Miongoni mwa sababu za Elimu ya Tanzania kuonekana duni na ya kukaririshana tu

Miongoni mwa sababu za Elimu ya Tanzania kuonekana duni na ya kukaririshana tu

adriz

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2017
Posts
12,207
Reaction score
26,521
Moja kwa moja..

1. Kusovu past papers imekuwa dili kwa Wanafunzi
Kumekuwa na misemo maswali au mitihani inajirudia na hili ni ukweli ambao hauna shaka. Unakuta Wanafunzi pamoja na walimu wanawekeza muda wao sio kusoma kuelewa bali kusovu mitihani ya Taifa iliyopita kwa lengo kuu ni kuwa yakijirudia mwanafunzi asikose, na ni kweli mtu ambaye anayesovu pastpaper nyingi anauwezekano mkubwa wa kufaulu na vyema mitihani. Kungekuwa na utungaji makini wa mitihani kwa kupima uelewa maswali yasingeisha kiasi cha kujirudia sana na wala Wanafunzi wasingehangaika kukarira mapast papers ili wafaulu.

2. Vitu vya kusoma practicality (kwa njia ya vitendo vinasomeshwa theoretically (kwa njia ya nadharia)
Pamoja na kuwa na maabara karibia shule nyingi lakini bado unakuta vitu vingi vya kujifunza kwa njia ya vitendo bado mnapewa kwa njia ya nadharia na unakuta maabara nyingi shuleni na vyuoni zina upungufu mkubwa wa vitendea kazi au kukuta vitendea kazi duni na havitosholezi kuendana na idadi ya Wanafunzi.

Mfano unakuta mwalimu anasema tu Sodium ikiungana na element Fulani inatengeneza kitu Fulani ambacho kina rangi na harufu Fulani , na Mwanafunzi anakariri tu bila kuona reaction husika.

3. Kuvuja na kuiba mitihani
Kwa miaka mingi kumekuwa na skendo za kuvuja mitihani karibia ngazi zote za Elimu haswa vyuoni , kama elimu yetu ingekuwa inapimwa kwa uelewa na sio kukariri pamoja na kuwa na udhibiti mkali basi swala hilo lingepungua kwa kiasi kikubwa sana.

FCm6P-YWEAAke0i.jpg


4. Kukithiri kwa matukio ya udanganyifu kwa Wanafunzi


Vyuoni watu wanafanyiana mitihani , wananunua tafiti na kughushi data.

IMG_20241112_122023.jpg


MABADILIKO

Pamoja na kuwepo changamoto hizo juhudi mbalimbali za serikali zinaonekana katika kubadilisha mifumo mbalimbali katika utoaji wa Elimu mfano shule za misingi ,sekonadari na Advanced level Kuna mabadiliko katika vitabu vya sasa na baadhi ya mifumo ikilenga katika kupunguza na kuthibiti kadhia n hizi.

Changamoto ipo kwa upande wa vyuoni naona bado kumesahaukika sana na mambo yanaenda kienyeji..

Je , juhudi zipi zifanyike ili Elimu yetu iwe katika ubora mzuri?
 
Moja kwa moja..


1. Kusovu pastpapes imekuwa dili kwa Wanafunzi.
Kumekuwa na misemo maswali au mitihani inajirudia na hili ni ukweli ambao hauna shaka
Unakuta Wanafunzi pamoja na walimu wanawekeza muda wao sio kusoma kuelewa bali kusovu mitihani ya Taifa iliyopita kwa lengo kuu ni kuwa yakijirudia mwanafunzi asikose , na ni kweli mtu ambaye anayesovu pastpaper nyingi anauwezekano mkubwa wa kufaulu na vyema mitihani
#Kungekuwa na utungaji makini wa mitihani kwa kupima uelewa maswali yasingeisha kiasi cha kujirudia sana na wala Wanafunzi wasingehangaika kukarira mapast papers ili wafaulu.

