Milioni 8 yako itakupa milioni 20 kwa mwaka mmoja

Milioni 8 yako itakupa milioni 20 kwa mwaka mmoja

Biashara Kwa kuiandika inapendeza,ingia Sasa ndio utajuwa mbichi na mbovu.
 
Kuna wakati vijana hua hamjielewi kabisa, then mnakuja na nadharia za utajiri na mafanikio ya kwenye simulizi.
Sasa nikionaga upuuzi kama huu hua naishia kukasirika, mwisho natafuna meno kwa hasira tu...☹️
 
Naomba unipe chimbo la kuja kuuzia huko Dar es Salaam.
Nashangaa watu wanahangaika dubai na UK zanzibar pekee inaweza kukufanya ukawa tajiri chukua vitu vya electronic zanzibar njoo navyo dar unapiga hela.
 
Habari za mchana wakuu, natumai hamjambo kabisa na mnaendelea katika harakati za kusaka mkate na kwa wale wanaugua Mungu awaponye kwa uwezo wake tuseme Amin !!

Kwanza kabisa mimi ni mtu ambaye karibia kila baada ya dakika 5 lazima nizame kwenye deep thinking kuhusu kitu chochote ( positive lakini 😀 😀 ) kwahiyo katika hali hiyo najikuta kwa siku nakuwa nachanganua mambo mengi sana hasahasa ya kibiashara na ujasiriamali. Kichwani mwangu nina ideas kibao za kibiashara na ujasiriamali ambazo zipo nilizoziandika na zipo ambazo zipo tu kichwani na siwezi kuzitekeleza zote.

Leo nimeona nilete huu mchongo wa kuuza simu used ( refurbrished smartphones ) kutoka Dubai, UK, USA na Japan. Kama tunavyojua mahitaji ya kuendana na kasi ya globalizationa ni makubwa sana kwa sasa na kila mmoja anataka apate internet akiwa kiganjani kwake, sasa kupata internet kiganjani lazima uwe na simu yenye uwezo na simu nyingi zenye uwezo na imara zina gharama kubwa kwa sisi watu wa kawaida.

Njia pekee ni kutumia zile simu ambazo watu walioendelea wamezitumia na kuziacha kwa kuamua kubadili brand au zilikuwa na tatizo dogo then wataalam wanazitengeneza na kutuletea huku Afrika na sisi tufaidi.

KWA MILIONI 8 YAKO

Hapa naona nilete biashara inayohitaji mtaji wa kueleweka ili uweze kupata faida ya kueleweka pia, kwa mtaji wa milioni nane unaweza kuzungusha kwa mwaka mmoja ukajikuta na faida ya milioni 20 huku mtaji wako ukiwa bado uko vile vile. Ngoja nitoe mchanganuo wa haraka haraka.

KODI
Frame kwa miezi 6 = Tsh 600,000
- Marekebisho ya frame na vifaa vyake = Tsh 400,000
JUMLA = TSH 1,000,000

USAJILI
Usajili wa biashara = 500,000

PESA YA MZIGO WA KWANZA
  • Kiasi cha Tsh milioni 6 kitatumika kuagiza mzigo.
  • Wastani wa bei ya kuagizia piece moja ni Tsh 100,000 ambapo zitapatikana simu 60 na jumla yake ni Tsh 6,000,000.
  • Makadirio ya Gharama za usafirishaji hadi kupokea mzigo = Tsh 500,000
JUMLA = TSH 6,500,000

MALIPO YA MUUZAJI KWA MWEZI
- Muuzaji = Tsh 300,000

MAKADIRIO YA MAUZO KWA MWEZI
  • Simu zitakazouzwa = 60 ambapo piece moja itauzwa kwa Tsh 150,000
  • Jumla yake kwa simu 60 itapatikana Tsh 9,000,000

