Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Habarini za kutwa wanajamvi ,bila shaka wote mko bìèn!.

Kwanza kabisa nianze kwa kusema ninayo mikasa miwili ambayo nimewahi kuishuhudia kwa macho yangu na kuifanya kwa mikono yangu mwenyewe,mkasa wa kwanza ulituhusu mimi na ndugu zangu ambapo wakati huo nikiwa nina miaka 14 - 15 mwaka 2000 - 2001 huko mkoani Mara,wilaya ya Tarime,nchini Tanzania.
Mkasa wa pili unanihusu mimi mwenyewe pia,huu mkasa niliufanya wakati ambapo nishakuwa mtu mzima,hii ilikuwa kuanzia mwaka 2012 - 2018,mkasa huu unahusu maisha ya kitajiri yaliyohusisha nguvu za giza.
Kuna nyuzi kadhaa humu nimekuwa nikizisoma za watu mbalimbali kusimulia visa na mikasa ya maisha yao au jamaa zao ambayo waliwahi pitia. Hivyo nami nikaona sasa ni muda muafaka wa kuleta simulizi nilizo pitia maishani ili kuwafundisha na kuwaonya vijana wenzangu wote wenye tamaa ya kutafuta mali kwa njia niliyoifanya mimi waache mara moja kwani Mwisho wake unaweza kuwa kifo mikononi mwa shetani,ingawa mimi niliponea chupuchupu.


MKASA WA KWANZA - MWAKA 2000 - 2001.


Sehemu ya 1.


Nilizaliwa mwaka 1986 wilayani Tarime,mkoa wa Mara,nchini Tanzania.Wazazi wangu walinipatia Jina ambalo nisingependa niliweke wazi,ila jina maarufu au a.k.a nafahamika kama Lwanda Magere,kwenye tumbo la mama yangu tulizaliwa watoto 4,mtoto wa kwanza ni dada yetu mkubwa,mtoto wa pili ni kaka yangu ambaye alimfuatia dada yangu kuazaliwa,mtoto wa tatu ni dada yangu mwingine ambaye ndiye niliyemfuatia katika uzao,na mwisho kabisa nilizaliwa mimi.Elimu yangu ya msingi niliipata kwenye shule mbili tofauti,kuanzia darasa la kwanza mpaka la tatu,nilisoma shule ya msingi Sabasaba,hiyo ilikuwa mwaka 1997 - 1999;Darasa la nne mpaka la saba nilisoma shule ya msingi Turwa,hiyo ilikuwa mwaka 2000 - 2003.

Mimi na ndugu zangu pamoja na wazazi wangu tulikuwa tunaishi wilaya ya Tarime,mitaa ya Bomani,(wenyeji wa Tarime wanaielewa vizuri hii mitaa) sisi hatukuwa wenyeji wa Tarime ila mama na baba walienda huko kikazi miaka ya nyuma, hivyo tukajikuta tumekuwa wenyeji wa huko,ndugu zangu walionitangulia katika uzao,wao walizaliwa mkoani Mwanza,ila mimi pekee ndiye niliyezaliwa Tarime.Wazazi wangu kikabila ni Wasukuma,mama yangu alikuwa mwenyeji wa wilaya ya Kwimba,akitokea kijiji kimoja kinaitwa Sumve;Baba yangu yeye alikuwa mwenyeji wa wilaya ya Misungwi.Baba yangu alikuwa ni mtu wa kusafiri sana kikazi na mama yangu yeye kazi alikuwa anazifanyia pale mjini,japo pia walikuwa wakitoka kikazi mikoani,anaweza kukaa hata miezi 6 hajarudi nyumbani,mama alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni ya ujenzi,hivyo nadhani zile pilika pilika za ujenzi pia zilimfanya kuwa bize sana.Baba yangu yeye alikuwa akifanya kazi kwenye shirika lisilokuwa la kiserikali,kwa wakati huo kwakuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufahamu hilo shirika lao lilikuwa likijihusisha na kitu gani.

