Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Dah natamani hata ungekuwa unaweka episode kumi ili sisi tuhangaike nazo tu wakati we unajipanga kuandika upya
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 14.


Inaendelea.............



Tuliendelea na safari kwa muda mrefu na kwakuwa ilikuwa mchana niliendelea kulishangaa ziwa Tanganyika namna lilivyokubwa na kwa upande wa Kongo kiukweli kulikuwa na misitu mikubwa sana!.Ile nchi ya Kongo ilibarikiwa sana kuwa na uoto wa asili na kijani kibichi.Kwenye lile boti kulikuwa na vijana 5 lakini mmoja wao ambaye ndiye niliyemlipa kile kiasi cha fedha ilionekana kama ndiye Bosi wa ile boti,ile boti ilikuwa ni boti fulani tu la mbao lakini lilikuwa limepachikwa injini,nilimuuliza jamaa itatuchukua muda gani mpaka kufika Kalemii?,jamaa aliniambia ingetuchukua kama masaa 3.Basi kweli,baada ya masaa 3 tulikuwa tumefika Kalemii,Kiukweli ule mji wa Kalemii ulikuwa mkubwa sana kama vile kigoma tu!,Kwakuwa mimi safari yangu haikuishia pale nilimuuliza jamaa aniambie namna ya kufika kwenye kijiji cha Kirungu!,jamaa alishangaa sana na kuniuliza "Kirungu unaenda kufanya nini?".

Nilimwambia kuna shughuli ilikuwa inanipeleka huko.Jamaa aliniambia kwamba,kijiji cha Kirungu kiko mbali kutoka hapo Kalemii na endapo nikitumia usafiri wa pikipiki itanighraimu pesa nyingi,pia kupita maporini huko kungekuwa na uwezekano kukutana na waasi wakanifanya kitu mbaya!.Yale maeneo tuliyokuwa tumetia nanga yalikuwa nje ya bandari ya Kalemii kwasababu inaonekana wale jamaa walikuwa wanafanya biashara za magumashi hivyo walikwepa mkono wa serikali.Jamaa aliniambia hiyo Kirungu ipo kusini mwa Kalemii hivyo ningepaswa kutumia njia ya maji ili iwe rahisi mimi kufika huko,jamaa aliendelea kunipatia maelekezo kwamba kabla ya kufika Kirungu,kuna bandari bubu inaitwa Moba,sasa nikishafika hapo Moba nitatafuta bodaboda za kunipeleka Kirungu maana ukitoka hapo Moba kwenda Kirungu hakukuwa mbali.
Aliniambia "itabidi nikutafutie bodaboda akupeleke ng'ambo ya pili kuukwepa mji halafu kuna njia ya kurudi tena ziwani kwa ng'ambo ya kusini!,utakapofika huko lazima utazikuta boti za kwenda Moba,na ukifika Moba ni kama umefika Kirungu!".Basi nilishuka ndani ya lile boti jamaa akanitafutia boda maeneo yale.

Yule jamaa alimwambia "Mpeleke huyu jamaa kwenye boti za kwenda Moba".

Yule bodaboda aliniambia nimpe faranga elfu 3.Tuliondoka zetu kupita mitaani ambako alikuelewa yeye,ule mji ulikuwa umechangamka sana nami kama kawaida niliendelea kushangaa mitaa hiyo ya mji wa Kalemii,baada ya muda si mrefu jamaa alifika maeneo ya ziwani kwa upande wa kusini,alinielekeza mahali ambapo kulikuwa kuna maboti ya mbao kibao yamepaki pembeni mwa ziwa.Niliachana na yule jamaa wa bodaboda kisha nikaelekea kutafuta usafiri wa boti unaoelekea huko Moba.Kuna jamaa mmoja nilimkuta anafuma nyavu za samaki nikamsalimia,jamaa alionekana anakifahamu kiswahili vyema,nilimuomba anielekeze wapi ambapo ningepata usafiri wa kwenda Moba.Jamaa aliniambia mara nyingi usafiri wa kwenda Moba unategemeana na mizigo ya kwenda huko,kama hakuna mizigo inakuwa ngumu sana kwenda huko labda nipite barabarani!.Nilianza kuishiwa nguvu pale maana sikutaka kupita barabarani kwa maana sikuwa na pasipoti na ukizingatia ile nchi ya Kongo kulikuwa na mambo ya Waasi,hivyo nilijua inaweza kuniingiza matatizoni.

