Uchaguzi 2020 Mimi Leslie Oscar Mbena ninayejulikana pia kama Msemakweli Chakubanga, natangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Morogoro Mjini

Uchaguzi 2020 Mimi Leslie Oscar Mbena ninayejulikana pia kama Msemakweli Chakubanga, natangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Morogoro Mjini

Nakwenda kumhubiria "house Nigger" ajikomboe toka kwa mwarabu,

"House Nigger ukimwambia toka ujikomboe atakwambia hapa Mimi nalishwa na mzungu,napewa mkate na maziwa,nikitoka niende kujikomboa nani atanipa mkate na Maziwa!?"-Malcom x
Kazi kweli kweli

Jitahidi lakini maana penye nia pana njia
 
Nimekudharau hapo uliposema umesoma Masters Mzumbe!

Masters za Mzumbe ni za kununua tu. Ushahidi ninao. Ukibisha naushusha hapa.

Ni bora hata aliyesoma VETA au Amazon Catering College kuliko MBA za Mzumbe.
 
Masters za Mzumbe ni hovyo kabisa.

Una shahada ya OUT, bado unajiona huna ajira na unajitutmua kutafuta wanachama wajiunge CCM? kweli ? hizo nguvu si ungetumia kuanzisha biashara ama kampuni yako na kufanya MARKETING?

Poor education inazalisha watu wa hovyo ambao hawaliwezi soko na wanakimbilia siasa kwakuwa huko "unahitajika kujua kusoma na kuandika tu"
 
Hongera ila njoo Chadema achana na hawa CCM wewe kama msomi unajua CCM walivyotuangusha kwa miaka 60 sasa. Morogoro pekee ilipashwa kulisha Tanzania yote ni mkoa mzuri ajabu ila kuendekeza ccm kumewafanya wana Moro kuwa kati ya watu maskini, mimi sikubaliani na hili
 
Ninaona kama ni kijana mmoja mwenye determination. Kama ungelikuwa kaka yangu ningekushauri this year ukajiandikishe kusoma Ph.D in Business Adminstration au Ph.D in Public Administration ungeenda mbali hata kama sio kwenye siasa. Lakini ni ukweli usiopingika pia kwamba kumtoa Abood inabidi ujipange sana kaka maana yule jamaa waluguru wenzako wanamkubali sana
 
Siyo umeanza kampeni asubuhi mkuu. Jimbo lipo, walugulu wapo, ingawa mazingira yake ni magumu, sijui utawaambia kitu gani kuhusu yale mabasi ya misiba.
Hivi hilo jimbo shida yao ni mabasi ya misiba tu?
 
1. Utatumia njia gani kuifanya hiyo morogoro kuwa kama Kariakoo?
2. Je utaweza kupageuza kuwa K/Koo kwa muda gani na kwa bajeti gani?
3. Morogoro mjini kuna changamoto kubwa ya maji, je umeweka mikakati gani kuondoa hilo tatizo?
4. Huduma za elimu na afya ni changamoto haswa magari ya kubeba wagonjwa na vituo vichache vya afya. Umejipanga vp kutatua hilo?
5. Barabara nyingi ni za vumbi una mkakati gani kuboresha?
6. Je una sera gani kuhusu mazingira yaliyoharibika ya Morogoro kama ukipewa dhamana ya kuwa mbunge?
7. Je mipango yako ya kuibadilisha Morogoro inaendana na sera ya uchaguzi ya Chama ya mwaka 2015-20 au umeitoa tu kichwani?
8. Morogoro ni mkoa ambayo ni Big 6 ya kulisha nchi kwa kupitia kilimo. Kwa nini unataka uibadilishe kuwa mji wa wachuuzi tofauti na mipango ya Serikali
9. Je unafahamu kazi za Mbunge ukiwa kama msomi wa Chuo Kikuu?
10. Je mipango unayopanga ina chanzo cha mapato ya kuiwezesha kuifanya na vyanzo hivyo ni vipi?

