Miguna Miguna alaani vikali kuondolewa Kenya, asema hajawahi kuukana uraia wa Kenya

Miguna Miguna alaani vikali kuondolewa Kenya, asema hajawahi kuukana uraia wa Kenya

Hakuukana uraia wa Kenya wakati alisajili uraia wa Kanada kipindi hicho tukiwa kwenye katiba ya zamani, ambayo haikuruhusu uraia pacha. Baada ya kuzinduliwa kwa katiba mpya, alifaa kuomba uraia wa Kenya ili awe raia wa nchi zote mbili, sasa kaichukulia poa na kuendelea na harakati zake.

Kwa kifupi serikali ya Uhuru sasa hivi imepanic baada ya tukio la Raila kujiapisha, huu ni wakati hatari kwa mtu yeyote anayeichokonoa serikali, bora uhakikishe stakabadhi zako zote ziko poa, mamlaka ya kodi wasiwe na issue na wewe, yaani uwe msafi kama pamba maana sasa hivi usalama wa taifa wanazunguka kote kote na wapo tayari kufanya lolote, hatari sana. Hata wanakiuka amri za mahakama bila kupepesa macho.
Mhhh what happened to baba wa Demokrasia? Wapiga zumari wa kibongo humpamba sana huyu baba.

Wabongo wanapenda sana kujidharau wakati Africa ni ile ile.
 
Mhhh what happened to baba wa Demokrasia? Wapiga zumari wa kibongo humpamba sana huyu baba.

Wabongo wanapenda sana kujidharau wakati Africa ni ile ile.

Jamaa wanamchokonoa hadi kwenye macho, yaani huyu rais namuona akiwa mvumilivu hadi kero maana ingelikua mimi ndiye rais, pangekua patamu maana nchi yote ingejua mimi ndiye rais.
Ningetembeza kichapo mpaka waombe yaishe.

Hapa najaribu kuwaza, hivi Lowassa akajiapisha kama rais wa nchi, hivi japo Bongo pangekua vipi ikiwa leo hii hata hana ruhusa ya kuhutubia wananchi.
 
Jamaa wanamchokonoa hadi kwenye macho, yaani huyu rais namuona akiwa mvumilivu hadi kero maana ingelikua mimi ndiye rais, pangekua patamu maana nchi yote ingejua mimi ndiye rais.
Ningetembeza kichapo mpaka waombe yaishe.

Hapa najaribu kuwaza, hivi Lowassa akajiapisha kama rais wa nchi, hivi japo Bongo pangekua vipi ikiwa leo hii hata hana ruhusa ya kuhutubia wananchi.
Singekupa kura yangu wewe! Yaani hungeiona ng'oooo, kama anavopenda kusema mzee RAO.
 
Sijui sasa Raila nae watamdeport kumpeleka Chattle? Africa bado sanaaaaa.
 
Sijui sasa Raila nae watamdeport kumpeleka Chattle? Africa bado sanaaaaa.
Raila kwao ni Juba, hatutaki laana kwa kumtesa mzee. Tunangoja uhasama wa Machar na Kirr uishe kwanza kisha na yeye pia tumfanyie haki. Hakutakuwa na gharama za KLM hapo. 🙂
 
Sasa inakuwaje huko walikompeleka, ataingiaje ingiaje!!!??

ataingia bila tatizo kwa sababu yeye ni citizen wa Canada, ndio maana kwenye malalamiko yake hajabisha hata chembe kwamba yeye ni Mkanada.

Wakati anachukua uraia wa Canada Kenya ilikiwa haina dual citizenship, kwa hiyo automatically alijifuta uraia wa Kenya.

Kwenye community yeyote ya diaspora the one thing that everybody knows ni kwamba nani ana makaratasi, nani hana, nani kashachukua u-citizen, nani hajaenda kwao miaka 20, na nani anatafuta bwana wa makaratasi. Na hiyo sio siri hata kwa serikali ya kwenu wakitaka kujua kama ulichukua u-citizen huko. I mean, you are not fooling anybody.