Siku moja baba alipata safari ya kikazi kwenda mkoani Singida ambako alikaa kama miezi miwili, aliporudi alirudi na dada mmoja mwenye asili ya kiarabu(half cast)akiwa kama mfanyakazi wa ndani,kwa maelezo ya baba ni kwamba,yule dada alikuwa ni mfanyakazi wa ndani,nakumbuka mama yangu alimfokea sana baba akimtuhumu kwamba uenda yule mwanamke anaweza akawa mchepuko wake, ila baba anazuga kwamba ni mfanyakazi(siunajua tena mambo ya wivu).Baadae mambo yalikaa sawa,yule dada akawa mfanyakazi wa ndani pale nyumbani kwetu,Kiukweli alikuwa mzuri sana, kwasababu tulifundishwa nidhamu na heshima,tulimheshimu kama dada yetu na tukampenda pia.Siku zikasonga,hatimaye miezi nayo pia ikakata tukiishi kwa furaha,amani na upendo.
Wakati huo nakumbuka ilikuwa mwezi wa 12 mwaka 2000.Baba alihamishwa kikazi kupelekwa jijini Dar es salaam,hivyo pale nyumbani tukabaki na mama ambaye pia alianza kusafiri kikazi na kukaa hata miezi 5 au 6 hajarudi nyumbani, kilichokuwa kinafanyika ni kutumiwa pesa ya matumizi na kutupigia simu kutujulia hali.

Baada ya siku kadhaa kupita, siku moja usiku yule dada wa kazi, alituita sebuleni mimi pamoja na wale dada zangu akatueleza ya kwamba,yeye anawageni wake ambao ni ndugu zake watakuwa wanakuja kumtembelea kila mwisho wa mwezi,kwa kuwa tulifundishwa ukarimu, hivyo hatukuona taabu, ila alitueleza ya kwamba hao ndugu zake wanamashariti makali na inapaswa tuyaelewe ili watakapokuja tusipate taabu,hivyo sababu ya kutuita ilikuwa ni kutupa namna iliyo bora ya kuwapokea hao ndugu zake!.Kiukweli mimi nilipata mshituko kidogo, nilijiuliza maswaĺi kadhaa lakini sikupata majibu, tulikuwa tumezoea kuwapokea wageni mbalimbali siku zote na walikuwa wakija bila masharti!,sasa nikawa najiuliza hao ni wageni wa namna gani waliokuwa na masharti tena akasema ni makali na kila mtu anapaswa ayafuate si ombi bali ilikuwa ni lazima!.

Watu wote pale sebuleni tulikaa kimya,nilikuwa nikiziangalia sura za dada zangu zilibadilika ghafla na kuonyesha huzuni.Basi masharti yenyewe yakawekwa bayana kama ifuatavyo:-

1. Siku hiyo wote tutavaa nguo za kulalia(pajama)nyeupe.

2. Siku hiyo vyumba vya kulala vihakikishwe vinakuwa safi isionekane hata nukta ya uchafu.

3. Kabla ya kufika kwa wageni,ukihitaji kuoga basi hakikisha unaenda kuoga na sabuni ambayo alikuwa akiitumia yeye huyo dada wa kazi.

siikumbuki ile sabuni lakini ilikuwa na marashi makali sana na yenye harufu ya kupendeza.

4. Akawaambia dada zangu kwamba,siku hiyo ambayo wageni wake walikuwa wanakuja,endapo kuna mtu atakuwa kwenye siku zake za hedhi,basi hakutakiwa aonekane pale nyumbani maana angejuta!.


Hayo ndiyo yalikuwa masharti tuliyopewa siku hiyo.


Itaendelea.......................
Hii sijaisoma nimesabuskraibu kwanza
Karibu Baby Anka baby debby baby debby bab jesuss
 
Mwendelezo wa hii simulizi unapatikana kivipi?
Nahitaji mwendelezo wake LwandaMagere
Ingia youtube,search leanda magere iko yote
IMG_20230205_145810.jpg
 
UTAJIRI WA NGUVU ZA GIZA ULIVYOHARIBU MAISHA YANGU- Hiki ndicho kisa cha pili cha maisha yangu,hapo mwanzo nilisema nina visa viwili,cha kwanza nimeshakisimulia,hivyo hiki ni kisa cha pili.KARIBUNI MJIFUNZE.




