Misumari, malighafi kwa ajili ya SGR ya Tanzania vitatoka Uturuki, halafu wanaicheka Kenya

Misumari, malighafi kwa ajili ya SGR ya Tanzania vitatoka Uturuki, halafu wanaicheka Kenya

Unapatia hawa watu stress mengi juu hata ujenzi haujaanza na Labda haunzishwi hivi karibuni. Hapa ni "tuta" miaka nenda miaka rudi in fact they have no definite timelines and their projects are mostly done in the present through paperwork and word of mouth but in fact they are futuristic without a realistically reliable timeline.


Hii sasa inaitwa kuosha kinywa, huna hata aibu unaongea kumbe hujui chochote.












Eti hamna hata time frame ?

Designer : COWI & SENER
Consultant: KORAIL JV KOREA RAIL ROAD
Completion date:07/11/2019





21034538_2018377108381600_8303382125390571322_n.jpg



21032744_2018377115048266_2958574962329880277_n.jpg
 
Hajakosoa, ameuliza maswali muhimu sana yanayohitaji majibu, amekosa majibu hata kutoka kwa wizara zote husika, sasa nyie hapa JF huwa mpo kwenye automated gear, mnajibu hoja zake kwa kumshambulia bila hata kusoma anachokiuliza.
Hayo maswali yake ni mazuri, shida ni sehemu alipoyaulizia. Angeyauliza bungeni angepata majibu hapo hapo na ingetusaidia hata sisi watanzania kujua baadhi ya vitu. Hilo hakulifanya anaongelea kwenye press conference. Kwa utaratibu huo kweli atapata majibu?

Wewe ukijiuliza hayo maswali kwa nini hakuyauliza bungeni utapata jibu gani?
 
Hivi mbona huwa mnajitoa ufahamu kwa ushabiki na kugoma kumuelewa Zitto, jamaa hata huwa mnamkamata kamata badala ya kujibu hoja zake.
Hapa hajapinga mradi, ameuliza maswali ya msingi sana, na badala ya nyie kumjibu mnapambana kumjadili......
Kitendo cha serikali kupitia jeshi la polisi kuwakamata hawa wapinzani kinapingwa na watanzania walio wengi, sisi sote tunalipigia kelele hilo, lakini hata Zitto anapokuwa anafanya mambo ya hovyo ni lazima pia tumkemee, kwa mfano anadail tutmie chuma cha Lidanga badala ya kuagiza chuma toka nje, Liganga ni sehemu chuma kimegunduliwa, ni mlima mkubwa porini, serikali ipo mbioni kuchimba hicho chuma, ipo katika hatua za mwanzo hata pesa ya kuchimbia haijapata, ni sawa na mafuta ya Kenya ambayo bado yapo ardhini, hivi utamuelewa mtu anayesema kwanini Kenya inanunua mafuta toka nje wakati kuna mafuta huko Turkana?.

Reli hii ndiyo inayotegemewa kusafirisha hicho chuma cha Liganga ili kifike Bagamoyo kisafirishwe nje, kwa maana hiyo inabidi SGR imalizike haraka ili chuma kiweze kusafirishwa, sasa itakuwaje chuma kilichopo ardhini kitegemewe kujengea reli ambayo ujenzi wake unaendelea?, Zitto alikuwa enzi za Kikwete anajenga hoja nzuri kwa sababu serikali ya Kikwete ilikuwa na mapungufu mengi sana, ilikuwa rahisi kuichallenge, sasa hivu karibu madhahifu mengi sana, hasa upande wa uchumi na maendeleo Magufuli anafanya vizuri sana, wapinzani hawana hoja.

Mimi kitu kinachonishangaza kwenye huu upinzani wa Tanzania ni jambo moja, ikiwa wao wenyewe wanashindwa kujitetea, watawezaje kuwatetea wananchi?, ni ukweli kwamba Magufuli amekiuka katiba kwa kukataza mikutano ya vyama vya siasa na maandamano, kwanini wanashindwa kwenda kulipinga hili jambo muhimu kwa ustawi wa siasa za Tanzania, badala yake wanakimbilia kushabikia kukamatwa Bombadier na kusema taarifa za kukua uchumi sio za kweli, hayo yana umuhimu gani kwao zaidi ya hilo la kubanwa na Magufuli?.. Wanahitaji maombi hawa akina Zitto
Zitto kuna vi hela vya usnitch alikuwa anapewa enzi za mkwere jk sasa hili jamaa undumilakuwili wa zito haliutambui wala hapewi commision ya kuvuruga upinzani na enzi zile zito alikuwa anatoka na hoja nzito za kitaifa kwa sababu alikuwa anapitishiwa na kwa mlango wa nyuma na CCM B" na TISS walimeguka wengine walikuwa wanafanya kazi kwa interest ya taifa na wengine walikuwa wanafanya kazi kwa interest za viongozi wa siasa.SO MSITEGEMEE ZITO KUWA HOJA ZENYE MSHIKO TENA ANAWEWESEKA PENGO LA LISSU ANAHISI ANAWEZA FIT YEYE
 
