Mifumo ya kidunia ilishaamua mwanaume aishi kwa kukandamizwa na kufanyiwa ulaghai/ udanganyifu

Basi dada angu ishi na mumeo kwa namna utakayoona wewe ni sahihi
 
Uzi umeniumiza sana!

Kinachoniumiza ni kile sisi wanaume tunachopendewa na Hawa wanawake si kingine ni "hatma ya uchumi wetu"!!!

Unafanya mapenzi na mtu ambae unahisi anakuoendea kitu Fulani na si wewe kama wewe!hii inaumiza mno!!

Wanawake wengi hawajui kwanini tunapoteza mzuka nao,ni pale tunapoonekana maroboti yatumikayo kuwafanikisha kiuchumi lakini hakuna anaejali hayo maroboti!!
 
Halafu mkiachana mwanamke anafidiwa kwa kupewa mgao wa mali huku wanaume tunafarijiwa kwa kuambiwa mwanaume kaumbiwa mateso
 
Mimi najadili uhalisia sitoi mawazo yangu binafsi mimi kurejea utamaduni haimaanishi kwamba nasupport au napinga hakuna mahali nilipoonesha msimamo wangu, kuhusu gender roles nisome vizuri sijakataa kwamba jukumu la mwanamke ni kutii mume na kufanya kazi za nyumbani ila hoja yangu ni kwamba hayo majukumu mwanamke anatakiwa kufanya endapo tu mume wake anamhudumia, sasa inashangaza kuona wanaume wa leo wanalalamika kuhusu hilo jukumu wanataka eti wanawake nao watafute pesa halafu hapo hapo wawatii na wafanye kazi za nyumbani hilo unaliongelea vipi
 
Wewe unajuaje kama wameamua kukaa kimya kwa sababu hoja zimewapiga kwenye mshono na si kwa sababu nyingine tu, kama ulisoma na kuelewa comment yangu ya kwanza vizuri niliandika kwamba siku hizi wanawake wameacha kulalamika wameamua kujibu mapigo kimya kimya na matokeo yake wanaume ndio mnalalamika, sasa hata kuacha kubishana kwenye mada kama hizi mitandaoni nako ni ishara kuwa wanawake wa siku hizi wamepunguza kulalamika baada ya kuona wamelalamika kwa muda mrefu bila jamii kuwasikiliza
 
Hakuna sheria kandamizi hapo bali wanaume mnataka tu muendelee kutumia mamlaka mliyopewa kuwaonea wanawake, kama huyo mwanamke angekuwa hajaolewa na wewe maana yake angekuwa anajitafutia pesa zake na anajiamulia maisha yake ila kwa sababu umemuoa inabidi aache hayo yote aje kutimiza majukumu mengine kwa ajili yako, sasa mnapoachana unategemea anaondoka na nini ambacho kitamsaidia kuenda kuanza maisha mengine na wewe kama mume unataka upewe nini maana kumbuka mwanaume ndio main provider of the family

By the way mali mnazogawana ni zile zilizopatikana ndani ya ndoa kwa vyovyote vile kila mmoja anahesabika ana mchango wake katika upatikanaji wa hizo mali hivyo mnahesabika mmechuma wote, halafu mbona unaandika kana kwamba mwanamke anaondoka na mali zote wakati mnagawana nusu kwa nusu sasa wewe unaposema kwamba mwanaume anapata nini kwa kutimiza majukumu yake, si ndio hiyo nusu ambayo unagawana na mkeo au wewe ulitaka iweje hebu fafanua vizuri maana hadi sasa naona unarukaruka tu

Mimi nimekujibu maswali yote ila wewe kwa sababu zako binafsi umeamua tu kukataa majibu halafu unasema eti sijakujibu sasa hapo tatizo ni la nani, hao walioweka hizo sheria siyo wajinga kuna mambo mengi sana wamezingatia halafu ninyi wanaume msiotaka kuwajibika mnakuja na visingizio eti ni sheria za kumkandamiza mwanaume, kwani hao waliopitisha hizo sheria ni wanawake na kama ni wanaume kwanini wapitishe sheria za kupendelea mwanamke wanafanya hivyo kwa faida ya nani
 
Imelose nini ? Na ime gain nini ?

Kwa nini mtumwa alikuwa ana thaminishwa kwa pesa au mali ?

Kwamba unakataa kuwa mwanamke anunuliwi ? Process za ulipaji mahari mpaka kukamilika malipo wazifahamu ?
 
Imelose nini ? Na ime gain nini ?

Kwa nini mtumwa alikuwa ana thaminishwa kwa pesa au mali ?

