Kashaija72
JF-Expert Member
- May 18, 2020
- 2,225
- 5,258
Daaah mwanangu hii dunia chafu sanaDaaah haya Mambo haya
Usikute hata ile ajali ya Majinjah mwaka ule Kuna chalii moja ilipiga pesa ndefu Sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Daaah mwanangu hii dunia chafu sanaDaaah haya Mambo haya
Usikute hata ile ajali ya Majinjah mwaka ule Kuna chalii moja ilipiga pesa ndefu Sana.
Kwahiyo watu walikuwa wanaenda chumvin bila kujua...ndo maaana kila nkienda kula baadhi ya migahawa huwa najikuta nadindishaMKASA WA PILI - Sehemu ya 21
Inaendelea.............
Nikiwa geto nilisikia sauti kama kawaida ikiniambia niende mbeya na nikifika hapo mbeya nitapewa ishara ya nini cha kufanya!
Kwakuwa tayari nishazoea ile hali hivyo nilikuwa siogopi wala kuwa na wasiwasi!
Kwa wakati ule sikuwa kabisa na akili nyingine zaidi ya kuona ninayafaidi maisha kwa maana kila nilichokitaka nilikipata kwa wakati!
Basi nilijiandaa na niliushika mkono wangu wa kushoto na kutamka "Ninataka niwe mbeya muda huu",ilikuwa ni kitendo cha kufumbua nikajikuta nipo uyole mbeya!
Kiukweli ile irizi ambayo iliwekwa mkononi mwangu na yule malikia kule chini ya ziwa Tanganyika ilikuwa na nguvu za ajabu na ilinipatia kiburi sana mpaka nikawa nawaoana binadamu wenzangu kama TAKA TAKA!
Namshukuru sana Mungu kwa kunitoa huko!Mungu ni mwema sana na uwezo,rehema na fadhili zake hazina kikomo!
Basi nilipofika yale maeneo kuna gari nililiona lilikuwa costa na kwa muonekano nililifahamu kwamba ndilo gari ambalo inapaswa nikalipige mzinga,Lilipofika yale maeneo nilipokuwa lilisimama na konda akawa anasema "Kyela hiyooooooo,twenzetu tukuyu mpaka kyela hiyoooooo!",Nilipanda ndani ya ile costa na kama kawaida sikulipa nauli na yule konda hata hakuniuliza kuhusu nauli!
Lile gari lilifika kwenye mji mmoja nadhani ulikuwa unaitwa Kimo kama sijakosea(Kama kuna wenyeji wa huko wanaosoma huu uzi watanikumbushia,maana ni muda kidogo),Huo Mji wa kimo ulikuwa kabla ya kufika Tukuyu!,Ile sauti iliniambia nishuke na niendee mbele ya Tukuyu kuelekea kyela kulikuwa kuna mtelemko mkali sana pale nikaisubiri pale!
Nilifanya kama ile sauti ilivyonitaka nifanye na nilipotea ghafla yale maeneo na nikafika eneo la tukio!
Kiukweli kilikuwa na mtelemko mkali sana yale maeneo na sikumbuki palikuwa wapi maana kulikuwa na miti mingi sana ile ya mbao!,Nadhani ni hapo hapo tukuyu kwa ndani ndani,Wenyeji wa huko watatusaidia!
Basi niliweka tego kama kawaida nikiwa nimeshika kibuyu cha kazi,Baada ya kusubili kwa muda niliiona ile costa ikiwa inakuja kwa mwendo wa kasi!,Ilipofika yale maeneo ilikula mzinga wa maana sana!
Niliisogelea ile costa na kwenda kuanza kuchukua kilichonipeleka!,Lakini ghafla ndani ya ile costa niliwaona akina mama wawili wakiwa wananiangalia wakisema "We mtoto unafanya nini"?
Wale kina mama walikuwa washirikina na watu wengine walipokuwa wamelaliwa na viti wao walikiwa wamekaa wakinikodolea macho!
Waliniita mimi mtoto si kwamba umri wangu nilikuwa mtoto bali walionyesha dharau kwamba mimi si lolote wala chochote!
Niliwaambia kwakuwa wameniita mimi mtoto ninataka niwaonyeshe mimi si mtoto kwenye ile kazi kama wao walivyodhani!,Kama nilivyosema hapo awali kwamba nilikuwa nina uwezo wa ajabu na kiburi kilikuwa kimenijaa sana!
Niliwasogelea na kuanza kushindana nao pale kichawi lakini nilipotamka ya kwamba "Naomba mkauke muwe kama samaki",haikuchukua muda walikuwa wamekauka kauuu!