HELA YA MAUZO KWA MWEZI - HELA YA MZIGO KWA MWEZI
9,000,000 - 6,500,000 = 2,000,000
INAYOBAKIA = TSH 2,500,000

FAIDA YA MAUZO KWA MWEZI - MSHAHARA KWA MFANYAKAZI
2,500,000 - 300,000 = 2,200,000
INAYOBAKIA = TSH 2,200,000

FAIDA YA BIASHARA KWA MWEZI = 2,200,000

Kwenye faida hapo toa TSH 500,000 kwa ajili ya kulipia matangazo ya social media ambayo ni kama $200 ili uendelee kuuza zaidi mwezi unaofuata.

Utabaki na faida ya TSH 1,700,000 KWA MWEZI

Ukiwa na consistency ya namna hiyo kwa mwaka mzima lazima upate faida ya milioni 20 wakati huo mtaji wako uko palepale. Lakini inahitaji nidhamu, kujituma na maombi kwa Mungu.

Kama una hiyo pesa jitose hapo upambane nayo, kama utahitaji ideas zingine za kufanya basi nicheki.
WHATSAPP: 0683535699
👏👏👏
 
Ni Hii Biashara ya simu ninayoijua na kuifanya mimi au unazungumzia simu aina kwa maana nyingine
 
Sorry ww unafanya bznes hii?



KAZI ni kipimo cha UTU
 
Post yako ipo kinadharia sana umeweka assumptions nyingi sana kuliko reality kwa mfano.
What if mteja amenunua simu kisha ikamsumbua akairudisha?
Umepigia hesabu kuwa simu zote utanunua kwa bei ya laki 1 maana yake utanunua simu za kufanana let say oppo A57 20pcs,Oppo A83 20pcs,Infinix hot 5 20pcs na wateja wakija wanaulizia Iphone 12 promax,Samsung note 20 that means hiyo stock yako uliyonunua itakaa mwaka mzima ili uzimalize na wakati huo mfanyakazi anataka mshahara wake,kodi ya fremu inaisha.
Mambo sio rahisi hivyo ingia field ndio utajua hujui
 
Kwanza kabisa mimi ni mtu ambaye karibia kila baada ya dakika 5 lazima nizame kwenye deep thinking kuhusu kitu chochote ( positive lakini 😀 😀 ) kwahiyo katika hali hiyo najikuta kwa siku nakuwa nachanganua mambo mengi sana hasahasa ya kibiashara na ujasiriamali. Kichwani mwangu nina ideas kibao za kibiashara na ujasiriamali ambazo zipo nilizoziandika na zipo ambazo zipo tu kichwani na siwezi kuzitekeleza zote.
Katika huko kufikiria, wewe unafanya biashara gani?

#YNWA
 
Habari za mchana wakuu, natumai hamjambo kabisa na mnaendelea katika harakati za kusaka mkate na kwa wale wanaugua Mungu awaponye kwa uwezo wake tuseme Amin !!

Kwanza kabisa mimi ni mtu ambaye karibia kila baada ya dakika 5 lazima nizame kwenye deep thinking kuhusu kitu chochote ( positive lakini 😀 😀 ) kwahiyo katika hali hiyo najikuta kwa siku nakuwa nachanganua mambo mengi sana hasahasa ya kibiashara na ujasiriamali. Kichwani mwangu nina ideas kibao za kibiashara na ujasiriamali ambazo zipo nilizoziandika na zipo ambazo zipo tu kichwani na siwezi kuzitekeleza zote.

Leo nimeona nilete huu mchongo wa kuuza simu used ( refurbrished smartphones ) kutoka Dubai, UK, USA na Japan. Kama tunavyojua mahitaji ya kuendana na kasi ya globalizationa ni makubwa sana kwa sasa na kila mmoja anataka apate internet akiwa kiganjani kwake, sasa kupata internet kiganjani lazima uwe na simu yenye uwezo na simu nyingi zenye uwezo na imara zina gharama kubwa kwa sisi watu wa kawaida.

