Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Alooooo mkuu ume hustle sio mchezo
 
Mrume ndago kwa hisani ya ghost members naomba ni koment uko byeee


Mrume ndago shusha vitu
 
Jamaa ananifanya najiona msahaulifu sana.

Anakumbuka details ndogondogo sana kama majina ya watu, majina ya sehemu alizopita mpaka muda wa matukio.

Mimi mpaka muda huu sikumbuki hata ulisema faranga moja ni sawa na sh ngapi ya TZ.
Kichwa chako kibovu.
 
Jamaa ananifanya najiona msahaulifu sana.

Anakumbuka details ndogondogo sana kama majina ya watu, majina ya sehemu alizopita mpaka muda wa matukio.

Mimi mpaka muda huu sikumbuki hata ulisema faranga moja ni sawa na sh ngapi ya TZ.
Mkuu IQ Yako ndogo [emoji22][emoji846][emoji846][emoji2]

Ukiona haukumbuki hata jana ulifanya nn jua wewe unaishi leo tu
 
Jamaa ananifanya najiona msahaulifu sana.

Anakumbuka details ndogondogo sana kama majina ya watu, majina ya sehemu alizopita mpaka muda wa matukio.

Mimi mpaka muda huu sikumbuki hata ulisema faranga moja ni sawa na sh ngapi ya TZ.
Ukisema nisimulie maisha yangu vya nyuma vitaenda mbele vya mbele vitakaa nyuma na vya katikati vitapachikwa juu kwa juu
 
Jamaa ananifanya najiona msahaulifu sana.

Anakumbuka details ndogondogo sana kama majina ya watu, majina ya sehemu alizopita mpaka muda wa matukio.

Mimi mpaka muda huu sikumbuki hata ulisema faranga moja ni sawa na sh ngapi ya TZ.
hata mm mwanangu inaniumizaga kukosa kumbukumbu kwenye vitu vidogo vidogo
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 15.

Inaendelea.............


Asubuhi kulipokucha mzee Nchabironda aliniambia inapaswa sasa twende porini ambako ingenibidi kukaa kwa wiki nzima nikifundishwa kuchanganya madawa mbalimbali kwakutumia miti pori.Kusudi la kufundishwa namna ya kuchanganya dawa ni namna nitakavyokuwa ninahusika na kafara na namna ya kuishi na utajiri nitakaoupata.Basi mzee Nchibaronda aliniambia inapaswa niache kila kitu hapo nyumbani kwake na huko ninako elekea inapaswa nibebe Kisu tu!.

Mzee aliniuliza "Uko tayari?".

Nilimjibu "nipo tayari mzee".

Mzee aliniambia kwakuwa ninautaka utajiri inapaswa chochote nitakachokiona huko msituni inapaswa nishinde na nisiogope kwani hayana budi kutokea ili kunikomaza,mzee aliniambia akiangalia nyota yangu anaona kabisa mimi ni jasiri kama dume la Simba hivyo akasema sipaswi kushindwa!.Kwakuwa nilikuwa nimedhamiria kuwa tajiri kiukweli sikuona jambo lolote la kunizuia,nilikuwa nikikumbuka kauli za dharau na nyodo za yule shemeji wa Mwanza nilikuwa napata kama uchizi! Nilikuwa nikijisemea kwamba "siwezi kusafiri umbali mrefu,nimevuka mabonde na milima halafu nishindwe".

Mzee Nchibaronda aliendelea kusisitiza kwamba mara baada ya kunipeleka porini yeye atarudi na ataniacha huko mpaka siku saba zitimie yeye ndiyo angekuja kunichukua!.Nilimuuliza huko porini nitakula nini?.

Akasema "kuna mzee mtakuwa naye huko atakueleza kila kitu cha kufanya!".

