Unapatia hawa watu stress mengi juu hata ujenzi haujaanza na Labda haunzishwi hivi karibuni. Hapa ni "tuta" miaka nenda miaka rudi in fact they have no definite timelines and their projects are mostly done in the present through paperwork and word of mouth but in fact they are futuristic without a realistically reliable timeline.
Hayo maswali yake ni mazuri, shida ni sehemu alipoyaulizia. Angeyauliza bungeni angepata majibu hapo hapo na ingetusaidia hata sisi watanzania kujua baadhi ya vitu. Hilo hakulifanya anaongelea kwenye press conference. Kwa utaratibu huo kweli atapata majibu?Hajakosoa, ameuliza maswali muhimu sana yanayohitaji majibu, amekosa majibu hata kutoka kwa wizara zote husika, sasa nyie hapa JF huwa mpo kwenye automated gear, mnajibu hoja zake kwa kumshambulia bila hata kusoma anachokiuliza.
Kitendo cha serikali kupitia jeshi la polisi kuwakamata hawa wapinzani kinapingwa na watanzania walio wengi, sisi sote tunalipigia kelele hilo, lakini hata Zitto anapokuwa anafanya mambo ya hovyo ni lazima pia tumkemee, kwa mfano anadail tutmie chuma cha Lidanga badala ya kuagiza chuma toka nje, Liganga ni sehemu chuma kimegunduliwa, ni mlima mkubwa porini, serikali ipo mbioni kuchimba hicho chuma, ipo katika hatua za mwanzo hata pesa ya kuchimbia haijapata, ni sawa na mafuta ya Kenya ambayo bado yapo ardhini, hivi utamuelewa mtu anayesema kwanini Kenya inanunua mafuta toka nje wakati kuna mafuta huko Turkana?.Hivi mbona huwa mnajitoa ufahamu kwa ushabiki na kugoma kumuelewa Zitto, jamaa hata huwa mnamkamata kamata badala ya kujibu hoja zake.
Hapa hajapinga mradi, ameuliza maswali ya msingi sana, na badala ya nyie kumjibu mnapambana kumjadili......
Zitto kuna vi hela vya usnitch alikuwa anapewa enzi za mkwere jk sasa hili jamaa undumilakuwili wa zito haliutambui wala hapewi commision ya kuvuruga upinzani na enzi zile zito alikuwa anatoka na hoja nzito za kitaifa kwa sababu alikuwa anapitishiwa na kwa mlango wa nyuma na CCM B" na TISS walimeguka wengine walikuwa wanafanya kazi kwa interest ya taifa na wengine walikuwa wanafanya kazi kwa interest za viongozi wa siasa.SO MSITEGEMEE ZITO KUWA HOJA ZENYE MSHIKO TENA ANAWEWESEKA PENGO LA LISSU ANAHISI ANAWEZA FIT YEYE
Hayo maswali yake ni mazuri, shida ni sehemu alipoyaulizia. Angeyauliza bungeni angepata majibu hapo hapo na ingetusaidia hata sisi watanzania kujua baadhi ya vitu. Hilo hakulifanya anaongelea kwenye press conference. Kwa utaratibu huo kweli atapata majibu?
Wewe ukijiuliza hayo maswali kwa nini hakuyauliza bungeni utapata jibu gani?
Hoja muflisi. Ni defence mechanism ya mkosa hojaZitto anaanza kuchanganyikiwa, ninadhani hii ni kwasababu ya Magufuli amebana kila kona upinzani unakosa agenda za kuzungumza, hicho chuma cha Liganga anachosema, hata kuanza kuzalishwa hakuna hiyo dalili, huenda reli hii ikakamilika mapema kabla hicho chuma hakijaanza kuzalshwa, ni sawa na kusema kwanini Tanzania inaagiza gesi ya kupikia toka nje wakati kuna gesi nyingi Mtwara, au kwanini Kenya na Uganda wanaagiza diesel na petrol toka nje wakati wamegundua mafuta, Zitto amekuwa mropokaji sana siku hizi
Hapo kwenye aya ya pili ndo kuna mzizi wote wa hoja hii. Huu ndio huwa ni udhaifu wa baadhi ya wanasiasa hasa hawa wa kiafrika. Hivi inakuwaje mtu ambaye ni mbunge kushindwa kutumia haki yake ya kibunge kuuuliza hoja nzito kama ile bungeni?Maswali yake yote ni muhimu sana, japo kama ilivyo kawaida yenu mpo kikazi huku kwenye mitandao, mumeishia kumshambulia yeye binafsi. Amesema mkataba hauna kifungu cha kufungamanisha na sekta nyingine, imekaa ovyo sana hiyo na haijalishi mtapindisha pindisha kivipi kwenye mitandao, uhalisia bado utaonekana wenye kunuka.
