Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Wenye kuanda bando naomba kesho mnunue mabando ya kutosha,wenye kuchaji simu chajini ziwe full chaji,wenye kuazima simu hakikisheni mnaazima ili mkae nazo muda wote,kuanzia kesho tunaanzia tulipoishia,ila kila siku itakuwa ni episode 1.

HUO NDIO UTAKUWA UTARATIBU
Haya
 
Kwanza kabisa nianze kuwashukuru wale wote waliyofanikisha hadi mimi kuwa hapa pamoja na changamoto nilizopitia kama mwanadamu,pia niwaombe radhi watu wote ambao huu mkasa wangu wa maisha ya kitajiri yaliyohusisha nguvu za giza yalivyo ondoa roho za wapendwa wao.
Pia ndugu zangu huu mkasa naendelea kuusimulia pale RADIO FREE AFRICA kwenye kipindi chao cha SITOSAHAU ambacho huruka hewani kila siku ya Jumapili kuanzia saa 4 -5 asubuhi.

Vilevile pia kama nilivyowajulisha ya kwamba,kile kitabu changu kilichosheheni hiki kisa cha kweli cha maisha yangu kipo tayari na kinajulikana kama UTAJIRI WA NGUVU ZA GIZA ULIVYOHARIBU MAISHA YANGU,kipo sehemu 1 & sehemu ya 2,Kwakuwa mambo yote niliyoyafanya yaliyokuwa yanatisha,sitoweza kuyaweka hapa ila kwenye kitabu nimeyaandika pasipo kificho chochote.

Mods pia niwaombe msamaha kwa yale yaliyojitokeza hapo mwanzo mpaka kufikia kunipiga Ban,sitorudia tena na nimejifunza,pia niwaombe muwe mnanielekeza ambapo mnaona navuka mipaka ya kitaaluma,anuani yangu ni hii - lwandamagere2012@gmail.com


KARIBUNI.





MKASA WA PILI - Sehemu ya 24

Inaendelea.............


Nilihamia pale nyumbani kwangu rasmi na nilitenga chumba maalumu ambacho hakuruhusiwa kuingia mtu mwingine yeyote ila mimi tu!
Kile chumba kabla ya kuhamia pale nilimwambia yule Mwanamke niliyempa kazi ya ku-decorate nyumba asikiguse maana nilimdanganya kuna mafundi wanakuja kukikarabati!
Na kweli!yule mwanamke hakukigusa kile chumba!.

Baada ya kufika hapo nyumbani mboni ya jicho langu na roho yangu ilikuwa kwenye hicho chumba!,basi niliingia kwenye kile chumba nikakisafisha kikawa cheupe peee!,kuna mazulia makubwa mekundu nilinunua nikatandika chumba kizima!
Nilichukua kile kibuyu nikakiweka katikati ya kile chumba na lile begi la kuhifadhi pesa nikaliweka kando ya kile kibuyu.Baada ya kuwa nimemaliza na kuhakikisha mle ndani pako sawa nilitoka zangu!,
Kumbuka kule ziwani Tanganyika niliambiwa nikishakuwa na chumba na kukitenga ingenipasa kuingia mara mbili tu!
Mara ya kwanza ni kila tarehe 15 ya kila mwezi kuingia kuchukua pesa na kila mwisho wa mwezi kuhakikisha nakiingiza kibuyu kikiwa na damu ambazo ilipaswa kila mwezi niwe natoa kafara!

Sasa kule geto sikuweza kuyafanya hayo yote maana nilikuwa kwenye chumba kimoja na bahati nzuri nilikuwa nikisikia sauti ikinipa maelekezo hivyo ingekuwa jambo baya nisingemaliza hata dakika moja ningekaushwa!.Huku kwangu niliko hamia jamaa hawakutaka kabisa masikhara.

Nilipanga kwenda kumwambia mama yangu kwamba nimenunua nyumba maana hapo awali nilikua nimemdanganya ya kwamba nimechukua mkopo!
Basi nilimpigia simu nikamwambia dereva awachukue yeye pamoja na ndugu baadhi waliokuwa nyumbani Nyegezi awalete mpaka Igoma.Baada ya mama kufika pale kwenye mjengo wangu alihamaki sana na kiukweli aliniuliza pesa za kununua ule mjengo nimetoa wapi?,Niliendelea kumdanganya kwamba nimechukua mkopo na hii nyumba nimeilipia nusu, najitahidi kuendelea kutafuta pesa ili niweze kumalizia pesa za watu!
Miongoni mwa watoto ambao mama yangu alikuwa akiwaamini, basi ni mimi,hakuwa na shaka kabisa!

