Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Share link ya uzi basiNimeshaanza nayo hii ya Zabron leo niko episode ya tatu
Huwa sipendi ujinga
Kweli kabisa maombi ni muhimu sana.Hapa nimejifunza kitu..
Usione mtu kachepuka/kakuacha /upendo umepungua ukajua ni hali ya kawaida aisee jamani maombi ni muhimu sana kwenye mahusiano/ndoa zetu, Mungu atusaidie kwakweli..
Wakongo 😀Mkuu huko chini ya ziwa yule mungu bonge na malkia wake ni watu wa asili gani? weupe au waswahili??
We utakuwa tajiri wa tegeta. Unajaribu kumtrace jamaa [emoji28][emoji28]Unatumia mtandao gan,nkutumie vocha
Wacha tutoe sapot kwakweliWakuu yeyote anayetaka kunitumia hela ya mafuta(Mbs)basi anaweza kunitumia kwenye namba hii 0768173820.Majina ni FREDERIKA JAMES
Nipigeni tafu ndugu zangu japo pia si lazima bali ni ombi tu ndugu zangu
Mkuu tayari angalia.Wakuu yeyote anayetaka kunitumia hela ya mafuta(Mbs)basi anaweza kunitumia kwenye namba hii 0768173820.Majina ni FREDERIKA JAMES
Nipigeni tafu ndugu zangu japo pia si lazima bali ni ombi tu ndugu zangu
Hip mji ni kiwilaMKASA WA PILI - Sehemu ya 21
Inaendelea.............
Nikiwa geto nilisikia sauti kama kawaida ikiniambia niende mbeya na nikifika hapo mbeya nitapewa ishara ya nini cha kufanya!
Kwakuwa tayari nishazoea ile hali hivyo nilikuwa siogopi wala kuwa na wasiwasi!
Kwa wakati ule sikuwa kabisa na akili nyingine zaidi ya kuona ninayafaidi maisha kwa maana kila nilichokitaka nilikipata kwa wakati!
Basi nilijiandaa na niliushika mkono wangu wa kushoto na kutamka "Ninataka niwe mbeya muda huu",ilikuwa ni kitendo cha kufumbua nikajikuta nipo uyole mbeya!
Kiukweli ile irizi ambayo iliwekwa mkononi mwangu na yule malikia kule chini ya ziwa Tanganyika ilikuwa na nguvu za ajabu na ilinipatia kiburi sana mpaka nikawa nawaoana binadamu wenzangu kama TAKA TAKA!
Namshukuru sana Mungu kwa kunitoa huko!Mungu ni mwema sana na uwezo,rehema na fadhili zake hazina kikomo!
Basi nilipofika yale maeneo kuna gari nililiona lilikuwa costa na kwa muonekano nililifahamu kwamba ndilo gari ambalo inapaswa nikalipige mzinga,Lilipofika yale maeneo nilipokuwa lilisimama na konda akawa anasema "Kyela hiyooooooo,twenzetu tukuyu mpaka kyela hiyoooooo!",Nilipanda ndani ya ile costa na kama kawaida sikulipa nauli na yule konda hata hakuniuliza kuhusu nauli!
Lile gari lilifika kwenye mji mmoja nadhani ulikuwa unaitwa Kimo kama sijakosea(Kama kuna wenyeji wa huko wanaosoma huu uzi watanikumbushia,maana ni muda kidogo),Huo Mji wa kimo ulikuwa kabla ya kufika Tukuyu!,Ile sauti iliniambia nishuke na niendee mbele ya Tukuyu kuelekea kyela kulikuwa kuna mtelemko mkali sana pale nikaisubiri pale!
Nilifanya kama ile sauti ilivyonitaka nifanye na nilipotea ghafla yale maeneo na nikafika eneo la tukio!
Kiukweli kilikuwa na mtelemko mkali sana yale maeneo na sikumbuki palikuwa wapi maana kulikuwa na miti mingi sana ile ya mbao!,Nadhani ni hapo hapo tukuyu kwa ndani ndani,Wenyeji wa huko watatusaidia!
Basi niliweka tego kama kawaida nikiwa nimeshika kibuyu cha kazi,Baada ya kusubili kwa muda niliiona ile costa ikiwa inakuja kwa mwendo wa kasi!,Ilipofika yale maeneo ilikula mzinga wa maana sana!
