Misingi ya kisera na Kisheria inayosimamia tasnia ya Habari Kimataifa

Misingi ya kisera na Kisheria inayosimamia tasnia ya Habari Kimataifa

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
SRBFG.png

Mikataba mbalimbali ya kimataifa, bara na kanda inalinda tasnia ya habari, waandishi wa habari, na watetezi wa haki za binadamu kutoingiliwa na Serikali. Mikataba hiyo inaweka wajibu kwa Serikali kufuata, kuendeleza, na kulinda uhuru wa kutoa maoni na kujieleza.

MIKATABA YA KIMATAIFA TAMKO LA KIMATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU (UDHR)

Kifungu cha 19 cha Tamko hilo kinasema: Kila mtu ana haki ya uhuru wa kutoa maoni na kujieleza; haki hii pia inahusisha uhuru wa mtu kuamini katika maoni yake bila kuingiliwa kwa namna yoyote, na uhuru wa kutafuta na kusambaza taarifa, maoni na mawazo yake kwa njia yoyote bila ya kujali mipaka.

Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR) Tanzania imeridhia mkataba huu mwaka 1976, na hivyo inawajibika kisheria kufuata masharti ya mkataba huo.

Kifungu cha 19 cha mkataba huo kinazungumzia uhuru na haki ya kujieleza:

1. Kila mtu atakuwa na haki ya kuwa na maoni na kuyaamini maoni hayo bila ya kuingiliwa kwa namna yoyote.
2. Kila mtu atakuwa na haki na uhuru wa kujieleza; haki hii itahusisha mtu kutafuta, kupokea, na kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali, kwa njia ya mdomo au maandishi, na bila ya kujali mipaka, kwa kuandika au kuchapisha, kwa njia ya sanaa, au njia nyingine yoyote atakayoichagua.
3. Utekelezaji wa haki zilizoainishwa kwenye aya ya 2 ya kifungu hiki kinaendana wajibu na majukumu maalum.

Kwa hivyo, haki hiyo inaweza kuhusisha vikwazo mbalimbali, hata ambavyo ni vya muhimu na vitawekwa kwa mujibu wa sheria:
(a) Vinavyolenga kulinda haki na heshima ya watu wengine;
(b) Vinavyolenga kulinda usalama wa nchi au utulivu wa kijamii, au afya na maadili ya jamii.

Haki ya uhuru wa kujieleza inahusisha kuchambua, kujadili kwa uwazi, kutoa kauli zinayoweza kukwaza, kushitua, kusumbua na kukosoa wengine.
 
Upvote 1
Wiki iliyopita kulikuwa ni kikao mjini kwetu, na ajenda kubwa ilikuwa ni kuhusu hate speech, pamoja na misinformation. Kwa Marekani hate speech in federal crime, ila freedom of speech ni consititutional right ambayo haimpangii mtu kitu cha kusema.Mjadala ukagota mwamba.

Swala la misinformation lilichukua hatua ya ajabu kwa sababu hiyo ya freedom speech na hasa kwa sisi ambao pia tunalindwa ni kitu kingine kinaitwa academic freedom. Swali likawa, je mwalimu akiingia darasani na kuwafundisha wanafunzi wake mambo ya uongo tu asichukuliwe hatua kwa sababu ya academic freedom na freedom of speech ilihali inaonekana wazi kuwa anasambaza misinformation? Mwishoni tukashindwa kulimaliza jambo hilo likabaki kama lilivyo!
 

Mikataba mbalimbali ya kimataifa, bara na kanda inalinda tasnia ya habari, waandishi wa habari, na watetezi wa haki za binadamu kutoingiliwa na Serikali. Mikataba hiyo inaweka wajibu kwa Serikali kufuata, kuendeleza, na kulinda uhuru wa kutoa maoni na kujieleza.

MIKATABA YA KIMATAIFA TAMKO LA KIMATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU (UDHR)

Kifungu cha 19 cha Tamko hilo kinasema: Kila mtu ana haki ya uhuru wa kutoa maoni na kujieleza; haki hii pia inahusisha uhuru wa mtu kuamini katika maoni yake bila kuingiliwa kwa namna yoyote, na uhuru wa kutafuta na kusambaza taarifa, maoni na mawazo yake kwa njia yoyote bila ya kujali mipaka.

Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR) Tanzania imeridhia mkataba huu mwaka 1976, na hivyo inawajibika kisheria kufuata masharti ya mkataba huo.

Kifungu cha 19 cha mkataba huo kinazungumzia uhuru na haki ya kujieleza:

1. Kila mtu atakuwa na haki ya kuwa na maoni na kuyaamini maoni hayo bila ya kuingiliwa kwa namna yoyote.
2. Kila mtu atakuwa na haki na uhuru wa kujieleza; haki hii itahusisha mtu kutafuta, kupokea, na kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali, kwa njia ya mdomo au maandishi, na bila ya kujali mipaka, kwa kuandika au kuchapisha, kwa njia ya sanaa, au njia nyingine yoyote atakayoichagua.
3. Utekelezaji wa haki zilizoainishwa kwenye aya ya 2 ya kifungu hiki kinaendana wajibu na majukumu maalum.

Kwa hivyo, haki hiyo inaweza kuhusisha vikwazo mbalimbali, hata ambavyo ni vya muhimu na vitawekwa kwa mujibu wa sheria:
(a) Vinavyolenga kulinda haki na heshima ya watu wengine;
(b) Vinavyolenga kulinda usalama wa nchi au utulivu wa kijamii, au afya na maadili ya jamii.

Haki ya uhuru wa kujieleza inahusisha kuchambua, kujadili kwa uwazi, kutoa kauli zinayoweza kukwaza, kushitua, kusumbua na kukosoa wengine.
hivi katiba yetu inatambua hivyo vifungu hii ya jamuhuri wa muungano wa tanzania kwenye haki za binadamu
 
"Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR) Tanzania imeridhia mkataba huu mwaka 1976, na hivyo inawajibika kisheria kufuata masharti ya mkataba huo."

Hapa ulivyoandika, Tanzania inakuwa 'inawajibika' kufuata masharti ya mkataba huo kwa sheria zake au sheria za nje?
Kwa sababu pale mikataba ya jumuiya za kimataifa inaposainiwa, nchi inahitajika 'kimkataba' kutekeleza kwa ku-implement sheria (kama inahitajika); ila hakuna 'sheria' za nchi au jumuiya fulani 'zinazoiwajibisha' nchi nyingine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom