Mitandao ya simu Tanzania ipo 'compromised'?

Mitandao ya simu Tanzania ipo 'compromised'?

Hii kesi ina mkanganyiko mwingi mpaka basi! Ngoja tuone huo mwisho wake utakuwaje.

Ila mpaka hapa ilipofikia naona matokeo ni Utetezi fc wanaongoza kwa 5, huku Jamhuri fc wakiambulia goli 1 tu, tena ni la kuotea! Na mfungaji akiwa ni Jaji Siyani.
 
Tatizo lilianzia hapa🐒👇
 
Je hawawezi kutoa hata siri nyingine ambazo si za nchi (za binafsi). Tumekuwa tukishuhudia wizi kwenye mitandao mpaka unashangaa mtu amejuaje balance yako.
Napendekeza sheria irekebishwe ili utoaji wa siri hizo uombwe na mahakama, siyo mr.A anaomba miamala ya B na anapewa tena bila kutaja sababu za kuiomba
 
Tigo wamejiharibia sana tu. Hawa akina Frank sijui Fredy ndio wanahusika kutoa siri za Mihamala kwa matepeli wa mtandaoni. TCRA wangekuwa wana akili TIGO inapaswa kushushiwa rungu kali sana. Mbowe afungue mashitaka dhidi ya TIGO kudai fidia.
Vodacom wametoa ushahidi huko Arusha dhidi ya Sabaya na Benk inetoa footage za CCTV Camera kumtia hatiani Sabaya. Kuna ubaya?
 
Je hawawezi kutoa hata siri nyingine ambazo si za nchi (za binafsi). Tumekuwa tukishuhudia wizi kwenye mitandao mpaka unashangaa mtu amejuaje balance yako.
Napendekeza sheria irekebishwe ili utoaji wa siri hizo uombwe na mahakama, siyo mr.A anaomba miamala ya B na anapewa tena bila kutaja sababu za kuiomba
Amesema wewe kutaka taarifa za mkeo au mumeo hawezi toa! Kumbuka hapo alipokea barua ya maombi kutoka Police kitengo cha uchunguzi wa kisayansi. Hoji je utaratibu wa ulifuatwa wa kutoa hizo taarifa?
 
Hii nchi tunaweza kushika namba 1, 2 na 3 duniani kwa unafiki. Wiki iliyopita shahidi katika kesi ya Ole Sabaya alitoka Vodacom akiwa ameletwa mahakamani na Jamhuri hatukusikia watu wakilalamikia faragha ya mteja. Jana Jamhuri imemleta mahakamani shahidi kutoka Tigo watu wanalalamika kuhusu faragha ya mteja. Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana. Tunapozungumzia faragha tusibague watu maana wote wako sawa kwenye jicho la sheria na wanapasws kutendewa haki.
 
Hii nchi tunaweza kushika namba 1, 2 na 3 duniani kwa unafiki. Wiki iliyopita shahidi katika kesi ya Ole Sabaya alitoka Vodacom akiwa ameletwa mahakamani na Jamhuri hatukusikia watu wakilalamikia faragha ya mteja. Jana Jamhuri imemleta mahakamani shahidi kutoka Tigo watu wanalalamika kuhusu faragha ya mteja. Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana. Tunapozungumzia faragha tusibague watu maana wote wako sawa kwenye jicho la sheria na wanapasws kutendewa haki.
Nayo ilikuwa kesi ya ugaidi?
 
Kwa issue ya ugaidi mkuu hakuna na cha kulinda maslahi ya mtuhumiwa,acha huyo mtumishi wa hiyo kampuni atoe ushahidi tuujue ukweli,tunaogopa nini kama viongozi wetu wana uweledi tunaodhani wapo nao,acha kesi iendelee Mkuu,kama atakuwa ameonewa tutajua tu ila acha Mahakama isikilize hadi mwisho hilo shauri
 
Mshana umeongea point yenye mashiko, ila vilaza hawawezi kunga'mua kwamba hili halikufanyika kiuweledi....yaani ni sawa na kumwonyesha adui mtego wako ulipo halafu utarajie siku nyingine atanasa kwenye mtego huo huo.
 