Kiukweli heshima ilikuwepo kwa wajinga wote waliyokuwa wakitudharau, habari zilianza kumfikia yule shemeji ambaye alikuwa na nyodo na niliapa kumfunza adabu kwa kumfanya mke wangu!.
Ndugu zangu yule shemeji asingekuwa kajaaliwa na mwenyezi Mungu ningeachana naye,lakini kilichomponza ni namna alivyokuwa kuwa kanona na kiuweli alikuwa kajaaliwa shepu na uzuri,niliapa nitamshughulikia kisawasawa.Mpaka wakati huo nilikuwa nimeagiza gari Dar es salaam aina ya VX V8 Amazon,Lile gari la Vx v8 amazon kuna jamaa mmoja hapo mjini Mwanza alikuwa na maduka ya spea za magari alikuwa anatembelea ,hivyo kwakuwa nililipenda niliamua kuagiza Dar es salaam na nilikuwa nimelipia pesa nusu!.

Baada ya muda mama na ndugu aliyokuwa amekuja nao waliondoka,nilimwambia baadae nitaenda kupata chakula hivyo waniandalie.Sasa kwenye akili yangu nilikuwa ninamuwaza Zainati pamoja na Yusta na niliapa hakika usiku huo lazima wakione cha mtema kuni!.Kwakuwa yale maduka yaliyokuwa yakiuza vito yalikuwa yakiwahi kufungwa,niliingia ndani nikaandaa dawa ambayo hakuna mwanamke yeyote chini ya jua ambaye nilikuwa nikimuhitaji angekataa, nikaiweka kwenye mfuko wa suruali,uzuri wa ile dawa hata kama ungeichukua kama kitone cha mbegu ya mchicha huyo mwanamke uliyemkusudia alikuwa anaisoma namba!
Niliondoka zangu kuelekea hapo dukani kwao Zainati, ilikuwa kama mida ya saa 9 alasiri,Kwa bahati nzuri nilimkuta yeye akiwa dukani!,Lile duka lilikuwa kubwa na kuna jamaa mwingine aliyekuwa bize na mambo yake wakati naingia.

Japo nilikuwa nina dawa lakini sikutaka kuonekana mnyonge kwenye suala la kupendeza,nilikuwa navaa ki-gentlemen na nguo zilikaa sana hasa ukizingatia nilikuwa nina ka-kitambi ka kuzugia hivyo yeyote ambaye aliniona hakuwa na shaka kwamba nina hela!.

Nilimsabahi Zainati na alinichangamkia sana!.
Nilimuuliza "Vp mrembo mbona umekaa kiunyonge unaumwa?".

Alinijibu "Hapana ni uchovu tu".

Sikutaka kupoteza muda,nilimwambia "leo nataka nikutoe out"

Alinijibu"Niwewe tu na roho yako!"

Nilijua tayari magome ya mzee nchibaronda yameshafanya kazi!.

Nilimwambia "Nipe namba yako ya simu nitakucheki baadae".
Alinitajia namba yake pasipokuwa na shaka yoyote na safari hii hakuwa na ubavu wa kukataa kutoa namba!.

Aliniambia nihakikishe saa 1 jioni naenda kumchukua na atanielekeza maeneo nimfuate!.Basi nilimuaga nikaondoka zangu.Zainati alikuwa mzuri sana mtoto wa kiarabu na niliapa ningemshughulikia usiku huo mpaka maji aite mmah!.Niliondoka hapo dukani kwao kuelekea kupanda taxi ili niende Nyegezi na akili yangu ilihamia kwa Yusta, nilisema kabla ya kwenda kwa mama, nitaanzia kwao Yusta ili nimalize kila kitu.

Nilipofika kwao niligonga kengele na baada ya muda kidogo alikuja kufungua geti dogo mmoja wa kiume!.

Nilimuuliza "dogo baba yako yupo?".

Dogo akasema "Hayupo".

Nikamuuliza "Mama je?".

Pia akasema "hayupo,wameenda kazini".

Nilimuuliza "Nani yupo?"

Aliniambia "yupo dada Yusta na dada emy".

Nikamwambia "Niitie dada Yusta,mwambie kuna mgeni wake".

Kati ya wanawake wote niliyokutana nao katika kipindi hicho cha utajiri wa nguvu za giza niliyekuwa nikimwona natetemeka,alikuwa Yusta,sijajua mpaka leo kwanini ilikuwa hivyo,nadhani uenda kwasababu alikuwa mzuri sana!.

Alipokuja aliniambia "Ooh Braza J karibu".

Nikamwambia "Kwahiyo mara hii Yusta nishakuwa braza wako?"

Alicheka sana akaniambia "jamani!,kwani kukuita braza kuna ubaya,haya niambie handsome wa mama.......".(alitaja jina ambalo mama alikuwa akiitwa kutokana na dada yetu kuwa wa kwanza).

Nilimwambia "Kwanini Yusta unaendelea kunitesa mama,shida yako kubwa ni nini?".

Kwa mara ya kwanza akaniambia "basi wewe niambie leo chochote nitafanya ili nikuridhishe".Baada ya hiyo kauli nilisema kimoyo moyo "leo utanitambua mimi ni nani"

Nilimwambia "Nataka leo nikutoe out na ikiwezekana tukalale kwangu".

Aliniangaliaa akakosa jibu kwa muda kisha akaniambia "so nitawaaga wazazi wangu naenda wapi?".

Hapo hapo akili ikanituma nikwambia "Utamwambia mama unaenda kwa rafiki yako amekuita".

Akaniambia "unadhani itakuwa rahisi kihivyo?".

Sasa kwakuwa nilikuwa nimedhamilia nilimwambia "wewe ukimwambia hivyo tu mama atakubali na hatokuwa na maswali"

Aliniambia "Sawa kwahiyo unakuja kunichukua saa ngapi?".

Nilimwambia mimi naelekea nyumbani kwa mama kula,hivyo wewe jiandae na msubiri mama yako na baba yako uwaage ili iwe vyepesi mimi kukufuata baadae!,basi akaniambia mida ya saa 1 niende nikamchukue!.Nilipoondoka hayo maeneo nilivuta mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na ile irizi ya maajabu na kuanza kuongea ya kwamba "Chochote atakachosema mbele ya wazazi wake,wakubali na wasiwe na maswali".




Itaendelea.................
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 25

Inaendelea.............


Nilielekea nyumbani kwa mama kupata chakula cha jioni na ilipofika mida ya saa 1 :30 Usiku,Yusta alinitumia sms akitaka nimpigie.

Nilipompata kwenye simu nilimuuliza "Vp mtoto mzuri uko wapi?".

"Mimi nipo hapa nyumbani kwetu kwa nje nakusubiri wewe,kwani uko wapi jamani" aliniuliza kwa shauku!.

Nilimwambia nipo kwa mama tulikuwa na kikao kidogo ila ndani ya dakika moja nitakuwa hapo.Kama nilivyosema hapo awali kwamba nilitembea na wanawake wachache lakini walikuwa na viwango vya kimataifa!,nisingekubali nina dawa na uwezo wa kumpata mwanamke nimtakaye halafu nikachukue takataka!.

Nilimuuliza "vp kuhusu wazazi wako,hawajaleta ngumu?"

Aliniambia "Nimemuaga mama nikamwambia naenda kwa rafiki yangu anakaa Pasiansi,kesho tutakuwa na mazoezi ya viungo".

Akaendelea kuniambia kwamba "Yaani sijaamini ambavyo leo mama kawa mpole kuliko hata siku zote maana kaniambia tu kesho mazoezi yakiisha niwahi kurudi".

Tayari nishajua ile dawa inafanya kazi pamoja na ile Irizi niliyokuwa nayo mkononi.Basi nilimwambia tutembee kidogo kuelekea barabara kuu ambako tungepata taxi tupande kuelekea maeneo ya mjini.

Tulifanikiwa kupata taxi, nilimwambia dereva atupelekee maeneo ya Igoma kulikuwa na hoteli moja nzuri ambayo walikuwa wakichoma samaki,hivyo nilitaka twende hapo kwanza nikampigishe msosi wa maana.Tulipokuwa hapo maeneo ya kujidai,Zainati naye alinipigia simu na akaniambia nikamchukue,nilimchukua Yusta nikamwambia achukue kila alichokihitaji na afungiwe ili tuelekee nyumbani.Tuliondoka na Yusta mpaka nyumbani kwangu, kwa sababu ile nyumba ilikuwa kubwa na ilikuwa na vyumba 4 vya kulala ambavyo kila kitu kilikuwa ndani!,nilipofika nilimuingiza chumbani nikamwambia anisubiri kidogo narudi.

Niliondoka na ile taxi mpaka maeneo ya mjini mahali alipokuwa amenielekeza Zainati nimkute,Yule mtoto wa kiarabu alijua sana kupendeza,na kwa vile alikuwa mweupe alikuwa akivutia sana.Zainati hakuwa mnene sana ila alikuwa mzuri na umbo la wastani.

Nilimwambia "Umependeza sana Zainati".

Aliitikia "Ahsante"

Nilimwambia "ingia kwenye taxi tuondoke zetu".

Na yeye pia nilimpeleka maeneo yaleyale ya ile hoteli tulipokuwa na Yusta muda si mrefu.Nilimwambia aagize anachotaka,alikuwa kama akiona haibu lakini nilimwambia ajisikie huru.Basi aliagiza Reds akaanza kunywa na nilimuagizia samaki lakini akasema yeye keshakula nyumbani kwao.

Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale na niliwaza namna ambavyo ningewashughulikia wale warembo kwa usiku huo.Watu wengi waliyokuwa pale kwenye hiyo hoteli walikuwa wakinishangaa namna nilivyokuwa na mwanamke mzuri vile tena ukizingatia ni mwarabu!,Wengi walikuwa wakiniangalia hawanimalizi.

Baadae akasema tuondoke twende nyumbani maana kachoka anataka kupumzika,tuliondoka maeneo yale kuelekea nyumbani,nilipofika nyumbani yeye pia nilimwingiza kwenye chumba kingine ambacho kilikuwa na kila kitu ndani.Kwa namna ile nyumba ilivyokuwa, isingekuwa rahisi mtu kujua kama kuna mwanamke chumba kingine.

Nilimwambia afanye kila kitu kwa uhuru maana hapo sasa ni kwake!,niliendelea kumjaza upepo wa sifa kedekede.Kwakuwa ile dawa ya kuwashughulikia bila kuchoka niliyopewa na mzee nchibaronda ilikuwa chumbani kwangu,nilienda kuiandaa kwa ajili ya kuinywa kama chai,niliingia jikoni nikachukua birika la kuchemshia maji na nikatengeneza kama kawaida,nilipomaliza nilirudi chumbani kwa Yusta nikiwa nainywa ile dawa kama chai,nikamkuta alikuwa akiangalia luninga.

Aliniuliza "Umerudi saa ngapi?"

Nilimwambia "sina muda mrefu".

Basi baada ya kuwa nimemaliza kuinywa ile chai iliyokuwa na dawa niliingia bafuni kwa Yusta kuoga na nilimwambia twende tukaoge wote!.

Aliniambia "Mimi tayari nishaoga labda nikusindikize wewe".

Alipovua zile nguo zake alizokuwa kavaa kiukweli nilitaka kuzimia na niliapa usiku huo ningetambulika vizuri kwenye vitabu vya rekodi za kidunia,Kiukweli nilishawahi kukutana na wanawake lakini nilijisemea kwa Yusta,nilikuwa nimelamba dhahabu!.Tulielekea wote bafuni kuoga na nilijaza maji kwenye yale masinki ya kuogea na baada ya kujaa niliweka sabauni nikayatingisha kukawa na povu la kutosha!,tuliingia wote kwenye lile sinki na kuanza kuoshana,tulipomaliza kuoshana humo kwenye sinki huku fimbo ikiwa imesimama imara kama chuma nilimshika nikamtoa kwenye maji kuelekea kitandani
Kiukweli hata sikuoga nikatakata ila sema tu nilichukua taulo na kujifuta maji maana nilizidiwa.

Nilianza kumtembezea bakora za kim-kakati mpaka usiku mnene sana,baada ya kuhakikisha yupo hoi,nilimuacha amelala nikaelekea tena kuchukua kikombe cha chai na kuingia chumbani kwa Zainati,Zainati nilimkuta kalala na alikuwa kajifunika shuka!,nilipomaliza kupiga ile chai kama kawaida nilijitupa kitandani kwa Zainati.

Akaniuliza "Ulikuwa umeenda wapi?"

Nilimwambia"kuna kazi nilikuwa naifanya kidogo hapo sebuleni ila nimemaliza".

Mpaka wakati huo hakufahamu kabisa kwamba,ndani ya nyumba wapo wanawake wawili katika vyumba viwili tofauti.

Mwanzoni nilipoanza kumkung'uta bakora za kim-kakati,Zainati aliona kama ni nguvu ya soda,lakini kadri masaa yalivyozidi kusogea alianza kugugumia kwa miguno ya ajabu na mimi nikajua tayari treni limefika kigoma.Baada ya kuona sasa naweza kumuua nilimuachia apumzike kidogo.

Nilipokuwa nashuka kitandani kuelekea kule chumbani kwa Yusta kumuangalia,Zainati alinivuta akinisihi nisiondoke.

Nilimwambia "nakuja mama".

Aliniambia kwamba,hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kupigwa bakora za kim-kakati kiasi kile,hivyo aliniona kama mwanaume wa ajabu duniani.

Alikuwa akisema "Kumbe siku zote nilikuwa nachezewa tu".

Nilimwambia "Usijali mama hapa umefika"

Basi niliondoka kuelekea chumbani kwa Yusta ambaye nilimkuta amelala akiwa bado yuko hoi!.Nilirudi chumbani kwa Zainati kuendeleza fimbo kama kawaida,uzuri ni kwamba Zainati alikuwa mzoefu hivyo sikupata shida yeyote!.Ilipofika mida ya saa 9 usiku,nilirudi tena chumbani kwa Yusta, nikamuamsha na kuanza kumshughulikia tena.



Itaendelea...................
 
