Missing my mom!!

Missing my mom!!

Zuriel_cfc

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2017
Posts
4,092
Reaction score
9,063
As i lie down my bed the whole day today, all I am thinking of, is u mama!

Nakukumbuka sana mama yangu. Wakati mwingine siku inakuwa mbaya, nzito, chungu sana, natamani hata ungekuwepo nikakuegemea begani nikueleze yaliyonisibu, nikusimulie vile siku yangu imekuwa mbaya, naamini ungetabasam na kunitia moyo, ungefuta machoz yangu na kunichekesha kidogo. Ungenipiga piga mgongoni na kuniambia "pambana mwanangu, maisha ni mapambano, na mapambano si lelemama" na mwisho ungeniombea kwa upendo na kumaanisha...

Ooh! My Dear mama, kutokuwepo kwako ktk maisha yangu ni mtihani mkubwa, ni pengo ambalo kamwe haliwezi kuzibika. Najitahidi sana kujipa moyo na kuendelea bila wewe lkn inafikia wakati siku haiendi kabisa mama, hitaji langu juu yako halina kikomo... Sijui kwa nini uliniacha mapema kiasi hiki mama yangu kipenzi....

Uendelee kupumzika kwa amani mama yangu. Atleast njoo unikumbatie ndotoni..

Bintiyako C
 
Nikikumbuka ya nyuma nataman hata angekuwa tu kalal kitandan nimwambie yanayonisibu naumia sana ila ktk kuteseka nikaja kupata namna ya kutuliza mind yangu

Usiku saa 7 nawasha mishumaa nafanya maombi kisha huwa nasemezana na mama nafumba macho nahis kama tumeketi naye nasema kila lililonisibu ..kama n kulia nalia majonzi yanitoke ,, kwa kweli nikimaliza huwa napata nafuu kubwa sana
 
Move on girl, move on. Mungu alivyoumba dunia, aliput into consideration hayo yote. Kuna kufa.

Kaza buti songa mbele.

Inawezekana mama yako huko alipo, anakutizama na anakuombea ufanye mema ili siku moja mkutane mbinguni.

Unapozidi kusikitika, nothing will change.

Samahani kwa kuwa harsh.
 
Back
Top Bottom