Hata hivyo nakubaliana na wewe kwenye issue moja tu, kwamba alifaa kuuliza hayo maswali bungeni kama hoja ili ashinikize majibu. Sasa yeye kama ilivyo wapinzani hata wa huku kwetu ametafuta kiki kwenye press conference, ndivyo tulivyowazoea wapinzani hapa, hawaulizi bungeni, wataita wana habari na kutoa matamko ambayo hayajathibitishwa na huwa inabidi wajibiwe kwenye magazeti, wakati maswali yakiulizwa bungeni, serikali inalazimka kutoa majibu yaliyotuia.
Haya jibu wewe mwenye akili, kwanini Kenya inaagiza diesel na petrol toka nje wakati hapo Turkanamkuna mafuta ya kutosha kwa Kenya nzima?Hoja muflisi. Ni defence mechanism ya mkosa hoja
Nivizuri kumjibuHivi wewe una akili kweli?, mbona unashindwa kujenga hoja vizuri ili tuweze kuumiza vichwa wakati wa kukujibu badala yake unajenga hoja kama mwendawazimu, ujenzi wa reli toka Nairobi- Naivasha nao haupo?, kwani reli unaanza na tuta ndiyo unaweka vyuma au unaanza na vyuma ndiyo unajenga tuta?, timeframe ipi unayotafuta wakati umeambiwa kila kipande cha reli kilichokabidhiwa contractor analazimika kumaliza ndani ya miezi 36 tangu siku mkataba umesainiwa?, tangu kipande cha Dar - Morogoro kuanza kujengwa huu ni mwezi wa tano, ulitegemea tayari wawe wamelaza mataruma ya reli ndani ya kipindi hicho ambacho sehemu kubwa ni mobilization and ground cleaning?, acha kuwa kama umekunywa chang'aa, jadili kwa kutumi akili ili ujibiwe kwa kutumia akili
Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.Kwa mujibu wa uchambuzi wa Zitto Kabwe, misumari, malighafi na hata makampuni ya kuchimba kokoto zitatoka kwa Waturuki. Watanzania wataishia kupokea tu basi, sasa nashangaa wale hukesha huku JF wakibeza reli ya Kenya wakati sisi tulihakikisha makampuni ya ndani yalinufaika pakubwa Local Procurement in SGR Stands at 10 Billion - Ministry of Industry, Trade and Cooperatives
-------------------------------------------------------------------
Mwenyekiti wa Chama cha Siasa cha ACT Wazalendo, Mh.Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma, amesema kuwa, ni jambo la kushangaza kuona Serikali ikasaini mkataba wa shilingi Trilioni 7 kujenga Reli bila kuweka vifungu vya kufungamanisha na sekta nyingine nchini.
Mh.Zitto akahoji kuwa, inawezekanaje kweli hata misumari ( screws) nchi hii haiwezi kutengeneza mpaka iagizwe kutoka Uturuki na kwamba yani hata kampuni ya kuchimba kokoto itoke Uturuki,”? alihoji.
Akiendelea kuonyesha kushangazwa na jambo hilo alisema kuwa, mpaka serikali itegemee malighafi hizo kutoka nje hivi viwanda vya chuma nchini CTI, TPSF vinafanya kazi gani sasa.
“Nielezeni hili, hamuwezi kuzalisha kitu chochote kulisha ujenzi wa Reli ya Kati ya SGR katika BOQ ya Mradi wa SGR, hamna muwezalo? Serikali iliwapa BOQ mkashindwa?” alihiji Mbunge huyo.
Akasema, ata ukiwauliza watu wa Wizara hawana majibu, wanasema Mkataba ali alifanya makubaliano Rais mwenyewe.