Kwa issue ya ugaidi mkuu hakuna na cha kulinda maslahi ya mtuhumiwa,acha huyo mtumishi wa hiyo kampuni atoe ushahidi tuujue ukweli,tunaogopa nini kama viongozi wetu wana uweledi tunaodhani wapo nao,acha kesi iendelee Mkuu,kama atakuwa ameonewa tutajua tu ila acha Mahakama isikilize hadi mwisho hilo shauri
Ushahidi sio tatizo tatizo liko kwa mashahidi na namna ya kuwasilisha ushahidi husika.. Afisa kipenyo ama pandikizi hatakiwi kujulikana popote pale na kwa hali yoyote ile.. Hiyo ni kwa usalama wake, idara yake na maslahi ya mwajiri wake
 
Ushahidi sio tatizo tatizo liko kwa mashahidi na namna ya kuwasilisha ushahidi husika.. Afisa kipenyo ama pandikizi hatakiwi kujulikana popote pale na kwa hali yoyote ile.. Hiyo ni kwa usalama wake, idara yake na maslahi ya mwajiri wake
Unafikiri yeye mwenyewe hajafikiria usalama wake na Mwajiri wake hawajafikiria usalama wa kampuni pia?

Pia kama ni kesi ya kubumba jaji atatoa hukumu sahihi na naamini hao watuhumiwa watabakia huru kama misingi ya kisheria ikizingatiwa
 
Hakuna siri kwenye makampuni ya simu, ukitaka taarifa na ukiwa na hela utaambiwa kila kitu.
 
Unafikiri yeye mwenyewe hajafikiria usalama wake na Mwajiri wake hawajafikiria usalama wa kampuni pia?

Pia kama ni kesi ya kubumba jaji atatoa hukumu sahihi na naamini hao watuhumiwa watabakia huru kama misingi ya kisheria ikizingatiwa
Nijuavyo kwenye hizi ishu ukiharibu ni lako hilo.. Utaachwa mataa ya ubungo.. Sirbuyer alitumikia maagizo lakini akaharibu... Kilichompata wote tunakijua
 
Nijuavyo kwenye hizi ishu ukiharibu ni lako hilo.. Utaachwa mataa ya ubungo.. Sirbuyer alitumikia maagizo lakini akaharibu... Kilichompata wote tunakijua
Yap anaweza kutolewa kafara na kampuni na kufukuzwa kwa kuichomesha kwa wateja kuwa kampuni haina siri ila tukija kwenye kesi sasa kama ushahidi wake ukihold water mtuhumiwa anaweza kuwa kwenye trouble sana,kwani hapo kumbukumbu za sauti zitawekwa wazi,sijui itakuwa vp.

Mawakili wa utetezi wa mtuhumiwa wanatakiwa kutulia sana hapo kwenye huo ushahidi wa sauti
 
Kazi ya kampuni za simu sio kulinda Siri za wahalifu!!! Au magaidi.

Kama wewe ni mhalifu ujue kabisa huko salama kwenye mtandao wowote wa simu
HUYU NI MMOJA WA WAPUMBAVU WACHACHE TULIOBARIKIWA NCHI HII
 
wakati hao vipenyo na nyoka wanaharibu biashara za watu kwa kujichomeka, ajabu nyingine hao nyoka na vimeo wapo kwenye nyumba za ibada, ni viongozi na waumini wa kawaida, ukijaribu kuusema uovu wa wa mamlaka utatulizwa kwa neno la mungu utii mamlaka na usiinyoshee kidole imetoka kwa mungu, ukishupaza shingo utajikuta mikononi mwa mamlaka unashitakiwa kwa uchochezi
Hata nyumba za ibada maafisa vipenyo wapo kuanzia kwenye jumuiya wapo.Unashangaa Nini? Lengo ni nchi iwe salama.Ulitaka nyumba za ibada wasiwepo?

Wapo kila Kona kuanzia maaskofu,mapdre,mashehe,wachungaji, masisita,nk
 
Baba Mchungaji, nani kakwambia kutumia simu ya kiganjani kuna siri? Popote pale ulimwenguni hadithi ni ile ile.

Osama was compromised largely by Al Kuwait phone call to his family. Snowden amekimbia US sababu alisema watumiaji wa simu na mitandao, mambo yenu yanaangaliwa.

Ukitaka tusijue wewe ni nani, achana na technojia. It has gone even worse...kuna nuclear scientist wa Iran aliuwawa mwaka huu na silaha ambazo hazina mtumiaji..using artificial intelligence.

Kiufupi, TIGO hawana kosa lolote. Kama wewe ni clean, kwanini uogope record zako za mawasiliano kuwekwa wazi?
 
FB_IMG_1635929182729.jpg
 
Back
Top Bottom