Tuliondoka hapo nyumbani kwake kuelekea porini,msitu ule ulikuwa umefunga sana na katikati ya ule msitu kulikuwa na mto mkubwa!,wakati tunaenda mzee aliniambia nitakapokuwa kule porini nisije kuwa na mawazo ya mwanamke wala tamaa!.Baada ya kufika kwenye lile pori mara ghafla mzee siku muona na nilisikia tu sauti ikisema "Nitarudi".Kiukweli niliogopa sana lakini sikuwa na namna maana nilisema kwakuwa niliutaka utajiri sikuwa na budi kuvumilia,mpaka wakati huo sikuwa na kitu chochote zaidi ya kisu na nguo nilizokuwa nimevaa tu!,lilikuwa ni pori zito lililofunga,sikuona nyumba wala mtu yeyote zaidi ya mto mkubwa!.

Nilipiga hatua kadhaa mbele nikasikia sauti ikisema "Kombo na yo?",ilikuwa ikimaanisha "Unaitwa nani?".

Nilimwambia naitwa...........

Kiukweli ndugu zangu mpaka leo huwa sijui ni nini kilitokea kule msituni maana kwa wiki hiyo yote nilikuwa naweza kuongea na kuelewa lingala vizuri bila shida yeyote ila nilivyotoka tu msituni ikawa tia maji tia maji!,japo niliendelea kuelewa maneno baadhi!.

Ile sauti iliendelea kuniuliza "Mpo na nini ozali awa?",ilikuwa ikimaanisha "Kwanini uko hapa?".

Niliijibu "Ninataka kuwa tajiri".

Baada ya muda kidogo nilihisi kama kuna mtu alikuwa nyuma yangu,ile nageuka nikakutana na mzee mmoja ambaye alikuwa uchi kama alivyozaliwa!,nilishituka sana ndipo mzee aliniambia "Kobanga te!",yaani "Usiogope".

Yule mzee alinichukua mpaka mahali fulani porini kwa ndani zaidi,baada ya kufika huko aliniambia nivue nguo nibaki uchi kama yeye alivyokuwa!.Kiuweli kulikuwa na baridi kali lakini hukukuwa na namna!,basi mzee alianza kunionyesha miti mbalimbali na namna ya kuichanganya mpaka inakuwa dawa!,Kuna mti fulani alinionyesha na namna ya kuuchanganya na miti mingine hatimaye ukawaka moto!.

Mzee aliniuliza "Omoni alingaki ete tokolya?" ,yaani "Je unataka kula?".

Nilimjibu "Boye",nilimaanisha "Ndiyo".

Basi yule mzee alianza kunifundisha namna ya kuchanganya dawa ambayo ningeweza kumkamata mnyama yeyote hapo porini pasipo shida yeyote!,aliendelea kunifundisha dawa za aina mbalimbali ikiwemo ya kusimama mahala popote pasipo kuonekana na mtu yeyote na nikafanya chochote nitakacho.Siku zilisonga nikiwa humo msituni nikifundishwa na huyo mzee,ndani ya siku zote hizo saba sikuwahi kupata usingizi wa aina yeyote na nilipokuwa nikihisi njaa nilitengeneza dawa ambayo ilinielekeza mnyama yeyote alipo,nilipofika hapo nilimkamata na kuchinja kisha nilitengeneza dawa ya kuwasha moto na kuanza kupiga kitoweo kama kawaida,niliwala sana digidigi pamoja kware kwa kipindi hicho cha wiki nzima niliyokuwa huko porini!.Siku moja kabla kumaliza zile siku saba nikiwa mle porini,yule mzee kwa wakati ule hakuwepo maana yeye alikuwa akija na kutoweka!,wakati huo nilikuwa uchi kama nilivyozaliwa.Niliteremka kwenda mtoni ili nikamate kambale ambao nije nichome nile,mara ghafla nikakuta mwanamke mzuri ambaye sijawahi kumuona toka nizaliwe akiwa anaoga pembeni ya mto akiwa kama alivyo zaliwa!.

