Mirathi kwa watoto nje ya Ndoa

Mirathi kwa watoto nje ya Ndoa

Unaongea kwa mihemko! Moja ya sheria zinazotumika kwenye mahakama zetu ni Sheria za Kiislam, na kwa mujibu wa Sheria za Kiislamu, mtoto wa nje ya ndoa sio mrithi halali wa baba, hali kadhalika baba nae hawezi kumrithi mtoto wake endapo anayetangulia kufa ni mtoto; kwahiyo ni double-edged knife.

Hata hivyo, Waislamu wengi huwa wanajaribu kutumia huo mwanya ili kuwatenga hao watoto wa nje ya ndoa na hapo ndipo mahakama inakuwa na wajibu wa kutaka kufahamu maisha ya marehemu kabla ya umauti wake. Je, marehemu kweli alikuwa anaishi kama mwislamu au hawa warithi halali wanataka tu kutumia huo mwanya hata kama marehemu alikuwa mwislamu jina tu!! Mahakama ikiona marehemu alikuwa mwislamu jina tu, itapiga chini sheria ya kiislamu na kutumia secular law itakayowa-include watoto wa nje ya ndoa.

Lakini kwa upande mwingine kama marehemu alikuwa mwislamu kweli kweli ukiacha na hilo lake la uzinzi basi atakuwa ameacha wosia kwa ajili ya watoto wa nje ya ndoa kwa sababu ndivyo dini yao inawataka. Mimi kuna mshikaji wangu alikuwa kwenye hiyo situation. Alizaliwa nje ya ndoa lakini siku baba yake alipofariki, katika kuchunguza makarabrasha ya marehemu, wakakuta kaacha wosia wa nini mwanae huyo wa nje ya ndoa atapewa. Na marehemu akiacha huo wosia, hakuna wa kupinga provided umekidhi masharti ya kiislamu kwenye kuacha wosia, kwa mfano, mali ya wosia isizidi 1/3 na wosia ni kwa ajili ya wale tu ambao hawana haki ya kurithi kwa mujibu wa dini yao.
Kwenye kesi moja huko Kenya kuanzia kadhi hadi mahakama kuu walikuwa na mtazamo Kama wako lakini maamuzi yao yalikuja kutupiliwa mbali na mahakama ya rufaa.Mke mkatoliki na watoto wake wakatoliki waliokuwa na baba muislamu bila ndoa ,waliamuliwa kumrithi baba yao.Katiba ya Kenya ni Kama yetu inahimiza usawa na kupinga ubaguzi.
 
Unaongea kwa mihemko! Moja ya sheria zinazotumika kwenye mahakama zetu ni Sheria za Kiislam, na kwa mujibu wa Sheria za Kiislamu, mtoto wa nje ya ndoa sio mrithi halali wa baba, hali kadhalika baba nae hawezi kumrithi mtoto wake endapo anayetangulia kufa ni mtoto; kwahiyo ni double-edged knife.

Hata hivyo, Waislamu wengi huwa wanajaribu kutumia huo mwanya ili kuwatenga hao watoto wa nje ya ndoa na hapo ndipo mahakama inakuwa na wajibu wa kutaka kufahamu maisha ya marehemu kabla ya umauti wake. Je, marehemu kweli alikuwa anaishi kama mwislamu au hawa warithi halali wanataka tu kutumia huo mwanya hata kama marehemu alikuwa mwislamu jina tu!! Mahakama ikiona marehemu alikuwa mwislamu jina tu, itapiga chini sheria ya kiislamu na kutumia secular law itakayowa-include watoto wa nje ya ndoa.

Lakini kwa upande mwingine kama marehemu alikuwa mwislamu kweli kweli ukiacha na hilo lake la uzinzi basi atakuwa ameacha wosia kwa ajili ya watoto wa nje ya ndoa kwa sababu ndivyo dini yao inawataka. Mimi kuna mshikaji wangu alikuwa kwenye hiyo situation. Alizaliwa nje ya ndoa lakini siku baba yake alipofariki, katika kuchunguza makarabrasha ya marehemu, wakakuta kaacha wosia wa nini mwanae huyo wa nje ya ndoa atapewa. Na marehemu akiacha huo wosia, hakuna wa kupinga provided umekidhi masharti ya kiislamu kwenye kuacha wosia, kwa mfano, mali ya wosia isizidi 1/3 na wosia ni kwa ajili ya wale tu ambao hawana haki ya kurithi kwa mujibu wa dini yao.
Mzigo huo,soma kama Kuna ugumu wapo wajuba hapa watasaidia
Screenshot_20210103-074103.jpg
 
MAHAKAMA TANZANIA YASEMA HAKUNA MWANAHARAMU, ILA KUNA WAZAZI HARAMU TU.

Kuna hukumu-rejea ilitolewa tarehe 28/5/2020 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupitia Mh. Jaji Mlyambina.

Ni hukumu ya kesi ya mirathi no. 50 ya mwaka 2016 (ina maana kesi ilichukua miaka 4 kwisha).

Ishu ya msingi katika kesi hiyo ni kuna mume wa mtu alifariki bila ya kuacha wosia. Aliacha mke ambaye alikuwa amemuoa kwa ndoa ya kikristo na watoto wa ndoa hiyo, na wengine wa michepuko (nje ya ndoa).

Watoto wa nje ya ndoa wakaweka pingamizi la mirathi maana walikuwa wameenguliwa wasipate kitu na msimamizi wa mirathi hiyo ambaye ni mtoto wa ndoa.

Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa anawasomesha watoto hao (ambapo wengine tayari walikuwa ni watu wazima), vyeti vyao vya kuzaliwa vilikuwa na jina la marehemu kama baba mzazi, na alishawatambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.

Mahakamani mama na dada wa marehemu walitoa ushahidi kwamba wanawatambua hao watoto kama watoto wa marehemu.

Upande wa wa kwenye ndoa walikataa DNA test kufanyika kupima kama hao ni watoto wa marehemu.

Katika hukumu yake, Mahakama ikatumia sheria zifuatazo:

1. Katiba ambayo inasema watu wote ni sawa
2. Sheria ya Mtoto kifungu cha 5 ambacho kinakataza kubagua watoto
3. Sheria ya Mtoto kifungu cha 10 ambacho kinampa mtoto haki ya "ku-enjoy" mali ya mzazi wake.
4. Mikataba ya kimataifa kuhusu haki za mtoto ambayo Tanzania imeridhia.

Katika majumuisho yake, Mahakama ikasema, "Watoto hawana hatia maana hawachagui kuzaliwa au kwamba watazaliwa wapi. Msemo wa "kitanda hakizai haramu" maana yake ni hakuna watoto haramu. Ila kuna wazazi haramu."

Kwa hiyo mama za watoto wa nje ndoa ndo wakatambuliwa kwamba ni wazazi haramu na hawastahili kurithi mali ya marehemu. Ila watoto wa nje ya ndoa wakaingizwa katika orodha ya warithi, ambayo ilijumuisha na mjane wa marehemu na mama wa marehemu.

Pia ikaonekana mtoto wa ndani ya ndoa kusimamia mirathi hiyo haitakuwa vyema, ikateua Kabidhi Wasii Mkuu (yaani serikali) awe msimamizi.

------------------------------
Kwa kuwa hii ni hukumu-rejea kwa sasa hii ndo tafsiri ya sheria nchini Tanzania, mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo na Mahakama ya Rufaa, au mpaka Bunge litakapotunga sheria tofauti na tafsiri hii ya mahakama.

Je wewe unaonaje? Mahakama iko sahihi, au tuendelee kufuata misimamo ya kidini ambayo inawabagua watoto wa nje ya ndoa na watoto wanaozaliwa kabla ya ndoa?

Hukumu hii inapatikana hapa:[emoji116]

https://tanzlii.org/tz/judgment/hig...me-mwimbe-other-prob-admincause-no50-2016.pdf

Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app
Oya hukumu mbona haifunguki hii
 
Mzigo huo,soma kama Kuna ugumu wapo wajuba hapa watasaidiaView attachment 1666201
Huo mfano wako hauingii hapo kwa sababu nimeshasema issue sio marehemu kuwa Mwislamu, na ndo maana nikasema kabla ya kutumika sheria ya Kiislamu, mahakama inatakiwa kujiridhisha ikiwa marehemu alikuwa Mwislamu anayeuishi Uislamu alikuwa ni Mwislamu Jina tu na kwahiyo kuna watu wanataka kutumia kete ya Uislamu ili kuwatupa wengine nje!!