Aidha aliendelea kusema kuwa, inawezekanaje kuamini hili na kwamba hawezi kumuuliza rais na kwamba wao kazi yao ni kukosoa tu.
“Amekasirika, Siwezi kumwuliza mtu aliyekasirika, tena Amiri Jeshi Mkuu” alisema.
Wakati wa Mdororo wa Uchumi Asia mwaka 1997-1998 Waziri Mkuu wa Malaysia Tun Mahathir Mohammed alifanya miradi mikubwa sana ikiwemo kujenga Mji Mpya, barabara kubwa na Jengo la Petronas.
Ili kuingiza fedha kwenye uchumi na kuchochea shughuli nyengine za uchumi na kukuza mahitaji ( aggregate demand). Malaysia ikawa nchi ya kwanza kuibuka kutoka Asian Financial Crisis.
Aliongeza kuwa, sisi watawala wetu wamekwenda madarasa tofauti na kusoma vitabu tofauti vya Uchumi? Unajenga Reli kwa pesa yako ( inavyodaiwa), kwa hiyo unakusanya kodi kutoka kwa watu wako, unanunua US$, unamlipa Mkandarasi. Mkandarasi ananunua kila kitu kutoka nchini kwao Uturuki, mataruma ya Reli, Chuma, Screws na Misumari na hata mchimba kokoto Mturuki.
“Kwenye uchumi hii inaitwa leakages. Uchumi wetu unahitaji more inflows, unajengaje Reli kwa kutumia Chuma kutoka nje wakati una hazina ya chuma Ludewa?, unamwaga TZS 7 Trilioni bila kuhakikisha offsetting? Natamani kuiona hiyo BOQ ya Reli ya Kati”, akasema Mh.Zitto.
Alisema, suala hili linanisumbua sana, ni vigunu kuamini kuwa watawala waliokwenda shule na wenye uzoefu Serikalini hawakuona faida kubwa ya offsets na kwamba Baraza la Mawaziri limejaa wasomi wenye PHDs, inashangaza kuona kama ni kweli wameshindwa kuona hili.
Alimaliza kusema kuwa, fedha zetu wenyewe tunatengeneza ajira nje ya nchi huku sisi tukiwa vibarua tu na wagonga reli, Trilioni 7 zingechochea sana uchumi.akasema, kutokana na hili ni vyema watetezi wa Serikali, mnaojua kuitafsiri Serikali, lifanyieni kazi suala hili. nisaidieni.
INASHANGAZA SERIKALI KUWEKA MKATABA WA TRILIONI 7 KUJENGA RELI BILA KUSHIRIKISHA SEKTA NYINGINE- MH.ZITTO
Kwa mujibu wa uchambuzi wa Zitto Kabwe, misumari, malighafi na hata makampuni ya kuchimba kokoto zitatoka kwa Waturuki. Watanzania wataishia kupokea tu basi, sasa nashangaa wale hukesha huku JF wakibeza reli ya Kenya wakati sisi tulihakikisha makampuni ya ndani yalinufaika pakubwa Local Procurement in SGR Stands at 10 Billion - Ministry of Industry, Trade and Cooperatives
-------------------------------------------------------------------
Mwenyekiti wa Chama cha Siasa cha ACT Wazalendo, Mh.Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma, amesema kuwa, ni jambo la kushangaza kuona Serikali ikasaini mkataba wa shilingi Trilioni 7 kujenga Reli bila kuweka vifungu vya kufungamanisha na sekta nyingine nchini.
Mh.Zitto akahoji kuwa, inawezekanaje kweli hata misumari ( screws) nchi hii haiwezi kutengeneza mpaka iagizwe kutoka Uturuki na kwamba yani hata kampuni ya kuchimba kokoto itoke Uturuki,”? alihoji.
Akiendelea kuonyesha kushangazwa na jambo hilo alisema kuwa, mpaka serikali itegemee malighafi hizo kutoka nje hivi viwanda vya chuma nchini CTI, TPSF vinafanya kazi gani sasa.
“Nielezeni hili, hamuwezi kuzalisha kitu chochote kulisha ujenzi wa Reli ya Kati ya SGR katika BOQ ya Mradi wa SGR, hamna muwezalo? Serikali iliwapa BOQ mkashindwa?” alihiji Mbunge huyo.