MKASA WA PILI- Sehemu ya 1.



MWAKA 2012.



Baada ya kuwa nimemaliza shule ya sekondari nilirudi nyumbani Mwanza,baada ya mama kuwa ameuza ile nyumba ya Tarime ilibidi ajenge nyumba nyingine Mwanza,japo haikuwa kubwa kama ile ya Tarime lakini kwa kiasi fulani ilikuwa nzuri naya wastani!,nilirudi nyumbani nikawa nafundisha wanafunzi tuisheni ili angalau niweze kupata hela za kununua sabuni na mahitaji madogo madogo,sikuweza tena kumuomba mama pesa maana tayari nishakuwa mtu zima,pia kwa wakati huo hali ya mama haikuwa nzuri kifedha,kuna shuke moja ambayo haikuwa ya serikali huko maeneo ya buhongwa,waliniajiri kama mwalimu wa muda na wakawa wananilipa kutoka na vipindi ambavyo nilikuwa nikihudhuria,hivyo nilikuwa nikitoka hapo shuleni naelekea ilipokuwa kituo cha tuisheni kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi masomo ya ziada,nilikuwa nalipwa na wale wanafunzi Tsh elfu 3000 kila nilipokuwa nikimaliza topic.

Basi kuna siku katika pitapita zangu mtaani wakati natoka huko shuleni,kwa mbali kidogo nikamuona jamaa mmoja tuliyekuwa tumesoma wote shule ya msingi Turwa kule Tarime,kiukweli sikuweza kufahamu kama ndiye au nilimfananisha,jamaa alikuwa pembeni anaongea na simu,hivyo nilijaribu kusogea karibu nione kama ndiye!.Kweli!,baada ya kusogea karibu nikamwita jina lake,jamaa aliitika na aliponiona alinifanyia ishara kwamba nisubiri kwanza amalize kuongea na simu,basi jamaa alipomaliza kuongea na simu alifurahi sana kukutana na mimi,mimi pia nilifurahi sana maana jamaa alikuwa kabadilika sana na kanenepa ile kishenzi,watoto wa mjini wanasema "Shavu dodo",kiukweli jamaa alikuwa kanawili,nilivyomuona tu nilifahamu lazima alikuwa na maisha mazuri.

Jamaa aliniuliza "Aisee za miaka mingi?".

Nikamjibu "Nzuri".

Jamaa akaniambia "Hebu nikumbushe wewe ni nani na nilikuona wapi vile!".

Kimoyo moyo nilijisemea "Ina maana jamaa mara hii kanisahau au ndiyo mambo ya mjini?".

Basi ilibidi nimkumbushie jina langu na tulisoma wote Tarime,jamaa alicheka sana,ndipo tukaanza kukumbushiana matukio,vimbwanga na vitimbi vya shule!,tulipiga michapo sana na nikamueleza mimi niliendelea na shule na nikamwambia Tarime tulihama muda sana.Jamaa alinichukua tukasogea mbele kidogo kumbe alikuwa kapaki gari!.Tulipanda kwenye gari kuelekea maeneo ya Igoma ambako alikuwa kachukua hoteli huko.Wakati tukiwa kwenye gari alikuwa ananiambia kwamba yeye baada ya kumaliza shule ya msingi matokeo yake hayakuwa mazuri,hivyo ilibidi aende kutafuta maisha,akaniambia yupo huko mkoani Geita sehemu moja inaitwa Katoro,kajenga huko na maisha yake yapo huko,ila siku hiyo alikuwa kaja hapo Mwanza kwa ajili ya biashara zake nyingine.Huyu jamaa kipindi tunasoma alikuwa hajiwezi kimasomo(kilaza),kiukweli ningeshangaa sana kusikia aliendelea na Shule!.

