Mitambo ya viatu Magereza yawasili

Mitambo ya viatu Magereza yawasili

diana chumbikino

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
428
Reaction score
368
1583426727291.png



AWAMU ya kwanza ya mitambo ya Kampuni ya Kutengeneza Viatu ya Jeshi la Magereza imeshawasili nchini kutoka nchini Italia. Hayo yamebainishwa na Msemaji wa Jeshi la Magereza nchini, Amina Kavirondo alipozungumza na HabariLEO.

Kavirondo amesema makontena 15 kati ya 80 ya mitambo hiyo yaliwasili nchini mwisho wa mwezi uliopita na yameshafikishwa kwenye kiwanda hicho mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. Amesema awamu ya pili itakuwa na kontena 23 na awamu ya tatu itakuwa na kontena 42, hivyo kufanya mzigo wote kuwa na jumla ya kontena 80.

Kuja kwa mitambo hiyo kutalifanya Jeshi la Magereza kupitia kampuni yake ya Karanga Leather Industries kuimarisha uwezo wake wa kujitegemea kutokana na uwezo litakaokuwa nao katika kuzalisha viatu vya kijeshi na viatu vya kiraia. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Masoud Omari amesema mitambo hiyo haijafungwa kwa kuwa inasubiri awamu ya pili ya mitambo mingine ambayo iko njiani ili ifungwe kwa pamoja.

Kwa mujibu wa Omari, kampuni hiyo kwa sasa inazalisha buti za jeshi pekee lakini mitambo inayokuja itawapa fursa ya kuanza kutengeneza viatu vya kiraia vya wanawake, wanaume na watoto kuanzia Agosti mwaka huu endapo kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa
 
Kweli maana kuvaa vya wachina nayo enzi hizi za corona, yahitaji moyo.
 
Nimeiona hiyo mitambo mitatu hapo juu kwa mfano huo wa kushoto hapo unatumia umeme kidogo sana.

Na hata huo wa chini hapo haupatikani sehemu nyingine yoyote zaidi ya hapa Tanzania.

Hongera sana awamu ya 5 kwa mitambo hiyo hapo juu.
 
Nimeiona hiyo mitambo mitatu hapo juu kwa mfano huo wa kushoto hapo unatumia umeme kidogo sana.

Na hata huo wa chini hapo haupatikani sehemu nyingine yoyote zaidi ya hapa Tanzania.

Hongera sana awamu ya 5 kwa mitambo hiyo hapo juu.
Sasa kama mitambo hiyo haipatikani sehemu nyingine ispokuwa TZ,kwenye makonte imeingia ikitokea/kutengenezwa Dodoma au Geita?
 
Aibu sana, wabongo kibao wanaviwanda vya kuweza kutengeneza hizi mambo. Hata hao magereza wenyewe wanaweza kwa kutumia wafungwa kwa teknolojia zetu wakawa wanatengeneza viatu vya kutosha.

Tanzania ya viwanda itafika lini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Magereza ni watengenezaji wazuri sana wa furniture, ila bei zao ni shidaa!
Lakini ni high quality, durable clean and nit"

Furniture zao sio kwa ajili ya wanyonge"
Kama vile vitanda pale sabasaba!


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Redmi Y2
 
View attachment 1378032


AWAMU ya kwanza ya mitambo ya Kampuni ya Kutengeneza Viatu ya Jeshi la Magereza imeshawasili nchini kutoka nchini Italia. Hayo yamebainishwa na Msemaji wa Jeshi la Magereza nchini, Amina Kavirondo alipozungumza na HabariLEO.

Kavirondo amesema makontena 15 kati ya 80 ya mitambo hiyo yaliwasili nchini mwisho wa mwezi uliopita na yameshafikishwa kwenye kiwanda hicho mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. Amesema awamu ya pili itakuwa na kontena 23 na awamu ya tatu itakuwa na kontena 42, hivyo kufanya mzigo wote kuwa na jumla ya kontena 80.

Kuja kwa mitambo hiyo kutalifanya Jeshi la Magereza kupitia kampuni yake ya Karanga Leather Industries kuimarisha uwezo wake wa kujitegemea kutokana na uwezo litakaokuwa nao katika kuzalisha viatu vya kijeshi na viatu vya kiraia. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Masoud Omari amesema mitambo hiyo haijafungwa kwa kuwa inasubiri awamu ya pili ya mitambo mingine ambayo iko njiani ili ifungwe kwa pamoja.

Kwa mujibu wa Omari, kampuni hiyo kwa sasa inazalisha buti za jeshi pekee lakini mitambo inayokuja itawapa fursa ya kuanza kutengeneza viatu vya kiraia vya wanawake, wanaume na watoto kuanzia Agosti mwaka huu endapo kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa
80 containers? Ina maana wataanzia kwenye kuchakata ngozi mbichi?

Jr[emoji769]
 
Sasa kama mitambo hiyo haipatikani sehemu nyingine ispokuwa TZ,kwenye makonte imeingia ikitokea/kutengenezwa Dodoma au Geita?
Tanzania hata twiga anapanda ndege na anafika salama kabisa, usicheze na watz wewe
 
Back
Top Bottom