NAOMBA UYAJIBU HAYO MASWALI KUMI KWANZA
Maswali mazuri Sana haya
 
Hongera sana naunga mkono hoja
Kuna watu watasema Abood anatoa mabasi ya kuzikia,Abood ametoa ambulance,Abood ana redio na tv lakini hii sio hoja,

Hoja ni kipato cha mtu mmoja mmoja kwa Mwananchi wa Morogoro,ajira hakuna ,hivi ndio vitu vinavyotakiwa vipigiwe kelele ikiwezekana Mh Rais Magufuli achukue Viwanda vyote na vifufuliwe watu wapate ajira. Mh Rais alikuja Morogoro 2016 akasimama Msamvu akasema Viwanda alivyouziwa Abood vianze kufanya kazi mara moja lakini huu Mwaka wa tano Viwanda bado havijaanza kufanya kazi.
 
Kumbe ili kuwa Mbunge unatakiwa kuwa na digrii ya UD. Sikujua hilo. Mbona Kibajaji wa Mtera ana darasa la saba tu. Mbona Msukuma hana darasa la saba na ni Mbunge. Mbona majimbo kibao tu ni wabunge bila kuwa na digrii na wengi tu wana digrii za vyuo vingine. Hivi na Abood ana digrii ua UD?

Mwacheni kumkatisha jamaa. Aende akajaribu bahati yake.
Pesa Huna na digrii za kuunga. Hoja Huna.
 
Wanaposema hivyo hawamaanishi kupingana nawe ila wanakujulisha ukubwa wa ukuta uliopo mbele yako kutokana na Abood ameshika daily life ya wana moro....ambao out of ignorance huwezi kuwaambia vinginevyo.

Binafsi nakuelewa mwana Kizito [emoji3] mwenzangu ila layman wa morogoro hatokuelewa...

Mipango yako ya viwanda iko way juu ya kidogo wanachopata wananchi kutoka kwa Abood.

Tazama pia uwezo wake wa kutoa rushwa..
Mizizi yake ndani ya chama na serikali..
Abood ana tabia ya kuua pia ( sikutishi ila be careful).
Kuna watu watasema Abood anatoa mabasi ya kuzikia,Abood ametoa ambulance,Abood ana redio na tv lakini hii sio hoja,

Hoja ni kipato cha mtu mmoja mmoja kwa Mwananchi wa Morogoro,ajira hakuna ,hivi ndio vitu vinavyotakiwa vipigiwe kelele ikiwezekana Mh Rais Magufuli achukue Viwanda vyote na vifufuliwe watu wapate ajira. Mh Rais alikuja Morogoro 2016 akasimama Msamvu akasema Viwanda alivyouziwa Abood vianze kufanya kazi mara moja lakini huu Mwaka wa tano Viwanda bado havijaanza kufanya kazi.
 
ELIMU YANGU
 Elimu ya chuo kikuu Shahada ya uzamili katika Utawala na Uongozi, Mzumbe
University Dar es Salaam.
Kumbe ndio maana, ni Mzumbe product! Kazi ipo, hivi ile kashfa ya kuuza degree iliishsje hapo??
 
Anagusa daily life ya wananchi...
Anajisgijikiza kwenyw nafsi za maskini na wasio elimika
Morogoro Mjini inahitaji mtu mwenye muono tofauti na muono alionao Abood hivi sasa,Abood juzi kilosa anasimama anasema Mh Rais Wananchi wa Morogoro wamenituma kukushukuru kwa kutuletea ambulance na helikopta kuchukua wagonjwa hospital kubwa kuwapeleka Muhimbili!
 
Sekulu na mwana sps mwenza hii kitu ungeanza 10 years ama 5 years a go...

Kugusa maisha ya watu na
Nakwenda kumhubiria "house Nigger" ajikomboe toka kwa mwarabu,

"House Nigger ukimwambia toka ujikomboe atakwambia hapa Mimi nalishwa na mzungu,napewa mkate na maziwa,nikitoka niende kujikomboa nani atanipa mkate na Maziwa!?"-Malcom x
 
Back
Top Bottom