Zitto ni mtu aliyekengeuka ambaye hata cku moja usitegemee atatoa hoja yenye kuonyesha upeo wa jambo kutatulika badala yake ni mtu wa Aina ya kutoa hoja zikwepazo majibu ya moja kwa moja Yaani ataongea hili akiona linakaribia kutatulika ataibua lingine akiona nalo linaanza kuwezekana atarukia lingine nk kwanza alisema uwezekano wa kujengwa reli haupo ameona kazi zimeanza anatafuta flaws ambazo hazijulikani kuna kampuni kibao za ndani ambazo zmekula shavu mfano kuna kampuni ya Becco Ltd ambayo ndio inachonga barabara na kutengeneza tuta pia kuna viwanda vya nondo na cement vya hapa ambavyo vimekula shavu kuleta materials wakat kiwanda cha soga cha concrete sleepers kikianza kufanya kazi sasa anachoongea ni kipi
 
Hayo maswali yake ni mazuri, shida ni sehemu alipoyaulizia. Angeyauliza bungeni angepata majibu hapo hapo na ingetusaidia hata sisi watanzania kujua baadhi ya vitu. Hilo hakulifanya anaongelea kwenye press conference. Kwa utaratibu huo kweli atapata majibu?

Wewe ukijiuliza hayo maswali kwa nini hakuyauliza bungeni utapata jibu gani?

Maswali yake yote ni muhimu sana, japo kama ilivyo kawaida yenu mpo kikazi huku kwenye mitandao, mumeishia kumshambulia yeye binafsi. Amesema mkataba hauna kifungu cha kufungamanisha na sekta nyingine, imekaa ovyo sana hiyo na haijalishi mtapindisha pindisha kivipi kwenye mitandao, uhalisia bado utaonekana wenye kunuka.

Hata hivyo nakubaliana na wewe kwenye issue moja tu, kwamba alifaa kuuliza hayo maswali bungeni kama hoja ili ashinikize majibu. Sasa yeye kama ilivyo wapinzani hata wa huku kwetu ametafuta kiki kwenye press conference, ndivyo tulivyowazoea wapinzani hapa, hawaulizi bungeni, wataita wana habari na kutoa matamko ambayo hayajathibitishwa na huwa inabidi wajibiwe kwenye magazeti, wakati maswali yakiulizwa bungeni, serikali inalazimka kutoa majibu yaliyotuia.
 
Zitto anaanza kuchanganyikiwa, ninadhani hii ni kwasababu ya Magufuli amebana kila kona upinzani unakosa agenda za kuzungumza, hicho chuma cha Liganga anachosema, hata kuanza kuzalishwa hakuna hiyo dalili, huenda reli hii ikakamilika mapema kabla hicho chuma hakijaanza kuzalshwa, ni sawa na kusema kwanini Tanzania inaagiza gesi ya kupikia toka nje wakati kuna gesi nyingi Mtwara, au kwanini Kenya na Uganda wanaagiza diesel na petrol toka nje wakati wamegundua mafuta, Zitto amekuwa mropokaji sana siku hizi
Hoja muflisi. Ni defence mechanism ya mkosa hoja
 
Maswali yake yote ni muhimu sana, japo kama ilivyo kawaida yenu mpo kikazi huku kwenye mitandao, mumeishia kumshambulia yeye binafsi. Amesema mkataba hauna kifungu cha kufungamanisha na sekta nyingine, imekaa ovyo sana hiyo na haijalishi mtapindisha pindisha kivipi kwenye mitandao, uhalisia bado utaonekana wenye kunuka.

