Mimi ndio mwenye nyota ya kusalitiwa, vipi wenzangu haya mnayapata pia?

Waswahili hawatakiwi kufanyiwa huruma kama wewe unavyojitolea bora uwe mbinafsi ndio heshima itakuja. siku ukikosa pesa ndio utajua waswahili hawana jema

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Pole sana kaka, ikawaje sasa?
 
Hahaha pole sana mkuu ila kama kweli una moyo nipe connection ili tuweze kusonga mbele zaidi! Hapa nilipo sipafurahii sana nahitaji kukua zaidi kimikakati unaonekana upo vizuri kwenye planning!
 
Waswahili hawatakiwi kufanyiwa huruma kama wewe unavyojitolea bora uwe mbinafsi ndio heshima itakuja. siku ukikosa pesa ndio utajua waswahili hawana jema

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Wanasema tenda wema usonge mbele, sio kila mtu ana moyo wa shukrani wapo watakaojiongeza ila wengine watachukulia poa!

Ila it depends na msaada unatolewa kwa mtindo gani maana wengine mtu anakusaidia kwa masimango balaa, katika hali kama hio usitegemee mtu atageuka nyuma baada ya kuvushwa! Ubongo wa binadamu hukumbuka bad experiences zaidi kuliko good ones! Unaweza ukafanya mema 100 ila ukafanya baya moja tu yale 99 yote yakasahaulika.
 
Huna master's degree. Kuna makosa mengi sana ya kiuandishi ambayo mtu aliyekwenda shule hawezi kuyaandika.
Unapenda sana kusifiwa hujawasikia wahenga wakisema "tenda mema nenda zako"
Mfanyabiashara yoyote akishafanya kosa la kutembea nje ya ndoa ajue imekula kwake. Wanawake wa nje Wana nuksi sana.
Ulitembea nje ya ndoa bila kondom, hii inaonyesha wewe sio mtu makini.
 
Wanadamu tunahesabu mabaya sana kuliko mema..Mema 100 yanaweza kufutwa na baya 1. Ndo mana ukaambiwa tenda wema nenda zako..

Japo umewasaidia sana uenda kuna mahali uliwahi/ulikuwa unateleza..Hilo ndo kubwa wanalokumbuka..
 
Kutumia condom kipimo cha umakinifu?

Then umewahi kuexprience matatizo ya ndoa?

Unasema kuhusu makosa ya kiuandishi! Umesahau Profesa kabisa alikosea kusoma badala ya "Rais" yeye aliona "mungu"? Mwengine ni Dokta ila maisha yake yote alikua anajua Sadam Hussein alikua Rais wa kuweit?
 
Kaka. Unajua implications za kutotumia kondom kwa mtu asiye mke wako?
Unaweka rehani Maisha yako, ya mkeo na ya wototo wako kwa starehe ya dakika nne. Mind you four minutes.
Ukifanya huo upuuzi hata kuongea na wewe siwezi maana najua naongea na mpumbavu +++
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…