Akasema, ata ukiwauliza watu wa Wizara hawana majibu, wanasema Mkataba ali alifanya makubaliano Rais mwenyewe.
Aidha aliendelea kusema kuwa, inawezekanaje kuamini hili na kwamba hawezi kumuuliza rais na kwamba wao kazi yao ni kukosoa tu.
“Amekasirika, Siwezi kumwuliza mtu aliyekasirika, tena Amiri Jeshi Mkuu” alisema.
Wakati wa Mdororo wa Uchumi Asia mwaka 1997-1998 Waziri Mkuu wa Malaysia Tun Mahathir Mohammed alifanya miradi mikubwa sana ikiwemo kujenga Mji Mpya, barabara kubwa na Jengo la Petronas.
Ili kuingiza fedha kwenye uchumi na kuchochea shughuli nyengine za uchumi na kukuza mahitaji ( aggregate demand). Malaysia ikawa nchi ya kwanza kuibuka kutoka Asian Financial Crisis.
Aliongeza kuwa, sisi watawala wetu wamekwenda madarasa tofauti na kusoma vitabu tofauti vya Uchumi? Unajenga Reli kwa pesa yako ( inavyodaiwa), kwa hiyo unakusanya kodi kutoka kwa watu wako, unanunua US$, unamlipa Mkandarasi. Mkandarasi ananunua kila kitu kutoka nchini kwao Uturuki, mataruma ya Reli, Chuma, Screws na Misumari na hata mchimba kokoto Mturuki.
“Kwenye uchumi hii inaitwa leakages. Uchumi wetu unahitaji more inflows, unajengaje Reli kwa kutumia Chuma kutoka nje wakati una hazina ya chuma Ludewa?, unamwaga TZS 7 Trilioni bila kuhakikisha offsetting? Natamani kuiona hiyo BOQ ya Reli ya Kati”, akasema Mh.Zitto.
Alisema, suala hili linanisumbua sana, ni vigunu kuamini kuwa watawala waliokwenda shule na wenye uzoefu Serikalini hawakuona faida kubwa ya offsets na kwamba Baraza la Mawaziri limejaa wasomi wenye PHDs, inashangaza kuona kama ni kweli wameshindwa kuona hili.
Alimaliza kusema kuwa, fedha zetu wenyewe tunatengeneza ajira nje ya nchi huku sisi tukiwa vibarua tu na wagonga reli, Trilioni 7 zingechochea sana uchumi.akasema, kutokana na hili ni vyema watetezi wa Serikali, mnaojua kuitafsiri Serikali, lifanyieni kazi suala hili. nisaidieni.
INASHANGAZA SERIKALI KUWEKA MKATABA WA TRILIONI 7 KUJENGA RELI BILA KUSHIRIKISHA SEKTA NYINGINE- MH.ZITTO
CAG anatoa taarifa ya miradi tarajiwa?Mimi nilifikiri hii ni taarifa kutoka kwa CAG kumbe inatoka kwa mtu ambaye mimi na yeye hatuna tofauti?
MK254 kwa hili ntakushusha credit bure.
Zitto sio Mkenya wewe, acha kutuaibisha...hoja za Zitto zimekuwa NZITO hadi tunatafuta Wakenya wa kuwalaumu.Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.
Ukifuatilia post zangu utaona nikimtaka mtoa mada asubiri taarifa ya CAG. Nikimanisha mradi ukiisha ndo analysis kamili itatolewa.CAG anatoa taarifa ya miradi tarajiwa?
Dah! Tusizime moto, bali tusubiri nyumba iteketee halafu mkemia apime majivu atujibu?Ukifuatilia post zangu utaona nikimtaka mtoa mada asubiri taarifa ya CAG. Nikimanisha mradi ukiisha ndo analysis kamili itatolewa.
Moto unazimwa kwenye press?Dah! Tusizime moto, bali tusubiri nyumba iteketee halafu mkemia apime majivu atujibu?
Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.
Usisahau vile vile alishasema kwa statistics alizonazo tuna baa la njaa. Watu wangekufa sana kwa njaa, akatoa data feki mapato ya serikali nkzitto alishawahi kusema tumenunua terrible teen akashindwa kuthibitisha