2. Vitu vya kusoma practicality (kwa njia ya vitendo vinasomeshwa theoretically (kwa njia ya nadharia).
Pamoja na kuwa na maabara karibia shule nyingi lakini bado unakuta vitu vingi vya kujifunza kwa njia ya vitendo bado mnapewa kwa njia ya nadharia na unakuta maabara nyingi shuleni na vyuoni zina upungufu mkubwa wa vitendea kazi au kukuta vitendea kazi duni na havitosholezi kuendana na idadi ya Wanafunzi .

Mfano unakuta mwalimu anasema tu Sodium ikiungana na element Fulani inatengeneza kitu Fulani ambacho kina rangi na harufu Fulani , na Mwanafunzi anakariri tu bila kuona reaction husika.

3. Kuvuja na kuiba mitihani.
Kwa miaka mingi kumekuwa na skendo za kuvuja mitihani karibia ngazi zote za Elimu haswa vyuoni , kama elimu yetu ingekuwa inapimwa kwa uelewa na sio kukariri pamoja na kuwa na udhibiti mkali basi swala hilo lingepungua kwa kiasi kikubwa sana .
View attachment 3150158

4.Kukithiri kwa matukio ya udanganyifu kwa Wanafunzi.

Vyuoni watu wanafanyiana mitihani , wananunua tafiti na kughushi data .
View attachment 3150200

MABADILIKO.
Pamoja na kuwepo changamoto hizo juhudi mbalimbali za serikali zinaonekana katika kubadilisha mifumo mbalimbali katika utoaji wa Elimu mfano shule za misingi ,sekonadari na Advanced level Kuna mabadiliko katika vitabu vya sasa na baadhi ya mifumo ikilenga katika kupunguza na kuthibiti kadhia n hizi.

Changamoto ipo kwa upande wa vyuoni naona bado kumesahaukika sana na mambo yanaenda kienyeji..

Je , juhudi zipi zifanyike ili Elimu yetu iwe katika ubora mzuri ?
Matumizi ya kalamu (uandishi) yamepungua na badala yake ku type kwenye simu janja. Pia usomaji wa vitabu umefutika na sasa tuna google tu. Tatu kuwaza mambo ya msingi tumeacha badala yake tumejikita kwa vitu visivyo na mchango moja kwa moja kwenye maendeleo kama kubeti, tamthilia, pombe, michezo, siasa. Mzungu ameweka matakataka kibao kwenye simu ambayo yamemeza akili zote badala ya kufikiri mambo ya maana.
 
Moja kwa moja..

1. Kusovu past papers imekuwa dili kwa Wanafunzi
Kumekuwa na misemo maswali au mitihani inajirudia na hili ni ukweli ambao hauna shaka. Unakuta Wanafunzi pamoja na walimu wanawekeza muda wao sio kusoma kuelewa bali kusovu mitihani ya Taifa iliyopita kwa lengo kuu ni kuwa yakijirudia mwanafunzi asikose, na ni kweli mtu ambaye anayesovu pastpaper nyingi anauwezekano mkubwa wa kufaulu na vyema mitihani. Kungekuwa na utungaji makini wa mitihani kwa kupima uelewa maswali yasingeisha kiasi cha kujirudia sana na wala Wanafunzi wasingehangaika kukarira mapast papers ili wafaulu.

2. Vitu vya kusoma practicality (kwa njia ya vitendo vinasomeshwa theoretically (kwa njia ya nadharia)
Pamoja na kuwa na maabara karibia shule nyingi lakini bado unakuta vitu vingi vya kujifunza kwa njia ya vitendo bado mnapewa kwa njia ya nadharia na unakuta maabara nyingi shuleni na vyuoni zina upungufu mkubwa wa vitendea kazi au kukuta vitendea kazi duni na havitosholezi kuendana na idadi ya Wanafunzi.

Mfano unakuta mwalimu anasema tu Sodium ikiungana na element Fulani inatengeneza kitu Fulani ambacho kina rangi na harufu Fulani , na Mwanafunzi anakariri tu bila kuona reaction husika.

