sembo
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 4,350
- 3,451
Mnamo 01.04.2015 Klabu ya Simba S.C iliingia mkataba wa MIAKA MITANO na kampuni EAG Group Limited ambao utahusu kuitafutia na kusimamia biashara au biashara mbadala zinzoiingizia au zitakazoiingizia klabu hiyo Mapato.
Tukiwa tunaelekea kutimiza miezi 6 tangu tuingie mkataba na hii kampuni bora kabisa katika masuala ya kutangaza brand ya kampuni au taasisi, ushauri wa jinsi gani uwekeze.. n.k... EAGGroup imeifanyia yafuatayo Simba S.C mpaka sasa;
22.06.2015: Kuzindua Tovuti ya Klabu.
Lengo kuu la kuzindua tovuti hii [ http://simbasports.co.tz ] bora kabisa kuwahi kushuhudiwa ukanda wa CECAFA ni kukuza mawasiliano na wadau wake mbalimbali hususani; wanachama, wapenzi, vyombo vya habari na wadau wengine muhimu.
Tovuti hii sio tu itaiwezesha Simba kuwapa wadau wake taarifa mbalimbali bali pia itatumika kwa ajili ya uuzaji wa
vifaa na bidhaa mbalimbali za Simba S.C.
Baadhi ya mambo yaliyopo katika website hiyo, hapo 👇👇.
https://www.jamiiforums.com/sports/882018-hongera-uongozi-wa-simba-kwa-website-bora.html
02.07.2015: Kuzindua Kadi za Ki-Electronic.
Kuonesha ni kwa jinsi gani Simba S.C imejipanga, ilizindua kadi mpya, ambapo kila mwanachama atapata bima ya maisha inayojulikana kama "Simba Pamoja".
Bima hii itampatia mwanachama ambaye amelipa malipo yake ya mwaka ya uanachama fedha taslimu zisizopungua Sh. 250,000 ikiwa atapata msiba kwa kufiwa na mtoto, mke au kufariki dunia yeye mwenyewe.
Source: Simba yazindua kadi za ki-electronik
03.07.2015: Kuzindua huduma ya Simba News.
Lengo kuu la huduma hii ni ni kuwapatia wateja wanaotumia mitandao ya Tigo na Voda taarifa zinazoihusu klabu ya Simba popote walipo nchini.
Ili kujiunga na huduma hizi unatakiwa kutuma neno kuu SIMBA kwenda 15460. Utakapo jiunga tu mteja utapokea habari kila siku na utatozwa kiasi cha shilingi za kitanzania 150 kwa siku.
Na kwa siku utapokea kiwango cha chini cha habari nne (04) zina zohusu klabu ya Simba.
Source: MICHUZI BLOG: SIMBA SPORT CLUB YAZINDUA HUDUMA MPYA YA SIMBA NEWS
27.07.2015: Kuzindua uuzaji wa jezi katika Duka la Mtandao.
Mtandao wa Klabu ya Simba kwa kushirikiana na Jumia walizindua huduma ya kununua jezi za Simba kupitia duka la mtandao la Jumia [ www.jumia.co.tz ]. Dhumuni la huduma hii ni kuwapatia wapenzi wa klabu ya Simba njia bora ya kuweza kununua jezi popote walipo
Tanzania.
Jinsi ya kununua Uzi wa Mnyama mtandaoni.. Pita hapa 👇👇
https://www.jamiiforums.com/sports/897211-jinsi-ya-kununua-jezi-za-mpya-za-simba-mtandaoni.html
26.09.2015: Kuzindua Tuzo za mwezi kwa Wachezaji wake.
Katika Tuzo hizo, wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio watakao chagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza kwenda kwenye namba 15460.. na hii ni kwa wale tu ambao wamejiunga na Simba News kupitia mtandao wa Voda na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa Simba.
Source: SIMBA DAMU FANS: SIMBA YAANZISHA TUZO ZA MWEZI KWA WACHEZAJI WAKE
NB: Katika miezi sita tu ya mkataba wao wa miaka mitano.. EAGGroup imeonesha ni kwa jinsi gani imedhamiria kuifanya Simba S.C iwe klabu ya Kiulaya Ulaya [na si kimataifa].
Kama kwa mda mfupi tuu huu Simba S.C imekua mfano wa kuigwa katika ukanda huu wa CECAFA.. sipati picha baada ya miaka mitano, itakua imefika wapi?!