Niliisogelea ile costa na kwenda kuanza kuchukua kilichonipeleka!,Lakini ghafla ndani ya ile costa niliwaona akina mama wawili wakiwa wananiangalia wakisema "We mtoto unafanya nini"?
Wale kina mama walikuwa washirikina na watu wengine walipokuwa wamelaliwa na viti wao walikiwa wamekaa wakinikodolea macho!
Waliniita mimi mtoto si kwamba umri wangu nilikuwa mtoto bali walionyesha dharau kwamba mimi si lolote wala chochote!
Niliwaambia kwakuwa wameniita mimi mtoto ninataka niwaonyeshe mimi si mtoto kwenye ile kazi kama wao walivyodhani!,Kama nilivyosema hapo awali kwamba nilikuwa nina uwezo wa ajabu na kiburi kilikuwa kimenijaa sana!
Niliwasogelea na kuanza kushindana nao pale kichawi lakini nilipotamka ya kwamba "Naomba mkauke muwe kama samaki",haikuchukua muda walikuwa wamekauka kauuu!
Wao ndo walikuwa wa kwanza kuchukua damu yao na baada ya hapo nilianza kukusanya damu za abiria wengine!,Nilipomaliza kufanya lile zoezi nilipotea yale maeneo! Na nikatokezea pale nilipokuwa mwanzo Uyole!
Basi kwakuwa nilikuwa nina njaa kuna mgahawa mmoja ambao ulikuwa mkubwa tu kama hotel kwa ajili ya kupata chakula!,Nilipofika hapo kwa kuwa bado nilikuwa nimevaa uhusika wa kishirikina maana sikutaka bugudha!,Ile nimeingia ndani ya huo mgahawa niliona kina mama ambao walikuwa wakitoa huduma hapo hotelini walikuwa uchi wa mnyama!,Alikuwa mwanamke mmoja mnene na Binti yake ambaye pia alikuwa uchi!
Huyo binti yake yeye alikuwa akivuja damu kutoka kwenye uke wake na alikuwa akizichukua zile damu na kuziweka pakaza kwenye vile vyakula vya wateja walivyokuwa wamemwagiza!
Sasa kwa bahati mbaya sana hakuna mteja ambaye alikuwa akiona yale matukio yote isipokuwa mimi niliyekuwa na uwezo huo!Hicho ki-mgahawa kilikuwa kimechangamka sana maana hadi madereva wa magari makubwa niliona walikuwa wakiingia kula pale!,ukimuondoa yule mama na yule Binti niliyewakuta uchi pale pia kulikuwa na wahudumu wengine wawili,Mmoja alikuwa mpishi na mwingine pia alikuwa akihudumia lakini hawa wao walikuwa wamevaa nguo zao tu za kawaida!
Sikupata shida kuelewa kwamba yule mama ndiye alikuwa mmiliki wa ule mgahawa na yule aliyekuwa akivuja damu ukeni alikuwa binti yake wa kumzaa!
Yule mama aliponiona tu alinifanyia ishara ya kidole kwamba nikae kimya!Yule binti alikuwa akinitolea macho na nilimuona anakuwa na wasiwasi!
Basi nilimwita yule mwanamke nikamwambia aniletee chakula ila kiwe kisafi tofauti na hapo ningemuumbua!
Alimwita yule binti aliyekuwa kavaa nguo akamwambia "Mpe yule kaka chakula"
Zilikuja ndizi zimejaa sahani na nyama na kwakuwa nilikuwa nina uwezo wa kukiangalia kama ni kisafi ama la!,baada ya kujiridhisha kilikuwa kisafi kwa maana kwamba hawakuweka mambo yao ya kishirikina nilianza kula!
Wakati nakula watu wengi walikuwa wakiingia kupata msosi wakiamini ni msosi mtamu kumbe yule binti alikuwa akichanganya na damu zake zilizokuwa zinatoka ukeni!
Wakati nikiwa bado naendelea kupata msosi waliingia jamaa mmoja akiwa na mwanamke na bila shaka walikuwa mke na mume,Walipotengewa chakula kabla ya kula walifanya pale ishara ya msalaba kwa maana nadhani walikuwa wakiomba na hii ishara ya msalaba haikusaidia kitu kwani walilishwa uchafu kama wenzao!
Kiukweli ule mgahawa ulikuwa na wateja sana na yule mama kama ni pesa basi alikuwa akiingiza ki-kwelikweli!
