Mimi nimemuelewa Masoud Kipanya. Wewe je?

Hapo inaonyesha kuwa bastola bado haijafytuliwa, isipokuwa mkono upo kwenye "trigger" huku "barrel" ikiwa imeelekezwa mguuni. La sivyo kama ingalitumika tungaliona alama ya moshi kutoka, damu, na pia ishara ya mtu kugugumia kwa maumivu makali.

Uwepo wa bendara ya Tanzania katika kikaragosi hiki huenda ikawa ni ishara ya dola ya nchi yetu. Miguu ni mhimili mkuu wa mnyama yoyote yule aweze kusimama wima ama imara. Kwa hiyo huyo mtu kujielekezea mwenyewe mtutu mguuni ili kujilipua, ni dalili ya kuwa dola kwa kufanya vitu fulani fyongo inajihatarisha yenyewe ama hata kupelekea anguko lake lenyewe.

Wajuvi watadadavua zaidi.
 
Hiyo inaitwa "self shooting" mama kuruhusu vyama vya upizani kuponda CCM na serikali ni 'political suicide' amuji-shooti mwenyewe mguni.
@Covax
Mimi pia nimemuelewa hivyo!
 
Very good Explanations mkuu mbenge !

Umeitendea haki hii topic!
 
Kiasi fulani umeelewa..

Lakini specific huyu ni Waziri wa fedha Mwigulu Nchemba.

Amejikanganya na kujichanganya vilivyo ktk kujibu hoja za wabunge juu overpayment nje ya bajeti ya kiasi cha pesa zaidi 360bn kwa hoja zilizoibuliwa na kamati ya bunge na ripoti ya CAG.

Mwangalie hata kwenye picha. Yeye ndiye huvaa (mavazi) shati/tai yenye rangi hizo = national flag
 
So brighter 🥰
 
Masudi akichora huwa anaweka tarehe specifically hii ni catoon ya 25/09 ambapo kamati ya bunge au bunge lilikuwa halijamuhoji Mh. Mwigulu. Re-think again
 
Hiyo inaitwa "self shooting" mama kuruhusu vyama vya upizani kuponda CCM na serikali ni 'political suicide' amuji-shooti mwenyewe mguni.
Katiba inaruhusu hilo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…