Mikopo ya mitandaoni lawama zinawahusu pia TCRA, msikwepe

Mikopo ya mitandaoni lawama zinawahusu pia TCRA, msikwepe

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,311
Reaction score
15,640
Nimeskia redioni TCRA wanasema hawahusiki na hiki kinachoendelea kwenye mikopo mitandaoni. TCRA mnaweza kuwa hamuhusiki kweli ila na nyie pia mmezembea sana kama wenzenu BOT licha ya makelele mengi kuhusu hawa mikopo mitandaoni ambao wengi hawajajisajili na wala hawana physical address.

kwanza jina lenu linatumika sana na hawa mikopo mitandaoni kuwa mnashirikiana nao na mpo kimya hamjakemea. Pili hamjaonesha hatua yoyote ya kudhibiti hili ikiwemo tabia ya hawa wakopeshaji kusajili line za simu zaidi ya 20 ili kutukana na kudhalilisha watu.

Na tayari imeonekana kuwa hizi line nyingi ambazo wanatumia kutukana watu wamezisajili kwa kutumia vitambulisho vya wateja wao, kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa mteja aliekabidhi data zake.

Tatu hamjachukua hatua zozote kudhibiti hizi Apps licha ya BOT kutoa muongozo ambao nao hawajachukua hatua zozote zaidi, ila nyie mngeshachukua hatua kwa upande wenu.

Mngeshachukua hatua za dharura ili watu wazireport hizo namba kwenu kwa hatua za kiuchungizi au kudhibiti.
 
Hawahusiki?
Ukitaka kujua wanahusika tumia mitandao kuipinga serikali.
Chap tu taarifa zako zinapatikana.
 
HAO WENYE APP za mikopo wanatoa matangazo ya uongo kuwa utakopeshwa na utalipa kwa mwezi ! wakati unatakiwa ulipe ndani ya siku sita ! mfano APP ya HIPESA lakini TCRA hawajali hawafuatilii wamekaa tu kwenye vuyoyozi wanasubiri kina Sativa kina CHADEMA NK
 
HAO WENYE APP za mikopo wanatoa matangazo ya uongo kuwa utakopeshwa na utalipa kwa mwezi ! wakati unatakiwa ulipe ndani ya siku sita ! mfano APP ya HIPESA lakini TCRA hawajali hawafuatilii wamekaa tu kwenye vuyoyozi wanasubiri kina Sativa kina CHADEMA NK
chadema wakorofi lazima wadhibitiwe wanahatarisha usalama wa nchi sasa hao wakopeshaji wanahatari gani?
 
Majina ya Bakhressa, Mo Dewji, Tulia, Jokate,Nandy nk yantumika kutapeli watu na wenye majina wamekanusha kuhusika na matapeli Hawa iwaje TCRA wapo kimya au kuna wenye maslahi.
 
Hao wakopeshaji mtandaoni wenye namba nyingi wamesajiliwa vizuri kabisa kwa sababu namba zinasoma majina ya kampuni hizo.
Wasitufanye wajinga.
 
We shotocan madeni yana taratibu zake sio hayo ya kausha damu za APP kulipa nndani ya siku tano sita unapigiwa simu saa nane za usiku ukiwa umelala !
 
Back
Top Bottom