Miezi 9 imetimia lakini mtoto hajageuka tumboni

Hyo ultra sound ilionyesha mtoto yuko kawaida au ilikuwaje?
Maana wanawake wengi hupitiliza siku ambazo hufikiria zimetimia
KIPIMO KIPO VIZURI AKATUONYESHA KUANZIA KICHWA HADI MIGUU YUPO SAWA!
 
SERIOUS NDUGU! NAMPELEKA LEO
 
Ujauzito hauhesabiwi kwa miezi zinahesabiwa week , hiyo miezi 9 yaweza kua wiki 36,37,38 au 39 na hizo zote zina maana tofauti kuhusu ukomavu wa mtoto , fika hospitali wape tarehe ya mwisho ya kuona hedhi watakuhesabia wiki ,then kitafanyika kitu kinaitwa "breech score" kuangalia kama ataweza kujifungua kawaida au atahitaji upasuaji. Lakini kwa umri huo wa miezi 9 mtoto hageuki tena room ni ndogo.
 
Kitaalamu Bado Kuna chance ya kuendelea kugeuka, Lakini Kwa ushauri wa kitabibu... Aende akajitazamie/Akajifungue Kwenye Hospital Kubwa yenye vifaa na wataalamu wenye ujuzi zaidi Kwa dharura yoyote.
 
Kama ni Breech presentation, delivery is possible without any complications.
Ishu nyingi za Radiology inategemea na msomaji..... Naomba nirudie kwa herufi kubwa

ISHU NYINGI ZA RADIOLOGY DEPARTMENT INATEGEMEA NA MSOMAJI

nenda katika taasisi nyingine fanya comparison ya majibu husika

Kama mtoto ka present tofauti it's better uje aina ya position plus aina ya delivery

All the best
 
Naongea kwa experience ..Watoto wangu 2 walikua na ishu kama yako..hawakugeuka mpaka muda unatimia na walipitiliza kidogo...the only option ilikua ni upasuaji na wakatoka salama. Hii ilipendekezwa na madaktari bingwa wa Muhimbili na Selian ambako walizaliwa kwa wakati tofauti na miaka tofauti. So brother onana na madaktari bingwa mapema watakusaidia sana, hili jambo hutokea. Kila la kheri.
 
SHUKRANI WAPENDWA! NIMEENDA HOSP WANAITA KITONKA SI MBALI SANA NA HOME! AMEFANYIWA TENA ULTRASOUND, NIMEAMBIWA MAKADIRIO YAKE MBAKA TAREH 22 MWEZI HUU! NIMEAMBIWA NIONDOE HOFU, NI HALI YA KAWAIDA! ILA TAREHE 11 TUNARUD TENA
 
Watoto wanaozaliwa wametanguliza miguu wenyewe inakuwaje ?
 
SHUKRANI WAPENDWA! NIMEENDA HOSP WANAITA KITONKA SI MBALI SANA NA HOME! AMEFANYIWA TENA ULTRASOUND, NIMEAMBIWA MAKADIRIO YAKE MBAKA TAREH 22 MWEZI HUU! NIMEAMBIWA NIONDOE HOFU, NI HALI YA KAWAIDA! ILA TAREHE 11 TUNARUD TENA
Wewe acha kujidanganya na hayo mahosptal binafsi. Mpeleke mwananyamala waelezee tatizo wakiona nikubwa atafanyiwa oparesheni haraka sana, na kama ni kubwa zaidi atapelekwa muhimbili. Nimekuambia mwananyamala sio amana wala temeke. Wife wangu mimba ya 4 wakati muda haujafika ni miezi 8 waliona kuna tatizo kwa mama ikabidi aambiwe ajiandae kuwekewa dripu la uchungu kwani kuna tatizo.ukiona hosp kubwa nako wamekuambia hakuna tatizo basi ondoa hofu
 
SHUKRANI MKUU
 
Ashukuriwe mungu! Mke wangu amejifungua salama salmini..! Nawashukuru wote mlionipa support ya ushauri na maarifa kwenye uzi wangu nilioomba msaada wa fikra na ushauri juu ya kupita siku za kujifungua kwa mama mtoto wangu! Amefanikiwa kujifungua jana mtoto wa kiume! Bila upasuaji wowote.

Namshukuru Mungu naitwa baba....
 
Mungu ni mwema sana
 
Hongera sana. Japo nilichelewa kuona uzi. Nina uhakika umepata experience kubwa hata kwenye uzao ujao
 
Hongera sana. Japo nilichelewa kuona uzi. Nina uhakika umepata experience kubwa hata kwenye uzao ujao
kweli bi dada! ila nimeambiwa na mke wangu mtoto alikuwa mvivu kugeuka! mbaka dk za mwisho hakugeuka! akalazimisha mazoezi akafanikiwa, lakini bdo kidogo sana apelekwe theater
 
Hongera mzee,pole kwa wife....
 
Hongera sana
Mungu ni mwema sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…