Huo mfano wako haujitoshelezi kwa sababu ulitakiwa kuonesha marehemu alikuwa ni mwislamu aliyekuwa anaishi kwenye misingi ya Uislamu na sio just because he's a muslim! Lakini kwa upande mwingine, pia ulitakiwa kueleza sheria za mirathi nchini Kenya zinasemaje kwa sababu Tanzania kuna sheria za aina tatu zinatumika ambazo ni sheria ya serikali/secular law, sheria ya kimila na sheria ya kiislamu!!
 
Huo mfano wako hauingii hapo kwa sababu nimeshasema issue sio marehemu kuwa Mwislamu, na ndo maana nikasema kabla ya kutumika sheria ya Kiislamu, mahakama inatakiwa kujiridhisha ikiwa marehemu alikuwa Mwislamu anayeuishi Uislamu alikuwa ni Mwislamu Jina tu na kwahiyo kuna watu wanataka kutumia kete ya Uislamu ili kuwatupa wengine nje!!

Huo mfano wako haujitoshelezi kwa sababu ulitakiwa kuonesha marehemu alikuwa ni mwislamu aliyekuwa anaishi kwenye misingi ya Uislamu na sio just because he's a muslim! Lakini kwa upande mwingine, pia ulitakiwa kueleza sheria za mirathi nchini Kenya zinasemaje kwa sababu Tanzania kuna sheria za aina tatu zinatumika ambazo ni sheria ya serikali/secular law, sheria ya kimila na sheria ya kiislamu!!
Google hiyo kesi usome utapata kila kitu.
 
Google hiyo kesi usome utapata kila kitu.
Sioni sababu ya ku-Google kwa sababu ni wewe mwenyewe ndie umeweka hiyo screenshot na kwahiyo ni wewe mwenyewe ndie ulitakiwa kuweka taarifa zilizokamilika! Binafsi sina haja ya kufanya hivyo kwa sababu tayari nafahamu, linapokuja suala la mirathi, moja ya sheria zinazotambulika Tanzania ni Islamic Law!!! Aidha, nimeshasema ni mazingira yapi Islamic Law inaweza kupigwa chini hata kama marehemu alikuwa Mwislamu!
 
Sioni sababu ya ku-Google kwa sababu ni wewe mwenyewe ndie umeweka hiyo screenshot na kwahiyo ni wewe mwenyewe ndie ulitakiwa kuweka taarifa zilizokamilika! Binafsi sina haja ya kufanya hivyo kwa sababu tayari nafahamu, linapokuja suala la mirathi, moja ya sheria zinazotambulika Tanzania ni Islamic Law!!! Aidha, nimeshasema ni mazingira yapi Islamic Law inaweza kupigwa chini hata kama marehemu alikuwa Mwislamu!
Matakwa ya katiba ya nchi inayozuia ubaguzi,sheria ya mtoto inatambua usawa wa watoto wote ,matamko ya haki za binadamu yote yanatambua usawa na haki za binadamu.Katika kesi ya hizo mirathi zenye kuhusu mtoto wa out of wedlock yatapelekwa pale ambapo mtoto anatambulika na mahakama inayomtambua.Nikukumbushe pia kwamba sheria namba moja ya nchi ni katiba ya nchi,sheria nyingine yoyote inayokinzana nabkatiba itawekwa kando popote pale.
 
Sioni sababu ya ku-Google kwa sababu ni wewe mwenyewe ndie umeweka hiyo screenshot na kwahiyo ni wewe mwenyewe ndie ulitakiwa kuweka taarifa zilizokamilika! Binafsi sina haja ya kufanya hivyo kwa sababu tayari nafahamu, linapokuja suala la mirathi, moja ya sheria zinazotambulika Tanzania ni Islamic Law!!! Aidha, nimeshasema ni mazingira yapi Islamic Law inaweza kupigwa chini hata kama marehemu alikuwa Mwislamu!
Matakwa ya katiba ya nchi inayozuia ubaguzi,sheria ya mtoto inatambua usawa wa watoto wote ,matamko ya haki za binadamu yote yanatambua usawa na haki za binadamu.Katika kesi ya hizo mirathi zenye kuhusu mtoto wa out of wedlock yatapelekwa pale ambapo mtoto anatambulika na mahakama inayomtambua.Nikukumbushe pia kwamba sheria namba moja ya nchi ni katiba ya nchi,sheria nyingine yoyote inayokinzana nabkatiba itawekwa kando popote pale.Najua hapa utabisha na mimi sitatumia tena muda wangu kufafanua ila siku ukikutana nayo utanikumbuka.
 