Kwamba unakataa kuwa mwanamke anunuliwi ? Process za ulipaji mahari mpaka kukamilika malipo wazifahamu ?
Kama ulisoma vizuri ile comment yangu uliyoiquote basi usingeuliza maswali ya kipuuzi kama hayo, kwa sababu nilishafafanua familia ya mke inalose nini na ya mume inagain nini, au wewe ulitaka familia ya mke ipewe nini kwa kulose mtoto na ile heshima ya kuendeleza jina la ukoo
 
Kama ni ya kipuuzi usinge jisumbua kuandika.

Turudi kwenye maswali yangu tufanye sio ya kipuuzi, naomba majibu
 
Kuimba kupokezana. Poleni...
 
Kama ni ya kipuuzi usinge jisumbua kuandika.

Turudi kwenye maswali yangu tufanye sio ya kipuuzi, naomba majibu
Mjomba maswali yako nimeshayajibu, ni wewe tu kwa sababu zako binafsi umeamua kukataa majibu, onesha ni wapi sijajibu
 
Sasa mbona unajikaaanga, Men uim

Kwahiyo nikiwa namhudumia lakini yeye anafanya kazi nyumbani na hatuna watoto, inamaana hatutagawana mali?
 
Kama sababu ya kumlipa mwanamke 50% kisa wakati anafanya kazi za nyumbani nilimpotezea muda, kwamba nisingemuoa pengine angekuwa anafanya kazi mahala, angepata pesa, je namimi nisingemuoa si ningekuwa nina pesa nyingi tu? Kwasababu kala chakula changu, kavaa nguo zangu, katibiwa kwa pesa zangu, na bado mizinga ya baba mkwe na mashemeji, huoni kuwa sababu uliyoitoa haina mashiko?
 
Sasa mbona unajikaaanga, Men uim



Kwahiyo nikiwa namhudumia lakini yeye anafanya kazi nyumbani na hatuna watoto, inamaana hatutagawana mali?

Sasa ambacho hujaelewa ni nini wewe kumhudumia ni jukumu lako kama naye anavyotimiza majukumu yake sasa ulitaka hizo huduma apate wapi wakati umemuoa ni mama wa nyumbani, kwenye kugawana ni kwa sababu mnahesabika mmechuma wote yeye ametimiza majukumu yake kama mke ili wewe ufocus kwenye kutafuta hizo pesa tu, hivyo naye ana mchango wake na ndio maana mnagawana hachukui zote

Kama unaona hiyo ni hasara basi mruhusu naye atafute pesa kama wewe ili usiwe unamhudumia hapo hata mkigawana itakuwa afadhali, maana angalau naye alikuwa anachangia pato la familia lakini ndio ukubali kwamba majukumu ya nyumbani inabidi asifanye yeye tena bali muwe na msaidizi, au kama vipi muwe mnasaidiana wenyewe na pia ukubali kupoteza ile full authority kama mwanaume kwa sababu humhudumii

Waliotunga hizi sheria siyo wajinga waliona kwamba wasipoweka huu utaratibu wanawake watakuwa wanaachika sana huku wakiondoka mikono mitupu, kwa sababu jamii ilishajenga mtazamo kwamba mwanaume kuoa na kuacha mara kwa mara ni kawaida ila mwanamke kuolewa na kuachwa mara kwa mara ni umalaya, kwahiyo hili liliwafanya wanawake wajitahidi kuvumilia maovu ya wanaume na wapambanie ndoa ili wasiachike

Sababu wanajua wakiachika jamii itawatukana huku wanaume kwao kuacha siyo shida, muda wowote akijisikia kumuacha mkewe kwa sababu yoyote ile hata kama ni ya kijinga, anamuacha tu sababu anajua jamii haitamfanya chochote

Kama mnaona huu wanaofanyiwa wanawake ni upendeleo basi sidhani kama kuna jinsia iliyopendelewa kama yenu, maana enzi za wazee wetu wanaume mlipendelewa zaidi hata ya wanawake wanavyopendelewa leo hii, lakini mliona sawa na mlifurahia wanawake walipokuwa wanavumilia manyanyaso yenu sasa meza zimegeuka mnaona kama mnaonewa
 
Halafu mkiachana mwanamke anafidiwa kwa kupewa mgao wa mali huku wanaume tunafarijiwa kwa kuambiwa mwanaume kaumbiwa mateso
Mkuu mi nimegoma kiapo cha ndoa kabisa!!

Bora nizae nae tujenge nyumba na vitega uchumi halafu niwe huru TU kama upepo!!

Nikiona wenge limezidi napanga room la kutuliza stress za kila siku!.
Nakuja home mara Moja Moja tu kucheki watoto wanaendeleaje!!
 
Kwahiyo unafikiri hiyo michango inafanana mpaka kila mmoja apewe nusu?
 
Hiyo sheria kandamizi ndo inafanya wanawake wawe majeuri, maana wanajua wakiachwa wanalipwa, hivi nimemkamata mke wangu kanichiti halafu nikimuacha nimlipe, upumbavu gani huo? Kwanini wasingeweka hata exception kwa kosa hilo tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…