Jamaa aliniambia "kwanini nisikodi mtumbwi ukupeleke Moba?".

Nilimuuliza "gharama za kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani?".

Jamaa aliniambia "ni namna mtakavyoelewana na mwenye mtumbwi!".

Basi nilimwambia yule jamaa aniulizie kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani kwa wale wavuvi wenzie,Kuna jamaa alikuja pale tukaanza kuelewana naye na alikubali kunipeleka ila alitaka nimlipe faranga elfu 40.Kabla ya kuondoka maeneo hayo nilimuomba jamaa anielekeze maeneo ya kupata chakula maana nilikuwa nina njaa sana!.Muda huo ilikuwa saa 8 mchana.Jamaa alinichukua mpaka kwenye banda moja lililokuwa jirani nikakuta wanauza vyakula kadhaa wa kadhaa,mimi niliagiza wali samaki,nilipomaliza kupata msosi nilishusia na maji,nikamlipa yule mama faranga elfu 2 nikaondoka zangu!.Jamaa tuliyekubalina kunipeleka Moba alimchukua rafiki yake mwingine hivyo kwenye ule mtumbwi tukawa watu 3,mimi nilikaa katikati na kibegi changu halafu wale jamaa mmoja alikaa nyuma na mwingi mbele wakaanza kupia makasia!.Tuliyakata maji kwa umbali mrefu sana na mida ya saa 11 jioni tukawa tumefika pale Moba,nakumbuka jamaa alinielekeza kwamba nikifika hapo Moba nitafute usafiri wa kunipeleka Kirungu maana haikuwa mbali.Nilitafuta usafiri pale Moba nikafanikiwa kupata na safari ya kuelekea Kirungu ilianza.Wakati tukiwa njiani nilijaribu kumuuliza yule dereva wa bodaboda kama anamfahamu mganga maarufu maeneo hayo ya Kirungu aliyekuwa akiitwa Nchibaronda!.Jamaa aliniambia alikuwa akimfahamu hiyo mzee na angenipeleka mpaka kwake maana alikuwa anakaa nje ya mji wa Kirungu huko milimani maporini!.

Baada ya mwendo mrefu tuliingia hapo mjini Kirungu,kiukweli Kongo nilipapenda kwasababu kila mji ulikuwa mkubwa na ulikuwa na huduma zote mpaka usafiri wa angani,yaani unakuta mji ni mdogo tu lakini mpaka una kiwanja cha ndege tofati kabisa na Tanzania ambapo viwanja vya ndege ni kwenye miji mikubwa ambayo ni makao makuu ya mikoa lakini Kongo ilikuwa tofauti kidogo!.Tuliikamata barabara ya kuelekea huko milimani kwa mzee Nchibaronda na haikuchukuwa muda mrefu tukawa tumefika.Nilimlipa yule dereva wa bodaboda pesa tuliyokuwa tumekubaliana na akanielekeza kwa mzee Nchibaronda,nilitembea kidogo maana haikuwa mbali na pale jamaa aliponiacha.Nilipofika hapo kwa huyo mzee nilipokelewa na mama mmoja na nilikaribishwa kwa lugha ya lingala "boyei bolamu",alimaanisha "Karibu".

Sasa kwakuwa mimi nilikuwa sielewi lingala na kifaransa nilimuitikia kwa kiswahili "Ahsante".

Nilipokuwa huko kuna maneno baadhi ya lugha ya lingala nilikuwa nimeshayaelewa,hivyo sikupata taabu sana.Baada ya kuwa nimekaribishwa niliambiwa nikae hapo nje maana mtaalamu (Mganga)alikuwa kaenda porini kuwaagua watu.Mpaka hapo kwa mzee ilikuwa mida ya saa 12 jioni.Kiukweli nilikuta kuna watu wengi,kuna jamaa wawili walikuwa wametoka Tanzania,nilipowaona nilijua tu zilikuwa chata kutoka Tanzania maana mbongo anafahamika tu hata mkikutana naye nchi za watu!.Niliwasalimia kwa bahati nzuri walinionyeshea ushirikiano,mmoja alikuwa mnene alionyesha alikuwa na maisha mazuri,basi hatukupiga sana stori maana niliona kama wana nikwepa ile kiaina!.