Sioni sababu ya ku-Google kwa sababu ni wewe mwenyewe ndie umeweka hiyo screenshot na kwahiyo ni wewe mwenyewe ndie ulitakiwa kuweka taarifa zilizokamilika! Binafsi sina haja ya kufanya hivyo kwa sababu tayari nafahamu, linapokuja suala la mirathi, moja ya sheria zinazotambulika Tanzania ni Islamic Law!!! Aidha, nimeshasema ni mazingira yapi Islamic Law inaweza kupigwa chini hata kama marehemu alikuwa Mwislamu!
Inapokinzana na katiba ,hata sheria iliyotungwa na bunge ikikinzana na katiba inapigwa chini.
 
Inapokinzana na katiba ,hata sheria iliyotungwa na bunge ikikinzana na katiba inapigwa chini.
Matakwa ya katiba ya nchi inayozuia ubaguzi,sheria ya mtoto inatambua usawa wa watoto wote ,matamko ya haki za binadamu yote yanatambua usawa na haki za binadamu.Katika kesi ya hizo mirathi zenye kuhusu mtoto wa out of wedlock yatapelekwa pale ambapo mtoto anatambulika na mahakama inayomtambua.Nikukumbushe pia kwamba sheria namba moja ya nchi ni katiba ya nchi,sheria nyingine yoyote inayokinzana nabkatiba itawekwa kando popote pale.Najua hapa utabisha na mimi sitatumia tena muda wangu kufafanua ila siku ukikutana nayo utanikumbuka.
Unaweza kutaja sheria inayokiukwa kwenye katiba?! Wakati I doubt kama unaweza kutaja hicho kifungu, katiba hiyo hiyo ibara ya 19 inazungumzia uhuru wa mtu kuamini dini atakayo! Na hapo hapo ndogo ya 1 inasema "Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini.."

Sasa unaweza kuwakataza vipi Waislamu wasitumie sheria ya kiislamu kwenye mirathi kama inavyotakiwa na imani yao wakati pia katiba imewapa uhuru wa uchaguzi wa mambo ya dini?
 
Tuzae wisely.

Mtoto hujacheza naye, hajakufulia nguo, hujamtuma dukani, n.k anakuja kugawana sawa na wale waliokunywesha dawa ukiwa mgonjwa, kukufulia, kukupikia, kuzungumza nawe daily, kukuchekesha, kukutoa stress n.k
Na hisi hoja yako ni swali lingine hili kutokana na matakwa ya kisheria, hapa inaongelewa haki za mtoto awe amekuhudumia au hajakuhudumia, awe ameishi nawe hajaisgi nawe enzi za uhai wa marehemu basi juwa watoto hao wana haki ya msingi ya kurithi mali,


Swali lako labda sasa ukaliweka kwa michepuko yani marehemu aliishi vizuri sana mchepuko kuliko mke wake na kukawa na wosia basi mke halali wa ndoa atatolewa katika wale watakaorithi mali maana wosio utachukua nafasi kubwa kuliko matakwa ya sheria ya kumuangalia mke wa ndoa
 
Bahati nzuri sheria zetu za dini zinasema mtoto aliezaliwa nje ya ndoa halali (mwanaharamu) huyo ni mtoto wa mama yake na harithi chochote kwa baba.
Dini ipi ya kikristo au Kiislamu

Lakini pia kama dini inatambua hivyo ni Kwanini sasa mahakama inaenda kinyume ilihali mahakama inatambua sheria za mila, sheria za kidini nk
 
Wengine mnajibu ilimradi mmejibu lakini hamna knowledge kwenye mambo ya kisheria, tuwaachie wanasheria watolee ufafanuzi zaidi, kuliko kubishana
 
MAHAKAMA TANZANIA YASEMA HAKUNA MWANAHARAMU, ILA KUNA WAZAZI HARAMU TU.

Kuna hukumu-rejea ilitolewa tarehe 28/5/2020 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupitia Mh. Jaji Mlyambina.

Ni hukumu ya kesi ya mirathi no. 50 ya mwaka 2016 (ina maana kesi ilichukua miaka 4 kwisha).

Ishu ya msingi katika kesi hiyo ni kuna mume wa mtu alifariki bila ya kuacha wosia. Aliacha mke ambaye alikuwa amemuoa kwa ndoa ya kikristo na watoto wa ndoa hiyo, na wengine wa michepuko (nje ya ndoa).

