Mikutano ya hadhara imeruhusiwa ili itumike kuua legacy ya Hayati Magufuli ya kufunika kasoro za sasa

Mikutano ya hadhara imeruhusiwa ili itumike kuua legacy ya Hayati Magufuli ya kufunika kasoro za sasa

Kosinde

Member
Joined
Jun 7, 2018
Posts
49
Reaction score
61
Kwa mara ya kwnza tunashuhudia upinzani wa aina yake nchini Tanzania, upinzani ambao unaacha kupigana na utawala uliopo na badala yake unapigana na kivuli cha marehemu Magufuli.

Naomba ieleweke kuwa hili halitokei kwa bahati mbaya, Zitto Kabwe kukejeli ndege zilizonunuliwa na Serikali ya awamu ya tano, si kwa bahati mbaya, Tundu Lissu kumsema vibaya Magufuli na uongozi wake ni mkakati wa kuua kabisa legacy aliyoiacha ili aliyepo aweze kung'ara maana bila hivyo anaonekana hajafanya kitu.

Haya yanayoendelea ni utekelezaji wa kinachoitwa "maridhiano" ya 'scrach my back I scrach yours' vyama vya upinzani vimeingia maridhiano ya kusaidia utawala uliopo ili na wao waweze kulegezewa maisha yao yaende.

Naposema maisha yao yaende muelewe kwamba upinzani haujawahi kuwa kwaajili ya kusaidia wananchi bali wananchi ndio wanaowasaidia kutimiza malengo yao ya kuitisha Serikali na kuweza kuitwa Ikulu kupewa vibahasha (hii waliikosa kipindi cha awamu ya tano) .

Hii inayoitwa nguvu ya umma ndiyo mtaji wa vyama vya upinzani kujaza matumbo yao. Mbowe anapoonekana kuwa na ushawishi wa watu wengi basi lazima Serikali itamwogopa na kumwita mezani hali kadhalika Zitto na wachumia tumbo wengine.

Watanzania tusitarajie kipya katika mikutano hii ya hadhara zaidi ya kusikia Magufuli alifanya baya hili na lile, wanalipa bili kwa aliyewapa kazi hiyo na wanafanya hivyo wakijua Watanzania watasema ni kwasababu Magufuli aliwabana hivyo wanalipa kisasi lakini ukweli ni zaidi ya kulipa kisasi. Wanalipa bili.

Yapo mambo mengi sana yanayotokea sasa hivi ambayo upinzani unapaswa kusaidia kuyasemea lakini wao wamebaki kumshambulia Magufuli ambaye masikini wa Mungu kajipumzikia.

Mfano mzuri mtakumbuka huyu Zitto wakati wa nyuma alikuwa mkosoaji mkubwa sana wa kuongezeka kwa deni la Taifa, hakuna bajeti iliyokuwa inapita bila Zitto kuonya na kufanya analysis kuhusu kuongezeka kwa deni la Taifa, lakini kama walivyosema wahenga njaa ikiamia kichwani ni mbaya, sasa hivi Zitto amekuwa muimba mapambio na wala hazungumzii kabisa kasi ya ongezeko la Deni la Taifa kipindi ambacho hata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Geterres, ameonya kuwa madeni ndiyo yanayozimaliza nchi za Afrika

Zitto yupo kimya kipindi ambacho alipaswa kupiga kelele kama mwehu, kuliko ambavyo aliwahi kufanya huko nyuma, ila kwasababu tu ya kuwa kwenye payroll ya nyumba nyeupe, ameacha na anawahadaa Watanzania kwa kusema ndege zina kutu lakini hasemi vipi kuhusu zilizoagizwa na Serikali ya awamu ya sita ambazo nazo ni matoleo hayo hayo.
 
Yesu anasemwa vibaya iwe ajabu kwa mwanadamu?

Wacha watu wawe huru kuzungumza watakacho bhana hii dunia ni ya Mungu tu. Mungu mwenyewe ndo anajua kipi kitastahili mbeleni
 
Kwa trend ya Upinzani ninayoiyona ninashawishika kukuunga maneno yako
 
Yesu anasemwa vibaya iwe ajabu kwa mwanadamu?

Wacha watu wawe huru kuzungumza watakacho bhana hii dunia ni ya Mungu tu. Mungu mwenyewe ndo anajua kipi kitastahili mbeleni
Kwani yesu sio binadamu?
 
Asante Kasinde.

Niongeze, kwa kutofautiana kidogo,Legacy yake haifutiki.
Wanacho kifanya(yeyote yule) ni kubadilisha nadharia na kuweka taswira ya kwamba, akitokea yeyote aliyekuwa na fikra kama za Hayat Rais, basi utakufa, na utawekewa kejeli, matusi na mabezo yatakuandama mpaka kaburini. Yaani ni ugaidi wa namna fulani.

Inajulikana Aliwakwaza mabeberu na mabepari wa ndani na nje, aliwafinyia mirija, sasa kwa uwezo wao, wanawatumia wasiojielewa kusambaza uwongo kwani wanajua wana visasi.

Ni aibu.
 
Nyie watu mlifaidika nini na uuwaji wa Magufuli? Je, mnapenda bado kuendelea kushiriki naye laana zake zinazotokana na vitendo viovu alivyofanya?
 
Wewe bogus kabisa! Lucifer Magufuli lazima atukanwe na asemwe sana kwa sababu aliendesha utawala wa kijizi, kijambazi, kifisadi, kikatili, kiuaji nk nk!

Mbwa yule anastahili hata kaburi lake lilipuliwa kwa bomu afutike kabisa katika historia ya nchi yetu!

Jitu katili mpaka shetani mkuu alishangaa!
 
Hawataweza. Labda wabadili hali ya hewa na kudhibiti mfumko wa bei.

Yaani wananchi 'wa kawaida' wanavyomchukia huyo mama unaweza kusema yeye ndio kasabaisha ukame na ugumu wa maisha.
 
0BCD0CD8-C8E4-4AB6-BBDA-9CB37E907233.jpeg
 
Wewe bogus kabisa! Lucifer Magufuli lazima atukanwe na asemwe sana kwa sababu aliendesha utawala wa kijizi, kijambazi, kifisadi, kikatili, kiuaji nk nk!
Mbwa yule anastahili hata kaburi lake lilipuliwa kwa bomu afutike kabisa katika historia ya nchi yetu!

Jitu katili mpaka shetani
Hivi inasaidia nini kumsema marehemu kama sio tu ajenda ya kuua legacy yake? Asemwe sawa lakini isiwe ajenda ya watu fulani kwa malengo fulani hapo ndo inakuwa fedheha inapobainika
 
You people are truly bent on forming a cult.

So be it then.
 
Back
Top Bottom