Hata hivyo nakubaliana na wewe kwenye issue moja tu, kwamba alifaa kuuliza hayo maswali bungeni kama hoja ili ashinikize majibu. Sasa yeye kama ilivyo wapinzani hata wa huku kwetu ametafuta kiki kwenye press conference, ndivyo tulivyowazoea wapinzani hapa, hawaulizi bungeni, wataita wana habari na kutoa matamko ambayo hayajathibitishwa na huwa inabidi wajibiwe kwenye magazeti, wakati maswali yakiulizwa bungeni, serikali inalazimka kutoa majibu yaliyotuia.
Hapo kwenye aya ya pili ndo kuna mzizi wote wa hoja hii. Huu ndio huwa ni udhaifu wa baadhi ya wanasiasa hasa hawa wa kiafrika. Hivi inakuwaje mtu ambaye ni mbunge kushindwa kutumia haki yake ya kibunge kuuuliza hoja nzito kama ile bungeni?


Kuhusu kumshambulia zito kwenye mitandao, japo wengine halituhusu, lakini ni kwa sababu njia aliyoitumia kufikisha ujumbe wake sio muafaka. Lakini pia sio wote wanaomshambulia, kuna wanaomuunga mkono. Pengine ni suala la mtazamo juu ya hoja yake.

Lakini yote hayo yanakuja kutokana na mambo yake. nimekupa mfano wa mambo ambayo alishawaahidi watanzania na akashindwa kuyatekeleza. Hilo lilisababisha aondolewe imani kwenye mambo anayosema bila ushahidi.
 
Kama ni kweli basi serikali wamebugi sana.
Ila it is hard to believe huyo mtoa hoja (ZZK).
 
Hivi wewe una akili kweli?, mbona unashindwa kujenga hoja vizuri ili tuweze kuumiza vichwa wakati wa kukujibu badala yake unajenga hoja kama mwendawazimu, ujenzi wa reli toka Nairobi- Naivasha nao haupo?, kwani reli unaanza na tuta ndiyo unaweka vyuma au unaanza na vyuma ndiyo unajenga tuta?, timeframe ipi unayotafuta wakati umeambiwa kila kipande cha reli kilichokabidhiwa contractor analazimika kumaliza ndani ya miezi 36 tangu siku mkataba umesainiwa?, tangu kipande cha Dar - Morogoro kuanza kujengwa huu ni mwezi wa tano, ulitegemea tayari wawe wamelaza mataruma ya reli ndani ya kipindi hicho ambacho sehemu kubwa ni mobilization and ground cleaning?, acha kuwa kama umekunywa chang'aa, jadili kwa kutumi akili ili ujibiwe kwa kutumia akili
Nivizuri kumjibu
lakini sio kila kichaa lazima ajibiwe
 
Kwa mujibu wa uchambuzi wa Zitto Kabwe, misumari, malighafi na hata makampuni ya kuchimba kokoto zitatoka kwa Waturuki. Watanzania wataishia kupokea tu basi, sasa nashangaa wale hukesha huku JF wakibeza reli ya Kenya wakati sisi tulihakikisha makampuni ya ndani yalinufaika pakubwa Local Procurement in SGR Stands at 10 Billion - Ministry of Industry, Trade and Cooperatives
-------------------------------------------------------------------

Mwenyekiti wa Chama cha Siasa cha ACT Wazalendo, Mh.Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma, amesema kuwa, ni jambo la kushangaza kuona Serikali ikasaini mkataba wa shilingi Trilioni 7 kujenga Reli bila kuweka vifungu vya kufungamanisha na sekta nyingine nchini.

Mh.Zitto akahoji kuwa, inawezekanaje kweli hata misumari ( screws) nchi hii haiwezi kutengeneza mpaka iagizwe kutoka Uturuki na kwamba yani hata kampuni ya kuchimba kokoto itoke Uturuki,”? alihoji.

Akiendelea kuonyesha kushangazwa na jambo hilo alisema kuwa, mpaka serikali itegemee malighafi hizo kutoka nje hivi viwanda vya chuma nchini CTI, TPSF vinafanya kazi gani sasa.

“Nielezeni hili, hamuwezi kuzalisha kitu chochote kulisha ujenzi wa Reli ya Kati ya SGR katika BOQ ya Mradi wa SGR, hamna muwezalo? Serikali iliwapa BOQ mkashindwa?” alihiji Mbunge huyo.

Akasema, ata ukiwauliza watu wa Wizara hawana majibu, wanasema Mkataba ali alifanya makubaliano Rais mwenyewe.

Aidha aliendelea kusema kuwa, inawezekanaje kuamini hili na kwamba hawezi kumuuliza rais na kwamba wao kazi yao ni kukosoa tu.