Labda niseme kitu hapa kidogo!,Ndugu zangu ukiamua kuwa mfuasi wa kristo basi achana na mabo mengine ya duniani vinginevyo unaweza ukadhani Yesu anakulinda kumbe tu kwakuwa unashika mambo mawili mawili ukawa huna tofauti na watu wasiyosali!Wale jamaa waliongia na mkewe kwenye ule mgahawa inaonekana walikuwa wakimpenda sana Yesu kwa maneno ila matendo hakuna!,Kiukweli wangekuwa watu wa maombi wasingelishwa ule uchafu,lakini kwasababu wengi wetu dini tumezifanya kama fasheni ilikuwa haijawasaidia kitu!
Mimi mwenyewe kuna wakati nilishindwa kufanya tukio lolote la ushirikina kwasababu kuna watu niliokutana nao wakiwa na nguvu ya Yesu na nilishindwa pamoja na ujanja wangu wote!
Baada ya kuwa nimemaliza kula niliondoka zangu bila kulipa na yule mama aliniita kabla ya kuondoaka na akaanza kuniuliza "Vp mwenzetu wewe niwa nchi gani"?
Nilimwambia mimi natokea Kigoma na hapo nilipo nilikuwa safarini kurudi kigoma
Alikuwa akinishangaa sana kwa namna nilivyokuwa jasiri,na wakati huo naongea nae alikuwa uchi kama alivyozaliwa ila watu wengine walikuwa wakimuona kavaa nguo!
Nipomaliza kuzungumza nae nilimwambia mi naondoka zangu!
Basi nilitamka tu kwamba "Nahitaji hivi sasa kuwa Mwanza"
Ndani ya sekunde nilijikuta nipo Geto na kama kawaida nilikiweka kile kibuyu chini ya uvungu na mimi nilijipumzisha kidogo kisha baada ya kuamka nilielekea nyumbani kwa Bi mkubwa!
Itaendelea......................
Wakuu yeyote anayetaka kunitumia hela ya mafuta(Mbs)basi anaweza kunitumia kwenye namba hii 0768173820.Majina ni FREDERIKA JAMES
Nipigeni tafu ndugu zangu japo pia si lazima bali ni ombi tu ndugu zangu
[emoji38][emoji38][emoji38]alost mbaya sanaMkuu tayari angalia.
Mkuu sorry naomba Kama ikiwezekana chimbua chimbua kidogo kwenye hayo matukio unapo sababishia ajali. Naona Kama untupitisha juu kwa juu Ila niseme ukweli we jamaa unajua kusimulia big up kwako.MKASA WA PILI - Sehemu ya 19
Inaendelea.............
Baada ya kuwa nimepata zile pesa niliona kwanza nianze ukarabati wa nyumba yetu hiyo ya hapo Nyegezi!
Mama yangu alikuwa na wasiwasi pesa ya ukarabati nimepata wapi!,Nilimwambia mama kuna mahali nimepata kazi ya kufundisha na hivyo ninalipwa vizuri!.
Basi kauli ile ilimtoa mama wasiwasi
Ile nyumba nilianza kuikarabati upya na kuanzia hapo kila nilipokuwa nikipata pesa kutokana na ajali zile nilizokuwa nikisababisha hapo mjini Mwanza na miji kama Geita na Magu,niliendelea kuisuka upya nyumba yetu na ikawa ya kisasa kabisa kama nyumba za matajiri!
Ulikuwa ukifika hapo nyumbani huwezi kuamini maana nyumba ilikuwa kama ya waziri fulani!
Nyumbani hawakutia shaka sana maana uwezo niliokuwa nao wasingeweza kufahamu zaidi!
Miaka nayo ilikuwa ikienda mbio na mimi pia niliendelea kufanya kafara!,Kuna siku nilishika mkono wangu huu uliokuwa na Irizi nikaanza kuongea "Mbona kafara natoa lakini bado napata pesa kidogo?"
Sauti ilinijibu kwamba muda wa kuwa tajiri haujawadia ila uko karibu!
Hiyo ilikuwa mwaka sasa wa 2013
Basi siku moja nikiwa Geto nilisikia sauti ikiniambia nielekee Mkoani Singida maeneo ya Sekenke ambako ilipaswa kuna watu wafe ili niweze kupata mali nyingi!