Wao ndo walikuwa wa kwanza kuchukua damu yao na baada ya hapo nilianza kukusanya damu za abiria wengine!,Nilipomaliza kufanya lile zoezi nilipotea yale maeneo! Na nikatokezea pale nilipokuwa mwanzo Uyole!
Basi kwakuwa nilikuwa nina njaa kuna mgahawa mmoja ambao ulikuwa mkubwa tu kama hotel kwa ajili ya kupata chakula!,Nilipofika hapo kwa kuwa bado nilikuwa nimevaa uhusika wa kishirikina maana sikutaka bugudha!,Ile nimeingia ndani ya huo mgahawa niliona kina mama ambao walikuwa wakitoa huduma hapo hotelini walikuwa uchi wa mnyama!,Alikuwa mwanamke mmoja mnene na Binti yake ambaye pia alikuwa uchi!
Huyo binti yake yeye alikuwa akivuja damu kutoka kwenye uke wake na alikuwa akizichukua zile damu na kuziweka pakaza kwenye vile vyakula vya wateja walivyokuwa wamemwagiza!
Sasa kwa bahati mbaya sana hakuna mteja ambaye alikuwa akiona yale matukio yote isipokuwa mimi niliyekuwa na uwezo huo!Hicho ki-mgahawa kilikuwa kimechangamka sana maana hadi madereva wa magari makubwa niliona walikuwa wakiingia kula pale!,ukimuondoa yule mama na yule Binti niliyewakuta uchi pale pia kulikuwa na wahudumu wengine wawili,Mmoja alikuwa mpishi na mwingine pia alikuwa akihudumia lakini hawa wao walikuwa wamevaa nguo zao tu za kawaida!
Sikupata shida kuelewa kwamba yule mama ndiye alikuwa mmiliki wa ule mgahawa na yule aliyekuwa akivuja damu ukeni alikuwa binti yake wa kumzaa!
Yule mama aliponiona tu alinifanyia ishara ya kidole kwamba nikae kimya!Yule binti alikuwa akinitolea macho na nilimuona anakuwa na wasiwasi!
Basi nilimwita yule mwanamke nikamwambia aniletee chakula ila kiwe kisafi tofauti na hapo ningemuumbua!
Alimwita yule binti aliyekuwa kavaa nguo akamwambia "Mpe yule kaka chakula"
Zilikuja ndizi zimejaa sahani na nyama na kwakuwa nilikuwa nina uwezo wa kukiangalia kama ni kisafi ama la!,baada ya kujiridhisha kilikuwa kisafi kwa maana kwamba hawakuweka mambo yao ya kishirikina nilianza kula!
Wakati nakula watu wengi walikuwa wakiingia kupata msosi wakiamini ni msosi mtamu kumbe yule binti alikuwa akichanganya na damu zake zilizokuwa zinatoka ukeni!
Wakati nikiwa bado naendelea kupata msosi waliingia jamaa mmoja akiwa na mwanamke na bila shaka walikuwa mke na mume,Walipotengewa chakula kabla ya kula walifanya pale ishara ya msalaba kwa maana nadhani walikuwa wakiomba na hii ishara ya msalaba haikusaidia kitu kwani walilishwa uchafu kama wenzao!
Kiukweli ule mgahawa ulikuwa na wateja sana na yule mama kama ni pesa basi alikuwa akiingiza ki-kwelikweli!
Labda niseme kitu hapa kidogo!,Ndugu zangu ukiamua kuwa mfuasi wa kristo basi achana na mabo mengine ya duniani vinginevyo unaweza ukadhani Yesu anakulinda kumbe tu kwakuwa unashika mambo mawili mawili ukawa huna tofauti na watu wasiyosali!Wale jamaa waliongia na mkewe kwenye ule mgahawa inaonekana walikuwa wakimpenda sana Yesu kwa maneno ila matendo hakuna!,Kiukweli wangekuwa watu wa maombi wasingelishwa ule uchafu,lakini kwasababu wengi wetu dini tumezifanya kama fasheni ilikuwa haijawasaidia kitu!
Mimi mwenyewe kuna wakati nilishindwa kufanya tukio lolote la ushirikina kwasababu kuna watu niliokutana nao wakiwa na nguvu ya Yesu na nilishindwa pamoja na ujanja wangu wote!
Baada ya kuwa nimemaliza kula niliondoka zangu bila kulipa na yule mama aliniita kabla ya kuondoaka na akaanza kuniuliza "Vp mwenzetu wewe niwa nchi gani"?
