Mimi ni Simba lakini siwezi kuwa mnafiki na shabiki maandazi kwa kuiponda Yanga hii

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
1. Hii timu ya Yanga haina cha friends of Simba wala nini, ni GSM tu

2.Hii timu ya Yanga kwa namna ilivyojipanga itachukua miaka 10 mfululizo ubingwa wa bongo

3. Hii timu ya Yanga kwa namna navyoiona ingawa siipendi kishenzi haitokuja kufungwa tena na Simba ya jana

4.Hii timu ya Yanga ambayo siipendi na naichukia sana sioni dalili ya kushushwa kileleni na Simba yetu kichefuchefu

5.Hii timu ya Yanga imeshafuzu kwenda robo na ina uwezo wa kucheza fainal bila hofu

Shida yetu sisi ukisifia mpinzani unaambiwa mjinga, fala na matusi kibao lkn pamoja na kuichukia san Yanga ukweli unabaki pale pale kuwa ni timu ya ushindani haswa.
 
Ukweli umuweka mtu huru, wao wache wakutukane lakini ndio ukweli, Yanga wanakula matunda ya uwekezaji wao, Walifanya usajili bora na wamejipanga nje ndani, kiufupi ni timu ambayo iko complete package, wanayo mapungufu machache ambayo wataendelea kuboresha na kuongeza quality ya wachezaji, pale yanga kwa sasa akuna janja janja za wazee wa 10% kununua wachezaji aina ya sawadogo ama baleke, pale kwa sasa hivi Eng,Hersi anaonana na mchezaji yeye mwenyewe na anamaliza biashara yeye mwenyewe akishajiridhisha na uwezo wa mchezaji husika, Kwa maana iyo wanaendelea walipoishia na sio kurudi nyuma
 
Sasa timu yenu inasajili kapama na abdul swamadu sjui samadi unataka imfunge ngaya!???kazi ipo mwaka huu..kwa kifupi simba inaenda robo kwa sababu ya uzoefu tu ila performance ni MBAYAAAAAAA timu ina wahuni wahuni wengi kocha ni mwehu tu bora mgunda ,jana kocha anaona kabisa katikati jamaa wamechukua kiungo chote anakuja kufanya sub ya saidoo dk ya 90!!???

Jana ndo nikajua wazi kwanini nabi anaitwaga professor,ni kwa sababu ya kujua kusoma game na kufanya sub za kiufundi.

Sasa jana timu ina goli moja,afu inawindwa kama swala then kocha anakodoa macho tu na saidoo ambaye game ilishamshinda mapema.

Huyu mbrazil kama hataletewa wachezaji wa maana ilo siku atatia aibu huko super league,unajichanganya unakutana na mamelodi kwenye kiungo una kapama mbona utajuta kwanini uliingiza timu.
 
Acheni kujadili upumbavu na ujuha. Wachezaji ni binadamu na hutumia damu mwilini hivyo kuna kùchoka. Amini nakwambia Mchezaji akimudu kuwa kwenye peak ya nguvu ile ile uwezo ule ule ni misimu minne tu.
Hata hao unaowabeza Simba wamechoka na walichofanya na hatua waliyofikia hao SUKARI FC itawachukua miaka 10 kufanya SIMBA alichofanya. Usibeze mafanikio ya aliyekuzidi Kimataifa kisa tu umeshinda TuMechi tuwili nyumbani na wakati unayembeza yuko Kombe la juu zaidi kwenye Ubora wa juu zaidi. KICHWA CHAKO UBONGO UMELIWA NA FUNGUS WA UTI kapimwe Mirembe
 
Sawa ndo washiriki kombe la malooser!!?
 
Yan timu inatolewa club bingwa na kushushwa Kwa maloser ndio inaonekana inafanya vizur, afu aliyebakia club bingwa Kwa wanaume ndo anaonekana kafanya vibaya. Ugumu wa mashindano ni tofauti, ubora wa wapinzani ni tofauti. Yanga angebakia club bingwa akacheza hiv anavyocheza kidogo maneno yako yangeonekana na mashiko. Lakin Kwa sasa huwez kulinganisha Simba na Yanga mashindano ya kimaitaifa Kwan wapo level tofauti.
 
Hii timu ina uwezo wa kucheza kombe la losers tu ila huku CAFCL huo uwezo haina. Na ndiyo Maana hadi sasa inacheza na ma losers wenzake waliofuruhushwa kutoka mashindano makubwa ya CAFCL
 
Hakina umenena kweli sisi Simba tuna lakujifunza kutoa yanga
Yaani aliyefaulu mtihani wa form two akaenda zake form three akajifunze tena kwa aliyeshindwa huo mtihani akarudishwa tena nyuma darasa ? Tuache utani kwenye mambo ya msingi tafadhali.
 
Siku hizi si shabiki na mfuasi mkubwa wa mpira ila naona kizazi chenu kama kimekuwa kizazi Cha wasiojitambua na mashabiki maandazi. Hii ipo wazi kabisa japo vijana wa Simba watanisha na kukutukana ila ni ukweli sasa Simba imeanguka na hawana uwezo wowotw uwanjani wanalazimisha ushabiki na kujitoa ufahamu. Uwezo wa Yanga sasa ni Mkubwa sawa na Simba ya miaka 4 iliyopita ila jamaa wanakaza fuvu na kujitoa akili huku wakibisha bila logic yoyote Ile.
 
Wewe ni YANGA
 
Simba imecheza Klabu Bingwa Group stage mara ngapi katika miaka mitano iliyopita?
 

Umejiunga JamiiForums February ss unafosi kuleta nyuzi ili upate umaarufu kizazi cha JK bhaana mnafurahisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…