Kwenye hilo eneo la mganga Nchibaronda kulikuwa na vijumba vingi vya nyasi vilivyokuwa vidogo vidogo!,kama kawaida ya pale pia ulipofika usiku walikoka moto tukawa tunaota nje.Ilipofika mida ya saa 2 usiku yule mzee Nchibaronda alifika na alisema wageni waitwe waingie ndani mmoja mmoja,sasa kwakuwa mimi kuna watu niliwakuta pale ilibidi waanze wao,zamu yangu ilipofika ilikuwa mida ya saa 4 usiku,nilipofika ndani nilimsalimia yule mzee,kabla ya kuongea naye chochote nilitoa kile kingozi kilichokuwa kimekazwa kama kijiti ambacho nilipewa kule Kasulu na yule mama akaniambia ile ni rufaa ya mimi kwenda pale nikampatia mzee Nchibaronda. Mzee Nchibaronda alikipokea akaniambia alifahamu ninakuja na alikuwa akiniona kila hatua niliyopiga,Yule Mzee aliniambia kwamba hapo kwake nimefata utajiri na nitaupata;Nilishangaa sana yule mzee aliwezaje kufahamu kama mimi pale nilikuwa nimefata utajiri!.

Aliniuliza "Je utaweza?".

Kwakuwa nilikuwa nimedhamiria nilimwambia "Nitaweza".

Mzee Nchibaronda aliniambia hakuna aliyefata hapo kwake utajiri akashindwa kufanikiwa,aliendelea kuniambia kwamba hata hao watanzania niliyowakuta hapo nje walikuwa wamekuja kumlipa shukurani baada ya kufanikiwa kwenye shughuli zao.Baada ya mazungumzo mle ndani aliniambia kwakuwa kazi yangu ilikuwa ngumu,alinitaka nikae pale wiki nzima maana kuna safari ya kwenda ziwa Tanganyika ambako huko ndiko nitapatiwa utajiri,na akaendelea kusisitiza kwamba yupo atakayenipa utajiri ila siyo yeye!,Yeye kazi ambayo angeifanya ni kuniandaa kuweza kuishi na huo utajiri,pia aliniambia kwamba kazi yake ilikuwa kuniweka sawa ili safari ya kwenda ziwani itakapofika nisije kupata madhara!.


Itaendelea................
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 14

Inaendelea.............

Tuliendelea na safari kwa muda mrefu na kwakuwa ilikuwa mchana niliendelea kulishangaa ziwa Tanganyika namna lilivyokubwa na kwa upande wa Kongo kiukweli kulikuwa na misitu mikubwa sana!
Ile nchi ya Kongo ilibarikiwa sana kuwa na uoto wa Asili na kijani kibichi!

Kwenye lile boti kulikuwa na vijana 5 lakini mmoja wao ambaye ndiye niliyemlipa kile kiasi cha fedha ilionekana kama ndiye Bosi wa ile Boti,Ile boti ilikuwa ni boti fulani tu la mbao lakini lilikuwa limepachikwa injini lakini ilikuwa kubwa!,Nilimuuliza jamaa itatuchukua muda gani mpaka kalemii,Jamaa akanambia kama masaa 3!
Basi kweli,baada ya Masaa 3 tulikuwa tumefika kalemii!,Kiukweli ule mji wa kalemii ulikuwa mkubwa sana kama vile kigoma tu!,

Kwakuwa mimi safari yangu haikuishia pale nilimuuliza jamaa aniambie namna ya kufika kwenye kijiji cha Kirungu!,Jamaa alishangaa sana "Kirungu unaenda kufanya nini"?
Nilimwambia kuna shughuli inanipeleka kule!
Jamaa alinambia Kijiji cha kirungu kiko mbali kutoka hapo kalemii na endapo nikitumia Usafiri wa pkpk itanighraimu pesa nyingi,pia kupita maporini huko kuna uwezekano kukutana na waasi wakanifanya kitu mbaya !