Nilimwambia mimi natokea Kigoma na hapo nilipo nilikuwa safarini kurudi kigoma
Alikuwa akinishangaa sana kwa namna nilivyokuwa jasiri,na wakati huo naongea nae alikuwa uchi kama alivyozaliwa ila watu wengine walikuwa wakimuona kavaa nguo!
Nipomaliza kuzungumza nae nilimwambia mi naondoka zangu!
Basi nilitamka tu kwamba "Nahitaji hivi sasa kuwa Mwanza"
Ndani ya sekunde nilijikuta nipo Geto na kama kawaida nilikiweka kile kibuyu chini ya uvungu na mimi nilijipumzisha kidogo kisha baada ya kuamka nilielekea nyumbani kwa Bi mkubwa!
Itaendelea......................
𝕂𝕦𝕟𝕒 𝕞𝕦𝕕𝕒 𝕞𝕒𝕞𝕓𝕠 𝕞𝕒𝕫𝕦𝕣𝕚 𝕙𝕦𝕥𝕠𝕜𝕒𝕟𝕒 𝕟𝕒 𝕪𝕒𝕝𝕖 𝕞𝕒𝕓𝕒𝕪𝕒 𝕞𝕜𝕦𝕦. 𝕟𝕒𝕥𝕒𝕜𝕒 𝕟𝕚𝕥𝕖𝕤𝕥 𝕞𝕚𝕥𝕒𝕞𝕓𝕠 𝕞𝕨𝕚𝕤𝕙𝕠 𝕨𝕒 𝕞𝕨𝕒𝕜𝕒 𝕙𝕦𝕦[emoji4][emoji4][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Naona Jambo limekukonga moyo
[emoji23][emoji23]Kwahiyo watu walikuwa wanaenda chumvin bila kujua...ndo maaana kila nkienda kula baadhi ya migahawa huwa najikuta nadindisha
Hii habari imenitisha. Siku chache zilizopita nimetoka kupata msosi kwenye mgahawa hapo hapo Uyole karibu na zinapopaki Coaster za Dar.Kanuni ya maisha yangu huwa sipendelei kupata chakula kwenye mgahawa wenye wateja wengi maana mingi huwa haina chakula halisi zaidi ya Ushetani.
Ulete mkuu watu wapate dawa.Yaah ni kweli huo mti upo Tabora kwa wingi tu hasa wilaya za uyui,sikonge na urambo sie wakazi wa huko tunaujua ila ni lazima upate dawa nyingine flan ya kuchanganyia kabla ujaiweka kwenye chai au uji. Na sie kule wamama wanalijua wakaiona mzee anatumia wanaaga kwenda kwao kwa mida na vile vile sometimes wengine huwa wanaotumia kutibia uhanithi.
Acha niendelee kuupitia na huu uzi wakati nasubiria hapaHadithi: Uchawi wa bilionea Bazoka
NYEMO CHILONGANI. UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA. 0718069269 Ndiyo kwanza mwanga wa asubuhi ulikuwa ukitokeza, watu waliokuwa wakifanya kazi sehemu za mbali, wakaamka na kuanza kujiandaa kwenda makazini, kwa wale waliokuwa njiani kuelekea makazini kwao, wakaongeza kasi ili kuwahi na kuanza kazi...www.jamiiforums.com
Nafanya mipango ya kukutoa kafara
Mi sijaendaVenye naona wakaka wamejazana pm kuhusu mti wa kupiga shipa la kimkakati 😊
Hii habari imenitisha. Siku chache zilizopita nimetoka kupata msosi kwenye mgahawa hapo hapo Uyole karibu na zinapopaki Coaster za Dar.
Warume ndago mnakiu hatari 😀😀Mkuu mkuu LwandaMagere huu ni mda mzuri Sana kama ukitupiga ka episode kamoja
Au mnasemaje wazee wenzangu
𝕦𝕝𝕖 𝕞𝕥𝕚 𝕨𝕒𝕫𝕖𝕖Warume ndago mnakiu hatari [emoji3][emoji3]
Amen[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Bora umeamua kuwa mkweli...kila la kheri
Ni uzi unaanza hovyo ila mbele wa motoAcha niendelee kuupitia na huu uzi wakati nasubiria hapa
Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
ile ilisemekana ni ugomvi wa maderevaDaaah haya Mambo haya
Usikute hata ile ajali ya Majinjah mwaka ule Kuna chalii moja ilipiga pesa ndefu Sana.
Nilikua bize ndio nika andika nais ni mmoja ambae umepata nimekutumia copyHutoingia tena humu!!!??
Hapana kaka mkubwa sijapataNilikua bize ndio nika andika nais ni mmoja ambae umepata nimekutumia copy