Njia pekee ni kutumia zile simu ambazo watu walioendelea wamezitumia na kuziacha kwa kuamua kubadili brand au zilikuwa na tatizo dogo then wataalam wanazitengeneza na kutuletea huku Afrika na sisi tufaidi.

KWA MILIONI 8 YAKO

Hapa naona nilete biashara inayohitaji mtaji wa kueleweka ili uweze kupata faida ya kueleweka pia, kwa mtaji wa milioni nane unaweza kuzungusha kwa mwaka mmoja ukajikuta na faida ya milioni 20 huku mtaji wako ukiwa bado uko vile vile. Ngoja nitoe mchanganuo wa haraka haraka.

KODI
Frame kwa miezi 6 = Tsh 600,000
- Marekebisho ya frame na vifaa vyake = Tsh 400,000
JUMLA = TSH 1,000,000

USAJILI
Usajili wa biashara = 500,000

PESA YA MZIGO WA KWANZA
  • Kiasi cha Tsh milioni 6 kitatumika kuagiza mzigo.
  • Wastani wa bei ya kuagizia piece moja ni Tsh 100,000 ambapo zitapatikana simu 60 na jumla yake ni Tsh 6,000,000.
  • Makadirio ya Gharama za usafirishaji hadi kupokea mzigo = Tsh 500,000
JUMLA = TSH 6,500,000

MALIPO YA MUUZAJI KWA MWEZI
- Muuzaji = Tsh 300,000

MAKADIRIO YA MAUZO KWA MWEZI
  • Simu zitakazouzwa = 60 ambapo piece moja itauzwa kwa Tsh 150,000
  • Jumla yake kwa simu 60 itapatikana Tsh 9,000,000

HELA YA MAUZO KWA MWEZI - HELA YA MZIGO KWA MWEZI
9,000,000 - 6,500,000 = 2,000,000
INAYOBAKIA = TSH 2,500,000

FAIDA YA MAUZO KWA MWEZI - MSHAHARA KWA MFANYAKAZI
2,500,000 - 300,000 = 2,200,000
INAYOBAKIA = TSH 2,200,000

FAIDA YA BIASHARA KWA MWEZI = 2,200,000

Kwenye faida hapo toa TSH 500,000 kwa ajili ya kulipia matangazo ya social media ambayo ni kama $200 ili uendelee kuuza zaidi mwezi unaofuata.

Utabaki na faida ya TSH 1,700,000 KWA MWEZI

Ukiwa na consistency ya namna hiyo kwa mwaka mzima lazima upate faida ya milioni 20 wakati huo mtaji wako uko palepale. Lakini inahitaji nidhamu, kujituma na maombi kwa Mungu.

Kama una hiyo pesa jitose hapo upambane nayo, kama utahitaji ideas zingine za kufanya basi nicheki.
WHATSAPP: 0683535699
Mkuu, kwa mfano UK, soko la kupata hizo bidhaa ni wapi?
 
bia$hara sio rahisi hivyo ndugu, hayo ni makadirio tu ya kwenye makaratasi.
kila mtu afanye kile anachopenda, sio kuiga kitu ambacho huna uelewa nacho wala uzoefu wa kina, utaunguza MTAJI wako bure!
NB.
biashara za NADHARIA zinalipa sana.
 
Nimefanya biashara kwa miaka 20sasa ndio natambua kuwa mafanikio NI ngumu sana kwenye biashara...Tena ukizoea biashara zenye FAIDA kubwa kubwa unafilisika chap tu...Kama una huo mtaji fungua duka la nafaka uswazi au genge mix mpaka pombe za kupima....jitoe hasa...na lugha ya ushawishi uwe nayo...
 
Biashara yoyote kwenye maandishi inalipa Sana, ingia sasa mzigoni kama ujaanza kuongea peke yako.
 
Back
Top Bottom