Even MOre
JF-Expert Member
- May 6, 2023
- 204
- 298
Habari wana jamvi.
Naomba kuwasilisha mada hii kuviomba vyama vya Upinzani vipaze sauti kuhusu utaratibu mbovu ambao kwa sasa Halmashauri nyingi Nchini wanafanya kutoa mikopo kwa kigezo cha kuwa mwanachama wa CCM hasa vikundi vya wanachama wao ndivyo vinapewa mkopo.
Niko Mkoa x na ninafanya kazi katika vitengo ambayo vinapelekea kupata taarifa hizi. Mwaka juzi waliondoa majina ya baadhi ya wanakikundi ambao kwa maelezo yao walikuwa na mlengo wa kisiasa tofauti baada ya kupewa maelekezo na diwani wa eneo husika kuwa ikiwa watawaweka watu hao wasahau kuhusu mkopo na kama wanahitaji mkopo wawatoe haraka kwenye kikundi.
Kwa uelewa wangu ni kuwa fedha za 10% ya mikopo ya Wanawake, Vijana na Wazee ya Halmashauri ni fedha ambayo inatolewa na Serikali ikiwa ni mapato yatokanayo na kodi za wananchi wote pasipo kujali vyama wala itikadi zao na fedha hizi HAZITOLEWI NA CHAMA CHA CCM kwenda kwa wanachama wake.
Hivyo Serikali kupitia watendaji wake wanasimamia na kuratibu mambo haya ambayo yakiachwa baadae yatakuja kuleta athari kubwa hata mgawanyiko katika jamii.
Nawasilisha
Naomba kuwasilisha mada hii kuviomba vyama vya Upinzani vipaze sauti kuhusu utaratibu mbovu ambao kwa sasa Halmashauri nyingi Nchini wanafanya kutoa mikopo kwa kigezo cha kuwa mwanachama wa CCM hasa vikundi vya wanachama wao ndivyo vinapewa mkopo.
Niko Mkoa x na ninafanya kazi katika vitengo ambayo vinapelekea kupata taarifa hizi. Mwaka juzi waliondoa majina ya baadhi ya wanakikundi ambao kwa maelezo yao walikuwa na mlengo wa kisiasa tofauti baada ya kupewa maelekezo na diwani wa eneo husika kuwa ikiwa watawaweka watu hao wasahau kuhusu mkopo na kama wanahitaji mkopo wawatoe haraka kwenye kikundi.
Kwa uelewa wangu ni kuwa fedha za 10% ya mikopo ya Wanawake, Vijana na Wazee ya Halmashauri ni fedha ambayo inatolewa na Serikali ikiwa ni mapato yatokanayo na kodi za wananchi wote pasipo kujali vyama wala itikadi zao na fedha hizi HAZITOLEWI NA CHAMA CHA CCM kwenda kwa wanachama wake.
Hivyo Serikali kupitia watendaji wake wanasimamia na kuratibu mambo haya ambayo yakiachwa baadae yatakuja kuleta athari kubwa hata mgawanyiko katika jamii.
Nawasilisha