Yale maeneo tuliyokuwa tumetia nanga yalikuwa nje kidogo ya Bandari ya kalemii kwasababu inaonekana wale jamaa walikuwa wanafanya Biashara za magumashi hivyo walikwepa mkono wa serikali!
Jamaa aliniambia hiyo kirungu ipo kusini mwa Kalemii hivyo ningepaswa kutumia njia ya maji ili iwe rahisi mimi kufika huko!,Jamaa aliendelea kunipatia maelekezo pale kwamba Kabla ya kufika Kirungu kuna Bandari bubu inaitwa Moba,sasa nikishafika hapo Moba nitatafuta bodaboda za kunipeleka Kirungu maana ukitoka hapo Moba kwenda Kirungu si mbali!

Aliniambia sasa hapo Kalemii itabidi nikutafutie bodaboda akupeleke ng'ambo ya pili kuukwepa mji halafu kuna njia ya kurudi tena ziwani kwa ng'ambo ya kusini!,Utakapofika huko lazima utazikuta boti za kwenda Moba,na ukifika Moba ni kama umefika Kirungu!

Basi nilishuka pale nikatafuta Boda maeneo yale na nilimpo mpata nilimwambia jamaa amwelekeze namna nilivyo mwambia!,Yule jamaa alimwambia "Mpeleke huyu jamaa kwenye Boti za kwenda Moba",Yule Boda aliniambia nimpe faranga 3000!
Tuliondoka zetu kupita mitaani ambako alikuelewa yeye,Ule mji ulikuwa umechangamka sana nami kawa kawaida niliendelea kushangaa mitaa hiyo ya kalemii,Baada ya muda si mrefu jamaa alifika maeneo ya ziwani kwa upande wa kusini!,alielekeza kulikuwa kuna maboti ya mbao kibao yamepaki pembeni mwa ziwa!

Niliachana na yule jamaa wa Boda boda pale mi nkaelekea kutafuta usafiri wa boti unaoelekea huko Moba!
Kuna jamaa mmoja nilimkuta pale anafuma nyavu za samaki na nikamsalimia!,Jamaa alionekana kama kiswahili anakijua vyema na nilimuomba anielekeze wapi ambapo ningepata usafiri wa kwenda Moba!
Jamaa aliniambia mara nyingi usafiri wa kwenda Moba unategemeana na mizigo ya kwenda huko ila kama hakuna mizigo inakuwa ngumu sana kwenda huko labda nipite barabarani!

Nilianza kuishiwa nguvu pale maana sikutaka kupita barabarani kwa maana sikuwa na pasipoti na ukizingatia ile nchi ya Kongo kulikuwa na mambo ya Waasi,hivyo nilijua inaweza kuniingiza matatani!
Jamaa aliniambia kwanini nisikodi mtumbwi unipeleke Moba?,Nilimuuliza gharama za kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani?,Jamaa aliniambia ni namna nitakavyoelewana na mwenye mtumbwi!

Basi nilimwambia yule jamaa aniulizie kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani kwa wale wavuvi wenzie!
Kuna jamaa alikuja pale tukaanza kuelewana nae na alikubali kunipeleka ila nimlipe faranga 40000/=,nilimlipa ile hela nami nikabaki mfukoni kama na faranga 38000/=,Hizi faranga nilizobaki nazo ni zile nilizochenji Kule kigoma na nilikuwa na pesa za kitanzania kama 202000/=

Kabla ya kuondoka maeneo hayo nilimuomba jamaa anielekeze maeneo ya kupata chakula maana nilikuwa nina njaa sana!
Muda huo ilikuwa kama saa 8 mchana!,Jamaa alinichukua mpaka kwenye banda moja lililokuwa jirani nikakuta wanauza vyakula kadhaa wa kadhaa,Mimi niliagiza wali samaki,Nilipomaliza kupata msosi nilishusia na maji na nikamlipa yule mama pale kama faranga 2000/= nikaondoka zangu!

