marehem x
JF-Expert Member
- Dec 28, 2022
- 513
- 792
Link tafadhaliNaomba link ya telegram ILIPO hii hadithi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Link tafadhaliNaomba link ya telegram ILIPO hii hadithi
Bora hata link ya telegram. Pana majitu mapumbavu Sana.Naomba link ya telegram ILIPO hii hadithi
Mkuu you tube Hilo bando ni kufa mtuHii stori nimesikiliza YouTube inatisha sana [emoji119]
Mkuu Mimi nashangaa Sana. Nilikuwa naifuatilia Sana. Lkn nikisoma comment za hayo majini watu nashangaa Kwa nn wanamkatisha jamaa .Hii simulizi imekuwa tamu, ukitishia kusababisha isiletwe unatafuta ugomvi.
[emoji856][emoji856]UTAJIRI WA NGUVU ZA GIZA ULIVYOHARIBU MAISHA YANGU- Hiki ndicho kisa cha pili cha maisha yangu,hapo mwanzo nilisema nina visa viwili,cha kwanza nimeshakisimulia,hivyo hiki ni kisa cha pili.KARIBUNI MJIFUNZE.
MKASA WA PILI- Sehemu ya 1.
MWAKA 2012.
Baada ya kuwa nimemaliza shule ya sekondari nilirudi nyumbani Mwanza,baada ya mama kuwa ameuza ile nyumba ya Tarime ilibidi ajenge nyumba nyingine Mwanza,japo haikuwa kubwa kama ile ya Tarime lakini kwa kiasi fulani ilikuwa nzuri naya wastani!,nilirudi nyumbani nikawa nafundisha wanafunzi tuisheni ili angalau niweze kupata hela za kununua sabuni na mahitaji madogo madogo,sikuweza tena kumuomba mama pesa maana tayari nishakuwa mtu zima,pia kwa wakati huo hali ya mama haikuwa nzuri kifedha,kuna shuke moja ambayo haikuwa ya serikali huko maeneo ya buhongwa,waliniajiri kama mwalimu wa muda na wakawa wananilipa kutoka na vipindi ambavyo nilikuwa nikihudhuria,hivyo nilikuwa nikitoka hapo shuleni naelekea ilipokuwa kituo cha tuisheni kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi masomo ya ziada,nilikuwa nalipwa na wale wanafunzi Tsh elfu 3000 kila nilipokuwa nikimaliza topic.
Basi kuna siku katika pitapita zangu mtaani wakati natoka huko shuleni,kwa mbali kidogo nikamuona jamaa mmoja tuliyekuwa tumesoma wote shule ya msingi Turwa kule Tarime,kiukweli sikuweza kufahamu kama ndiye au nilimfananisha,jamaa alikuwa pembeni anaongea na simu,hivyo nilijaribu kusogea karibu nione kama ndiye!.Kweli!,baada ya kusogea karibu nikamwita jina lake,jamaa aliitika na aliponiona alinifanyia ishara kwamba nisubiri kwanza amalize kuongea na simu,basi jamaa alipomaliza kuongea na simu alifurahi sana kukutana na mimi,mimi pia nilifurahi sana maana jamaa alikuwa kabadilika sana na kanenepa ile kishenzi,watoto wa mjini wanasema "Shavu dodo",kiukweli jamaa alikuwa kanawili,nilivyomuona tu nilifahamu lazima alikuwa na maisha mazuri.
Jamaa aliniuliza "Aisee za miaka mingi?".
Nikamjibu "Nzuri".
Jamaa akaniambia "Hebu nikumbushe wewe ni nani na nilikuona wapi vile!".
Kimoyo moyo nilijisemea "Ina maana jamaa mara hii kanisahau au ndiyo mambo ya mjini?".
Basi ilibidi nimkumbushie jina langu na tulisoma wote Tarime,jamaa alicheka sana,ndipo tukaanza kukumbushiana matukio,vimbwanga na vitimbi vya shule!,tulipiga michapo sana na nikamueleza mimi niliendelea na shule na nikamwambia Tarime tulihama muda sana.Jamaa alinichukua tukasogea mbele kidogo kumbe alikuwa kapaki gari!.Tulipanda kwenye gari kuelekea maeneo ya Igoma ambako alikuwa kachukua hoteli huko.Wakati tukiwa kwenye gari alikuwa ananiambia kwamba yeye baada ya kumaliza shule ya msingi matokeo yake hayakuwa mazuri,hivyo ilibidi aende kutafuta maisha,akaniambia yupo huko mkoani Geita sehemu moja inaitwa Katoro,kajenga huko na maisha yake yapo huko,ila siku hiyo alikuwa kaja hapo Mwanza kwa ajili ya biashara zake nyingine.Huyu jamaa kipindi tunasoma alikuwa hajiwezi kimasomo(kilaza),kiukweli ningeshangaa sana kusikia aliendelea na Shule!.