3. Kuvuja na kuiba mitihani
Kwa miaka mingi kumekuwa na skendo za kuvuja mitihani karibia ngazi zote za Elimu haswa vyuoni , kama elimu yetu ingekuwa inapimwa kwa uelewa na sio kukariri pamoja na kuwa na udhibiti mkali basi swala hilo lingepungua kwa kiasi kikubwa sana.

View attachment 3150158

4. Kukithiri kwa matukio ya udanganyifu kwa Wanafunzi


Vyuoni watu wanafanyiana mitihani , wananunua tafiti na kughushi data.

View attachment 3150200

MABADILIKO

Pamoja na kuwepo changamoto hizo juhudi mbalimbali za serikali zinaonekana katika kubadilisha mifumo mbalimbali katika utoaji wa Elimu mfano shule za misingi ,sekonadari na Advanced level Kuna mabadiliko katika vitabu vya sasa na baadhi ya mifumo ikilenga katika kupunguza na kuthibiti kadhia n hizi.

Changamoto ipo kwa upande wa vyuoni naona bado kumesahaukika sana na mambo yanaenda kienyeji..

Je , juhudi zipi zifanyike ili Elimu yetu iwe katika ubora mzuri?
LUGHA... LUGHA....LUGHA. lugha ya kiswahili ifutwe shule za msingi. Kingereza kiwe ndo lugha ya shuleni kwakuwa ndio lugha inayofanya wanafunzi wakariri wanapoanza sekondari
 
Uduni wa kukimanya Kingereza hata baada ya mtu kukisoma kwa miaka 10
Hili nalo tatizo kubwa , wengi wanajua kingereza vya kujibia mitihani tu cha uwongo na kweli.
 
Matumizi ya kalamu (uandishi) yamepungua na badala yake ku type kwenye simu janja. Pia usomaji wa vitabu umefutika na sasa tuna google tu. Tatu kuwaza mambo ya msingi tumeacha badala yake tumejikita kwa vitu visivyo na mchango moja kwa moja kwenye maendeleo kama kubeti, tamthilia, pombe, michezo, siasa. Mzungu ameweka matakataka kibao kwenye simu ambayo yamemeza akili zote badala ya kufikiri mambo ya maana.
Huu ni ukweli wa wazi kabisa.
 
Mzungu ameweka matakataka kibao kwenye simu ambayo yamemeza akili zote badala ya kufikiri mambo ya maana.
Siku mkiacha kumlaumu mzungu kwa matatizo yenu mtapona,,,,, hamna kitu chenu hata kimoja,,, vyote vya mzungu na lawama juu….🥺
 
Kusomeshwa mambo ambayo haufanyii kazi na hayana umuhimu mkubwa katika maisha l
 
Mshana mwambie mtoto asisahau kuwa chawa. Africa hakunaga "dream comes true", ndio maana Elon Musk alihamia ulaya ili ndoto zake ziwe kweli.
Wasomi wa computer science wanamsemo wao mmoja unasema hivi " Usisome/jifunze kuunda software ili uwe tajiri bali jifunze utatue tatizo, ukitatua tatizo pesa zitakuja automatically" mtoto anatakiwa arekebishe vision iwe kutatua matatizo ya waafrika na umaarufu utakuja wenyewe badala ya kuutafuta umaarufu bali maarufu i
umtafute wenyewe.Elon Musk hajawahi jinadi kuwa maarufu bali vitu alivyofanya vimemfanya ajulikane.
Kingine wachawi hawapendi watoto ndoto zao ziwe kweli, kwa hio mentor wa mtoto awe makini sana.
 
Wakati sisi impact wrench tu kuishika ni ukubwani na upo field, hebu ona dogo kwa umri huo anaweza kutoa maelekezo kama hayo wakati wengine internal combustion engine tumejifunza vyuoni.