Jamaa alimchukua rafiki yake mwingine hivyo kwenye ule mtumbwi tukawa watu 3,mimi nilikaa katikati na kibegi changu halafu wale jamaa mmoja alikaa nyuma na mwingi mbele wakaanza kupia makasia!
Tuliyakata maji kwa umbali mrefu sana na mida ya saa kumi na moja tukawa tumefika pale Moba,Nakumbuka Jamaa alinielekeza kwamba nikifika hapo moba nitafute usafiri wa kunipeleka Kirungu maana si mbali!
Nilitafuta usafiri pale Moba nikafanikiwa kupata na safari ya kuelekea kirungu ilianza!
Wakati tukiwa njiani nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa boda boda kama anamfahamu mganga maarufu maeneo hayo ya Kirungu anafahamika kama Nchibaronda!
Jamaa aliniambia alikuwa akimfahamu na atanipeleka mpaka kwake maana alikuwa anakaa nje ya mji wa Kirungu huko milimani maporini!

Baada ya mwendo mrefu tuliingia hapo mjini kirungu,Kiukweli mimi Kongo nilipapenda kwasababu kila mji ulikuwa mkubwa na ulikuwa na huduma zote mpaka usafiri wa Anga,yaani unakuta mji ni mdogo tu lakini mpaka una kiwanja cha ndege tofati kabisa na Tanzania ambapo viwanja vya ndege ni kwenye miji mikubwa ambayo ni makao makuu ya mikoa lakini kongo ilikuwa tofauti kidogo!
Tuliikamata barabara ya kuelekea huko milimani kwa Nchibaronda na haikuchukuwa muda mrefu tukawa tumefika pale!

Nilimlipa jamaa pesa tuliyokuwa tumekubaliana na akanielekeza kwa Mzee Nchibaronda!,Nilitembea kidogo maana haikuwa mbali na pale Boda aliponiacha!
Nilipofika hapo kwa huyo mzee nilipokelewa na mama mmoja na nilikaribishwa kwa lugha ya kilingala "boyei bulamu"
Boyei bulamu alimaanisha "Karibu",sasa kwakuwa mimi nilikuwa sielewi kilingala na kifaransa nilimwitikia kwa kiswahili "Ahsante"
Nilipokuwa huko kuna maneno baadhi ya lugha ya kilingala nilikuwa nimeshayaelewa hivyo sikupata taabu sana!

Baada ya kuwa nimekaribishwa niliambiwa nikae hapo nje maana mtaalamu (Mganga)kuna watu kaenda nao polini kuwaagua!
Hiyo ilikuwa mida ya saa 12 jioni mpaka nafika pale!
Kiukweli nilikuta kuna watu wengi kidogo na kuna jamaa kama wawili walikuwa wametoka Tanzania,nilipowaona nilijua tu hizi njema ni kutoka Bongoland maana mbongo anafahamika tu hata mkikutana nae nchi za watu!
Niliwasalimia na kwa bahati nzuri walinionyeshea ushirikiano,mmoja alikuwa mnene alionyesha alikuwa na maisha mazuri,basi hatukupiga sana stori maana niliona kama wana nikwepa ile kiaina!

Kwenye hilo eneo la Mganga Nchibaronda kulikuwa na vijumba vingi vya nyasi vilivyokuwa vidogo vidogo!,kama kawaida ya pale pia ulipofika usiku walikoka moto tukawa tunaota pale nje!
Ilipofika mida kama ya saa 2 Usiku yule Mzee Nchibaronda alifika na Alisema wageni waitwe waingie mmoja mmoja,sasa kwakuwa mimi kuna watu niliwakuta pale ilibidi waanze wao!,Zamu yangu ilifika ilikuwa kama mida ya saa 4 za usiku!,Nilipofika ndani nilimsalimia yule Mzee na kabla ya kuongea nae chochote nilitoa kile kingozi kilichokuwa kimekazwa kama kijiti ambacho nilipewa kule Kasulu na yule Mama akiambia ile ni rufaa ya mimi kwenda pale!

