Mimi kama mjasiriamali, hili ndio nililojifunza kwa Rais Magufuli: Ni mshindi asiyekubali kushindwa

Mimi kama mjasiriamali, hili ndio nililojifunza kwa Rais Magufuli: Ni mshindi asiyekubali kushindwa

DocJayGroup

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2020
Posts
1,654
Reaction score
3,346
Introduction: Mimi sio mwanasiasa, mimi ni mjasiriamali. Shughuli zangu ni Pamoja na media, tourism, lodging, na transport services. Pia nafanya shughuli kati ya nchi ya Tanzania na USA. Ujasiriamali una faida sana, lakini pia una changamoto hasa ukiwa unasimamisha biashara mpya.

Napenda kufuatilia watu waliofanya mambo makubwa maishani, na mmojawapo ni Tiger Woods. Kama haumjui, mfuatilie Google, lakini yeye ni mtu mweusi aliyetesa sana wzungu kwa miaka mingi katika mchezo wa golf. Msemo mmoja anaoutumia sana TW, unasema “Winning takes care of everything.” Manake kwa Kiswahili ni kwamba “ushindi katika mchezo/ maisha ni kila kitu.”

Kwenda USA - Dharau Kisha Heshima: Mimi nakumbuka nikiwa nashughulikia mambo yangu ya kwenda USA. Nilikuwa kijana mdogo sana, nimechaguliwa kwenda Kibaha High School kusomea PCB kutokea Ilboru Secondary. Lakini baada ya kusoma tu muhula mmoja Form V, dili/ fursa ya kwenda USA ikajitokeza. Hio ilikuwa ndoto yangu hasa mtoto kutoka familia maskini sana niliamini kwenda abroad kutanitoa kimaisha. Jambo ambalo lilikuja kuwa kweli. Basi niliacha shule Form V ili kushughulikia fursa hio.

Nilitukanwa sana na watu wengi kwamba mimi ni mjinga na nimeachaje shule nzuri nazurura tu? Tena baba sina, na mama ni maskini ninafikiriaje nitaenda USA. Tiketi nitatoa wapi nk. Matusi mengi sana nilipewa hasa majirani walikuwa wananibeza hata nasikia kabisa. Ila watu hawakujua mipango yangu, ila siku napaa majuu, heshima ikaanza. Nikawa nakuja Tz kila mwaka ku-show off (nilikuwa mtoto na mjinga enzi hizo), na heshima ikazidi kweli. Kila mtu akawa ananiita mzee. Mademu wote wananitaka, na masela wote wanataka kuwa kwa crew yangu.

Maisha Leo - Ushindi Unaendelea: Off course nilikuja kutuliza akili baadaye na kufanya mambo ya maendeleo na ya maana kabisa, na heshima ikaja kuzidi hadi leo. Dhumuni la kusema haya ni kuonyesha kwamba pesa ukiwa nayo, kwa wengi ni kila kitu na wanakuona mshindi sana kimaisha. Unapata heshima kubwa, unapata watu wengi wanataka kukufanyia kazi kwa hio una chagua tu top yao, wafanyakazi wanajitahidi sana kufanya kazi kukupendeza ambayo ina faida kwa biashara. Kwa sababu hizo napambana na pia namwomba Mungu ili aendelee kunipa ushindi, manake sitaki kushindwa kimaisha, kibiashara, au kifedha.

About Magufuli: Magufuli ni mtu anayepitia challenges nyingi kama rais. Mimi sio CCM wala CHADEMA, mimi ni independent voter. Kiukweli lakini, sipendi kuona CCM imekosa challenge miaka yote hii, kwa hivyo nategemea siku moja watatoka madarakani ili at least mwingine ajaribu naye.

Lakini mtu upende usipende, hadi sasa JPM ni mshindi na mwanaume kwelikweli. Na si kwamba hakosi changamoto, lakini utakuta kwa changamoto nyingi anazopitia mwisho wa siku anaibuka mshindi. Ndege zake zimekamatwa sijui mara ngapi, ila kila mara wanaziachilia. Mpaka wa Zambia wengi tulisoma Habari zimeandikwa umefungwa, sasa jana usiku ma-lorries yameachiliwa na kuendelea na safari kiulaini kabisa.