Watoto wa nje ya ndoa wakaweka pingamizi la mirathi maana walikuwa wameenguliwa wasipate kitu na msimamizi wa mirathi hiyo ambaye ni mtoto wa ndoa.

Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa anawasomesha watoto hao (ambapo wengine tayari walikuwa ni watu wazima), vyeti vyao vya kuzaliwa vilikuwa na jina la marehemu kama baba mzazi, na alishawatambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.

Mahakamani mama na dada wa marehemu walitoa ushahidi kwamba wanawatambua hao watoto kama watoto wa marehemu.

Upande wa wa kwenye ndoa walikataa DNA test kufanyika kupima kama hao ni watoto wa marehemu.

Katika hukumu yake, Mahakama ikatumia sheria zifuatazo:

1. Katiba ambayo inasema watu wote ni sawa
2. Sheria ya Mtoto kifungu cha 5 ambacho kinakataza kubagua watoto
3. Sheria ya Mtoto kifungu cha 10 ambacho kinampa mtoto haki ya "ku-enjoy" mali ya mzazi wake.
4. Mikataba ya kimataifa kuhusu haki za mtoto ambayo Tanzania imeridhia.

Katika majumuisho yake, Mahakama ikasema, "Watoto hawana hatia maana hawachagui kuzaliwa au kwamba watazaliwa wapi. Msemo wa "kitanda hakizai haramu" maana yake ni hakuna watoto haramu. Ila kuna wazazi haramu."

Kwa hiyo mama za watoto wa nje ndoa ndo wakatambuliwa kwamba ni wazazi haramu na hawastahili kurithi mali ya marehemu. Ila watoto wa nje ya ndoa wakaingizwa katika orodha ya warithi, ambayo ilijumuisha na mjane wa marehemu na mama wa marehemu.

Pia ikaonekana mtoto wa ndani ya ndoa kusimamia mirathi hiyo haitakuwa vyema, ikateua Kabidhi Wasii Mkuu (yaani serikali) awe msimamizi.

------------------------------
Kwa kuwa hii ni hukumu-rejea kwa sasa hii ndo tafsiri ya sheria nchini Tanzania, mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo na Mahakama ya Rufaa, au mpaka Bunge litakapotunga sheria tofauti na tafsiri hii ya mahakama.

Je wewe unaonaje? Mahakama iko sahihi, au tuendelee kufuata misimamo ya kidini ambayo inawabagua watoto wa nje ya ndoa na watoto wanaozaliwa kabla ya ndoa?

Hukumu hii inapatikana hapa:[emoji116]

https://tanzlii.org/tz/judgment/hig...me-mwimbe-other-prob-admincause-no50-2016.pdf

Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app
Nadhani Mahakama zetu zilitakiwa kuzingatia na misingi ya Dini zetu. Angekua mwislam hao watoto wangejijua toka mwanzo kua hawapaswi kurithi chochote. Pengine wanapewa kama zawadi . Na kama wale watoto wa ndani ya ndoa wanahuruma basi wanaweza kuwatengea nusu ya mali ya urithi. Sio kugawa sawa kwa sawa.
 
Unaweza kutaja sheria inayokiukwa kwenye katiba?! Wakati I doubt kama unaweza kutaja hicho kifungu, katiba hiyo hiyo ibara ya 19 inazungumzia uhuru wa mtu kuamini dini atakayo! Na hapo hapo ndogo ya 1 inasema "Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini.."

Sasa unaweza kuwakataza vipi Waislamu wasitumie sheria ya kiislamu kwenye mirathi kama inavyotakiwa na imani yao wakati pia katiba imewapa uhuru wa uchaguzi wa mambo ya dini?
Acha porojo soma ibara ya 12 na 13 ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Bahati nzuri sheria zetu za dini zinasema mtoto aliezaliwa nje ya ndoa halali (mwanaharamu) huyo ni mtoto wa mama yake na harithi chochote kwa baba.
hilo neno mwanaharamu halipo kwenye hadithi wala qurani,
 
Acha porojo soma ibara ya 12 na 13 ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Umeshindwa kujibu kwanini Waislamu uwanyime haki ya ku-practice dini yao wakati katiba imewapa haki hiyo, hali kadhalika sheria ya mirathi inawapa hiyo haki. Na kwavile umeshindwa kujibu, better nikupuuze kwa sababu ibara ulizotaja hazijibu maswali niliyokuuliza!!!
 
Back
Top Bottom