Baada ya kufika hapo hotelini alipofikia mimi nilikaa nje yeye akaingia huko ndani,muhudumu alikuja kuniuliza natumia nini lakini nilisita kumwambia maana sikuwa na kitu, mtu ambaye ndiye mwenye pesa alikuwa kaingia ndani,hivyo nisingeweza kuagiza bila ruhusa ya mtoa pesa!,baada ya dakika kadhaa jamaa alikuja kwa mbwembwe huku akiniambia "Mwanangu agiza chochote uletewe ule".


Kabla sijamuita muhudumu jamaa alipaza sauti "Wewe muhudumu njoo umsikilize jamaa hapa".Mrume ndago niliagiza wali samaki pamoja na Soda.

Jamaa aliniuliza "Vipi mwanangu upigi mambo yetu?".

Nikamwambia "Hapana kaka sipigi".

Jamaa akaniambia "inaonekana kijana ushakuwa mlokole,yaani ukorofi na utundu wote ule wa shule ya msingi hupigi huang'unywa?".

Neno "Huang'unywa" alimaanisha pombe,ndizo lugha tulizokuwa tunazitumia kipindi hicho tukiwa wadogo.Basi stori za hapa na pale ziliendelea tukiendelea kukumbushana jamaa na marafiki tuliosoma nao,baada ya kumaliza kula ilibidi nimuulize jamaa alikuwa anapiga ishu gani!,maana alikuwa kanawili sana na ukiangalia mimi wakati huo nilikuwa nimechoka ile kishenzi.Jamaa aliniambia yeye anajihusisha na mambo ya madini ila akasema isingekuwa vyema tuongee pale hilo jambo ila aliniambia nijitahidi nitafute siku niende Geita,ndani ya siku chache ili nika-experience maisha ya kule namna yalivyo.Basi baada ya hapo jamaa akanipa elfu 30 ,mimi nikamuaga ila nilimwambia sina hata simu,aliniambia nisiwaze nijatahidi nitafute siku niende huko Geita kwani angesababisha hayo yote!,Baada ya maongezi nilimuaga jamaa ili kuondoka,alinipakia kwenye gari yake mpaka mabatini kisha nikachukua daladala za kuelekea Nyegezi nyumbani!.

Kiukweli ile elfu 30 niliona kama kanipa milioni,ukizingatia nilikuwa nimepigika na maisha ile sana!,Pia nilikuwa nawaza sana,inawezekanaje mtu niliyemzidi kila kitu kuanzia akili,elimu mpaka maisha enzi hizo leo anizidi maisha?,niliumia sana lakini sikuwa nala kufanya!,sasa pale nyumbani kuna hela nilikuwa nimesevu,hivyo nikachukua na hii jamaa ambayo alinipa nikajumlisha ikawa ya kutosha japo si haba!,kesho yake ilibidi niingie kwenye mitumba kusaka nguo za kushindia hapo mtaani.Nilipata suruali mbili nikanunua na makobazi pamoja na sweta.

Baada ya wiki nilianza kuwaza namna ya kwenda Geita ili nikaonane na jamaa uenda angenipataia kazi yoyote nifanye maana niliona kama nimechelewa sana katika maisha!,jamaa kipindi tupo hotelini kule Igoma, alinipa direction ya kwamba nikifika Katoro kuna jina alilokuwa analitumia huko lilikuwa maarufu sana,hivyo alinitajia hilo jina akasema endapo nitafika hapo nikimuuliza hata watoto wangenipeleka kwake!,lile jina lake la shule ya msingi aliniambia kule hakuna aliyekuwa analifahamu bali lilikuwa limebaki kwenye vyeti vya kuzaliwa tu.




Itaendelea......................
Hapa nime subscribe maana naona mauzauza.

Connectivity, how is main idea here.


Ndg mwandishi andika episode ndefu kidogo maana Kuna watu Wana comment ndefu kuliko Uzi(episody) yako
 
Telegram ni km jf tu unatumia username una hide kila kitu hakuna anaekujua huyu lwanda mwenyewe huku telegram hatumjui

Na buku sio kitu hata km unalipia stori kuna vitabu vinaizwa 20 jmn eb acheni kupenda vitonga mtu anatumia bundle na muda wake kukufurahisha unataka iwe bure

View attachment 1679442
Napataje hii link Mkuu
 
Back
Top Bottom