Asubuhi ya siku hiyo sikutaka kabisa kupoteza muda!,Kuna dawa nilizichanganya hapo ndani kwangu na nikatamka ya kwamba "Nahitaji kufika sekenke Singida"
Ilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua!,Mpaka muda huu nilikuwa nishasema liwalo na liwe kama ni maji nishayavulia nguo sharti niyaoge!
Kwakuwa nilikuwa nina kiburi kwa wakati huo nilijiona kama hakuna wa kuniweza hapa duniani!
Nilipofika maeneo hayo ya Sekenke kuna gari ambayo nilielekezwa toka Mwanzo na ndani yake kuna abiria ambao walikuwa wakisakwa kwa udi na uvumba kutoka huko majini nilikotoka hivyo siku hiyo ilikuwa ndo Mwisho wao!
Basi kuna dawa niliitupa kwenye barabara na ile gari ilipofika yale maeneo ilipasuka tairi ya mbele na kukosa uelekeo hali iliyofanya kupiga mzinga wa maana!Kiukweli nilikuwa nina roho ya kikatili sana kwa wakati huo!,Nilikuwa sina huruma kabisa hata chembe!
Niliokuwa nina huruma nao ni ndugu zangu pamoja na mama yangu!
Baada ya ile gari kuwa imepata mzinga nilisogea pale na kukuta wale watu niliokuwa nimetageti wamebanwa na viti kwa chini,Nilifika nikawachinja kichawi na kuchukua damu zao!Pia nilichukua damu za abiria wengine waliokuwa wamekufa kwa wakati huo na nilihakikisha nawakausha kabisa wasiwe na damu hata tone!
Nilipomaliza nilifanya fasta na kuondoka zangu na mara hiyo nikawa pale geto,Nilichukua kile kibuyu kama kawaida nikakiweka uvunguni!
Niliondoka zangu kuelekea kwa Bi mkubwa kuangalia maendeleo ya nyumba!
Nilipojiridhisha ya kwamba mambo ni mazuri nilirudi zangu tena geto!
Safari hii nilikuta kitandani kwangu kuna begi kubwa yale ya mgongoni ambayo watoto wa shule wanayowekaga madaftari nikakuta limejaa pesa!
Siku hiyo nilikuwa nina furaha sana maana sikuwahi kukamata pesa nyingi kiasi hicho!
Sasa nikaanza kuzihesabu pale nilipata kama milioni thelathini na tano pesa za kitanzania (35,000,000/=)
Niliondoka hapo geto kwangu kuelekea Igoma na lengo ilikuwa ni kutafuta eneo nianze ujenzi!
Kuna dalali nilimpata maeneo ya huko Igoma jamaa akaniambia viwanja vipo lakini kuna nyumba zipo zinauzwa!
Alipo niambia nyumba zipo zinauzwa wazo la kununua uwanja nikalitoa kichwani!,Nilimwambia anipeleke kwenye hizo nyumba anazozifahamu zinazouzwa.
Jamaa alipeleka kwenye nyumba ya kwanza ambayo ilikuwa ya kawaida!,Tuliendelea kutembelea zile nyumba ambazo zilikuwa zikiuzwa na kuna nyumba tulifika kiukweli niliipenda sana!
Jamaa aliniambia nimwachie namba ya simu na atakomuniketi na tajiri wa hiyo nyumba halafu atanijulisha!
Basi nilipoachana na yule dalali wazo lingime ambalo nilikuwa nalo ni kutafuta mwanamke wa kuishi naye ambaye niliambiwa atakuwa akibeba ujauzito wale watoto watakuwa wanatolewa kafara!,Yaani yule mwanamke ntakuwa ninaishi naye kwa kazi hiyo tu!
Na yeye hapaswi kuelewa kitu!
Sasa akilini mwangu niliwaza kwamba nataka nimchukue yule shemeji yangu aliyekuwa na nyodo niwe nampiga shipa na yeye awe kama mke wangu kwa kazi hiyo tu!
Kiukweli nilitaka nimkomoe maana alikuwa na nyodo sana!
Ila nilitaka kwanza nikiisha inunua hiyo nyumba na kuvuta usafiri ndo nifanyie kazi ilo suala!