Mzee Nchibaronda alikipokea na akaniambia alifahamu ninakuja na alikuwa akiniona kila hatua niliyopiga,Yule Mzee aliniambia hata kabla sijamweleza chochote mimi pale nimefata utajiri na nitaupata!
Aliniuliza "JE UTAWEZA"?,kwakuwa nilikuwa nimedhamiria nilimwambia "Nitaweza"
Mzee Nchibaronda aliniambia hakuna aliyefata hapo kwake utajiri na akashindwa kufanikiwa kwani wote wanafanikiwa,Aliendelea kuniambia kwamba hata hao watanzania niliowakuta hapo nje wamekuja kumlipa shukurani baada ya kufanikiwa kwenye shughuli zao!

Baada ya mazungumzo mle ndani aliniambia kwakuwa kazi yangu ilikuwa ngumu kidogo alinitaka nikae pale wiki nzima maana kuna safari ya kwenda ziwa Tanganyika ambako huko ndiko nitapatiwa utajiri,na akaendelea kusisitiza kwamba yupo atakayenipa Utajiri ila siyo yeye!,Yeye kazi ambayo angeifanya ni kuniandaa ili safari ya kwenda Ziwani itakapofika nisije kupata madhara!


Itaendelea................
Arostoooooooo
 
Kila unapofika ndo stry inazd kuwa ndefu...🙌🏽🙌🏽
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 14

Inaendelea.............

Tuliendelea na safari kwa muda mrefu na kwakuwa ilikuwa mchana niliendelea kulishangaa ziwa Tanganyika namna lilivyokubwa na kwa upande wa Kongo kiukweli kulikuwa na misitu mikubwa sana!
Ile nchi ya Kongo ilibarikiwa sana kuwa na uoto wa Asili na kijani kibichi!

Kwenye lile boti kulikuwa na vijana 5 lakini mmoja wao ambaye ndiye niliyemlipa kile kiasi cha fedha ilionekana kama ndiye Bosi wa ile Boti,Ile boti ilikuwa ni boti fulani tu la mbao lakini lilikuwa limepachikwa injini lakini ilikuwa kubwa!,Nilimuuliza jamaa itatuchukua muda gani mpaka kalemii,Jamaa akanambia kama masaa 3!
Basi kweli,baada ya Masaa 3 tulikuwa tumefika kalemii!,Kiukweli ule mji wa kalemii ulikuwa mkubwa sana kama vile kigoma tu!,

Kwakuwa mimi safari yangu haikuishia pale nilimuuliza jamaa aniambie namna ya kufika kwenye kijiji cha Kirungu!,Jamaa alishangaa sana "Kirungu unaenda kufanya nini"?
Nilimwambia kuna shughuli inanipeleka kule!
Jamaa alinambia Kijiji cha kirungu kiko mbali kutoka hapo kalemii na endapo nikitumia Usafiri wa pkpk itanighraimu pesa nyingi,pia kupita maporini huko kuna uwezekano kukutana na waasi wakanifanya kitu mbaya !

Yale maeneo tuliyokuwa tumetia nanga yalikuwa nje kidogo ya Bandari ya kalemii kwasababu inaonekana wale jamaa walikuwa wanafanya Biashara za magumashi hivyo walikwepa mkono wa serikali!
Jamaa aliniambia hiyo kirungu ipo kusini mwa Kalemii hivyo ningepaswa kutumia njia ya maji ili iwe rahisi mimi kufika huko!,Jamaa aliendelea kunipatia maelekezo pale kwamba Kabla ya kufika Kirungu kuna Bandari bubu inaitwa Moba,sasa nikishafika hapo Moba nitatafuta bodaboda za kunipeleka Kirungu maana ukitoka hapo Moba kwenda Kirungu si mbali!

Aliniambia sasa hapo Kalemii itabidi nikutafutie bodaboda akupeleke ng'ambo ya pili kuukwepa mji halafu kuna njia ya kurudi tena ziwani kwa ng'ambo ya kusini!,Utakapofika huko lazima utazikuta boti za kwenda Moba,na ukifika Moba ni kama umefika Kirungu!

