Mishahara, marupurupu ya viongozi na kupambana na umaskini Tanzania!!

Mishahara, marupurupu ya viongozi na kupambana na umaskini Tanzania!!

Mchukia Fisadi,
Nilipoanzisha mjadala wa hoja ya mishahara na marupurupu makubwa ya Wabunge, nilikuwa nikilenga hoja ya kuwa kunajengeka Gap kubwa sana kati ya watu mbalimbali katika Taifa letu. Kwa bahati mbaya wengi hawakuelewa hoja yangu wakati ule. Kimsingi hoja ile ililenga kuwa na mjadala wa kitaifa, na kufikia mahali tufunge hii gap kwa namna ambayo tutakubaliana, keki ndogo ya Taifa igawanywe kwa uwiano wenye mantiki, lakini pia wale wa chini waweze kunyanyuliwa ili nao waweze kuishi maisha yenye hadhi ya ki-utu na kibinadamu. Huu ndio mjadala unaotakiwa kuendelea. Nimetamka hadharani, hakuna soko la Wabunge au viongozi wa juu wa Serikali. Wote tunapata mahitaji yetu muhimu ya kibinadamu kwenye soko hilo hilo. Hivyo hakuna justification ya kundi fulani kuwa na mshahara au marupurupu makubwa ya kupindukia.Tunaachiana kwa majukumu kweli, lakini sote tunahitajiana. Tunaishi katika mfumo wa "chain". Pingili mmoja likidondoka, hakuna chain. Hivyo hata mhudumu mwenye jukumu la kufagia ofisini ni muhimu, akikosekana si Gavana, wala Kamishna Mkuu wa TRA au Spika anayeweza kufanya kazi kwa ufanisi. Kama tunahitajiana, ni lazima kuwe na uwiano fulani, unaojali nafasi, hadhi, lakini pia unajali ubinadamu wa wale wa chini sana. Vipi tutapata uwiano huu, ndio msingi wa mjadala wa kitaifa!

Mh, wengi tupo nyuma yako, na tungependa uendeleze huu mjadala kwa hali na mali kwa kusudi la kufikia wananchi wote. Lakini tatizo nionalo mimi sio kuwa na gap kubwa, bali ni matumizi mabovu ya pesa za umma. Pesa yetu itumike katika kutuwezesha, na sio kuhakikisha ugawaji wa mishahara kwa umakini zaidi. Kodi ni mali ya umma na sio ya serikali. Na katika Katiba, tuna wajibu wa kupigania na kulinda mali yetu kutoka ubadhilifu.
Ivi kweli mbunge anahitaji mil. 7 kwa mwezi?
Kamishna wa TRA je? - mil 18
Gavana - mil 16?
Mshahara wa mwalimu - je ni kiasi gani?
Tusipoangalia, tutatengeneza matabaka ya watawala na watawaliwa. Hivyo ningependa/tungependa kuona pesa yetu ikitumika kwa umakini zaidi, hasa kwa kutuletea maisha bora, sio kuishia mikononi mwa viongozi wetu.
 
Dr nakupongeza kubwa haswa ni kuthubutu kwani ndio jambo gumu au kizingiti kikubwa kwa viongozi wetu, wamebaki wakiwazia jee nikisema hili ntaonekanaje bila ya kufikiria je ni jambo sahihi? hata km linagusa maslahi wote ni watanzania pia twahitaji mambo muhimu woote, tunafanya shopping sehemu moja, anaelipwa mil20 na elfu 30 tunakutana kariakoo kununua nyanya. sasa kwa viongozi tulio nao hawalitambui hili. Ipo dhana kuwa ukiwa kiongozi wa siasa au kiserekali then kutumia akili kuishi hakutakiwi tena, hela ziwepo za kuchota, yani uwaze tu utumieje! ni vizuri kupata mshahara mkubwa, lakini je unafanya kazi gani kukupatia huo? kodi za wananchi?kufanya maamuzi tu sasa nataka level hii na iwe? ndio sababu kubwa inayorudisha nyuma africa, no sytem in place!hakuna kiongozi anaethubutu kuhoji mapato au maisha ya wenzake ya anasa!UK majuzi wabunge wamedaiwa hadi shs laki moja waliochukua kifisadi! sembuse mtu kuchota mil 300+ kununua benz ya spika? aibu. Ila wazee sisi vijana tumekaa mkao wa kula tumechoka na vitendo hivi, tunataka tupiga kazi tulipwe hela stahili, safari za kikazi stahili, tuwe na uchungu na nchi yetu.sio kujikalia kat V8 ukitembelea kijiji cha wasijua hata maji ya bomba, elimu bora etc, naeza kushusha uchozi nikiendelea kuandika!!
 
Hii nchi uzalendo ni bidhaa adimu kwa viongozi wetu. Natamani atokee dikteta mwenye mtizamo chanya. hatuhitaji wapiga porojo
 
Nakupongeza sana kwa juhudi zako za kupambana na ufisadi uliokubuhu katika jamii yetu.


Tatizo langu katika hoja yako hii ni jinsi gani unaweza kuniridhisha kwamba unachokisema ni kweli kinatoka moyoni, kwa dhati, ama ni mwendelezo ule ule wa siasa zisizokuwa na faida kwa jamii yetu. Kwa maana ya kwamba mnaongea tu ili kuwahadaa wananchi kwamba mnawatetea, na mkishamaliza mnaendeleze ufisadi ule ule.

(a) 1995-2000 ukaweka kibindoni kiinua mgongo (kimyaaaa)

(b) 2000-2005 ukaweka kibindoni kiinua mgongo (kimyaaaa)

(c) 2008, Miaka 13 baadae (tangu 1995) ndiyo unagundua ufisadi wabunge mnaolifanyia Taifa hili? MLAANIWE kwa unafiki huu.. Leo hii keki imekuwa ndogo tena?

Ni hivi: Kuna wabunge ambao wameingia kwa mara ya kwanza 2005 nao wanahitaji kunufaika kama wewe ulivyonufaika huko nyuma kwa kutunyonya sisi wananchi. Kwa hiyo usitegemee kwamba watakuunga mkono hata kidogo.

Sasa kwa mahesabu hayo hapo juu, mimi kama mwananchi wa kawaida nashindwa kukuelewa hadi hapo utakaponieleza jinsi ya kuzirudisha hizo mlizotuibia tangu mmeingia bungeni. Vinginevyo hizi ni siasa tu za nitoke vipi!
Wewe ni wale wale wanaotaka kujua kwa nini haikuwa 1995 siyo?
Sasa sikiliza kila jambo na wakati wake na majira yake.
Ufisadi najua siku zote unakuja na maswali kama yako ambayo hatuko tayari kuyapokea hata kama hapa ni mahali pa mawazo ya kila namna.
Tunahitaji watu wanaothubutu na si wale wanaokatisha watu tamaa.
Nyie ndio mnaokatisha watu tamaa kwa kuwambia kwamba hata kiongozi wa namna gani aje Tanzania ni lazima awe mwizi, hivyo waendelee kuchagua wezi tu waliopo sasa maana wataiba kidogo na wakileta wezi wapya wataiba vingi zaidi.
Ushindwe na ulegee.
 
Back
Top Bottom