suluhishojipya
Member
- Dec 10, 2017
- 57
- 143
Kwanza naomba kwa heshima na taadhima, admin msiunganishe uzi huu na mwingine.
Ndugu wanajukwaa, kama wote tupendavyo, juhudi za kupambana na rushwa na matumizi mabaya ya kodi za watanzania ni endelevu na popote pesa hizo zinapokwenda sisi watozwa kodi lazima tuhoji.
Nimeona uzi huku ndani
Hivi ndivyo Freeman Mbowe na genge lake anavyotafuna pesa za CHADEMA!
unaozungumzia ripoti ya CAG kwa mwaka 2016/17ambayo pamoja na mambo mengine inazungumzia pesa zilizolipwa M/S Milestone International Co. Ltd kiasi cha 866,600,000. Kumbuka malipo haya ni kwa mwaka mmoja wa 2016, hatujui miaka mingine ya nyuma, na 2017 na 2018.
Nilichotaka kuonyesha ni kuwa kampuni hii mmiliki wake ni Freeman Mbowe, na Managing Director ni Shemeji yake wa kike aitwaye, Kineneko Mtei mdogo wake Dr. Lilian Mtei, mke wa ndoa wa Freeman Mbowe.
Kwanza hapa kuna mgongano wa maslahi na harufu ya rushwa, haya machache ni kwa mujibu wa ripoti ya msajiri pale penye mashaka, kwa kweli CHADEMA kuna ufisadi, otherwise wangeweka wazi ripoti yao ya fedha wazi tuone matumizi yao kwa ujumla na wanaofaidika na kulipwa pesa hizo.
========
CHADEMA wamekanusha hii habari.
=========
Naomba kutoa ufafanuzi ufuatao kuhusu Kampuni ya Milestone kuhusishwa na Mhe.Freeman Mbowe kama ifuatavyo;
1. Mhe. Freeman Mbowe Mwenyekiti wa CHADEMA sio mmiliki na wala sio mjumbe wa bodi wa Kampuni tajwa na Hana maslahi nayo binafsi ya kifedha wala kibiashara.
2. Mhe.Freeman Mbowe sio mwanahisa na hajawahi kumiliki hisa za Kampuni ya matangazo ya Milestone kama ambavyo mwandishi mtoa tuhuma ametaka kuuaminisha umma kwenye andiko lake.
3. Mhe.Freeman Mbowe sio yeye aliyeingia mkataba na Kampuni ya Milestone ila ni Chama kilifanya hivyo mapema 2015 kabla ya Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2015 na hii ilikuwa baada ya kushindanisha makampuni kadhaa ya kutoa huduma za matangazo yaani Billiaboards na hatimaye Kampuni hii ikashinda zabuni husika ya kuweka mabango ya mgombea Urais wa UKAWA 2015 nchi nzima.
Kampuni hii ilikuwa na unafuu ukilinganisha na nyingine ambazo ziliomba zabuni husika ya kufanya kazi hiyo.
4. Tunamtaka mwazilishi wa tuhuma hizi atoe uthibitisho wowote alionao kuwa Kampuni hii inamilikiwa na Freeman Mbowe na sio kutoa tuhuma za jumla zenye lengo LA kuchafua watu na Chama kwa manufaa ya kipropaganda na yenye lengo ovu.
Mwisho, tunaishauri JF iweke utaratibu wa kuwataka uthibitisho Wanachama wake pale wanapoandika tuhuma nzito na zenye kuchafua watu binafsi na au taasisi kabla ya kuandika tuhuma nzito kama hizi.
CHADEMA tutaendelea kuwa imara Katika kusimamia matumizi bora ya rasilimali za taifa letu. Nawashukuru kwa ushirikiano.
John Mrema -Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA
Ndugu wanajukwaa, kama wote tupendavyo, juhudi za kupambana na rushwa na matumizi mabaya ya kodi za watanzania ni endelevu na popote pesa hizo zinapokwenda sisi watozwa kodi lazima tuhoji.
Nimeona uzi huku ndani
Hivi ndivyo Freeman Mbowe na genge lake anavyotafuna pesa za CHADEMA!
unaozungumzia ripoti ya CAG kwa mwaka 2016/17ambayo pamoja na mambo mengine inazungumzia pesa zilizolipwa M/S Milestone International Co. Ltd kiasi cha 866,600,000. Kumbuka malipo haya ni kwa mwaka mmoja wa 2016, hatujui miaka mingine ya nyuma, na 2017 na 2018.
Nilichotaka kuonyesha ni kuwa kampuni hii mmiliki wake ni Freeman Mbowe, na Managing Director ni Shemeji yake wa kike aitwaye, Kineneko Mtei mdogo wake Dr. Lilian Mtei, mke wa ndoa wa Freeman Mbowe.
Kwanza hapa kuna mgongano wa maslahi na harufu ya rushwa, haya machache ni kwa mujibu wa ripoti ya msajiri pale penye mashaka, kwa kweli CHADEMA kuna ufisadi, otherwise wangeweka wazi ripoti yao ya fedha wazi tuone matumizi yao kwa ujumla na wanaofaidika na kulipwa pesa hizo.
========
CHADEMA wamekanusha hii habari.
=========
Naomba kutoa ufafanuzi ufuatao kuhusu Kampuni ya Milestone kuhusishwa na Mhe.Freeman Mbowe kama ifuatavyo;
1. Mhe. Freeman Mbowe Mwenyekiti wa CHADEMA sio mmiliki na wala sio mjumbe wa bodi wa Kampuni tajwa na Hana maslahi nayo binafsi ya kifedha wala kibiashara.
2. Mhe.Freeman Mbowe sio mwanahisa na hajawahi kumiliki hisa za Kampuni ya matangazo ya Milestone kama ambavyo mwandishi mtoa tuhuma ametaka kuuaminisha umma kwenye andiko lake.
3. Mhe.Freeman Mbowe sio yeye aliyeingia mkataba na Kampuni ya Milestone ila ni Chama kilifanya hivyo mapema 2015 kabla ya Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2015 na hii ilikuwa baada ya kushindanisha makampuni kadhaa ya kutoa huduma za matangazo yaani Billiaboards na hatimaye Kampuni hii ikashinda zabuni husika ya kuweka mabango ya mgombea Urais wa UKAWA 2015 nchi nzima.
Kampuni hii ilikuwa na unafuu ukilinganisha na nyingine ambazo ziliomba zabuni husika ya kufanya kazi hiyo.
4. Tunamtaka mwazilishi wa tuhuma hizi atoe uthibitisho wowote alionao kuwa Kampuni hii inamilikiwa na Freeman Mbowe na sio kutoa tuhuma za jumla zenye lengo LA kuchafua watu na Chama kwa manufaa ya kipropaganda na yenye lengo ovu.
Mwisho, tunaishauri JF iweke utaratibu wa kuwataka uthibitisho Wanachama wake pale wanapoandika tuhuma nzito na zenye kuchafua watu binafsi na au taasisi kabla ya kuandika tuhuma nzito kama hizi.
CHADEMA tutaendelea kuwa imara Katika kusimamia matumizi bora ya rasilimali za taifa letu. Nawashukuru kwa ushirikiano.
John Mrema -Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA