Tetesi: Mikopo ya 10% ya Halmashauri imegeuka kuwa mikopo ya Wanachama wa CCM

Tetesi: Mikopo ya 10% ya Halmashauri imegeuka kuwa mikopo ya Wanachama wa CCM

Even MOre

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2023
Posts
204
Reaction score
298
Habari wana jamvi.

Naomba kuwasilisha mada hii kuviomba vyama vya Upinzani vipaze sauti kuhusu utaratibu mbovu ambao kwa sasa Halmashauri nyingi Nchini wanafanya kutoa mikopo kwa kigezo cha kuwa mwanachama wa CCM hasa vikundi vya wanachama wao ndivyo vinapewa mkopo.

Niko Mkoa x na ninafanya kazi katika vitengo ambayo vinapelekea kupata taarifa hizi. Mwaka juzi waliondoa majina ya baadhi ya wanakikundi ambao kwa maelezo yao walikuwa na mlengo wa kisiasa tofauti baada ya kupewa maelekezo na diwani wa eneo husika kuwa ikiwa watawaweka watu hao wasahau kuhusu mkopo na kama wanahitaji mkopo wawatoe haraka kwenye kikundi.

Kwa uelewa wangu ni kuwa fedha za 10% ya mikopo ya Wanawake, Vijana na Wazee ya Halmashauri ni fedha ambayo inatolewa na Serikali ikiwa ni mapato yatokanayo na kodi za wananchi wote pasipo kujali vyama wala itikadi zao na fedha hizi HAZITOLEWI NA CHAMA CHA CCM kwenda kwa wanachama wake.

Hivyo Serikali kupitia watendaji wake wanasimamia na kuratibu mambo haya ambayo yakiachwa baadae yatakuja kuleta athari kubwa hata mgawanyiko katika jamii.

Nawasilisha
 
Rc kada wa ccm
Ras kada wa ccm
Dc kada wa ccm
Ras kada wa ccm
Ded kada wa ccm
Alafu ongezea.. huwezi kuwa mkuu wa kitengo kama we sio mwanachama wa ccm.

Je unatarajia nini hapo?
 
Hii mbona iko wazi kitambo bila kadi ya kijani hunusi ni miaka sasa
 
Nepotism siyo kitu kigeni au kitu kipya kwenye nchi yoyote ile hapa duniani ambayo utawala wake umefitinika. Ina maana unataka kusema kwamba siku zote hizi wewe ulikuwa hujui kwamba tatizo hili kweli lipo hapa Tanzania?
 
Ile ni Mikopo ya Wanachama na watoto wa wazee wanaoshindwa kurejesha hakuna tatizo naona vijana wapo busy kuchukua kadi kisa hiyo Mikopo...kama sio Mwanakondoo mkopo haupewi hata iweje...
 
Muhumu ni kuhakikisha majiji,Manispaa zote next year zinachukuliwa na upinzani.

Ili uponzani upange uelekeo wa hiyo mikopo .
Hakikisheni mnapata madiwani wengi kuunda halmashauri hizo.
 
Ndugu,

Ondoa hilo neno Tetesi, kwani huo ni ukweli ulio dhahiri kwani mimi mwenyewe binafsi nimewahi kufuatilia mkopo huo na kigezo kikuu kilikuwa ni uwe mwanachama tena uwe na kadi ya uanachama. Anaepinga yeyote juu ya hili aje. Ilinibidi nifocus kwenye mambo mengine tu.
 
Ndugu,

Ondoa hilo neno Tetesi, kwani huo ni ukweli ulio dhahiri kwani mimi mwenyewe binafsi nimewahi kufuatilia mkopo huo na kigezo kikuu kilikuwa ni uwe mwanachama tena uwe na kadi ya uanachama. Anaepinga yeyote juu ya hili aje. Ilinibidi nifocus kwenye mambo mengine tu.
Ok asante kwa ushuhuda huo, ila neno tTETEZI MODS NDO WAMEWEKA
 
Ok asante kwa ushuhuda huo, ila neno tTETEZI MODS NDO WAMEWEKA
Basi halitakiwi kuwepo, tena ukiwa ni mwanachama wao lazima wajue unamapenzi na nani kwenye hiyo kata yenu na unamkubali mbunge yupi jimboni kwenu. Kwa ufupi kuna upumbavu mwingi mnoo!
 
Back
Top Bottom