Shipa la Kim kakati limegeuka Bakora ya Ki mkakati.

Ila ni True Wanawake wa Kiarabu wanapenda mwanaume amkune kipasavyo mimi nina uzoefu wa Wanawake wawili wa Kiarabu... dah huwa waswahili au wazungu husema stop au yatosha ila Waarabu mwisho... wow mwendo ni kuenjoy tu and then hawakauki down
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 26

Inaendelea.............


Ilikuwa yapata mida ya saa 10 usiku lakini hata na lepe la usingizi,nilianza tena kumshughulikia Yusta mpaka mida ya saa 11 alfajiri, kiukweli nilimshughulikia kisawasawa!,safari hii nilijua uenda nimemuua mtoto wa watu maana kila nilipompeleka alienda kama mzigo na akaanza kuyakunja macho kama mtu mwenye makengeza, ilibidi nimuache maana ningeendeleza bakora nilikuwa nampoteza.Basi nilimuachia mtoto wa watu akiwa hoi,nikatoka kuelekea chumbani kwangu, kwakuwa sikuwa na usingizi,nilienda tena kuchukua ile chai ili nielekee kwa Zainati.

Lengo langu mpaka wakati huo ni kwamba nilitaka niwashikishe adabu maana walinisumbua sana hasa huyo Yusta.Zainati yeye nyodo ndiyo zilimzidi na nilitaka kumfunza adabu kupitia bakora hizo za kim-kakati.Nilipomaliza kupiga kikombe cha chai ilikuwa kama mida ya saa 12 asubuhi,nielekea chumbani kwa Zainati,sikutaka kwenda kumsumbua Yusta maana nilifahamu fika kwa bakora zile asingekuwa na nguvu ya kuamka wakati huo.


Tuliuanza mchakamchaka toka saa 12 asubuhi tulipepea mpaka saa 3 asubuhi,Zainati alikuwa akiniangalia anaishia tu kuguna,hakuamini kama ningeweza kumfanya akasahau shida za dunia kwa muda ule.Ilipofika mida ya saa 4 asubuhi niliekea chumbani kwangu kuoga na kuvaa,nilirudi chumbani kwa Yusta nikamwamsha ajiandae twende nimsindikize arudi sasa nyumbani kwao.

Alijivuta hivyo hivyo kwa uchovu kuelekea bafuni ingawa alikuwa amechoka sana,nilienda chumbani kwa Zainati kumchungulia kama atakuwa ameamka,kiukweli alikuwa hata hajitingishi!.Yusta alipomaliza kuvaa nilimchukua tukaondoka zetu,tulitoka kwa nje nikampigia yule dereva taxi aje yale maeneo ya nyumbani kwangu kumchukua.Nilimpa Yusta laki moja kwa ajili ya matumizi yake.

Alniambia "Tafadhali usije kuniacha,mwenzio nakupenda ujue!".

Nilimwambia "Ondoa shaka mama,mimi pia nakupenda"

Yule dereva alipo ondoka nilirudi ndani kumwamsha Zainati ili ajiandae aende kazini,Zainati alinijibu kwamba hatoondoka siku hiyo maana bado alikuwa na hamu ya bakora.

Nilimwambia "Sawa wewe endelea kulala,ngoja kwanza nakuja".

Mpaka muda huo Zainati alikuwa akifahamu kwamba kile chumba ndicho huwa nalala maana kulikuwa na kila kitu,kumbe kile kilikuwa tu sehemu ya vyumba vyangu vya kawaida ndani ya ile nyumba.Chumbani kwangu sikutaka kumuingiza mtu yeyote ila yule ambaye niliambiwa atakuwa mke wangu kwa siku za baadae na ambaye atanizalia watoto,na mimi pia sikutaka kuharibu masharti nikapotezwa maana niliogopa sana kufa!.
Nilitoka nikaelekea supermaket kwenda kununua mahitaji na vyakula ili Zainati asishinde na njaa siku hiyo,niliporudi nilimkuta bado amelala,nilimwamsha nikamwambia akaandae chakula ale ili uchovu uishe.

Alinijibu "Ngoja kwanza nilale kidogo maana nimechoka sana nitakula baadae".

Basi mimi nilielekea chumbani kwangu kupumzika maana nilikuwa nimechoka sana kutokana na shughuli ya usiku,wakati nikiwa nimepitiwa na usingizi ndipo nilionyeshwa ndoto ya Kwamba inapaswa mwisho wa mwezi huo nielekee mkoani Pwani sehemu moja inaitwa Bungu, pale Bungu niliambiwa kulikuwa kuna Costa ambayo ilikuwa inatokea Kibiti,kabla ya kufika hapo Bungu ilipaswa niishughulikie na asibaki mtu yeyote.