Mwaka jana shilingi iliporomoka sana wengi tukafikiria Tanzania itakuwa Zimbabwe, ila walifanya yao, shilingi ikasimama tena vs other currencies. Sasa hivi wengi wamesema hajafanya lockdown, ila WHO nao wamesema COVID19 inawezekana watu ikabidi wajifunze kuishi nao. Mimi kwa Marekani naishi Los Angeles USA, kuna gazeti linasema “We shut down the economy to make progress against COVID-19 — and then made no progress”. Manake walifanya lockdown ili kupata ushingi dhidi ya COVID19, lakini hali bado ni mbaya. Manake JPM hajafunga kitu, na mwisho wa siku anaweza kuonekana alikuwa sawa kutokana na mambo kama haya.

Conclusion: Bado Tanzania ina changamoto nyingi. Mfano ajira kwa vijana, walimu na wengineo ni tete, mishahara ya wafanyakazi wa UMMA haijaongezewa kwa muda, na vitu vinapanda bei kama sukari nk. Lakini Magufuli kweli sio kwamba hapati changamoto, anazipata sana, lakini kwa asilimia kubwa anapambana na anasimama.

Tumuombee afanye maamuzi busara, na tuombee hayo matatizo mengine yapate ufumbuzi manake ya ajira nk. Kwa hivyo jambo nimejifunza kwa JPM mimi kama mjasiriamali ni kwamba mwisho wa siku, ushindi ni muhimu sana. Mambo yanaweza yumba, lakini ni muhimu kupambana hadi kupata ushindi, sababu hata waliokupinga, huwa wananyamaza tu kimya kabisa kama ukiibuka mshindi.
 
Yaani Magufuli ni bora muwe mnamsifia huko kwenu kwny kahawa kuliko hapa kwa great thinkers
Mimi nimetoa uchambuzi wangu. Magufuli ana weaknesses pia kama mwanadamu. Personally napenda kuwa positive, na kuangalia nitajifunza nini kwa huyu kiongozi. Kumbuka kulalamika ni sawa, lakini usilalamike tu pasipo kufanyia kazi malalamiko hayo.

Watu wengi wanakuja kwa JF wanasema nchi ni mbaya nk. Je hata udiwani umeugombea? Unafanya nini kubadili hali? Nyerere hakukaa tu kulaumu wakoloni, alichukua hatua.

Mimi kwa sasa nachukua hatua kujenga nchi kama mjasiriamali. Mambo ya siasa nawaachia wengine. Lakini tutambue kulalamika na kuwa negative ni victim mentality, na haisaidii kukujenga wewe kiuchumi au kimwili.
 
Magufuli kilichomfikisha hapo ni juhudi kubwa sana ya kujipendekeza kwa wakubwa.

Hata Makonda kapita njia hiyo hiyo.

Ni watendaji wazuri kama watakuwa wanapewa maono na watu wanaojipendekeza kwao (Ukiwa chawa wa mtu, unataka akukubali akikutuma kazi utakayopiga ili kumridhisha ni kubwa).

Inshort, Hawana legacy yoyote nzuri ya kukumbukwa wala hawafai kuigwa.
 
Magufuli kilichomfikisha hapo ni juhudi kubwa sana ya kujipendekeza kwa wakubwa.

Hata Makonda kapita njia hiyo hiyo.

Ni watendaji wazuri kama watakuwa wanapewa maono na watu wanaojipendekeza kwao ( Ukiwa chawa wa mtu, unataka akukubali akikutuma kazi utakayopiga ili kumridhisha ni kubwa ).

Inshort, Hawana legacy yoyote nzuri ya kukumbukwa wala hawafai kuigwa.
Haya maisha kuna kitu kinaitwa strategy. Utafanyaje ili strategies zako zifanikiwe. Jack Ma wa Ali Baba ni smart business man. Najua hakubaliani na serikali ya China kabisa, lakini anajua ili biashara zake ziende vizuri inabidi aendane na bendera ya nchi tu. Makonda kilichomuweka pale ni kujipendekeza indeed.

Lakini ndoto zake zimetimia leo nchi nzima inamfahamu. Anaongea mambo ya ajabu kwelikweli mimi huwa namshangaa sana, lakini ndoto zake yeye zimetimia. Tutafute strategies kufanya ndoto zetu zitimie. Cha muhimu strategies ziwe legal.
 
Humu JF siku hizi kumsifia JPM ni mwiko hata kama akifanya vizuri,utaitwa wa Lumumba,umepewa buku saba.

Ila yote kwa yote nyeupe itaendelea kuwa nyeupo ktk swala la Corona Magufuli alichanga vizuri karata zake.
 
Humu JF siku hizi kumsifia JPM ni mwiko hata kama akifanya vizuri,utaitwa wa Lumumba,umepewa buku saba.

