Mishahara ya viongozi wa Tanzania

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Kuna mtu anayejua mshahara wa raisi wa Tanzania ni kiasi gani?

Kuna mtu kaniambia ni $200,000 na kitu kwa mwaka...sikuamini lakini akanihakikishia kuwa taarifa zake ni za uhakika.

Bado ninasita kuamini ingawaje sina taarifa zozote na sijawahi kuona mahala popote pale kuhusu mshahara wa rais.

Na mshahara wa makamu wa raisi..?
Waziri mkuu..?
Spika wa bunge..?
Mkuu wa majeshi ya ulinzi, polisi,magereza..?
Jaji mkuu..?

Kama kuna mtu anayejua...ni wapi tunaweza kupata taarifa hizi?
 
Kwa bandiko lako inaonekana hata wewe hujui kama mimi.

Eniwei, mi nadhani kwa vile mishahara yao inalipwa kutokana na kodi za watu waliowapa dhamana ya kuongoza ni muhimu taarifa za malipo yao kuwekwa hadharani.
 
Hiyo nayo ni siri kubwa Watanzania hatustahili kuijua!!! Tunajua mshahara wa Rais wa Marekani lakini hatujui mshahara wa Rais wetu!

Bill clinton ndiye alikwa Rais wa mwisho wa Marekani kupokea mshahara wa $200,000 kwa mwaka alipomaliza awamu yake ya miaka minane mwaka 2000. Kuanzia 2001 mshahara wa Rais wa marekani uliongezwa na kufikia $400,000 kwa mwaka.

Kama kumbu kumbu zangi ni nzuri walidai wameoungeza maradufu kwa sababu ni miaka mingi imepita tangu nyongeza ya mwisho na pia gharama za maisha zimepanda sana. Lakini tukirudi kwa Rais wetu hatuujui mshahara wake!!! Mwe hii ni sirikali!!!
 
Niliona hapa, kama sikosei kwenye topic moja kuhusu mkapa, mdau moja alisema mshahara wa rais ni $12,000 kwa mwezi.

Kama nimekosea naomba nirekebishwe

Nadhani ilikuwa ni mshahara wa Gavana wa BOT ni $ 12,000 kwa mwezi, Rais mshahara wake ni tax free kwa hiyo anauchota kama ulivyo.
Kuna mchangiaji mmoja alisema mawaziri wetu wanalipwa $ 1,100 kwa mwezi http://jamboforums.com/showpost.php?p=40900&postcount=20
 
Hivi mishahara na marupurupu ya viongozi wa juu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania inajulikana? Viongozi hawa ni Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu na Spika.

Nauliza kwa sababu nadhani mishahara wa marais nyingine inakuwa wazi. Kwetu ikoje?
 
Mwaka jana Mbeki aliongezewa kutoka Rand 1.18 milioni hadi rand 1.27 milioni ingawa Tume ya Moseneke ilipendekezwa alipwe rand 1.89 milioni.

Rais Kibaki alikataa nyongeza ya 186% ambayo inasemekana ingemtoa kutoka US$ 10,000 kwa mwezi hadi US$ 27,600 na marupurupu ya US$ 18,600. Sisi wa kwetu analipwa ngapi? Na nani anayeamua kiasi gani anastahili?
 
Bwana hata mie ningependa kujua ila inaonekana ni siri kubwa sana,nachojua tu ni kwamba wanalipwa toka kwenye mfuko mkuu ambao hauko subject to debate by parliament,sasa sijui ndio kusema Rais huwa anajiuamulia au vipi.manaake huu mfuko mkuu unaoitwa consolidated fund sijui hata ni nani huwa anaushikilia
 
Nakumbuka kuna wakati Mwalimu alijipunguza mshahara kutoka shilingi 4000 hadi 2000 kwa mwezi!

Tukijadili kinadharia hivi kuna ubaya gani hii mishahara (na mingine inayolipwa kwa kodi ya wananchi)ikiwa wazi? Au kuna faida gani ikiwa wazi?
 
Heshima Mbele Wakuu,

Jana katika kikao cha wabunge kilichofanyika pale DIIC na kuhudhuliwa na baadhi ya wabunge,waliomba kuongezewa Posho na Mishahara,.

Spika wa bunge ak.a Mzee wa kukanususha 'Vilowassa' alitoa hoja kwa wabunge kwamba waongezee pesa katika bajeti ya bunge ili wao wapate maslahi zaidi,hoja hiyo iliungwa na Mhe. Masilingi na zitto ,ila zitto alissisitiza hilo liambatane na kurudishwa kwa pesa za EPA ili zifanye kazi ya kuendeleza Maendeleo ya Wananchi.

mhe. Massilingi alienda mbali zaidi na kusema inabidi posho iboreshwe ili wasifanye shughuli zingine na wawatumikie wananchi.

Je wakuu mnaona ni haki na bora kwa hawa waheshimiwa waongezee Mishahara??Je posho yao Haitoshi??

Kuna haja ya kuwa na wagombea ambao wanaojitosheleza kama Ndesamburo ili wawatumikie wananchi..sasa nimeanza kuyakumbuka maneno ya Ndesa Pesa wakati akichangia mjadala wa suala la RDC katika kiako nkilichopita cha bunge.

Wabunge wanastaili kuongezewa mishahara zaidi ya wafanyakazi wa Serikali.

Namnukuu Mzelohalisi hapa:

JF,

Mshahara na marupupupu ni milioni 7 kwa mwezi! Bado vikao vya kamati na maslahi mengine!

Kwa mwaka Mbunge hupata Shilingi milioni 84!

Na akimaliza mda wa miaka mitano hupata milioni 30 kama kifuta jasho!

Mwal Msingi hulipwa 150,000 kwa mwezi na kwa mwaka hupata 1,800,000! Hebu angalia tofauti ni shilingi 82,800,000 kwa mwaka!!!

Uwiii !!!!! Jamani hii tofauti kwa nchi maskini ni kubwa mno!!!

Ndo maana rushwa ktk uchaguzi haitaisha!

Hivi Jaji Mkuu, Spika, Raisi na PM kuna mtu ana data wanalipwa kiasi gani tz?

Source: Slaa akiongea Hedaru Bunge mradi wa ulaji

Pia hapa:


note:Villowassa=vimada=kashfa
 
These wabunge must understand the issue is not about pay rise; it is about increasing productivity. Kuongeza mishahara bila tija, ni chanzo cha mfumuko wa bei katika uchumi.

Every time, these wabunge will demand more and more pay rise as purchasing power falls since there is no TIJA. And if the government is not careful enough, this is a recipe for disaster--inflation spiral. TIJA,TIJA,TIJA ndio mbadala. Kuongeza mishahara isiyoendana na TIJA ni sawa na kubandika plasta juu ya donda ndugu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…