Nilishtuka kutoka usingizini na nikaondoka kuelekea chumbani kwa Zainati,alikuwa amekwisha amka,nilimuonyesha jiko lililokuwa la kisasa kwa ajili ya kuandaa chakula.Haukupita muda alinipigia simu Yusta na kuniambia kwamba ndiyo anafika nyumbani!.

Nilimuuliza "Mbona kama umechukua muda mrefu kufika nyumbani?"

Aliniambia"Nilipitia kwanza Pasiansi kwa rafiki yangu ili isije ikaonekana nimewahi nyumbani,pia kuna nguo nilipita hapo mjini kuichukua nilikuwa naipenda"

Nikamwambia "Ok sawa"

Baada ya kumaliza kula nilimuaga Zainati nikamwambia naelekea mjini mara moja maana kuna jambo ninakwenda kulifanya mara moja,aliniambia nisichelewe maana bado hajaridhika na zile bakora.Niliondoka hapo nyumbani kuelekea Yale maeneo ya yule jamaa mwenye Yadi ya magari kumuulizia kuhusu ile gari yangu niliyokuwa nimemuagizia ingefika lini maana nilikuwa nishachoka kutembea kwa gari za kukodi!.

Jamaa aliniambia "Unajua bosi gari lako liko tayari ila sema kuna vitu vidogo walikuwa wanavikamilisha,ila nakuahidi halitachukua muda mrefu litakuwa limefika".

Wakati nikiwa njiani narudi nyumbani kwangu,Mama alinipigia simu na kuniambia yule shemeji yetu mwenye nyodo na dharau alikuwa amekuja pale nyumbani,alipofika alibaki kushangaa namna ile nyumba yetu ilivyokuwa imebadilika na namna ambavyo hapo nyumbani walivyokuwa wakiishi maisha mazuri.

Katika vitu ambavyo nilikuwa sitaki kunyooshewa vidole ni hali ya nyumbani kwa mama yangu kuwa mbaya kifedha na kimuonekano,nilijiapiza ya kwamba ni heri mimi nikose mahali pa kukaa lakini mama yangu aishi maisha ya kitajiri.


Nilimuuliza mama "Alikuwa amefuata nini?".

Mama akasema "Alikuwa kaja kuomba msamaha maana anasema yeye hakusema yale maneno bali yule mtoto alimnukuu tu vibaya".

Nikamuuliza mama "Wewe umemwambia nini?".


Mama akajibu "Mimi sikutaka kuongea naye niliingia ndani maana sitaki hata kumuona kwenye macho yangu,aliongea na dada yako".

Nilimwambia "Usijali mama,mpe simu dada niongee naye".

Baada ya kuwa nimeongea na dada nilimwambia anitumie namba ya shemeji,lakini dada yangu alisisitiza kwamba nisije kumjibu vibaya.

Nilimwambia "wala usijali dada wewe nitumie namba yake"

Dada yangu yeye alijua labda nataka nimtukane wakati kumbe mimi nilikuwa nina jambo langu tangu zamani,nilitaka na yeye nimshikishe adabu ya bakora za kim-kakati na pia awe kama mke wangu, japo yeye alikuwa kanizidi miaka kama miwili lakini kutokana na uzuri na umbo alilokuwa nalo,sikutaka kabisa kumuachia anipite hivi hivi!.Muda kidogo kupita,dada alinitumia namba yake,sikutaka kumpigia simu muda ule bali niliisevu namba yake.Nilirejea nyumbani kwangu na nilipofika nilimkuta Zainati amelala,nilitambua ya kwamba kulala kule alikuwa kachoka sana.

Nilipoona amelala,nilienda kukifungua kile chumba cha siri maana nilikuwa nimesikia sauti ikiniita kule ndani muda mrefu.Nilipoingia sikumkuta mtu yeyote ila nilikuwa nikisikia tu sauti.

Niliposogea karibu na kile kibuyu nilisikia sauti ikiniambia "umeyapata maelekezo?".

Nilijibu"hapana".

Basi ile sauti ikaniambia ya kwamba ile niliyoiona usingizni haikuwa ndoto bali ni uhalisia na inapaswa nitekeleze hilo agizo siku si nyingi zilizokuwa mbele yangu.


Itaendelea..................
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 27

Inaendelea.............



Baada ya yale maelekezo nilitoka zangu mle chumbani na nilihakikisha hiko chumba hakuna anayekiingia zaidi yangu!
Nilielekea chumbani kwangu nikabadili nguo nilizokuwa nimevaa na nikaava nguo nyepesi za kushindia.Mpaka wakati huo naweza kusema sikuwahi kuwa na marafiki,namna tulivyokuwa tumelelewa toka wilayani Tarime nilikuwa na marafiki wachache sana na ni wale niliyokuwa nimesoma nao shule ya msingi,Sasa tulipohamia Mwanza ndiyo ilikuwa balaa kabisa labda wale niliosoma nao sekondari,sikupenda kabisa kuwa mtu wa kujichanganya sana na makundi ya vijana,nadhani hiyo ndiyo ilipelekea mimi kutokuwa na marafiki wa kudumu bali wale ambao tulifahamiana kwa muda mchache tu.

Nilipoangalia muda ilikuwa yapata saa 8 mchana, kwakuwa nilikuwa nimeshiba niliingia jikoni kama kawa nikaanda chai niliyokuwa nimechanganya na ile dawa ya mzee nikaanza kunywa.Ile dawa niliyopewa na mzee nchibaronda kule kijijini Kirungu,kama ulikuwa huna afya ya kuweza kuhimili wanawake wawili kwa wakati mmoja,ulikuwa unaenda na maji maana ilikuwa na nguvu zisizo za kawaida,wakati mimi nilipokuwa nikiitumia,kwanza ilikuwa ikikata usingizi wote,pili ilikuwa ikinipa nguvu za ajabu ambazo nilikuwa nikimshika mwanamke yeyote yule kumkung'uta bakora mpaka anachanganyikiwa mithili ya kufa ndiyo namwachia,hivyo kama ulikuwa huna afya ya kutosha ulikuwa unafia kufuani kwa mwanamke.
Nilipomaliza kuinywa ile dawa nilirudi chumbani kwa Zainati na bakora zilianza kumtembelea kama kawaida.Nilimkung'uta bakora mpaka saa 2 usiku na hakuweza tena kuendelea maana aliniambia kisima kilikuwa kinawaka moto!.
Sikumwacha mpaka nilipohakikisha nimefika mlima kilimanjaro ndiyo nikamwacha.

Alikuwa akiniangalia anatikisa kichwa tu kama mwendawazimu.Asubuhi nilimuamsha ili aondoke maana nilifahamu kama angeendelea kukaa hapo nyumbani basi ningemuua kwa bakora.Ilipofika mida ya saa 2 asubuhi nilimpigia simu yule dereva taxi akaja kumchukua pale nyumbani,yeye pia nilimpa laki mbili kama Yusta lakini akagoma kuzipokea.Aliniambia yeye hakuja hapo nyumbani kwa ajili ya pesa bali bakora ndiyo ilimleta, aligoma katakata kuichukua ile hela.Alipoingia kwenye taxi kabla ya kuondoka aliinita akaniambia "Nitakapokuja kufahamu kwamba una mwanamke mwingine,nitakuua".

Nilimwambia aondoe shaka kwani yupo peke yake!,nilifahamu fika Zainati alikuwa kapagawa na bakora ndiyo maana alikuwa anasisitiza hivyo.Alipoondoka nilirudi zangu ndani nikawa nawaza namna safari ya Pwani itakavyokuwa.Asubuhi hiyo kwakuwa ilikuwa mida ya saa 2 asubuhi nilijianda kuelekea kule shuleni kuzuga kama kawaida.Baada ya kumaliza vipindi pale shuleni ile mida ya jioni, nilipitia mjini kwenye kampuni moja ya ulinzi,nilitaka waje pale nyumbani wanifungie system ya ulinzi na nilihitaji pia na mlinzi ili nikiwa kwenye mishe zangu,hapo nyumbani kuwe na mtu ambaye angekuwa anaangalia usalama wa nyumba.

Siku zilipofika za mimi kueleka mkoani Pwani nilijiandaa kikamilifu, nilielekea mle chumbani kuchukua kile kibuyu na dawa ambazo zingenisaidia mimi kufanikisha ile kafara,baada ya kumaliza kila kitu mle ndani,niliukamata mkono wangu uliyokuwa na irizi ya ajabu na kuanza kutamka ya kwamba "Ninataka nifike pwani eneo lililokusudiwa".

Kilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua nilijikuta nipo maeneo hayo ya Bungu,Pia nilisikia sauti ikiniambia nisogee nikae katikati ya Bungu na Kibiti,kama kawaida nilitii yale maagizo,nilitumia uwezo niliyokuwa nao wakati huo kuangalia nani aliyekuwa mtu mbaya yale maeneo na kiukweli wote niliwaona ni weupe tu hawakuwa na lolote la kufanya nishindwe kutoa kafara.Mahali nilipokuwa nimetega kulikuwa na kona pamoja na mteremko,baada ya muda kupita,kwa mbali niliiona ile Costa inakuja ikitokea upande wa kibiti na kuna lori pia lilikuwa linakuja kwa kasi likitokea Dar es salaam.Nilipopiga darubini zangu za kishirikina kwa wakati ule kuiangalia ile costa sikuona mtu yeyote mwenye uwezo wa kunikwamisha,hivyo nilisogea katikati ya barabara nikaweka dawa,baada ya kumaliza nilisogea pembeni kushuhudia ile ajali itakavyokuwa.

