Miradi ya Meli, SGR na Maji yakwama Mwanza, pesa zinapigwa na Serikali yagoma kupeleka pesa

Miradi ya Meli, SGR na Maji yakwama Mwanza, pesa zinapigwa na Serikali yagoma kupeleka pesa

Nyanswe Nsame

Senior Member
Joined
Jul 9, 2019
Posts
165
Reaction score
181
Miradi ya Meli, SGR na Maji yakwama Mwanza, pesa zinapigwa na Serikali yagoma kupeleka pesa

Miradi mikubwa mitatu ya kimkakati iliyopo jijini Mwanza iliyoanzishwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya hayati John Pombe Magufu, imekwama kutokana na ukosefu wa fedha.

Miradi iliyokwama ni pamoja na mradi wa ujenzi wa meli kubwa ya ghorofa ya MV Victoria, Ujenzi wa kipande cha Reli ya Mwanza - Isaka na mradi wa maji Butimba.

Mradi wa meli hiyo yenye uzito wa tani 3500 itakayotoa huduma katika Ziwa Victoria imejegwa kwenye chelezo chenye uwezo wa kubeba meli yenye uzito wa hadi tani 4,000.

Chelezo hicho pia kitatumika kujengea meli mpya ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 na kukarabati meli ya mafuta ya MT. Nyangumi yenye uwezo wa kubeba lita 410,000 pamoja na kukarabati meli ya msaada ziwani ya MT. Ukerewe.

Mikataba yote ya ujenzi inagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 160 kutoka shilingi bilioni 84 iliyokuwa katika mkataba wa awali kabla ya kusimama mara kwa mara serikali ikidunduliza pesa za mikopo na walipa kodi.

Kuhusu ujenzi wa Reli ya kisasa ya mwendo kasi (SGR) kutoka Mwanza - Isaka wakandarasi wa kichina wanaojenga reli hiyo wameondoka site, leo lakini siku leo Mei 27 Kamati ya siasa ya CCM imefika kukagua mradi huo na kusifia kwamba kasi ya ujenzi ni kubwa jambo ambalo ni la uongo.

CCM imepita katika miradi hiyo tajwa hapo juu na kusifia ujenzi huo, licha ya wakandarasi kuondoka eneo la kazi kutokana na kukosekana kwa fedha licha ya kusingizikio kikubwa kikiwa ni ucheleweshaji wa vifaa kutoka nje.

Kipande hicho cha tano cha Mwanza - Isaka, kwa ujumla kilipaswa kukamilika mwezi huu (bado siku 4) mwezi kuisha tunasubiri kuona je, utakamilika?
Mradi mwingine ni mradi wa maji Butimba, mradi ambao unasifiwa kila kukicha lakini nao haujakamilika.

Mradi huo ulianza kutekelezwa februari 2021 na ulitakiwa kuwa kukamilika mwaka jana Oktoba cha kushangaza mradi umekwama licha ya kufanyiwa majaribio.

Mradi huo umegharimu shilingi bilioni 70, ambapo pia leo Mei 27, kamati ya siasa mkoa, imepita kukagua na kuusifia huku watanzania wakiambulia maji ya chumvi na tope kutoka ziwa Victoria.

Watu wanauliza pesa zinazotolewa na Serikali na 'machawa' ya CCM kusifia pesa hizo zinaenda wapi, miradi inakwama na hakuna hatua zozote zilizopo za kuikwamua.
 
Once a failure , always a failure .

Huwa napita pale Mwanza South kwenye karakana ya ujenzi wa hiyo meli na kujiuliza hivi muda wote huu miaka na miaka ,hii meli si ingekuwa tayari sasa hivi ?

Hata lile daraja la Magufuli la kutoka Mwanza kwenda Sengerema pale Busisi ,nasikia napo kazi imesimama kitambo .

Kuna siku niliwahi pita pale nikaona hamna kazi , wachina washakimbia .
 
Halafu ukiangalia hii ilikuwa miradi ya muhimu sana kwa huu mkoa wetu wa Mwanza ,
Ila vichwa maji wameshindwa kuendesha na kukamilisha miradi kisa wizi na ukanjanja na kukosa plan za miradi husika .....
Nchi ina laana ya asili
 
Once a failure , always a failure .
Huwa napita pale Mwanza South kwenye karakana ya ujenzi wa hiyo meli na kujiuliza hivi muda wote huu miaka na miaka ,hii meli si ingekuwa tayari sasa hivi ?
Hata lile daraja la Magufuli la kutoka Mwanza kwenda Sengerema pale Busisi ,nasikia napo kazi imesimama kitambo .

Kuna siku niliwahi pita pale nikaona hamna kazi , wachina washakimbia .
Sahihi, wachina wakiona viongozi na ziara uchwara wanaanza kuonekana 'site'
 
Watu wanasosomola tu hawajali, hata hela za mikopo na misaada wao wanasosomola tu.

Ndio yule Mwamba aliwaambia hela zipo tukamuona mwehu kumbe anajua mengi.

