BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Chama cha ACT-Wazalendo kimeiomba Serikali kupitia mfumo mzima wa ukopeshaji unaotekelezwa na taasisi zisizo za kiserikali nchini kwa kuwa wananyinywa na kuhatarisha maisha ya wanawake.
Kimetolea mfano wa mikopo inayojulikana kausha damu kuwa licha ya kuwasumbua wanawake pia imevunja ndoa nyingi.
Ombi hilo limetolewa leo jumanne jioni na Makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo Tanzania Bars,Doroth Samu wakati wa kongamano la kitaifa la wanawake lililofanyika jijini hapa.
Amesema kutokana na hali ngumu ya maisha wanawake wengi nameingia katika majukumu la kusaidiana na waume zao katika kulea familia hivyo wanalazimika kukopa kwa mategemeo ya kuendesha maisha na maendeleo kwa ujumla.
Amesema tofauti na matarajio yao wamejikuta wakifanya kazi za kuzitajirisha taasisi zinazowakopesha kwa sababu zinatoza riba kubwa isiyolipika kwa njia za rahisi.
"Wanawake ndiyo waathirika wakubwa wa mikopo hiyo kwa sababu wanalazimika kujiunga na mikopo mingi ili waweze kulipa...lakini wanajikuta wakiingia katika migogoro ya ndoa na wengine wanaamua kukatisha maisha yao kwa sababu ya msongo wa mawazo ya madeni," alisema Doroth.
Amesema njia ya kuwasaidia wanawake nchini ni kufanyia marekebisho mfumo mzima wa riba katika mikopo ya taasisi binafsi ili isiweze kuwanyonya wakopaji.
MWANANCHI
Kimetolea mfano wa mikopo inayojulikana kausha damu kuwa licha ya kuwasumbua wanawake pia imevunja ndoa nyingi.
Ombi hilo limetolewa leo jumanne jioni na Makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo Tanzania Bars,Doroth Samu wakati wa kongamano la kitaifa la wanawake lililofanyika jijini hapa.
Amesema kutokana na hali ngumu ya maisha wanawake wengi nameingia katika majukumu la kusaidiana na waume zao katika kulea familia hivyo wanalazimika kukopa kwa mategemeo ya kuendesha maisha na maendeleo kwa ujumla.
Amesema tofauti na matarajio yao wamejikuta wakifanya kazi za kuzitajirisha taasisi zinazowakopesha kwa sababu zinatoza riba kubwa isiyolipika kwa njia za rahisi.
"Wanawake ndiyo waathirika wakubwa wa mikopo hiyo kwa sababu wanalazimika kujiunga na mikopo mingi ili waweze kulipa...lakini wanajikuta wakiingia katika migogoro ya ndoa na wengine wanaamua kukatisha maisha yao kwa sababu ya msongo wa mawazo ya madeni," alisema Doroth.
Amesema njia ya kuwasaidia wanawake nchini ni kufanyia marekebisho mfumo mzima wa riba katika mikopo ya taasisi binafsi ili isiweze kuwanyonya wakopaji.
MWANANCHI