Na ndio maana hata hapa bongo Waziri Lukuvi alitoa onyo kali kwa wanaochukua uraia wa nje, wanakuja wanaficha passport za huo nje, akasema jamani eeh, you are not fooling anybody, msidhani mmejificha kiviiiiile!
 
Akatulie huko, amwambie dr Slaa ampe kibarua chake kwa muda
 
Jubilee wangeomba msaada kutoka CCM wa namna ya kuua upinzani wala wasingekuwa wanahangaika na mambo kama haya.
 
Singekupa kura yangu wewe! Yaani hungeiona ng'oooo, kama anavopenda kusema mzee RAO.

Hehehe!! Ndio maana sipo tayari na haitokuja siku nigombee wadhifa wowote nchi hii, kuna kipindi nilitaka kufuata ubunge ila nikaamua ifie huko. Mimi najijua sio mvumilivu, sipendi vitu vya kunipa presha, kama hauendani na uongozi wangu nakutupia dirishani, urais ni kazi gumu sana na inataka uvumilivu usio wa kawaida, yaani upo unaumiza kichwa jinsi ya kuboresha maisha ya mamilioni ya watu wakati huku kunao wanaokukwamisha kwenye kila hatua.

Hebu ona hii video hapa chini jinsi Tanzania huwa patamu, kiongozi wa upinzani Lipumba huyoooo
 
hivi alifikishiwa ubalozini au walimdampo airport?
 
Si ashukuru Mungu amekuwa deported ? Musando ama waziri wa mambo ya ndani anajua wapo wapi ?
 
Hehehe!! Ndio maana sipo tayari na haitokuja siku nigombee wadhifa wowote nchi hii, kuna kipindi nilitaka kufuata ubunge ila nikaamua ifie huko. Mimi najijua sio mvumilivu, sipendi vitu vya kunipa presha, kama hauendani na uongozi wangu nakutupia dirishani, urais ni kazi gumu sana na inataka uvumilivu usio wa kawaida, yaani upo unaumiza kichwa jinsi ya kuboresha maisha ya mamilioni ya watu wakati huku kunao wanaokukwamisha kwenye kila hatua.
Ate waat! 😀 Asee hiyo kali. Hata zile enzi za Baba Yao akiwa rudeboy hawakuwa wanamfanya hivo. Ila tumetoka mbali mkuu, sasa na udikteta wako 😀 huwa unatoboa vipi? Maanake hata watoto wadogo siku hizi kwenye nyumba huwa wanasema laivu kwamba wana haki zao?
 
Ate waat! 😀 Asee hiyo kali. Hata zile enzi za Baba Yao akiwa rudeboy hawakuwa wanamfanya hivo. Ila tumetoka mbali mkuu, sasa na udikteta wako 😀 huwa unatoboa vipi? Maanake hata watoto wadogo siku hizi kwenye nyumba huwa wanasema laivu kwamba wana haki zao?

Hamnaaa!! Mimi ni old school, hamna cha nini wala nini, mtoto lazima anyooke na hadi siku atakua na kwake tutaendelea kuwekana sawa tu.
Wakati wa kucheka nao huwa raha, nawapa mapochopocho yote, lakini wakipinda nawageuzia kibao mpaka wanatamani dunia ipasuke. Kiongozi lazima uwe na msimamo, sio kila kitu demokrasia na kushauriana, vinginevyo hamtasonga hata hatua moja, utakwamishwa kila siku.
 
Hamnaaa!! Mimi ni old school, hamna cha nini wala nini, mtoto lazima anyooke na hadi siku atakua na kwake tutaendelea kuwekana sawa tu.
Wakati wa kucheka nao huwa raha, nawapa mapochopocho yote, lakini wakipinda nawageuzia kibao mpaka wanatamani dunia ipasuke. Kiongozi lazima uwe na msimamo, sio kila kitu demokrasia na kushauriana, vinginevyo hamtasonga hata hatua moja, utakwamishwa kila siku.
Kweli, lazima uwe balanced. Si kama baba zetu bana. Ili umuone akiwa hayupo serious kama kawaida yake, labda kwenye umati wakati wa maombi akivua kofia afu afumbe macho. Hapo ndo tukiwa watoto tulikuwa tunachungulia kwa uoga, afu tunapigwa na butwaa tunaona ni kama anaigiza movie ya Mr. Bean! 😀 Ila hatukufhamu enzi hizo itakavokuwa majukumu mazito ikifika wakati wetu.
 