Nilirudi geto na kukuta tena pesa zimejaa kwenye lile lile begi ambalo mara ya kwanza nilitoa zile pesa!,Japo hazikuwa nyingi kama za mara ya kwanza,Safari hii nilipozihesabu ilikuwa kama milioni 20,Hivyo ukijumlisha na zile za mara kwa za ilikuwa kama milioni hamsini na tano(55,000,000/=),Kiukweli nilipagawa sana!
Nakumbuka siku hiyo nilimpigia mama yangu simu nikamwambia "Mama nimekuagizia gari na wiki hii itakuwa inaingia"
Bi mkubwa aliniuliza "Mwanangu pesa unatoa wapi"?,Niliendelea kumdanganya kwamba nimechukua mkopo kwenye kituo nilichokuwa ninafanya kazi kwa wakati huo!
Ndani ya wiki hiyo nilienda kwenye Show room moja iliyoko karibu na kamanga fery(nisingependa kuitaja) nilitoa pesa cash nikamnunulia Bi mkubwa Murano mpya!
Sasa kwakuwa mimi ilipaswa nikaonane na yule dalali wa Igoma nilimpigia simu nikamwambia anapelekea gari yake!
Kuna dereva wa pale show room nilimpa namba ya Bi mkubwa ili akifika maeneo yale amwelekeze!
Nilipofika Igoma yule dalali alinikutaniaha na mmiliki wa ile nyumba na nikaongea nae jamaa akasema nimpe milioni 60,kwa wakati huo nilikuwa nimebaki kama na milioni 30 maana pesa nyingine nilimnunulia Bi mkubwa gari, siku iliyofuata nilimpelekea na nikamwambia pesa nyingine ningempa siku si nyingi!,Lile jumba lilikuwa la kisasa halafu zuri,hivyo nikaona litanifaa kwenye mambo yangu!
Basi niliondoka kuelekea kwa Bi mkubwa na alifurahi sana maana sasa aliishi maisha kam mtu!
Kwakuwa hakujua kuendesha gari ilibidi nimtafutie dereva na nikawa namlipa kila mwezi!
Siku ziliendelea kusonga na siku moja nilielekea mkoani shinyanga kupiga tukio la kafara kama kawaida!
Itaendelea..............
Ni youtube mama sio uzi wa humuHebu nitag basi, hivi umeanza lini kunitosa kwenye mambo mazuri??
UPO SAHIHI KABISA.Ushauri kwa LwandaMagere we si upo mwanza mzee mtafute basi zabroni mwita akusaidie mtoe kitabu bila shaka wengi wana mjua ana kitabu cha sitoisahau gamboshi Maana ye alishachukuliwa na wachawi na kupelekwa ukogamboshi ila mungu mwema alifanikiwa kurudi duniani mzee kitabu hiki utapga pesa ndefu zabron alishapata mpaka m 100 na machenchi kupitia ushuhuda wake. kwa hicho kitabu chake alafu hapa usiache kusimulia, maliza na ukitoa kitabu utapiga pesa mim nimesoma kitabu chake zabron alinitumia kwa wasap through hard copy lakini pia kuna Chanel ipo YouTube ya davistar mata media story take ipo furu mpka zabron mwenyewe unamuona akisimulia na ameshawai simulia redio free Africa hii sitosahau gamboshi wengi humu wanamjua juzi kati ndio kamalizia story yake. Kwaiyo zabron alisimulia story yake ya maisha na akatoa na kitabu so asikuzie mtu kusimulia eti kisa autauza kitabu waongo, izo pesa sasa ndio utapata kwenye hiki kitabu. NB sija tangaza biashara ya mtu nimetoa ushauri kwa mshkaji maana naweza pokea mapovu kibao kwa watu ambao sio waelewa, ZABRON anafahamika na wengi wana mjua na hii story ya sitosahau GAMBOSHI mpaka boss wa publish jina kapuni ambae anajulikana kwa hadithi nyingi gazetini alitaka kumtapeli ambae saiz ni muheshimiwa mkubwa tu mjiongezee na bila shaka msha elewa ndio ivyo mzee ushauri wangu kwako.
Nilikuwa nashauri pia hizi contacts uziweke mwisho wa kila post yako, ili namba zako ziwe rahisi kuwa traced...!!Wakuu yeyote anayetaka kunitumia hela ya mafuta(Mbs)basi anaweza kunitumia kwenye namba hii 0768173820.Majina ni FREDERIKA JAMES
Nipigeni tafu ndugu zangu japo pia si lazima bali ni ombi tu ndugu zangu