Baada ya kufika hapo hotelini alipofikia mimi nilikaa nje yeye akaingia huko ndani,muhudumu alikuja kuniuliza natumia nini lakini nilisita kumwambia maana sikuwa na kitu, mtu ambaye ndiye mwenye pesa alikuwa kaingia ndani,hivyo nisingeweza kuagiza bila ruhusa ya mtoa pesa!,baada ya dakika kadhaa jamaa alikuja kwa mbwembwe huku akiniambia "Mwanangu agiza chochote uletewe ule".
Kabla sijamuita muhudumu jamaa alipaza sauti "Wewe muhudumu njoo umsikilize jamaa hapa".Mrume ndago niliagiza wali samaki pamoja na Soda.
Jamaa aliniuliza "Vipi mwanangu upigi mambo yetu?".
Nikamwambia "Hapana kaka sipigi".
Jamaa akaniambia "inaonekana kijana ushakuwa mlokole,yaani ukorofi na utundu wote ule wa shule ya msingi hupigi huang'unywa?".
Neno "Huang'unywa" alimaanisha pombe,ndizo lugha tulizokuwa tunazitumia kipindi hicho tukiwa wadogo.Basi stori za hapa na pale ziliendelea tukiendelea kukumbushana jamaa na marafiki tuliosoma nao,baada ya kumaliza kula ilibidi nimuulize jamaa alikuwa anapiga ishu gani!,maana alikuwa kanawili sana na ukiangalia mimi wakati huo nilikuwa nimechoka ile kishenzi.Jamaa aliniambia yeye anajihusisha na mambo ya madini ila akasema isingekuwa vyema tuongee pale hilo jambo ila aliniambia nijitahidi nitafute siku niende Geita,ndani ya siku chache ili nika-experience maisha ya kule namna yalivyo.Basi baada ya hapo jamaa akanipa elfu 30 ,mimi nikamuaga ila nilimwambia sina hata simu,aliniambia nisiwaze nijatahidi nitafute siku niende huko Geita kwani angesababisha hayo yote!,Baada ya maongezi nilimuaga jamaa ili kuondoka,alinipakia kwenye gari yake mpaka mabatini kisha nikachukua daladala za kuelekea Nyegezi nyumbani!.
Kiukweli ile elfu 30 niliona kama kanipa milioni,ukizingatia nilikuwa nimepigika na maisha ile sana!,Pia nilikuwa nawaza sana,inawezekanaje mtu niliyemzidi kila kitu kuanzia akili,elimu mpaka maisha enzi hizo leo anizidi maisha?,niliumia sana lakini sikuwa nala kufanya!,sasa pale nyumbani kuna hela nilikuwa nimesevu,hivyo nikachukua na hii jamaa ambayo alinipa nikajumlisha ikawa ya kutosha japo si haba!,kesho yake ilibidi niingie kwenye mitumba kusaka nguo za kushindia hapo mtaani.Nilipata suruali mbili nikanunua na makobazi pamoja na sweta.
Baada ya wiki nilianza kuwaza namna ya kwenda Geita ili nikaonane na jamaa uenda angenipataia kazi yoyote nifanye maana niliona kama nimechelewa sana katika maisha!,jamaa kipindi tupo hotelini kule Igoma, alinipa direction ya kwamba nikifika Katoro kuna jina alilokuwa analitumia huko lilikuwa maarufu sana,hivyo alinitajia hilo jina akasema endapo nitafika hapo nikimuuliza hata watoto wangenipeleka kwake!,lile jina lake la shule ya msingi aliniambia kule hakuna aliyekuwa analifahamu bali lilikuwa limebaki kwenye vyeti vya kuzaliwa tu.
Itaendelea......................
Japo comment yako niya muda mrefu ila nimewiwa nikujibu kwa kifupi.It's time for reasoning, ngoja tuwashe taa kidogo!
Hii ni hoja rahisi sana ambayo mpaka leo sijapata mtu wa kuikosoa.
