Mishahara Sekta Binafsi Corona (covid 19): Mwajiri analazimisha likizo bila malipo

Mishahara Sekta Binafsi Corona (covid 19): Mwajiri analazimisha likizo bila malipo

kindili kindili

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2013
Posts
242
Reaction score
54
Naandika kwa niaba ya rafiki:

Ninafanya kazi kwenye moja ya international schools Dar es Salaam. Agizo la waziri mkuu kwamba shule zifunge lilipotoka tulianza likizo na mwezi wa tatu tulilipwa, tulikua tukifundisha kutokea nyumbani.

Sasa week iliopita mwajiri aliandika ujumbe kwa baadhi ya wafanyakazi, Watanzania tu (Wageni hawajaguswa) kuwa shule inajiendesha kwenye mazingira magumu na hasara, kwamba wanafunzi waliotakiwa kulipa ada hawajalipa na gharama za uendeshaji ni kubwa hivyo anatuomba tuchukue likizo bila malipo hadi hapo serikali itakapotanganza kufunguliwa kwa shule tena.

Na kwamba tutarejea kwenye nafasi zetu na tutaendelea na mikataba yetu. Tukajaribu kuhoji kwamba ni uamuzi wa ghafla sana na sijajiandaa, Mwajiri akasema au kuchukua option ya kukaa pending au kuacha kazi kabisa. Na jana ametuma mkataba wa kukubaliana kuchukua likizo isiyo na malipo(hatujakubaliana ni maamuzi tu tuliletewa tuyajue).

Naomba ushauri wa kisheria, makataba wangu unatakiwa kuisha mwakani mwezi wa tisa.
 
Kiuhalisia biashara nyingi zimekwama kwa kipindi hiki, huyo mwajiri naye anataka ajiendeshe kwa faida, ushauri wangu, mambo ni magumu jaribu ku-feel ugumu anaopitia.

kubali kuchukua likizo hiyo ukizingatia kwamba ndo salama ya kibarua chako. Ukitaka sheria unaweza fanikiwa but ajira utaikosa labda kama umejipanga kivingine!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli mkuu shule za private sasa hivi zinapitia kwenye kipindi kigumu.
Ila kuna walakini kwenye maamuzi yake.
Kwa nini asingefanya maamuzi yanayowagusa wote bila ubaguzi?
 
Ni kweli mkuu shule za private sasa hivi zinapitia kwenye kipindi kigumu.
Ila kuna walakini kwenye maamuzi yake.
Kwa nini asingefanya maamuzi yanayowagusa wote bila ubaguzi?
Hapa ndio napoona walakini! wazungu wamepona wanakula tu dola zao!
 
Mkuu hiyo hali itazikuta taasisi nyingi sana. Amini nakwambia, corona ni game changer. Watu wengi sana wanaweza wakapoteza ajira zao kutokana na covid19, baadhi ya taasisi pia zinaweza kufilisika.

Mkataba wenu wa kazi wala sheria usidhani zitakupa upendeleo sana. Akiamua anakupa notisi kama sheria inavyosema then anakulipa mshahara wa mwezi mmoja kisha anakuachisha kazi moja kwa moja hata corona ikiondoka unabaki bila ajira.

Ushauri wangu ni mkubaliane terms and conditions za likizo bila malipo, vipengele viwe wazi kuwa ni kusimama kazi kwa muda corona ipite kisha mtarejeshwa kazini. Isionekane as if ww ndo unachukua likizo bila malipo bali mwajiri anakupa likizo hiyo kutokana na covid19 na masharti na vigezo baada ya covid19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kindili kindili, Hii ni changamoto ya kisheria. Sheria zetu za kazi hazitoi utaratibu upi ufanyike kwenye hali za majanga ya namna hii although yanatokea mara moja moja lakini ni muhimu sheria walau ingekuwa na vifungu vinavyogusa hali za unforeseeable circumstances kama hizi.