Wizi, Rushwa, Incompetency kila mahala hivi sasa, warsha, makongamano, ziara za hovyohovyo, mikutano, mafunzo hivi sasa vimetamalaki kila kona.
 
Meli inasubiri vifaa kama viti, fenicha za ndani za finishing, zimeagizwa ughaibuni, viko kwenye meli baharini vinakuja, asilimia 95 imekamilika.

Miradi inaenda vizuri sana.

Halafu umejiandaa kusafirisha bishara gani katika SGR? Au ndio wale hawalimi pamba, tumbqku, hawavui samaki wqpeleke nje yabukanda wa ziwa, wanataka tu kuona treni inatembea halafu haimsaidii kiuchumi
 
Jengo la uwanja wa ndege lilisainiwa mkataba kwa gishindo na magreda sasa hivi kimya Msukuma na Tabasamu tokezeni tuwasikie vinginevyo mtajivunjia heshima uchaguzi unakuja
 
Miradi ya Meli, SGR na Maji yakwama Mwanza, pesa zinapigwa na Serikali yagoma kupeleka pesa

Miradi mikubwa mitatu ya kimkakati iliyopo jijini Mwanza iliyoanzishwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya hayati John Pombe Magufu, imekwama kutokana na ukosefu wa fedha.

Miradi iliyokwama ni pamoja na mradi wa ujenzi wa meli kubwa ya ghorofa ya MV Victoria, Ujenzi wa kipande cha Reli ya Mwanza - Isaka na mradi wa maji Butimba.

Mradi wa meli hiyo yenye uzito wa tani 3500 itakayotoa huduma katika Ziwa Victoria imejegwa kwenye chelezo chenye uwezo wa kubeba meli yenye uzito wa hadi tani 4,000.

Chelezo hicho pia kitatumika kujengea meli mpya ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 na kukarabati meli ya mafuta ya MT. Nyangumi yenye uwezo wa kubeba lita 410,000 pamoja na kukarabati meli ya msaada ziwani ya MT. Ukerewe.

Mikataba yote ya ujenzi inagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 160 kutoka shilingi bilioni 84 iliyokuwa katika mkataba wa awali kabla ya kusimama mara kwa mara serikali ikidunduliza pesa za mikopo na walipa kodi.

Kuhusu ujenzi wa Reli ya kisasa ya mwendo kasi (SGR) kutoka Mwanza - Isaka wakandarasi wa kichina wanaojenga reli hiyo wameondoka site, leo lakini siku leo Mei 27 Kamati ya siasa ya CCM imefika kukagua mradi huo na kusifia kwamba kasi ya ujenzi ni kubwa jambo ambalo ni la uongo.

CCM imepita katika miradi hiyo tajwa hapo juu na kusifia ujenzi huo, licha ya wakandarasi kuondoka eneo la kazi kutokana na kukosekana kwa fedha licha ya kusingizikio kikubwa kikiwa ni ucheleweshaji wa vifaa kutoka nje.

Kipande hicho cha tano cha Mwanza - Isaka, kwa ujumla kilipaswa kukamilika mwezi huu (bado siku 4) mwezi kuisha tunasubiri kuona je, utakamilika?
Mradi mwingine ni mradi wa maji Butimba, mradi ambao unasifiwa kila kukicha lakini nao haujakamilika.

Mradi huo ulianza kutekelezwa februari 2021 na ulitakiwa kuwa kukamilika mwaka jana Oktoba cha kushangaza mradi umekwama licha ya kufanyiwa majaribio.

Mradi huo umegharimu shilingi bilioni 70, ambapo pia leo Mei 27, kamati ya siasa mkoa, imepita kukagua na kuusifia huku watanzania wakiambulia maji ya chumvi na tope kutoka ziwa Victoria.

Watu wanauliza pesa zinazotolewa na Serikali na 'machawa' ya CCM kusifia pesa hizo zinaenda wapi, miradi inakwama na hakuna hatua zozote zilizopo za kuikwamua.
Sukuma gang mnazidi kuwehuka
 
Once a failure , always a failure .

Huwa napita pale Mwanza South kwenye karakana ya ujenzi wa hiyo meli na kujiuliza hivi muda wote huu miaka na miaka ,hii meli si ingekuwa tayari sasa hivi ?

Hata lile daraja la Magufuli la kutoka Mwanza kwenda Sengerema pale Busisi ,nasikia napo kazi imesimama kitambo .

Kuna siku niliwahi pita pale nikaona hamna kazi , wachina washakimbia .
Magufuli alianzisha hiyo miradi kwa maamuzi yake hivyo lazima itakwama tu
 
Halafu ukiangalia hii ilikuwa miradi ya muhimu sana kwa huu mkoa wetu wa Mwanza ,
Ila vichwa maji wameshindwa kuendesha na kukamilisha miradi kisa wizi na ukanjanja na kukosa plan za miradi husika .....
Nchi ina laana ya asili
Magufuli alikuwa anaamua kuanzisha miradi bila kuishirikisha serikali yote( Baraza la mawaziri)
 
Back
Top Bottom