Daah wametisha sana.👏
Mkuu ni sawa ila bado wanatakiwa waende mbele zaidi kwenye creativity. Shule ya Elon haifundishi tu kufungua na kufunga bali ubunifu.What next baada ya kufungua na kufunga engine ? What about moulding, designing, materials , mechanics nk.
Elon Musk yeye shule yake sifa ya mwalimu ni kuwa mbunifu. Kwa hio shule kama hizo ziende mbele zaidi.
Wamiliki waajiri watu wabunifu sio wanaojua procedure au steps nayo ni kukalilisha kwa vitendo.
Wafundishwe kufinyanga aina mbali mbali za material kuanzia udongo, Plastic. Chuma nk.
Magereji huko tangu zamani watu wakimaliza drs7 walijufunza kufungua na kufunga engine. Je wamebuni nini ?
Bado kuna mis understanding kuhusu practical orientation., what is the connection between thermodynamics and the operation of engine.
Mi ningependa waweke na curriculum ili tujifunze zaidi.
 
Ubaya ni kuwa hata hizi solutions tunaziongelea hapa hazitafanyiwa kazi kamwe,...kazi bure!🥲😥😥
 
Mkuu ni sawa ila bado wanatakiwa waende mbele zaidi kwenye creativity. Shule ya Elon haifundishi tu kufungua na kufunga bali ubunifu.What next baada ya kufungua na kufunga engine ? What about moulding, designing, materials , mechanics nk.
Elon Musk yeye shule yake sifa ya mwalimu ni kuwa mbunifu. Kwa hio shule kama hizo ziende mbele zaidi.
Wamiliki waajiri watu wabunifu sio wanaojua procedure au steps nayo ni kukalilisha kwa vitendo.
Wafundishwe kufinyanga aina mbali mbali za material kuanzia udongo, Plastic. Chuma nk.
Magereji huko tangu zamani watu wakimaliza drs7 walijufunza kufungua na kufunga engine. Je wamebuni nini ?
Bado kuna mis understanding kuhusu practical orientation., what is the connection between thermodynamics and the operation of engine.
Mi ningependa waweke na curriculum ili tujifunze zaidi.
Ni kweli kabisa ila kwa sisi mkuu hiyo level bado sana yani tuunde kitu from scratch siyo leo, angalau basi watu wapewe hizo basic udogoni kuna chance ya wachache wao kujiongeza zaidi kufikia level za kuwaza kudesign wenyewe.
Kinachotukwamisha sisi ni pale kurelate tulivyo visoma darasani na uhalisia kamili kwenye field husika hasa huko kwenye technology.
 
ila kwa sisi mkuu hiyo level bado sana yani tuunde kitu from scratch siyo leo
Lini labda.
Mbona leo ndio rahisi zaidi kuunda vitu. Kuna machine nyingi sana za bei poa na hata za mtumba. Kubumba vitu/molding hata wahunzi wa kawaida hawajafika hata drs7 wanajua. Mashine za ku mold plastic zimejaa. CNC mashine hadi kenya hapo wanaunda locally. Printing machine hata wakenya wanajua teknolojia hio. Ni hivi "maamuzi " ndio mdudu anaesumbua TZ. Tuna amini kila kitu hakiwezekani. Tumeaminishwa kwamba mambo hayawezekani kumbe yanawezekana.
Usipoweza leo hutaweza kesho.
KANTANKA CAR COMP. ya ghana walianza ku mold engine na mashines mbali mbali, Nenda google kaone gari zao za sasa, ni nzuri sana. Waliunda hadi skaveta, winch, misile launcher kienyeji sana. Sasa hivi wanaunda military weapon.
Hivyo watu mmoja mmoja tunatakiwa tuamue kufanya na inawezekana kukua kwa mda mfupi sana.
Etheopia kuna kashirika ka wazawa kameanzisha After school curriculum, hapo wanajifunza programming, robotic nk. Sie tuendelee kusibiri mwokozi.
 
Back
Top Bottom