Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Mwezi wa kumi na mbili (December) na mwezi wa kwanza (January), ni miezi inayofanya jamii kutumia pesa sana na upande wa pili kunufaika sana.
Kwenye nyumba za ibada huwa ni msimu wa mavuno, huku upande wa pili ukiwa ni kugharamia (kutoa/kupoteza).
Kwenye majengo ya starehe, mapato yanaongezeka huku mwingine akiwa anapoteza.
Kwenye vyombo vya usafiri, abiria wanaongezeka na mapato kuongezeka pia.
Wamiliki wa mashule, hawa wanatamani mwezi wa kwanza ufike kwa haraka zaidi ili waweze kukusanya mamilioni. Huku wazazi na walezi wakitamani mwezi wa kwanza usifike kwa haraka ili waweze kujichanga upya katika ulipaji wa ada.
Kwa ujumla, wengi huwa wanasema mwezi wa kwanza ni mgumu, ila ni mwezi mzuri kwa wanaomiliki mashule, na wanatamani ufike haraka sana.
Kwenye nyumba za ibada huwa ni msimu wa mavuno, huku upande wa pili ukiwa ni kugharamia (kutoa/kupoteza).
Kwenye majengo ya starehe, mapato yanaongezeka huku mwingine akiwa anapoteza.
Kwenye vyombo vya usafiri, abiria wanaongezeka na mapato kuongezeka pia.
Wamiliki wa mashule, hawa wanatamani mwezi wa kwanza ufike kwa haraka zaidi ili waweze kukusanya mamilioni. Huku wazazi na walezi wakitamani mwezi wa kwanza usifike kwa haraka ili waweze kujichanga upya katika ulipaji wa ada.
Kwa ujumla, wengi huwa wanasema mwezi wa kwanza ni mgumu, ila ni mwezi mzuri kwa wanaomiliki mashule, na wanatamani ufike haraka sana.