Ila yote kwa yote nyeupe itaendelea kuwa nyeupo ktk swala la Corona Magufuli alichanga vizuri karata zake.
Ila ngoma haijaisha bado. Game inaendelea na movie inaendelea. Mwisho wa siku ndio dunia itaona imsifie au la. Kwa sasa bado anapata mshike mshike nyingi sana, na zinaweza endelea kuwa nyingi na tete zaidi. Ila ndio dalili zinaonesha anaweza ibuka mshindi pia.
 
Mimi nimetoa uchambuzi wangu. Magufuli ana weaknesses pia kama mwanadamu. Personally napenda kuwa positive, na kuangalia nitajifunza nini kwa huyu kiongozi. Kumbuka kulalamika ni sawa, lakini usilalamike tu pasipo kufanyia kazi malalamiko hayo. Watu wengi wanakuja kwa JF wanasema nchi ni mbaya nk. Je hata udiwani umeugombea? Unafanya nini kubadili hali? Nyerere hakukaa tu kulaumu wakoloni, alichukua hatua. Mimi kwa sasa nachukua hatua kujenga nchi kama mjasiriamali. Mambo ya siasa nawaachia wengine. Lakini tutambue kulalamika na kuwa negative ni victim mentality, na haisaidii kukujenga wewe kiuchumi au kimwili.

Hii point sana

Tuache kulalamika na badala yake tuingie kwenye vitendo hii hata kwenye maisha inatumika

Walalamishi wengi ni walioshindwa
 
Hii point sana

Tuache kulalamika na badala yake tuingie kwenye vitendo hii hata kwenye maisha inatumika

Walalamishi wengi ni walioshindwa
Huo ndio ukweli halisi. Rais ndio amechaguliwa kwa kura. Upende usipende, ndio rais wa nchi. Sasa kulalamika kila siku hizo nguvu hata mtu ungeziweka kwa shamba, hata mahindi ya familia yangepatikana.

Huwa personally sina muda wa kulalamika, ni ku-drain mental energy unnecessarily (manake ni kumaliza nguvu ya akili bila sababu) ambayo ningeitumia kufikiria kitu cha maendeleo.

Kwa ufupi, kama kitu kiko nje ya control yako, si vema kukiruhusu kikakupatia stress za maisha. Ni vema kutumia resources chache, na kupambania nazo kwa sasa mambo yaende mbele.

Tujifunze tusiwe watu wa maneno sana, tuwe watu wa vitendo.
 
Haya maisha kuna kitu kinaitwa strategy. Utafanyaje ili strategies zako zifanikiwe. Jack Ma wa Ali Baba ni smart business man. Najua hakubaliani na serikali ya China kabisa, lakini anajua ili biashara zake ziende vizuri inabidi aendane na bendera ya nchi tu. Makonda kilichomuweka pale ni kujipendekeza indeed. Lakini ndoto zake zimetimia leo nchi nzima inamfahamu. Anaongea mambo ya ajabu kwelikweli mimi huwa namshangaa sana, lakini ndoto zake yeye zimetimia. Tutafute strategies kufanya ndoto zetu zitimie. Cha muhimu strategies ziwe legal.
Nasemaga Bashite kweli ni mjinga.
Lakini kuna la kujifunza.
 
Nasemaga Bashite kweli ni mjinga.
Lakini kuna la kujifunza.
Ndio hivyo. Yani haya maisha ukiamua kuwa positive inasaidia sana kujifunza mambo mbalimbali kupitia wengine.

Hata kwa mtu kama yeye aliyepata sijui zero form Iv. Ila sasa ni mkuu wa mkoa hadi nchi kubwa kama Marekani inamtambua tena inamtaja kwa jina kabisa 😂😂😂.

Ndoto zake zimetimia, hata kuangalia tu huyu jamaa na Div zero yake alifanya hivi akatimiza ndoto, basi na mimi najua nitaweza.

Mfano mwingine ni movie ya Godfather ambayo ni negative kwa wengi, lakini ime-inspire wengi. Kwa hio there is always something to learn from others.

Manake siku zote kuna kitu cha kujifunza kutoka kwa wengine kikakusaidia mtu binafsi maishani na katika mapambano yako na malengo yako.
 
Haya maisha kuna kitu kinaitwa strategy. Utafanyaje ili strategies zako zifanikiwe. Jack Ma wa Ali Baba ni smart business man. Najua hakubaliani na serikali ya China kabisa, lakini anajua ili biashara zake ziende vizuri inabidi aendane na bendera ya nchi tu...
Kwa hiyo mkuu, unatufundisha tuwe wanafiki inapobidi na kujipendeza kupitiliza ili kutimiza malengo eti?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom