hawa traders ndio vimbelembele tu. Ole wenu, nasema tena ole wenu. Nimewafungulia code, kilio kipo jirani.