Kweli, lazima uwe balanced. Si kama baba zetu bana. Ili umuone akiwa hayupo serious kama kawaida yake, labda kwenye umati wakati wa maombi akivua kofia afu afumbe macho. Hapo ndo tukiwa watoto tulikuwa tunachungulia kwa uoga, afu tunapigwa na butwaa tunaona ni kama anaigiza movie ya Mr. Bean! 😀 Ila hatukufhamu enzi hizo itakavokuwa majukumu mazito ikifika wakati wetu.

Hehehe!! Umenikumbusha marehemu babangu, alikua mkali asiyependa maskhara, kila akiingia nyumbani ilikua inabidi tukae mkao wa kujishuku shuku maana hujui ataibuka na lipi. Nilikua namuona simba asiyependa upumbavu wa aina yoyote, tena dikteta asiyeshaurika wala kuomba mijadala au maoni, japo siku moja kuna tukio lilitendeka kitaani kwetu ambalo sikumbuki issue ilikua nini, ila ninachokumbuka ni kwamba askari wa GSU au fanya fujo uone (FFU) walivamia makazi yetu usiku.

Jamaa walitembeza kichapo nyumba baada ya nyumba, Kipindi hicho nilikua mdogo, hivyo watoto hatukuguswa, nakumbuka babangu pamoja na ubabe wake wa kila siku, hiyo siku alikua anaomba msamaha hadi dah.... Hapo ndio nilijua kumbe kuna mbabe wake, kumbe huko nje kuna simba anayeitwa serikali, kumbe huyu mzee na udikteta wake wote kunao wanamkalisha anakaa.....hehehehe Mungu ilaze mahali pema roho yake mzee wetu.
 
Hakuukana uraia wa Kenya wakati alisajili uraia wa Kanada kipindi hicho tukiwa kwenye katiba ya zamani, ambayo haikuruhusu uraia pacha. Baada ya kuzinduliwa kwa katiba mpya, alifaa kuomba uraia wa Kenya ili awe raia wa nchi zote mbili, sasa kaichukulia poa na kuendelea na harakati zake.

Kwa kifupi serikali ya Uhuru sasa hivi imepanic baada ya tukio la Raila kujiapisha, huu ni wakati hatari kwa mtu yeyote anayeichokonoa serikali, bora uhakikishe stakabadhi zako zote ziko poa, mamlaka ya kodi wasiwe na issue na wewe, yaani uwe msafi kama pamba maana sasa hivi usalama wa taifa wanazunguka kote kote na wapo tayari kufanya lolote, hatari sana. Hata wanakiuka amri za mahakama bila kupepesa macho.
Ile nyomi ya supporters ndio imewapanikisha
 
Hehehe!! Umenikumbusha marehemu babangu, alikua mkali asiyependa maskhara, kila akiingia nyumbani ilikua inabidi tukae mkao wa kujishuku shuku maana hujui ataibuka na lipi. Nilikua namuona simba asiyependa upumbavu wa aina yoyote, tena dikteta asiyeshaurika wala kuomba mijadala au maoni, japo siku moja kuna tukio lilitendeka kitaani kwetu ambalo sikumbuki issue ilikua nini, ila ninachokumbuka ni kwamba askari wa GSU au fanya fujo uone (FFU) walivamia makazi
Hahaha 😀 Nimecheka sana. R.I.P kwake lakini na walaaniwe sana hao jamaa wa G.S.U ambao huwa hawatambui kwamba kila simba ana pango lake.
 
Back
Top Bottom