Loading failed
JF-Expert Member
- Sep 14, 2023
- 2,603
- 7,501
Ndugu zangu..
Kumekua na tabia mbaya ya watu kuhudhuria kwenye misiba kwa kubagua kutokana na itikadi zao na hali ya kiuchumi ya marehemu au familia na ukoo wa harehemu husika kama tunavyojionea huko kwenye jamii zetu.
Ndugu utakuta kwenye misiba ya familia zinazojiweza kiuchumi watu wanaacha shughuli zao na wanajitokeza kuhudhuria kuliko misiba ya wasio navyo, asubuhi, mchana ,jioni na hata usiku wengine wanalala hapo kabisa hawaondoki hata iwaje iwe jua iwe mvua wanakomaa hapo. tofauti na misiba ya marehemu anaetoka kwenye familia za wasio jiweza hata mahudhurio yapo ya kusua sua sana na wakati mwingine hakuna kabisa labda tuu ile siku ya kuzika ndo utaona watu kwa kiasi kidogo
Ndugu zangu kwenye misiba ya matajiri hata ukitangazwa tuu leo, utakuta watu wapo kwa wingi wanazunguka zunguka hapo nyumbani na wengine kugeuza ndiyo vijiwe vya kupiga story kwa sababu wanajua asubuhi watapata chai, mchana watapata chakula na usiku pia kitapikwa chakula na chai itasambazwa au uji tofauti na misiba ya wasio navyo wanajua pale utaenda na rambi rambi yako na kurudi mtupu na njaa zako bila kula chochote hata maji ya kunywa hakuna labda tuu ya kudownload yasiyo ya uhakika kupatikana
Kwenye misiba ya matajiri na watu maharufu hata kama hawaendi kanisani, misikitini, na kwenye jumuiya au masinagogi utakuta viongozi wa dini kwa itikadi zao wanafanya unafiki kwenda kumzika kwa ibada na dua huku wakifumbia macho upande wapili kama hawajui kiimani hawakua akishiriki pamoja nao , hata kama alikana imani watajifanya wanafata itikadi za wazazi wao au watoto wao, tofauti na ilivyo kwa masikini (watu wa maisha ya chini) hata usipoenda jumuiya au kushiriki kijamii na wenzako huzikwi unasusiwa hapo haijalishi jina lako litasadifu imani husika ya kufikirika
Kwenye misiba ya matajiri na watu maarufu watajitokeza wakazi kwenda kuuza sura huko, kujitoa kwa bidii na hata wengine kugeuza ndiyo magenge ya kufanya biashara na kutafuta channel tofauti na misiba ya watu wasiojiweza watasingizia kule kumejaa wahuni au bodaboda wanaoleta fujo na vijana wavuta bangi wasio na maadili mema.
Kwenye misiba ya matajiri utakuta ni rahisi sana wazee kuchangamana na vijana ila kwenye misiba ya watu wa chini utakuta mara nyingi wazee wanajitenga na vijana huku wakipiga story kwamba vijana hawana maadili na wengi wakiopo hapo ni vijana wezi lengo ni kuhalalisha uharamu wao wa kuto kuhudhuria kwenye misiba ya wenzao wa hali ya chini.
Nb. Kila mwenye mwili atarudi mavumbini, udongo unakula na ndiyo kitanda cha watu wote haijalishi wewe ni tajiri au masikini, wale funza hawatokukula kwa kuangalia wewe una status gani na wakati mwingine hawajui hilo tubadilike tuache kuchagua misiba ya kwenda .
Kumekua na tabia mbaya ya watu kuhudhuria kwenye misiba kwa kubagua kutokana na itikadi zao na hali ya kiuchumi ya marehemu au familia na ukoo wa harehemu husika kama tunavyojionea huko kwenye jamii zetu.
Ndugu utakuta kwenye misiba ya familia zinazojiweza kiuchumi watu wanaacha shughuli zao na wanajitokeza kuhudhuria kuliko misiba ya wasio navyo, asubuhi, mchana ,jioni na hata usiku wengine wanalala hapo kabisa hawaondoki hata iwaje iwe jua iwe mvua wanakomaa hapo. tofauti na misiba ya marehemu anaetoka kwenye familia za wasio jiweza hata mahudhurio yapo ya kusua sua sana na wakati mwingine hakuna kabisa labda tuu ile siku ya kuzika ndo utaona watu kwa kiasi kidogo
Ndugu zangu kwenye misiba ya matajiri hata ukitangazwa tuu leo, utakuta watu wapo kwa wingi wanazunguka zunguka hapo nyumbani na wengine kugeuza ndiyo vijiwe vya kupiga story kwa sababu wanajua asubuhi watapata chai, mchana watapata chakula na usiku pia kitapikwa chakula na chai itasambazwa au uji tofauti na misiba ya wasio navyo wanajua pale utaenda na rambi rambi yako na kurudi mtupu na njaa zako bila kula chochote hata maji ya kunywa hakuna labda tuu ya kudownload yasiyo ya uhakika kupatikana
Kwenye misiba ya matajiri na watu maharufu hata kama hawaendi kanisani, misikitini, na kwenye jumuiya au masinagogi utakuta viongozi wa dini kwa itikadi zao wanafanya unafiki kwenda kumzika kwa ibada na dua huku wakifumbia macho upande wapili kama hawajui kiimani hawakua akishiriki pamoja nao , hata kama alikana imani watajifanya wanafata itikadi za wazazi wao au watoto wao, tofauti na ilivyo kwa masikini (watu wa maisha ya chini) hata usipoenda jumuiya au kushiriki kijamii na wenzako huzikwi unasusiwa hapo haijalishi jina lako litasadifu imani husika ya kufikirika
Kwenye misiba ya matajiri na watu maarufu watajitokeza wakazi kwenda kuuza sura huko, kujitoa kwa bidii na hata wengine kugeuza ndiyo magenge ya kufanya biashara na kutafuta channel tofauti na misiba ya watu wasiojiweza watasingizia kule kumejaa wahuni au bodaboda wanaoleta fujo na vijana wavuta bangi wasio na maadili mema.
Kwenye misiba ya matajiri utakuta ni rahisi sana wazee kuchangamana na vijana ila kwenye misiba ya watu wa chini utakuta mara nyingi wazee wanajitenga na vijana huku wakipiga story kwamba vijana hawana maadili na wengi wakiopo hapo ni vijana wezi lengo ni kuhalalisha uharamu wao wa kuto kuhudhuria kwenye misiba ya wenzao wa hali ya chini.
Nb. Kila mwenye mwili atarudi mavumbini, udongo unakula na ndiyo kitanda cha watu wote haijalishi wewe ni tajiri au masikini, wale funza hawatokukula kwa kuangalia wewe una status gani na wakati mwingine hawajui hilo tubadilike tuache kuchagua misiba ya kwenda .