Ni muhimu maslahi ya pande zote mbili yazingatiwe mwajiri na mwajiriwa asibanwe mwajiri halafu baada ya janga nae anakuwa insolvent at the same waajiriwa nao lazima wawe covered kwenye hali kama hizi.

Kibaya zaidi hata mikataba ya ajira yenyewe inaandikwa na lay persons ambao nao huwa hawaweki walau vifungu vinavyogusa situation kama hizi.

Ni wakati wa serikali kutoa muongozo juu ya hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vumilia tu Mwalimu Mkuu, hata sisi wazazi yametukuta hayo hatuwezi lipia Ada kwa wanafunzi kukaa majumbani (mm ninao watatu) kwani hawatumii Chakula, mabweni, wala kufundishwa, huku nyumbani nao watoto wamekuwa mzigo ambao inatubidi tuubebe wenyewe sasa
Serikali nayo imefuta Sherehe za Muungano na Mei Mosi hatujajua itafyeka mishahara ya viongozi au la lkn kuwaongezea sidhani.

Shule Binafsi mna gharama sana kaeni mjue Wazazi ndio tunaziendesha lkn mtoto akitoka faida inabki kwa mmiliki, sasa atoe akiba alizozivuna.
cc amu cc The Boss
 
Kaogopa kuwagusa foreigners maana anajua mziki wake; Wasingekubali kizembe zembe na wangeishia kushtakiwa. The most vulnerable employees ni wabongo, coz hawajui haki zao na hawana mtetezi. Waswahili wanasema "kamba hukatikia pembamba"
Bado nauliza wewe ungekuwa mwajiri ungefanyaje ?

Wafanyakazi ni kama assets, au kwa mfano mwingine ukiwa kwenye bahari jahazi lako likapigwa na dhoruba ikabidi uanze kupunguza mizigo kwenye mashua yako utaanza kupunguza zile mali unazoona you can live without (huenda hao foreigners ni muhimu zaidi kwake) au kama ulivyosema angefukuza hao foreigners huenda lawsuits n.k.

zikapelekea shule ikafirisika..., kwahio ni bora kupumzika mwezi bila mshahara au kuendelea kuwalipa wote kwa mwezi na mwisho wa siku kila mtu kukosa kazi?

Na maji yakizidi unga na hao foreigners wataguswa.., na ikizidi kuwa mbaya wote wataguswa hadi panya waliokuwa wanadokoa chakula jikoni...

(by the way huenda ameanza kujigusa yeye mwenyewe kwa kuweka rehani mali zake zote na kukopa mpaka kwa ndugu jamaa na marafiki)

Narudia tena ungekuwa wewe mwajiri ungefanyaje ?
 
Bado nauliza wewe ungekuwa mwajiri ungefanyaje ?

Wafanyakazi ni kama assets, au kwa mfano mwingine ukiwa kwenye bahari jahazi lako likapigwa na dhoruba ikabidi uanze kupunguza mizigo kwenye mashua yako utaanza kupunguza zile mali unazoona you can live without (huenda hao foreigners ni muhimu zaidi kwake) au kama ulivyosema angefukuza hao foreigners huenda lawsuits n.k...
Ningefanya hivyo hivyo tu mkuu...
 
Rejea tena mkataba wako wa kazi kuusoma vizuri,Waajiri wengi kwenye kipengere cha ikitokea dharura kama kufirisika mwajiri anaweza kusitisha mkataba wako,Muhimu ni kuvuta subira katika kipindi iki ama la ikiwezekana uombe japo nusu mshahara kipindi iki ili uweze kukizi mahitaji yako
 
Usipokuwa makini utaikosa ajira, Hata mm nahisi hata sheria inaweza ikambeba yeye ingawaje sijui sheria kutokana na kutodhalisha na hali halisi inaonekana...

Na ajira hujapoteza ww tu hadi nchi zilizo endelea watu wamepoteza ajira kiufupi ni bora ukubali bila malipo itakusaidia kuonesha nidhamu kazini na kujali.

Kwa sababu tatizo ni la muda, Ukienda kisheria baada ya kumaliza mkataba huna lako tena.
 
Back
Top Bottom