Mirathi ya Dk. Mengi: Mahakama ya Rufaa kutoa hukumu kesho tarehe 11.07.2022

Mirathi ya Dk. Mengi: Mahakama ya Rufaa kutoa hukumu kesho tarehe 11.07.2022

sajo

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
3,474
Reaction score
6,195
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania iliyo na vikao Dar es Salaam, kesho tarehe 11.07.2022 itatoa hukumu juu ya uhalali au ubatili wa wosia ulioachwa na marehemu Dk. Mengi. Hukumu hiyo katika rufaa ya madai namba 332/01/2021 iliyofunguliwa na mjane wa Dk. Mengi, Jackline Mengi itasomwa na majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa ambao ni Fikirini J.A, Mwambegele J.A na Makungu J.A.

Ikumbukwe, Mahakama kuu iliutupilia mbali wosia wa Dk. Mengi ambao ulimpa mali zote Jackline Mengi na watoto wake wawili, huku ukiwapa Tshs. 1,000/= tu watoto wengine wa marehemu. Mahakama kuu ilisema wosia huo ni batili kwa kuwa wakati wa kuandika wosia huo, Dk. Mengi alikuwa na ugonjwa wa akili.
 

Attachments

  • IMG_20220621_123437_1.jpg
    IMG_20220621_123437_1.jpg
    258.5 KB · Views: 21
Life is too short. Mzee wa watu mwendo ameumaliza sasa ndugu na mke wanaparuana hapo wote ni tamaa hakuna upande usio kuwa na tamaa. wameshindwa kuyamaliza kifamilia wameenda mahakaman. Wakishindwana huko watayamaliza kwa waganga wa kienyeji. Wakishindwana huko watayamaliza kwa kukodishiana makundi yasiyo julikana kwa ajili ya kazi maalumu.
 
Life is too short. Mzee wa watu mwendo ameumaliza sasa ndugu na mke wanaparuana hapo wote ni tamaa hakuna upande usio kuwa na tamaa. wameshindwa kuyamaliza kifamilia wameenda mahakaman. Wakishindwana huko watayamaliza kwa waganga wa kienyeji. Wakishindwana huko watayamaliza kwa kukodishiana makundi yasiyo julikana kwa ajili ya kazi maalumu.
Noma sana. Hii ya kukodiana makundi kuna uwezekano mkubwa sana ikafanyika
 
Tatizo tumeacha mila zetu na kukumbatia uzungu.

Mzee mengi angefunga ndoa ya kimila ya kimachame.

Wangemalizana wenyewe kwa mila zao
 
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania iliyo na vikao Dar es Salaam, kesho tarehe 11.07.2022 itatoa hukumu juu ya uhalali au ubatili wa wosia ulioachwa na marehemu Dk. Mengi. Hukumu hiyo katika rufaa ya madai namba 332/01/2021 iliyofunguliwa na mjane wa Dk. Mengi, Jackline Mengi itasomwa na majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa ambao ni Fikirini J.A, Mwambegele J.A na Makungu J.A.

Ikumbukwe, Mahakama kuu iliutupilia mbali wosia wa Dk. Mengi ambao ulimpa mali zote Jackline Mengi na watoto wake wawili, huku ukiwapa Tshs. 1,000/= tu watoto wengine wa marehemu. Mahakama kuu ilisema wosia huo ni batili kwa kuwa wakati wa kuandika wosia huo, Dk. Mengi alikuwa na ugonjwa wa akili.
Hapa kuna funzo kubwa sana kwa wale wote waliojaaliwa kuwa na mali,ni bora kama unaweza ukazigawa kabisa mali zako ungali hai,na kama utakuwa na mchepuko ama watoto wa nje ukagawa mapema ili ukija ukaumaliza mwendo ukaipushe familia yako na fedheha ama chuki kupitia mahakama kwa namna hii
 
Hapa kuna funzo kubwa sana kwa wale wote waliojaaliwa kuwa na mali,ni bora kama unaweza ukazigawa kabisa mali zako ungali hai,na kama utakuwa na mchepuko ama watoto wa nje ukagawa mapema ili ukija ukaumaliza mwendo ukaipushe familia yako na fedheha ama chuki kupitia mahakama kwa namna hii

Mengi hakuwa smart kwenye mambo ya kifamilia.

Ndoa yake ya kwanza ili fail

Watoto wake wakubwa wote hawajawai kuoa wala kuzaa

Mengi nae uzeeni kaoa ndoa ya kizungu

Kuna muhaya mmiliki wa shule za st matthew anaitwa thadeo mtembei alicheza vizuri sana kwenye ndoa yake ya pili. Fuatilia kesi yake kwa ku google tu uone alivyocheza kiakili
 
Mengi hakuwa smart kwenye mambo ya kifamilia.

Ndoa yake ya kwanza ili fail

Watoto wake wakubwa wote hawajawai kuoa wala kuzaa

Mengi nae uzeeni kaoa ndoa ya kizungu

Kuna muhaya mmiliki wa shule za st matthew anaitwa thadeo mtembei alicheza vizuri sana kwenye ndoa yake ya pili. Fuatilia kesi yake kwa ku google tu uone alivyocheza kiakili
ilikuwaje
 
Ngoja tusubiri, japo hizi kesi huwa zaweza chukua muda.
 
Back
Top Bottom