Nilipokaribia wale kambale ambao tayar nilishawafanyia dawa wakiwa wananisubiri niwatoe mtoni,yule mwanamke aliniita kwa jina langu,aliniambia nisogee nikamsugue mgongoni!.Kiukweli namna alivyokuwa mzuri nilishindwa kuelewa katokea wapi na ukizingatia mle ndani ya pori hakukuwa na makazi ya watu au viumbe wa kawaida!.Nilipomsogelea yule mwanamke nilijikuta uume umesimama ghafla,nilikumbuka ile kauli ya mzee Nchibaronda kwamba nisiwe na tamaa ya mwanamke yeyote nitakaye muona au kukutana naye!.Nilisikia sauti moja ilikuwa ikiniambia nishiriki naye ngono yule mwanamke na nyingine ilikuwa ikinisihi sana niache tamaa maana ningefanya hilo tendo kila kitu kilikuwa kinaharibika!,Kiukweli nilikuwa katika jaribu kali sana na hakuna mwanaume yeyote ambaye alikuwa mwenye uwezo kamili angemwacha yule mwanamke,ukizingatia nilikuwa nina muda mrefu sijakutana na mwanamke!.Niliwaza sana namna nilivyosota kufika hapo na kile kilichonipeleka huko,ghafla nilighairi mawazo mabaya na uume wangu ulianza kulala na ndipo ghafla yule mwanamke alipotea machoni pangu!.Nilichukua zangu kambale na kwenda kuchoma tayari kwa kuliwa,nikiwa porini pia nilifundishwa namna ya kukinga damu kwenye kibuyu na namna ya kutoa kafara kwa njia ya ajali.

Basi baada ya zile siku saba yule mzee Nchibaronda alinifata na alifurahi sana akawa anasema kama nimeweza kukaa kwenye pori na kuvumilia misuko suko yote ikiwemo baridi kali kusingekuwa na cha kunishinda!.Nilipofika hapo nyumbani kwake nilikaa siku mbili na siku ya tatu walikuja jamaa wawili ambao walikuwa watanzania,wao walikuwa wenyeji wa Sumbawanga.Hawa jamaa baadae nilikuja kufahamu kwamba wao walifuata uchaw.Hao jamaa siku ambayo nilikwenda ziwa Tanganyika niliongozana nao.Siku ya tano baada ya kutoka msituni mzee Nchibaronda alisema umewadia sasa wakati wa sisi kwenda Ziwa Tanganyika,na hatukupaswa kuvaa nguo za kawaida bali kila mtu alifungwa ngozi ya mnyama kufunika nyeti zake,sikuweza kuelewa ile ngozi ilikuwa ya mnyama wa aina gani!.

Wale jamaa mmoja alipewa shilingi iliyokuwa na tundu katikati,mzee Nchibaronda akatuambia hiyo ni nauli,yule mwingine alipewa irizi ikiwa imefungwa kwa ustadi wa hali ya juu na mzee akasema hiyo ni pasipoti ya tunapokwenda!,Pia mzee alinipatia unga fulani hivi ambao baadae nilikuja kugundua ulikiwa unga wa mifupa ya albino uliyokuwa umesagwa sana!.Mzee alitupatia maelekezo kila mtu kutokana na kitu alichopewa,mimi niliambiwa tutakapofika hapo kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika niumwage ule unga ziwani(Kwenye maji),maana ni chakula cha majini na ndiyo shukurani yetu kwa wakati huo,wale wenzangu pia walipewa maelekezo kila mtu kulingana nanalichopewa.Basi baada ya kukamilisha lile zoezi ilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua tukajikuta tupo kando ya Ziwa Tanganyika,tulikuta watu wanafanya shughuli mbalimbali kando ya lile ziwa lakini wao walikuwa hawatuoni lakini sisi tuliwaona wao!.



Itaendelea....................
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…