Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MIKUTANO YA HADHARA NA HARAMBEE ZA UJENZI WA SEKONDARI MPYA MUSOMA VIJIJINI
Wito:
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, ameombwa na wananchi wa baadhi za kata aungane nao kwenye ujenzi wa sekondari ya pili na ya tatu ya kata zao - Mbunge amekubali.
Takwimu:
Jumla ya Sekondari Jimboni mwetu:
(i) Sekondari 26 za Kata/Serikali
(ii) Sekondari 2 za Madhehebu ya Dini
(iii) Sekondari mpya 3 zinazojengwa kwa nguvu za wanavijiji na viongozi wao: Kisiwani Rukuba (Kata ya Etaro, sekondari ya pili), Kijijini Nyasaungu (Kata ya Ifulifu, sekondari ya pili) na Kijijini Muhoji (Kata ya Bugwema, sekondari ya pili - Serikali imeanza kuchangia).
Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025
(iv) Sekondari mpya 3 zinajengwa kwa kutumia fedha nyingi za Serikali: Kijijini Butata (Kata ya Bukima, sekondari ya pili), Kijijini Kasoma (Kata ya Nyamrandirira, sekondari ya tatu) na Kijijini Kurwaki (Kata ya Mugango, sekondari ya pili)
Sekondari hizi 3 zitafunguliwa Januari 2025
Jimbo letu lina Kata 21 zenye Vijiji 68 (jumla ya Vitongoji ni 374)
Ratiba ya Mikutano ya Hadhara na Harambee za ujenzi wa sekondari mpya:
Jumanne, 13.8.2024
Saa 4 Asubuhi: Kijijini Kataryo, Kata ya Tegeruka (sekondari ya pili)
Saa 9 Alasiri: Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro (sekondari ya tatu)
Jumatano, 14.8.2024
Saa 4 Asubuhi: Kijijini Chitare, Kata ya Makojo (sekondari ya pili)
Saa 9 Alasiri: Kijijini Kiriba, Kata ya Kiriba (sekondari ya tatu)
Alhamisi, 15.8.2024
Saa 4 Asubuhi: kazi maalumu
Saa 9 Alasiri: Kijijini Nyambono, Kata ya Nyambono (sekondari ya pili)
Ratiba ya Vijiji vya Butata (Kata ya Bukima), Kasoma (Kata ya Nyamrandirira) na Kurwaki (Kata ya Mugango) itatolewa baadae.
KARIBUNI TUCHANGIE UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Tarehe:
Ijumaa, 9.8.2024