Mimi sio mtoto wa kufikia. (Tafakuri)

Tafuta imani yako. Baki na imani yako. Tafadhali, don't push your FAITH to other people kama Wazungu walivyofanya kwakutusukumia imani zao kwetu ambazo mpk leo zinatutesa...

Km umeona ni mafanikio kutokumwamini "baba" yetu, basi wewe baki na mafanikio yako...usije kwetu kutulazimisha kukubaliana na ww kwamba mafanikio ni kutokumkubali "baba" yetu kama 'baba'.
Nikiamini kama 'baba' yupo nitakufa na nitaoza. Nisipoamini kama 'baba' yupo pia nitakufa na nitaoza. Options zote zinatoa FIXED ANSWER!

DON'T PUSH YOUR FAITH ON ME. YOU'LL BE DISAPPOINTED!
 

Unajua baba ni nani?
 
Inawezekana vp hayo mengine unaona wamebuni ila la kuhusu hiyo Baba ako ndio wanasema sahihi!

Vp ikiwa huyo unaedhani ni Baba ako kumbe sie?
Vp ikiwa huna Baba kabisa au hivyo unavyomdhania Baba hayupo hivyo kabisa? Maana jinsi unavyomfikiria hiyo baba ako alivyo ni kutokana na maelezo yanayoelezwa na hao hao unaowapinga.
 
Sio kila mwanadamu ni mwana wa Mungu, ndio maana kizazi cha kwanza Kaini alimuua nduguyake Abeli. Wana original wa Mungu Baba hawana mashaka nae humuomba na yeye huzisikia Sauti zao. Mleta mada jitathimini upya labda humjui baba yako kwa maana hata Ibilis(joka jeusi la kale) linazaa na wanawake wanadamu na kupata watoto wake ambao ni wanadamu kamili wanaoforce matendo yote maovu yawe huru Kama ushoga, uchangudoa, utoaji mimba, uvivu wa kufikiri, uchawi, kuiba wake za watu n.k. Kwa hiyo nenda kamlilie baba yako
 


Wapi nimempush mtu mkuu?
Huenda Baba yangu si Baba yako
 

Hata kusingekuwa na Biblia au Quran mtu mwenye akili asingekosa kujua kuwa Yupo Baba. Nenda kwenye jamii zisizotambua dini za watu weupe wao pia huamini Baba yupo. Hivyo madai ya kusema wao ndio wameleta hiyo dhana ni butu na hayana mashiko.

Siwezi dhani Baba yangu siye wakati mimi ndiye, uwepo wangu ni uthibitisho tosha kuwa Yupo Baba yangu.
Nawapinga kwa kunifanya mtoto wa kufikia kiasi kuwa sina uhuru wa kumfikia Baba yangu bila wao jambo ambalo hufanya na watoto wa kufikia
 


Baba yangu ndiye aliyemuumba Joka Jeusi la kale na kumpa kusudi la kuwa muasi. Bila Baba yangu hakikufanyika chochote(kiwe kizuri au kibaya) Baba yangu ndiye kila kitu yaani ubaya na wema ndio yeye. Kupewa uhusika wa ubaya au wema ni kusudi tuu lililopo katika mipango yake.

Vitu vyote vinatoka kwake. Hata huyo shetani ni asili ya Baba yangu.
 
Mkuu Mungu nayemjua mimi kamwe kamwe hawezi kumchoma kiumbe chake aliyekiumba mwenyewe kwa udhaifu kama huu..ila watu wa dini wametuamisha ivyo.God is love!


Baba yangu wamemfanya kitu cha hatari kuliko shetani
 

Baba yangu Baada ya kwenda safari za mbali na kutuachia mimi na ndugu zangu nyumba hii, baadhi ya ndugu hasa waliotutangulia walituhadaa na kuturubuni. Kisha wakasema maneno ya uongo yenye kutufarakanisha na kututenga kimakundi makundi
 
JOka jeusi baba yake atakuwa joka jeusi tiiiiiiiiiiii - baba yako yuko kuzimu mfuate huko huko; hapa duniani ni milki ya wanadamu. Tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge; minyororo ya shetani (joka jeusi tiiiii) imeshindwa!

Sawa Mkuu nitaenda kuzimu huko unapopasemea lakini tambua huko ndiko asili ya kila mwenye pumzi. Huko ndiko kwetu hapa ni wasafiri tuu. Ukija huko utaelewa kwa nini dunia ilikuwa tupu tena ukiwa huku giza likitawala uso wa dunia na roho ya Baba yangu ikitawala. Baba yangu ukija huku utamuona na utamsalimia Shikamoo naye atakujibu Marhaba
 
Ukishaelewa habari ya jumla kwamba baba Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezowote na upendo wote) kuwepo ni uzushi tu, hizi stories nyingine za rejareja hazitakusumbua.


Mkuu Amini Usiamini, Baba yangu yupo na hata kabla ya hizo stori za reja reja zenye ubinafsi, ukabila na utaifa. Stori zilizombinafsha Baba yangu na kumuita Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Stori zilizomtaifisha Baba yangu na kumuita Mungu wa Israel jambo ambalo ni mwamba ngoma huvutia kwake. Ndilo linakufanya usiamini uwepo wa Baba yangu.

Ila utakapo kufa ndipo utakapoamka
 
Thibitisha yupo na si stories tu.

Maana inawezekana unakataa uongo wa Mungu wa Ibrahimu, na kukubali uongo mwingine

Unajuaje unachoamini si uongo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…