Basi nilishuka pale nikatafuta Boda maeneo yale na nilimpo mpata nilimwambia jamaa amwelekeze namna nilivyo mwambia!,Yule jamaa alimwambia "Mpeleke huyu jamaa kwenye Boti za kwenda Moba",Yule Boda aliniambia nimpe faranga 3000!
Tuliondoka zetu kupita mitaani ambako alikuelewa yeye,Ule mji ulikuwa umechangamka sana nami kawa kawaida niliendelea kushangaa mitaa hiyo ya kalemii,Baada ya muda si mrefu jamaa alifika maeneo ya ziwani kwa upande wa kusini!,alielekeza kulikuwa kuna maboti ya mbao kibao yamepaki pembeni mwa ziwa!

Niliachana na yule jamaa wa Boda boda pale mi nkaelekea kutafuta usafiri wa boti unaoelekea huko Moba!
Kuna jamaa mmoja nilimkuta pale anafuma nyavu za samaki na nikamsalimia!,Jamaa alionekana kama kiswahili anakijua vyema na nilimuomba anielekeze wapi ambapo ningepata usafiri wa kwenda Moba!
Jamaa aliniambia mara nyingi usafiri wa kwenda Moba unategemeana na mizigo ya kwenda huko ila kama hakuna mizigo inakuwa ngumu sana kwenda huko labda nipite barabarani!

Nilianza kuishiwa nguvu pale maana sikutaka kupita barabarani kwa maana sikuwa na pasipoti na ukizingatia ile nchi ya Kongo kulikuwa na mambo ya Waasi,hivyo nilijua inaweza kuniingiza matatani!
Jamaa aliniambia kwanini nisikodi mtumbwi unipeleke Moba?,Nilimuuliza gharama za kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani?,Jamaa aliniambia ni namna nitakavyoelewana na mwenye mtumbwi!

Basi nilimwambia yule jamaa aniulizie kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani kwa wale wavuvi wenzie!
Kuna jamaa alikuja pale tukaanza kuelewana nae na alikubali kunipeleka ila nimlipe faranga 40000/=,nilimlipa ile hela nami nikabaki mfukoni kama na faranga 38000/=,Hizi faranga nilizobaki nazo ni zile nilizochenji Kule kigoma na nilikuwa na pesa za kitanzania kama 202000/=

Kabla ya kuondoka maeneo hayo nilimuomba jamaa anielekeze maeneo ya kupata chakula maana nilikuwa nina njaa sana!
Muda huo ilikuwa kama saa 8 mchana!,Jamaa alinichukua mpaka kwenye banda moja lililokuwa jirani nikakuta wanauza vyakula kadhaa wa kadhaa,Mimi niliagiza wali samaki,Nilipomaliza kupata msosi nilishusia na maji na nikamlipa yule mama pale kama faranga 2000/= nikaondoka zangu!

Jamaa alimchukua rafiki yake mwingine hivyo kwenye ule mtumbwi tukawa watu 3,mimi nilikaa katikati na kibegi changu halafu wale jamaa mmoja alikaa nyuma na mwingi mbele wakaanza kupia makasia!
Tuliyakata maji kwa umbali mrefu sana na mida ya saa kumi na moja tukawa tumefika pale Moba,Nakumbuka Jamaa alinielekeza kwamba nikifika hapo moba nitafute usafiri wa kunipeleka Kirungu maana si mbali!
Nilitafuta usafiri pale Moba nikafanikiwa kupata na safari ya kuelekea kirungu ilianza!
Wakati tukiwa njiani nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa boda boda kama anamfahamu mganga maarufu maeneo hayo ya Kirungu anafahamika kama Nchibaronda!
Jamaa aliniambia alikuwa akimfahamu na atanipeleka mpaka kwake maana alikuwa anakaa nje ya mji wa Kirungu huko milimani maporini!