“Amekasirika, Siwezi kumwuliza mtu aliyekasirika, tena Amiri Jeshi Mkuu” alisema.

Wakati wa Mdororo wa Uchumi Asia mwaka 1997-1998 Waziri Mkuu wa Malaysia Tun Mahathir Mohammed alifanya miradi mikubwa sana ikiwemo kujenga Mji Mpya, barabara kubwa na Jengo la Petronas.

Ili kuingiza fedha kwenye uchumi na kuchochea shughuli nyengine za uchumi na kukuza mahitaji ( aggregate demand). Malaysia ikawa nchi ya kwanza kuibuka kutoka Asian Financial Crisis.

Aliongeza kuwa, sisi watawala wetu wamekwenda madarasa tofauti na kusoma vitabu tofauti vya Uchumi? Unajenga Reli kwa pesa yako ( inavyodaiwa), kwa hiyo unakusanya kodi kutoka kwa watu wako, unanunua US$, unamlipa Mkandarasi. Mkandarasi ananunua kila kitu kutoka nchini kwao Uturuki, mataruma ya Reli, Chuma, Screws na Misumari na hata mchimba kokoto Mturuki.

“Kwenye uchumi hii inaitwa leakages. Uchumi wetu unahitaji more inflows, unajengaje Reli kwa kutumia Chuma kutoka nje wakati una hazina ya chuma Ludewa?, unamwaga TZS 7 Trilioni bila kuhakikisha offsetting? Natamani kuiona hiyo BOQ ya Reli ya Kati”, akasema Mh.Zitto.

Alisema, suala hili linanisumbua sana, ni vigunu kuamini kuwa watawala waliokwenda shule na wenye uzoefu Serikalini hawakuona faida kubwa ya offsets na kwamba Baraza la Mawaziri limejaa wasomi wenye PHDs, inashangaza kuona kama ni kweli wameshindwa kuona hili.

Alimaliza kusema kuwa, fedha zetu wenyewe tunatengeneza ajira nje ya nchi huku sisi tukiwa vibarua tu na wagonga reli, Trilioni 7 zingechochea sana uchumi.akasema, kutokana na hili ni vyema watetezi wa Serikali, mnaojua kuitafsiri Serikali, lifanyieni kazi suala hili. nisaidieni.


INASHANGAZA SERIKALI KUWEKA MKATABA WA TRILIONI 7 KUJENGA RELI BILA KUSHIRIKISHA SEKTA NYINGINE- MH.ZITTO
Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.
Kwa mujibu wa uchambuzi wa Zitto Kabwe, misumari, malighafi na hata makampuni ya kuchimba kokoto zitatoka kwa Waturuki. Watanzania wataishia kupokea tu basi, sasa nashangaa wale hukesha huku JF wakibeza reli ya Kenya wakati sisi tulihakikisha makampuni ya ndani yalinufaika pakubwa Local Procurement in SGR Stands at 10 Billion - Ministry of Industry, Trade and Cooperatives
-------------------------------------------------------------------

Mwenyekiti wa Chama cha Siasa cha ACT Wazalendo, Mh.Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma, amesema kuwa, ni jambo la kushangaza kuona Serikali ikasaini mkataba wa shilingi Trilioni 7 kujenga Reli bila kuweka vifungu vya kufungamanisha na sekta nyingine nchini.

Mh.Zitto akahoji kuwa, inawezekanaje kweli hata misumari ( screws) nchi hii haiwezi kutengeneza mpaka iagizwe kutoka Uturuki na kwamba yani hata kampuni ya kuchimba kokoto itoke Uturuki,”? alihoji.

Akiendelea kuonyesha kushangazwa na jambo hilo alisema kuwa, mpaka serikali itegemee malighafi hizo kutoka nje hivi viwanda vya chuma nchini CTI, TPSF vinafanya kazi gani sasa.

“Nielezeni hili, hamuwezi kuzalisha kitu chochote kulisha ujenzi wa Reli ya Kati ya SGR katika BOQ ya Mradi wa SGR, hamna muwezalo? Serikali iliwapa BOQ mkashindwa?” alihiji Mbunge huyo.

Akasema, ata ukiwauliza watu wa Wizara hawana majibu, wanasema Mkataba ali alifanya makubaliano Rais mwenyewe.

Aidha aliendelea kusema kuwa, inawezekanaje kuamini hili na kwamba hawezi kumuuliza rais na kwamba wao kazi yao ni kukosoa tu.