Ipo hivi,hakuna tofauti yoyote ile kati ya kisa cha kweli cha kichawi/ushirikina/maajabu(kama kimewahi kuwepo) na kisa cha kutunga(work of fiction) kinachohusu uchawi/ushirikina/maajabu
Hata kama katika kisa cha kutunga kumetajwa maeneo ya kweli ambayo wenyeji wamekili kuyafahamu
Filamu ya Titanic ime base katika tukio la kweli lakini sote tunajua Jack na Rose hawakua Real
Mwandishi yoyote makini anaweza Fanya extensive research ya maeneo mbalimbali,Lugha,na key people katika maeneo hayo kisha akaja na kisa cha kutunga ambacho kipo consistent na research aliyofanya
Point hapa ni hivi,ni vigumu kutofautisha kisa cha kweli cha kichawi/kishirikina/maajabu na kile kilichobuniwa
Hata kama una amini uchawi au imani za kishirikina ni mambo ya kweli bado ni vigumu kutofautisha kati ya kisa cha kweli na kile kilichotungwa unless upo tayari kuamini kila aina ya taka taka utakayosimuliwa na mgeni yoyote utakayekutana nae mtandaoni
Pia tukipiga mahesabu,probability ya simulizi hii kuwa ya tukio la kweli ni ndogo sana kuliko probability ya simulizi hii kuwa kisa cha kutunga
Kwa maneno mengine,kuna 99.9% kuwa kisa hiki ni cha kutunga kuliko 0.1% kuwa kisa hiki ni cha kweli.....
Kivipi,tukio moja tu katika kisa hiki,kama ni cha kweli kina uwezo wa ku "disprove" misingi yote ya Sayansi kwanzia kipindi cha Aristotle,Copernicus,Leibniz, Newton, Dirac,Einstein, Bohr,Gödel,Feyman,Hawking na wengine wengi
Mfano kama kweli mtu anaweza fumba macho na kufumbua(almost sekunde moja) akatoka Mwanza mpaka mbeya,hakuna Energy yoyote iliyotumika,na wala hakuonekana kuchoka
Then ni Obvious, Principle of conservation of Energy ambayo imekua msingi Wa sayansi kwa karne,na kutupa majibu sahihi mda wote ni ya "UONGO"
Kama kweli ziwa linaweza gawanyika,na ndani kukawa na mji mkubwa,Sayansi nzima kama tunavyoijua inakua ni "Takataka" kwasababu haiwezi tupa maelezo ya tukio hilo na matukio mengine yote ya kushangaza katika simulizi hii
Sasa kati ya maelezo haya mawili,yapi yanaweza kuwa sahihi?
1.Simulizi hii,ambayo ushahidi pekee tulio nao kuihusu,unatoka kwa msimulizi aliyetuletea simulizi hii na baadhi wanao support kuwepo kwa maeneo tajwa(means setting ya story ni ya kweli japo hii haiwezi count kama evidence) ni ya kweli,na Aristotle,Copernicus, Leibniz, Newton,Darwin,Einstein, Dirac,Bohr,Plank,Maxwell wote hawakua sahihi pamoja na scientific papers zote zilizowahi kuandikwa pamoja na tafiti zote za kisayansi zilizofanyika na zilizowahi kufanyika
Au
2.kisa hiki ni cha kutunga
Maelezo yapi yanaweza kuwa sahihi? 1 au 2?
Tuwe tunatumia akili zote kuhoji vitu,
The reason why nakua mgumu kuamini visa kama hivi ni jinsi gani haviweka "more details" haswa hapo kwenye matukio muhimu
Mfano,ni kwa jinsi gani alikua ananyonya damu za abiria kwenye kibuyu na kuwakausha kabisa,ili hali hakujawahi ripotiwa ajari yoyote ambayo maiti zote zilikutwa bila damu?
Huo ungo ulikua mkubwa kiasi gani kutosha watu watatu,uliundwa kwa material gani? Au ni zoom tu huu ungo wa kawaida?
Pia kwanini ungo?, hii imeshakuwa common trope kwenye simulizi za aina hii,
Achilia mbali characters waliokosa uhalisia kabisa kama "Mungu bonge mwenye sauti ya mtoto"
Kapoteza muda na nguvu kuandika gazeti akiliita uchambuzi, uchambuzi uchwara!!japo commentd yako niya muda
Japo comment yako niya muda mrefu ila nimewiwa nikujibu kwa kifupi.
1. haujui chochote kuhusu ulimwengu wa roho na utendaji kazi wake.
2. unajitoa fahamu , sihusian na mtoa maada ila kuna mengi sana yanaendelea ila wewe una macho ila ni KIPOFU
Na wewe nakusubiri kule kwa MUNGU wa walokole ndio umeishia pale au kuna muendelezoDuuuh story imeishia hapa😂🤣🤣🤣🤣🤣🤣Lwanda Magere kaishia mitini duuuh🤣🤣🤣🤣 wadau mna roho ngumu hamjachanga buku buku za bando
👁️Hadithi: Uchawi wa bilionea Bazoka
NYEMO CHILONGANI. UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA. 0718069269 Ndiyo kwanza mwanga wa asubuhi ulikuwa ukitokeza, watu waliokuwa wakifanya kazi sehemu za mbali, wakaamka na kuanza kujiandaa kwenda makazini, kwa wale waliokuwa njiani kuelekea makazini kwao, wakaongeza kasi ili kuwahi na kuanza kazi...www.jamiiforums.com