Baada ya mwendo mrefu tuliingia hapo mjini kirungu,Kiukweli mimi Kongo nilipapenda kwasababu kila mji ulikuwa mkubwa na ulikuwa na huduma zote mpaka usafiri wa Anga,yaani unakuta mji ni mdogo tu lakini mpaka una kiwanja cha ndege tofati kabisa na Tanzania ambapo viwanja vya ndege ni kwenye miji mikubwa ambayo ni makao makuu ya mikoa lakini kongo ilikuwa tofauti kidogo!
Tuliikamata barabara ya kuelekea huko milimani kwa Nchibaronda na haikuchukuwa muda mrefu tukawa tumefika pale!

Nilimlipa jamaa pesa tuliyokuwa tumekubaliana na akanielekeza kwa Mzee Nchibaronda!,Nilitembea kidogo maana haikuwa mbali na pale Boda aliponiacha!
Nilipofika hapo kwa huyo mzee nilipokelewa na mama mmoja na nilikaribishwa kwa lugha ya kilingala "boyei bulamu"
Boyei bulamu alimaanisha "Karibu",sasa kwakuwa mimi nilikuwa sielewi kilingala na kifaransa nilimwitikia kwa kiswahili "Ahsante"
Nilipokuwa huko kuna maneno baadhi ya lugha ya kilingala nilikuwa nimeshayaelewa hivyo sikupata taabu sana!

Baada ya kuwa nimekaribishwa niliambiwa nikae hapo nje maana mtaalamu (Mganga)kuna watu kaenda nao polini kuwaagua!
Hiyo ilikuwa mida ya saa 12 jioni mpaka nafika pale!
Kiukweli nilikuta kuna watu wengi kidogo na kuna jamaa kama wawili walikuwa wametoka Tanzania,nilipowaona nilijua tu hizi njema ni kutoka Bongoland maana mbongo anafahamika tu hata mkikutana nae nchi za watu!
Niliwasalimia na kwa bahati nzuri walinionyeshea ushirikiano,mmoja alikuwa mnene alionyesha alikuwa na maisha mazuri,basi hatukupiga sana stori maana niliona kama wana nikwepa ile kiaina!

Kwenye hilo eneo la Mganga Nchibaronda kulikuwa na vijumba vingi vya nyasi vilivyokuwa vidogo vidogo!,kama kawaida ya pale pia ulipofika usiku walikoka moto tukawa tunaota pale nje!
Ilipofika mida kama ya saa 2 Usiku yule Mzee Nchibaronda alifika na Alisema wageni waitwe waingie mmoja mmoja,sasa kwakuwa mimi kuna watu niliwakuta pale ilibidi waanze wao!,Zamu yangu ilifika ilikuwa kama mida ya saa 4 za usiku!,Nilipofika ndani nilimsalimia yule Mzee na kabla ya kuongea nae chochote nilitoa kile kingozi kilichokuwa kimekazwa kama kijiti ambacho nilipewa kule Kasulu na yule Mama akiambia ile ni rufaa ya mimi kwenda pale!

Mzee Nchibaronda alikipokea na akaniambia alifahamu ninakuja na alikuwa akiniona kila hatua niliyopiga,Yule Mzee aliniambia hata kabla sijamweleza chochote mimi pale nimefata utajiri na nitaupata!
Aliniuliza "JE UTAWEZA"?,kwakuwa nilikuwa nimedhamiria nilimwambia "Nitaweza"
Mzee Nchibaronda aliniambia hakuna aliyefata hapo kwake utajiri na akashindwa kufanikiwa kwani wote wanafanikiwa,Aliendelea kuniambia kwamba hata hao watanzania niliowakuta hapo nje wamekuja kumlipa shukurani baada ya kufanikiwa kwenye shughuli zao!

Baada ya mazungumzo mle ndani aliniambia kwakuwa kazi yangu ilikuwa ngumu kidogo alinitaka nikae pale wiki nzima maana kuna safari ya kwenda ziwa Tanganyika ambako huko ndiko nitapatiwa utajiri,na akaendelea kusisitiza kwamba yupo atakayenipa Utajiri ila siyo yeye!,Yeye kazi ambayo angeifanya ni kuniandaa ili safari ya kwenda Ziwani itakapofika nisije kupata madhara!


Itaendelea................
Jamaa umepambana duh
 
mkuu fanya mambo aiseeh!! endelea imeishia pazuri sana
 
Back
Top Bottom