Lile lori likawa linakaribia na ile costa nayo ikawa inasogea,kwa sababu lile lori lilikuwa spidi, ilipofika pale nilipoweka dawa liliacha njia na kwenda kuivagaa ile costa,muda huo huo watu waliokuwa humo kwenye costa walikuwa nyang'a nyang'a, kuna watu walivunjika na wengine walikufa pale pale!.

Nilisogea sasa kwa ajili ya kufanya kilichonipeleka hapo,nilianza kuzichukua zile damu za maiti na kuhakikisha nakausha kabisa ili asipone mtu.Niliwasogelea wale waliyokuwa wamevunjika miguu, kuna mama mmoja alikuwa kabeba mtoto lakini mtoto yeye alikuwa mzima kabisa bila hata mchubuko!,nilipomtazama yule mama kiukweli nilimuhurumia sana lakini sikuwa na namna maana mimi nilifuata maelekezo na masharti yalivyotaka!.Yule mama nilimkausha kama samaki nikachukua damu yake,yule mtoto mchanga aliyekuwa amembeba nilimuacha sikumgusa hata kidogo!, kale katoto kalikuwa hata hakaelewi kitu!.

Ndugu zangu niliyoyafanya ni mabaya sana na ndiyo maana naandika ili muone namna dunia ilivyo na wala si mambo ya kufurahisha hata kidogo!,baada ya kutubu na kumrudia Muumbaji wangu nikaona ngoja niandike haya masuala ili wengine mjifunze kitu.

Pia niseme kwamba ajali nyingi zinazosababishwa na wachawi huwa zina dalili kuu mbili,ukifika hayo maeneo na ukaona yafuatayo basi tambua fika wachawi ndiyo wanahusika!.

Moja,Mara nyingi ukifika eneo la tukio na ukakuta gari imeharibika sana na haitamaniki lakini tenki la mafuta bado zima na mafuta hayaja churuzika,tambua wachawi wamefanya yao.
Pili,ukifika eneo la tukio na ukakuta kuna joto kali au mgandamizo wa hewa umekuwa mzito kiasi kwamba hata kupumua ni shida tambua wachawi wamefanya yao!.

Hivyo ni viashiria tu ambavyo mara zote ajali za namna hiyo unakuta mchawi kahusika,huwezi kukuta mchawi kasababisha ajali na matenki ya mafuta yanapasuka!,sijajua kwa waliyokuwa wachawi sugu lakini kwa uwezo niliyokuwa nao mimi nilifahamu hivyo.
Pia huwa kuna damu kadhaa wanazipakaa yale maeneo ya ajali ili ionekane kama kweli watu wamekufa kwa kuvuja damu lakini huwa si kweli kwa maana unaweza kuta kuna ajali imetokea ya kawaida tu ambayo wamesababisha wao na watu hawajatoka damu lakini wamekufa.Ndugu zangu damu ndiyo uhai wa mwanadamu,sasa ukikuta mtu kapata ajali na hakuna damu yeyote iliyovuja na kafa,fahamu kabisa wachawi walishafanya ya kwao,japo pia wapo wanaokufa kwa kawaida lakini wengi wa namna hiyo wachawi huwa wanahusika.Nayazungumza haya kwasababu nilishiriki moja kwa moja.

Basi baada ya lile tukio niliondoka hayo maeneo na nilihakikisha hata wale watakaochukuliwa kupelekwa hospitali hawatomaliza siku maana wote niliwakausha damu ili wakiwa wanapelekwa hospitali wafie njiani.Niliinua mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na irizi kama kawaida na nikatamka ya kwamba"Nahitaji niwe Mwanza kwenye chumba changu cha siri muda huu".

Kilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua nilijikuta nimo mle ndani,nilikiweka kile kibuyu katikati ya kile chumba na bahada ya kuhakikisha nimekamilisha kila kitu niliondoka mle ndani.

Ilipofika usiku mida ya saa 6,nilisikia sauti ya yule Malikia niliyemkuta kule chini ya ziwa Tanganyika ambaye ndiye alinipatia masharti ya namna ya kutoa kafara,huyu Malikia ndiye pia aliyeniwekea irizi mkononi,ile sauti ilikuwa ikiniita kutokea kwenye kile chumba cha siri kulimo kuwa kunakaa kibuyu na vifaa vingine vya kazi ya utoaji wa kafara.

Niliamka kitandani usiku huo kuelekea kule kwenye kile chumba,niliufungua ule mlango na ndipo sikuamini nilipokutana na yule Malikia macho kwa macho.




Itaendelea......................
 
Back
Top Bottom