Mirathi

Mirathi

AZIMIO

Senior Member
Joined
Jun 15, 2011
Posts
188
Reaction score
52
Naomba kujua haki ya Mirathi kwa mtoto wa nje wakati mzazi anapofariki hasa baba mwenye taarifa nzuri tafadhari nazisubiri kwa hamu.Asanteni
 
nina ndugu yangu mtoto wa nje ya ndoa babake alipofariki aliitwa mahakamani kwa ajili ya kwenda kutambua msimamizi wa mirathi pamoja na mali za marehemu baada ya hapo mali zilipoanza kugawanywa alipewa sawa sawa na watoto wengine.
 
nina ndugu yangu mtoto wa nje ya ndoa babake alipofariki aliitwa mahakamani kwa ajili ya kwenda kutambua msimamizi wa mirathi pamoja na mali za marehemu baada ya hapo mali zilipoanza kugawanywa alipewa sawa sawa na watoto wengine.

Sio kweli, mtoto wa nje ya ndoa hana haki ya kurithi mali ya baba yake labda awe amempa kabla ya kufa aweke wazi kuwa atapata kadhaaa wa kadhaaa. Na ikumbukwe hampi kama mrithi bali rafiki!!!! kwa vile yeye hayumo katika warithi wa mali ya baba yake. Nilishawahi kujadili suala hili humu na gazeti la Majira jumapili zilizopita huko nyuma imefafanua sana jambo hili. Angalia kesi ya Violet kahangwa v Eudokia kahangwa and administrator general (angalia kama nimesite correct respondents) Court of appelal 1996 something like that ilitoa msimamo wa kisheria ambao unasimama mpaka sasa
 
Sio kweli, mtoto wa nje ya ndoa hana haki ya kurithi mali ya baba yake labda awe amempa kabla ya kufa aweke wazi kuwa atapata kadhaaa wa kadhaaa. Na ikumbukwe hampi kama mrithi bali rafiki!!!! kwa vile yeye hayumo katika warithi wa mali ya baba yake. Nilishawahi kujadili suala hili humu na gazeti la Majira jumapili zilizopita huko nyuma imefafanua sana jambo hili. Angalia kesi ya Violet kahangwa v Eudokia kahangwa and administrator general (angalia kama nimesite correct respondents) Court of appelal 1996 something like that ilitoa msimamo wa kisheria ambao unasimama mpaka sasa


Asante sana kwa ushauri wako,labda niongeze kidogo kwa mfano,Baba aliamua kuishi na mwanamke mwingine ambae hajamuoa na wakafanikiwa kuchuma baadhi ya mali na kuzaa watotot lakini bado alikuwa na mke wa ndoa,hapo hapo alizaa tena nje watoto kwa mama wengine ambao huko hakubahatika kutengeneza mali yoyote,je baba akifa ina maana mali zote hizi zichukuliwe na watoto w marehemu walioko kwenye ndoa tu?na vipi mali zilizozalishwa nje ya mji wa ndoa?na vp wale watoto wengine wa nje ambao wao mama zao hawakubahatika kuchumiwa chochote?
nasubiri ufafanuzi kabla ya kufungua kesi.
 
Naomba kujua haki ya Mirathi kwa mtoto wa nje wakati mzazi anapofariki hasa baba mwenye taarifa nzuri tafadhari nazisubiri kwa hamu.Asanteni
inategemeana na aina ya ugawaji mirathi (mirathi inayogawanywa kiislam, kimila au kiserikali). kwa waislam, huyo hatambuliki, vilevile kimila kama atakuwa hakukombolewa/tambulishwa kabla. vivyohivyo kiserikali kama hakukombolewa/tambulishwa etc. kwa ufafanuzi zaidi kupata vitabu kuhuru hili bofya SHERIA TANZANIA
 
Back
Top Bottom