Mungu ibariki EAGGroup, Mungu ibariki Simba S.C.
Tukiwa tunaelekea kutimiza miezi 6 tangu tuingie mkataba na hii kampuni bora kabisa katika masuala ya kutangaza brand ya kampuni au taasisi, ushauri wa jinsi gani uwekeze.. n.k... EAGGroup imeifanyia yafuatayo Simba S.C mpaka sasa;
22.06.2015: Kuzindua Tovuti ya Klabu.
Lengo kuu la kuzindua tovuti hii [ http://simbasports.co.tz ] bora kabisa kuwahi kushuhudiwa ukanda wa CECAFA ni kukuza mawasiliano na wadau wake mbalimbali hususani; wanachama, wapenzi, vyombo vya habari na wadau wengine muhimu.
Tovuti hii sio tu itaiwezesha Simba kuwapa wadau wake taarifa mbalimbali bali pia itatumika kwa ajili ya uuzaji wa
vifaa na bidhaa mbalimbali za Simba S.C.
Baadhi ya mambo yaliyopo katika website hiyo, hapo 👇👇.
https://www.jamiiforums.com/sports/882018-hongera-uongozi-wa-simba-kwa-website-bora.html
02.07.2015: Kuzindua Kadi za Ki-Electronic.
Kuonesha ni kwa jinsi gani Simba S.C imejipanga, ilizindua kadi mpya, ambapo kila mwanachama atapata bima ya maisha inayojulikana kama "Simba Pamoja".
Bima hii itampatia mwanachama ambaye amelipa malipo yake ya mwaka ya uanachama fedha taslimu zisizopungua Sh. 250,000 ikiwa atapata msiba kwa kufiwa na mtoto, mke au kufariki dunia yeye mwenyewe.
Source: Simba yazindua kadi za ki-electronik
03.07.2015: Kuzindua huduma ya Simba News.
Lengo kuu la huduma hii ni ni kuwapatia wateja wanaotumia mitandao ya Tigo na Voda taarifa zinazoihusu klabu ya Simba popote walipo nchini.
Ili kujiunga na huduma hizi unatakiwa kutuma neno kuu SIMBA kwenda 15460. Utakapo jiunga tu mteja utapokea habari kila siku na utatozwa kiasi cha shilingi za kitanzania 150 kwa siku.
Na kwa siku utapokea kiwango cha chini cha habari nne (04) zina zohusu klabu ya Simba.
Source: MICHUZI BLOG: SIMBA SPORT CLUB YAZINDUA HUDUMA MPYA YA SIMBA NEWS
27.07.2015: Kuzindua uuzaji wa jezi katika Duka la Mtandao.
Mtandao wa Klabu ya Simba kwa kushirikiana na Jumia walizindua huduma ya kununua jezi za Simba kupitia duka la mtandao la Jumia [ www.jumia.co.tz ]. Dhumuni la huduma hii ni kuwapatia wapenzi wa klabu ya Simba njia bora ya kuweza kununua jezi popote walipo
Tanzania.
Jinsi ya kununua Uzi wa Mnyama mtandaoni.. Pita hapa 👇👇
https://www.jamiiforums.com/sports/897211-jinsi-ya-kununua-jezi-za-mpya-za-simba-mtandaoni.html
26.09.2015: Kuzindua Tuzo za mwezi kwa Wachezaji wake.
Katika Tuzo hizo, wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio watakao chagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza kwenda kwenye namba 15460.. na hii ni kwa wale tu ambao wamejiunga na Simba News kupitia mtandao wa Voda na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa Simba.
Source: SIMBA DAMU FANS: SIMBA YAANZISHA TUZO ZA MWEZI KWA WACHEZAJI WAKE
NB: Katika miezi sita tu ya mkataba wao wa miaka mitano.. EAGGroup imeonesha ni kwa jinsi gani imedhamiria kuifanya Simba S.C iwe klabu ya Kiulaya Ulaya [na si kimataifa].
Kama kwa mda mfupi tuu huu Simba S.C imekua mfano wa kuigwa katika ukanda huu wa CECAFA.. sipati picha baada ya miaka mitano, itakua imefika wapi?!
Mungu ibariki EAGGroup, Mungu ibariki Simba S.C.