“Amekasirika, Siwezi kumwuliza mtu aliyekasirika, tena Amiri Jeshi Mkuu” alisema.

Wakati wa Mdororo wa Uchumi Asia mwaka 1997-1998 Waziri Mkuu wa Malaysia Tun Mahathir Mohammed alifanya miradi mikubwa sana ikiwemo kujenga Mji Mpya, barabara kubwa na Jengo la Petronas.

Ili kuingiza fedha kwenye uchumi na kuchochea shughuli nyengine za uchumi na kukuza mahitaji ( aggregate demand). Malaysia ikawa nchi ya kwanza kuibuka kutoka Asian Financial Crisis.

Aliongeza kuwa, sisi watawala wetu wamekwenda madarasa tofauti na kusoma vitabu tofauti vya Uchumi? Unajenga Reli kwa pesa yako ( inavyodaiwa), kwa hiyo unakusanya kodi kutoka kwa watu wako, unanunua US$, unamlipa Mkandarasi. Mkandarasi ananunua kila kitu kutoka nchini kwao Uturuki, mataruma ya Reli, Chuma, Screws na Misumari na hata mchimba kokoto Mturuki.

“Kwenye uchumi hii inaitwa leakages. Uchumi wetu unahitaji more inflows, unajengaje Reli kwa kutumia Chuma kutoka nje wakati una hazina ya chuma Ludewa?, unamwaga TZS 7 Trilioni bila kuhakikisha offsetting? Natamani kuiona hiyo BOQ ya Reli ya Kati”, akasema Mh.Zitto.

Alisema, suala hili linanisumbua sana, ni vigunu kuamini kuwa watawala waliokwenda shule na wenye uzoefu Serikalini hawakuona faida kubwa ya offsets na kwamba Baraza la Mawaziri limejaa wasomi wenye PHDs, inashangaza kuona kama ni kweli wameshindwa kuona hili.

Alimaliza kusema kuwa, fedha zetu wenyewe tunatengeneza ajira nje ya nchi huku sisi tukiwa vibarua tu na wagonga reli, Trilioni 7 zingechochea sana uchumi.akasema, kutokana na hili ni vyema watetezi wa Serikali, mnaojua kuitafsiri Serikali, lifanyieni kazi suala hili. nisaidieni.


INASHANGAZA SERIKALI KUWEKA MKATABA WA TRILIONI 7 KUJENGA RELI BILA KUSHIRIKISHA SEKTA NYINGINE- MH.ZITTO
 
Boss hii nchi inaenda ilimradi kuna kucha! Mkuu wetu wa serikali ubongo wake uko na shida kubwa sana...






Hao wanaodiss bila ushahidi thabiti ndio hao hao wanaomtetea Baba Ubaya kila ujinga aufanyao so isikushangaze buda
 
Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.
Zitto sio Mkenya wewe, acha kutuaibisha...hoja za Zitto zimekuwa NZITO hadi tunatafuta Wakenya wa kuwalaumu.
 
Duh hatari!!!!!! sana naona wegi hamjamuelewa Zito, wtzania walio wegi hatujui macro economics au micro economics hata fiscal policy hatuzielewi kabisa tumejaa siasa na ushabiki wa vyama kuenda mbele hatuwezi kufanya uchambuzi wa economic issues hata kame wegi tulisoma comb HKL HGL basi tu some vitabu tuongeze maarifa tuwe na upeo wakuelewa na kuchangia mambo mengine ya kitaifa........7trion kunjenga reli kwa kutumia kampuni za kigeni na mari ghafi za kigeni inakua "capital fright" ni hatari kwa unchumu we ndani na thamani ya shilling viza vie dollor ineleta economic stagnation kwa mda huo.....
 
Wakenya hatua hizi zinazochukuliwa na nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi ni lazima roho ziwaume sana. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilikuwa zinatuibia mali zetu. Mfano madini ya Tanzanite, mbunga zetu za wanyama, kuutangaza mlima Kilimanjaro hata ardhi yetu wanaionea wivu maana huko kwao ni jangwa hasa sehemu za kasikazini.. Juzi tu tumewanyang'anya mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda. Hivyo, kwa sasa wakenya hawawezi kuisema vizuri Tanzania.

Madini ya Tanzanite, Kenya na hoja ya Zitto wapi na wapi, mkilipwa kutetea serikali kwenye figisu zake muwe mnashirikisha na ubongo pia, sio kuandika andika tu.
 
Back
Top Bottom